Uchaguzi 2020 Mechi kali nne za Uchaguzi Mkuu wa Wabunge ni majimbo ya Arusha Mjini, Kawe, Mbeya Mjini na Tarime Vijijini


Hata kama hao waumini wote ni wa wakazi wa KAWE...

Lililo la kweli ni hili;

Kwamba, waumini hao watakuwa wanaugua "UGONJWA WA UKOSEFU WA MAARIFA YA KIROHO" kama baba yao aliyepewa jukumu la kuwalea KIROHO watampa jukumu la KISIASA badala ya "KUKAA NYUMBANI MWA BWANA (BABA MUNGU) SIKU ZOTE"....

Kwa maoni yangu, nina hakika uamuzi huu wa Mch. Gwajima utakuwa umewachanganya sana waumini wake.....

Lazima wamegawanyika Makundi mawili...

Hata Yesu Kristo jaribu hili la kutaka kufanywa mfalme (mwanasiasa) lilimkuta lakini alilishinda vyema...
(SOMA INJILI YA YOHANA SURA YA 6 YOTE)

Ilitokea kuwa, walipoona anatenda miujiza sana, walimfuata na kutaka kumfanya "mfalme wao"...

(Mstari wa 14, 15)

".... 14. Basi watu wale walipoiona ishara (muujiza) ile, walisema, hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni. 15. Hali Yesu akitambua walitaka kuja kumshika (kumchagua kwa kura) ili wamfanye Mfalme, akajitenga (akawakatalia), akaenda tena mlimani peke yake......"


Watu hao walitaka awe mfalme wao siyo kwa sababu kweli walikuwa na dhamira safi mioyoni mwao, bali ilikuwa ni kwa sababu ya miujiza aliyoitenda...

Katika mawazo yao, walidhani kuwa, kwa kuwa mfalme wao basi wapambe wangeweza kunufaika na faida ya miujiza hiyo....

Kwa ufupi ni kuwa kusudi lao la kutaka kumfanya mfalme lilikuwa motivated na tamaa za kimwili zaidi na siyo KIROHO au UPENDO WA KIMUNGU...

Kwa kutambua hilo, YESU KRISTO aliwakwepa....

Sijui motives za Mch. Josephat Gwajima ni nini kwa kweli. Je, ni msukumo wa Roho Mtakatifu au ni tamaa yake mwenyewe tu?

Kanuni iko hivi;

Kama ni Mungu mwenyewe kamtuma na kumwagiza aache kujikita kwenye kazi ya wito wake wa UINJILISTI na UCHUNGAJI na UALIMU na UTUME na UNABII badala yake agombee Ubunge (nafasi ya kisiasa) ili aliyemtuma (MUNGU YEHOVA) atimize kusudi lake, basi itakuwa vile bila kujali ana waumini Kawe au Charambe au popote pale kwa sababu KUSUDI LA MUNGU HALISHINDWI na HALINA MAJUTO....

Lakini, upande wa pili kama Mch. Josephat Gwajima kwa sababu ya tamaa zake tu kaamua kujituma kwenye jukumu jingine bila uongozi wa Mungu, HAKIKA huu ndiyo utakuwa mwanzo na mwisho wa wito wake....

Mungu atamnyang'anya huduma yake na kumpa mtu mwingine. Kwa kimombo tunasema, IT'S THE BEGINNING AND THE FALL OF GWAJIMA....!!
 
Kusema kw

Kusema kweli 'wateja' wake ni watu wenye wakati mgumu ktk maisha na wanaotaka short cut ya maisha na bado anawakamua hawa hawa bila huruma. na wengi wanatoka kweli ktk makazi duni.
Ni kweli maana hadi wengine anawa nanihii!!!!!
 
Kwanza issue yake ya uuzaji madawa ya kulevya iliishia wapi?
 
sasa naona wapambe wanaumiia mno kusikia wasichopenda kusikia hata kama kipo.
Kuna sababu nyingi za kijinga kwa nini watu wanaugua BP wkati hawakupaswa
Hawa wanyanyembe uwawanavijimaneno viingi vya kujifariji wakati limoti ya kubadili chanel awana.
 
Kama unatusimulia mipango yenu michafu ya chama chako. Uamuzi ni wa wananchi sina hakika kama watawaruhusu kuleta ujinga wenu kwenye matokeo, hawatokubali ninaamini!
 
Wacha maneno Leta takwimu tuzisome hapa
 
Udini hauna nafasi kwenye huu uchaguzi,
Hata angegombea Shekhe Issa Ponda kama kwa vile anaushawishi na mchapa kazi angepewa tu ushindi.

Propaganda za udini hazitafua dafu!

Tumuunge mkono Gwajima kwa maendeleo yetu sote bila kujali imani zetu wala itikadi.
 
Dada etu. Halima. Imefika wakati sasa wa kukaa nyumbani azae na alee watoto wake
 
Gwajima yupi??? Huyu aliyehamasisha siasa za kikabila za kisukuma????!

Huyu aliyesema atageuza madrasa kuwa Sunday schools????

Huyu anayejirekodi akifanya mapenzi na waumini wake?????
Ni Heri nisipige kura kuliko kumpigia Gwajima.
 
Hapo kweli pagumu sana ila kwa watawala sina shida! hofu ni figisu watakazo fanyiwa hao wapinzani wa upinzani mbona wataelewa nn maana ya chama tawala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…