Gia kubwa
JF-Expert Member
- May 28, 2020
- 470
- 495
Nyerere alitunga katiba feki ili imlinde na kuanzisha vita Uganda ili kumfurahisha na kumrudisha madarakani best yake Obote! askari wetu wengi wakafa bila hatia!! mara Mwalimu akaanzisha vita vya ukombozi Afrika nzima na kuharibu rasilimali za bongo bila ridhaa ya wananchi lengo ni kutafuta sifa za kijinga ili yeye na Kwame Nkrumah wapewe uongozi wa serikali ya Afrika!!Mzalendo anaenda kuuwa ndugu zetu waganda wakati Nyerere kaiba Mali za umma na kutunga katiba mbovu yakumlinda yeye .
Mwalimu akaanzisha ujamaa ili nchi ibaki maskini wabongo wamtukuze yeye tu daima na watu wengi waliliwa na simba walipohamishiwa maporini eti kuanzisha vijiji vya ujamaa akaona haitoshi akashikia bango kiswahili na kuua lugha ya malkia ili wabongo washindwe kuwasiliana na watu wa nje wakamkimbia!! na hadi leo nchi imebaki kisiwa wachache wanaojua English ndio huweza kwenda nje sote tunazaliwa na kufia hapa hapa!! hata mkulima kuwasiliana na masoko lukuki ya nje hawezi!!
ukisoma vizuri ujamaa unaona kuwa ni mfumo usiofaa na yatakiwa nchi ichukue ubepari kwanza ikishaendelea labda ndio inaweza kuhamia ujamaa, mawazo ya kina Mwalimu ndio yameifanya Afrika kubaki nyuma kimaendeleo ukienda ulaya huamini maendeleo unayoyaona!! unabaki kujiuliza hivi sisi tumekwama wapi?
kwa wasiojua vizuri ujamaa ni mfumo unaopingana na human nature sababu mwanadamu ni selfish by nature na daima hutaka kujiendeleza mwenyewe na familia yake kwanza sasa ujamaa unamtaka mtu kujikana na kujali maslahi ya nchi kwanza kitu kisichowezekana na hivyo watendaji kuishia kuiba mali ya umma na kuifilisi nchi kama serikali ndio inashika njia kuu za uchumi, ni afadhali ya ubepari unaowapa raia umiliki wa uchumi kwa sehemu kubwa na kuilipa kodi serikali na hapo watu hawawezi kujiibia wenyewe!! kwakuwa watu hawajiibii basi shughuli za kiuchumi wanazomiliki na kushindania soko basi hupata faida kubwa na kuilipa serikali kodi kubwa inayojenga miundombinu ya nchi kwa spidi ya rocket!!
basi mzee wa watu aka Mwalimu akajifia bila kumuona rais wa awamu ya tano kama alivyotuahidi akaja fisadi Chenge akaifanyia marekebisho katiba ikawa chuma cha pua cha kumchapia bakora heavy raia wa bongo! katiba ikaondoa mamlaka yote ya raia, ikautengeneza uchaguzi usio huru wala haki kuwapa rungu wakurugenzi kuamua mshindi na hapo kuhakikisha ushindi ni wetu siku zote!! shame on Chenge lile zee fisadi limesahau kifungu lilichoandika lenyewe likiwa ndio mwanasheria mkuu kinachosema mali za watanzania zitatumika kuwanufaisha watu wote basi Zee likajigawia mgao wa escrow bila aibu!!niliumia sana roho mchungaji kaiba sadaka!!