Mfanyabiashara Alex Msama akamatwa kwa tuhuma za Utapeli wa Viwanja vya Tsh. Milioni 800

Mfanyabiashara Alex Msama akamatwa kwa tuhuma za Utapeli wa Viwanja vya Tsh. Milioni 800

Ila huyu bwana ana mazuri yake pia.

Binafsi sikuwahi kumjua Hadi pale nilipokutana Hospital usiku saa sita nikiwa na mtoto wangu ambae alizidiwa GHAFLA nyumbani na kumpeleka hapo hospital nikitegemea Bima mfukoni shi. Mia mbovu Sina🤣

Basi mtoto alipimwa akawa amelala kwa benchi.

Ndipo yeye alipotokea na kumkuta mtoto kalala akasema mtoto msiponji,

Kishaa akaagiza nesi ampe panado.

Mimi nikajua ndo Mganga Mkuu wa hapo.

Akaagiza apimwe na Homa ya dengue,Kipimo kulipia 50,000/ sisi tukasema hatuna pesa hiyo.

Yeye akamwagiza nesi ampime mtoto,atalipia yeye!!!

Majibu yakatoka hakuna kitu ila mtoto kachemka mbaya sana!!

Akatuambia tuchukue Bima atupeleke hospital nyingine! Mimi nikajisemea huyu ni MMILIKI wa hii hospital hivyo anatupeleka hospital yake nyingine kubwa🤣

Wale wahudumu wote walokuwa kaunta aliwapa 15,000 Kila mmoja na WALIKUWA kama 4 hivi.

Wakati nachukua bima yangu alikuja nesi mmoja AKANIAMBIA unahama hospital huyo mnamjua ??

Nikasema Mimi simjui na Mimi najua nyie ndo mmetujamisha.!!

Nikasema asije kuwa mtekaji,Nikaandaa meseji ya maelekezo kwenda kwa Kamanda wa polis nikaitegesha kabisa ili nikiguswa tu naisend🤣🤣

Nilipotoka nje nilikuta Gari jeusi V8 MPYAAA😀Kwa woga woga na kwa tahadhari ya hali ya juu nilipanda😀

Aliendesha Dakika 10 nyingi tulifika hospital hiyo ,Hapo bima hawatumii ni kulipa kwa kesho ,

Akaagiza tuhudumiwe Kila kitu gharama atakuja kulipa yeye!!!


Kweli mtoto alianza vipimo upya na kifupi gharama ilikuja 136,000/

Tylipomaliza matibabu tukampigia sekunde nyingi alikuja akalipa gharama zoote👏

Nilimuomba namba yake alinipa , Nilimuuliza upo wapi hakusema .

Siku Moja tulienda tena kwenye hiyo hospital wife anajuana na nesi mmoja alimuuliza yule mtu wa siku ile alikuwa nani,?

Akamwambia huyo ni Alex Msama huwa anapenda sana kusaidia wakinamama na hasa Watoto😀

Milima haikutani ,Binadamu hukutana !! Tulikutana nae tena baada ya miezi mingi hapo hapo na majira hayo,Tulimkumbuka tukamsogelea tukamkumbushia akaja akamuona mtoto akatuachia tena 50,000/=

Ndo mwisho wa kuonana nae tena Hadi Leo YAPATA miaka sita nyuma!!
Kuna mtego alikuwa anakuwekea. Una bahati sana na nakushauri ukimuona siku nyingine usijirahisi hivyo.

Iko siku atakubebesha madawa ya kulevya kama alivyomtumia Rose Muhando
 
Du naona wana JF tumeshamhukumu Mr. Msama,tuangalie upande wa pili wa coin,je waziri kumpeleka suspect police ametumia sheria gani?,je suspect amefunguliwa docket police?je police wameshafanya uchunguzi na kuthibitisha tuhuma dhidi ya suspect?ni vema kama nchi tukaanza kuishi kisheria sio mihemko ya kisiasa,sasa huyu anatakiwa apelekwe kwa court within 48 hrs je police wana kesi dhidi yake?,KATIBA mpya ni muhimu maana walalamikaji wangeweza kwenda kwa PP kutoa malalamiko yao kama police haikuwasikiliza,kitendo hiki cha waziri kwangu ni NO na udhalilishaji,huwezi kumtoa suspect hadharani kabla ya kupanda kwa court
Wewe kama ni TAPELI kama Alex Msama tambua kuwa dawa yako inachemka na huwezi kukwepa kikombe anachokunywa Msama.

Masuala ya Polisi na Mahakama watayatatua wenyewe, sisi hayatyhusu
 
Safi sana, kazi nzuri Jerry Silaa. Huyu tapeli anatakiwa kupewa kifungo kabisa sio tu pingu pekee.
Ni vyema akapelekwa mahakamani ili apate haki yake kinyume na hapo bado hakutakuwa na ukweli kinyume chake ni kumvujia haki zake
 
Wewe ni mpumbavu na mshamba mno. Unadhani wauza madawa, magaidi na majambazi wakubwa huwa hawajitoi kwa jamii? Hiyo hela aliyokusaidia wewe ni machozi ya watu wengi sana.
Elewa wewe ni delinquent member wa JF,huu ni mjadala na kila mmoja wetu ana haki ya kuchangia kwa uhuru na elewa we have the right to disagree
 
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam kwa tuhuma za kutapeli viwanja vinne vya Beatrice Mshumbuzi, vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi milioni 800.

Msama amekabidhiwa kwa polisi leo na Waziri wa Ardhi, Jerry Silaa.

View attachment 2968425
Mawaziri Jerry Slaa na Dorothy Gwajima wanafanya kazi kwa vitendo, pongezi kwao ikiwa hatua kama hizi zitachukuliwa kwa wakati basi malalamiko ya wananchi yatapungua kama si kuisha.
 
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam kwa tuhuma za kutapeli viwanja vinne vya Beatrice Mshumbuzi, vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi milioni 800.

Msama amekabidhiwa kwa polisi leo na Waziri wa Ardhi, Jerry Silaa.

View attachment 2968425
KADA kawa TAPELI? AIBU
 
View attachment 2968415

Promota wa Muziki wa Injili , ambaye pia ni mlokole Alex Msama , akiwa pia ni Mkurugenzi wa Msama Promotion , amekamatwa na Polisi kwa makosa ya Utapeli wa viwanja

Msama Pia ni kada Maarufu wa CCM na Mgombea wa mara kadhaa wa nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama hicho

Amedakwa leo alipoitikia wito wa Waziri wa Ardhi aliyemraka aripoti ofisini kwake kwa Mahojiano
Ndio kwanza namuona huyu mtu anaishi wapi!
 
Matajiri wa bongi wengi matapeli ,mtu kafa ila unasikia alitapeli watu.
Huyu ukimpangisha tu eneo lako
Lazima ataleta uzushi,kufoji nyaraka atake akudhulumu
Hata ile ofisi yake iliyokuwa block41 kwa kina mzee sheta(rip)
Alitaka kuwaletea figisu wamiliki
Walikuja mtoa
Watu humu wakimtetea basi watakuwa hawamjui

Ova
 
A
Alafu watu wengi hawafahamu..ila huyu ruge ndy alimuibua jamaa alikuwaga hana hili wala lile...alianzaga kazi prime promotion ya clouds longtime
Badaye likajiongeza
Ni mtu wa 4 😄
So limetoka mbali.......sema alivyokuwa hana kitu alikuwa syo mzushi ila alivyopata kijinafasi ndy
Ego ikamjia

Ova
Alikua dereva tu Prime
 
Back
Top Bottom