Mfanyabiashara: Kiburi cha TRA kinasababishwa na Bosi wao Mwingulu Nchemba

Mfanyabiashara: Kiburi cha TRA kinasababishwa na Bosi wao Mwingulu Nchemba

Na ndo tatizo lingine. Kuna watu wana mzigo mkubwa hawana risiti za manunuzi inabidi awape machinga. Akiuza yeye kwa Tin yake hawezi claim VAT.

Halafu kuna wale sasa ambao input zao hazina VAT mfano hoteli ila Output keshafika M100 anatakiwa kuwa VAT.
Sasa huna receipt mzigo ameutoa wapi lazima mkwepa kodi, kama wewe umekwepa kodi utaweza vipi kudai kodi wakati huyo mtu ni muhujumu uchumi.

Lakini kama wewe ni mfanyabiashara umeagiza au umenunua mzigo una receipt zako za manunuzi kuonyesha kama ulilipa VAT.
 
Mafisadi yana nguvu sana awamu hii. Hivyo hakuna waziri atasimama awamu hii ambaye atapingana na mafisadi
 
𝐓𝐈𝐒𝐒 𝐬𝐚𝐦𝐚𝐡𝐚𝐧𝐢 𝐧𝐢 𝐮𝐬𝐚𝐥𝐚𝐦𝐚 𝐰𝐚 𝐓𝐚𝐢𝐟𝐚 𝐤𝐢𝐫𝐞𝐟𝐮 𝐜𝐡𝐚𝐤𝐞 𝐦𝐤𝐮𝐮 𝐬𝐚𝐦𝐚𝐡𝐚𝐧𝐢
Tanzania intelligence and security service
 
Sasa huna receipt mzigo ameutoa wapi lazima mkwepa kodi, kama wewe umekwepa kodi utaweza vipi kudai kodi wakati huyo mtu ni muhujumu uchumi.
Ukifanya biashara utaelewa.

Mfano 1. mpo 30, mmeagiza mzigo China ili kujaza contena, mzigo unapita kwa tin moja pale bandarini. Mkishagawana mzigo unatoa wapi risiti yenye tin yako?

Mfano 2. Una hoteli ww unahitaji hoho, biringanya, nyama n.k kwa wakulima wasio na risiti. Utanunua hayo mavitu yote bila risiti utaiclaim wapi?

Mfano 3. Contractors wadogo, umeshawahi kupata tenda vijijini? Sehemu ambayo hakuna hardware kubwa zenye risiti za VAT? Unabakiwa na option mbili, either usafirishe cement/nondo zako au ukubali VAT ikuumize.

VAT ni ya kutazamwa upya. Ni kisababishi cha kutokutoa risiti. Watu wanakwepa kuingia.
 
Back
Top Bottom