Mfanyabiashara: Kiburi cha TRA kinasababishwa na Bosi wao Mwingulu Nchemba

Mfanyabiashara: Kiburi cha TRA kinasababishwa na Bosi wao Mwingulu Nchemba

Mgogoro unaoendelea ni kwamba wafanyabiashara hawapendi kulipa kodi kama zile wanazolipishwa wafanyakazi kwa jina la PAYE.

Serikali kama inawasikiliza wafanyakazi basi iwasikilize wafanyakazi pia.
Sawasawa
 
Ukifanya biashara utaelewa.

Mfano 1. mpo 30, mmeagiza mzigo China ili kujaza contena, mzigo unapita kwa tin moja pale bandarini. Mkishagawana mzigo unatoa wapi risiti yenye tin yako?

Mfano 2. Una hoteli ww unahitaji hoho, biringanya, nyama n.k kwa wakulima wasio na risiti.

Mfano 3. Contractors, umeshawahi kupata tenda vijijini? Sehemu ambayo hakuna hardware kubwa zenye risiti za VAT? Unabakiwa na option mbili, either usafirishe cement zako au ukubali VAT ikuumize.
1. Bill of landing inaorodha ya mizigo yote ndani ya container, so unapata total ya kodi zote kama ni different products zinapigwa kodi tofauti.
(i ) mwagizaji ana option ya kushare copy ya hiyo receipt kwa kila mtu kuonyesha mzigo wake uliingia na container lipi ili akadai VAT yake huko mbele.
(ii) kuondoa hizo kero huyu shipper awaagizie na atoe; ila awacharge bei ya kununulia, jumlisha + import duty + VAT (alizolipia bandarini) akishatoa na kuwapa receipt kama wamenunua kwake and value chain starts from there awa retailers wanaweza kwenda kudai VAT wakishauza na wao kama wanesajiliwa, everything is legal and can be traced.

2. Ukishanunua bidhaa halafu wewe ndio final user i.e nyanya, nyama, vitunguu na vinginevyo; uruhusiwi kudai VAT wewe ndio final user unatengenezea product nyingine.

3. Same thing kwenye ujenzi wewe ndio final user wa hizo products; unless sheria inaruhusu baadhi ya manunuzi specifically kwa wakandarasi kudai VAT and if that’s the case commonsense ni kutafuta mtu anaekutoza VAT kama unataka ku claim.
 
Somo la kodi lingeanzia chini kabisa primary huko.
Kama hujasoma mambo ya uhasibu na uchumi mambo ya kodi yanakupita kushoto, matokeo yake ukiingia uraiani mambo unakuta vururu kabisa yaani tofauti na mategemeo yako.
Ni sahihi, lakini kodi zimezidi mno, kila kona kodi alafu unalipia kitu kimoja. Ni vyema kungekuwa na mfumo mmoja, ukilipa hapo basi. Sheria zetu pia zilekebishwe zinaleta mazingira ya Rushwa.
 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo, leo Mei 17, 2023.



Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kimataifa la Kariakoo wametoa malalamiko mbele ya Waziri Mkuu ambapo wameilaimu TRA kwa kutokufuata taratibu sahihi za utozaji kodi wakishirikiana na Jeshi la Polisi.

Mfanyabiashara mmoja akitoa malalamiko yake amesema kampuni yake imewahi kusumbuliwa na Askari wa Kituo cha Kamata akidaiwa kutokuwa na risiti halali za mizigo yake, jambo ambalo sio la kweli. Pia, amemtaja kwa jina moja Askari anayehusika na kashfa nyingi za hapo kuwa ni "Mpemba"

"Kuna Askari anaitwa Mpemba hapo Kamata amenipelekesha sana, pia kuna mwingine mweusi yuko hapohapo wanatupelekesha sana. Inashangaza sana Askari wanakusumbua kama vile TRA hadi unajiuliza kazi ya TRA inafanywa na Askari"

Ameendelea, "Kwa kuwa umesema tufunguke, niseme Nchi hii hadi Polisi ni wezi mno, hakuna wakati mgumu kufanya biashara kama wakati huu, tunaiwezesha Nchi lakini wanatukatisha tamaa

Ameongeza, "Tufanye mabadiliko makubwa ili twende mbele, mengine siwezi kusema hapa, nikiyasema watanikamata, nawajua hawa"

Aidha, mfanyabiashara mwingine aliyesimama kwa niaba ya wafanyabiashara wa Vitenge amemhoji Waziri Mkuu kama Serikali haitaki wanawake nchini wapendeze maana wamekuwa wanachukuliwa kama wanauza madawa ya kulevya.

Wamewalamumu pia watu wanaohusika na uzoaji wa taka kuwa wanadai pesa zisizotakiwa, kwani huenda hadi kwenye stoo zao. Pia, watu wa TRA wamekuwa wanawafata hadi majumbani wakitaka pesa. Mama huyo amehoji, "Kwa hiyo tukadange?, hapa sio mahali sahihi kwa kuongea, nitahatarisha maisha yangu. Nipe namba nije chemba tuzungumze"

Kuhusu sababu ya kufunga maduka, mfanyabiashara mmoja amesema walifanya hivyo kutokana na;
  1. Uwepo wa utitiri wa kodi usioendana na uhalisia, "Double Taxation"
  2. Kuhamia kwa maduka barabarani kwa jina maarufu la machinga, watu ambao wamekuwa wanatumiwa na wafanyabiashara wakubwa hivyo kubana biashara zao (wafanyabiashara waliosajiliwa). Duniani kote hakuna machinga kwenye vituo halisi vya kibiashara
  3. Adhabu za makosa ya kutolipa kodi zisizolipika sababu ya ukali wake hivyo kuweka mianya ya rushwa
Kero nyingine iliyotajwa ni maafisa wa TRA kuwa na mamlaka makubwa ya kukadiria faini za malipo pindi wanapowakatama wafanyabiashara kwa makosa mbalimbali, ambayo mengi ni ya kusingiziwa. Jambo hili huleta mianya ya rushwa kwa sababu TRA huwaalika kwa mazungumzo ya pembeni kinyume cha taratibu.

Mfanyabiashara huyo amesema, "TRA wanatufuata mpaka nyumbani jamani, tunaomba namba wakija ili tuwatumie picha, wanatutishia wanazuia Biashara zetu, kwanini watufuate nyumbani? Waziri Mkuu siwezi kukwambia kila kitu, hapa sio sehemu salama nipe namba nikufuate chemba, la sivyo nitahatarisha Maisha yangu

Ameendelea, "Kuna kodi mpya ya Stoo ambayo inaelekeza ukikutwa na kosa unapigwa faini ya Tsh. Milioni 4. Kodi hiyo inatengeneza mazingira ya Rushwa na hatujui kama ipo kihalali au la.

Ameongeza, "Mfanyabiashara hauwezi kukamatwa kwa Mwezi mara tatu, inabidi mzungumze pembeni"

Pia, urasimu kwenye mamlaka za serikali hasa utoaji wa leseni, kupandishwa kila mwaka kwa makadirio ya kodi kwa lugha maarufu ya "Maelekezo kutoka juu", kodi kubwa ya stoo za bidhaa, mfumo mbovu wa kodi ya forodha bandarini pamoja na kamatakamata za aina mbalimbali zinazofanyika sokoni hapo.

Hoja nyingine iliyoibuliwa ni Matamshi ya Waziri Mwigulu Nchemba kudharau wabunge wengine ambao ni wawakilishi wa wananchi, amekuwa na kauli chafu zinazokatisha tamaa wafanyabiashara, mfano ni ile ya kuwa yeye ni daktari wa uchumi, hawezi kubishana na waganga wa kienyeji.

Mfanyabiashara huyo amesema jeuri yote ya TRA inasababishwa na Waziri wa fedha ambae ni bosi wao mwenye jeuri, hashauriki, haambiliki. Wamewahi kuzungumza nae mara kadhaa lakini hajawahi kutekeleza hoja za mazungumzo hayo. Pia, mfanyabiashara huyo amesema Waziri Nchemba hafai kuwepo kwenye nafasi yake.

Waziri wa Biashara amelaumiwa pia kwa kutosimama na wafanyabiashara hasa kwa kauli yake ya Bungeni kuwa hakukuwa na mgomo Kariakoo. Wafanyabiashara hao wamesema kuwa haijawahi kutokea hata mara moja Waziri huyo akasimama na wafanyabiashara.

Urasimu mkubwa wa mizigo inayotoka Zanzibar umetajwa kuwepo tofauti na wafanyabiashara wanaotoa mizigo nchi zingine kama Dubai n.k. Pia, kumekuwepo na watu wengine wanaotoza kodi baada ya kutoa mzigo bandarini, watu hao wanapaswa kuwepo bandarini ili kurahisisha uliopaji wa kodi na kuokoa muda.

Mfanyabiashara mwingine amesema TRA wamepewa mamlaka ya kuomba rushwa kisheria, kwa kuwa wanalindwa na Sheria mbovu, wanataka rushwa kwa nguvu. "Rushwa ni mfumo, na sheria inawalinda. Wanatumia loophole ya elimu ndogo ya wafanyabiashara kudai rushwa....."

Mfanyabiashara wa vitenge (Mama Bonge) ametoa dukuduku lake la kudaiwa kodi zaidi ya bilioni 30, kisha baadae kutakiwa kulipia bilioni 10.3 ambazo hajalipa hadi leo.

Baada ya kushindwa kulipa alitakiwa kupelekwa mahakamani kwa kesi ya uhujumu uchumi kisha kutakiwa walau moja ya tatu ya gharama zote (3.4 bilioni) wakati hajafanya kazi kwa zaidi ya miezi 8 na kontena zake 10 za vitenge zimekamatwa na TRA Ubungo.

===

UPDATE:
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Anazungumza

Amesema Serikali ya Samia Suluhu Hassan inayo dhamira ya dhati ya kuwasaidia wafanyabiashara wa Nchii kwa kuwasikiliza na kutatua matatizo yao.

Waziri Majaliwa amesema kikao hiki sio cha mwisho, bali vikao zaidi vitaendelea kufanyika ili kutatua kero na kuinua Sekta hii muhimu kwa uchumi wa Nchi.

Hoja zote zimechukuliwa na Serikali na zinaendelea kufanyiwa kazi kwa mfumo Shirikishi baina ya Serikali na wafanyabiashara wenyewe ikiwemo kuunda tume ya pamoja kati ya Serikali na wafanyabiashara. Timu hiyo itakuwa na watu 14, itapaswa kupitia na kuchukua yote yanayotekelezeka ili yafanyiwe kazi haraka, yanayohusu sheria yatapaswa kushughulikiwa bungeni haraka.

Amewataka Polisi kulinda usalama wa Raia na sio kujihusisha na kazi za TRA na task force hiyo imeondolewa.

Hiyo ni kero au siasa? Hapa Chadema wamechomeka watu wao Kwa mlango wa kero za biashara..

Mtu anasema eti kama Wabunge hawaheshimu itakuwa sie watu wa kawaida?
Mwigulu na watu wa TRA kukiuka taratibu inahusikaje?
 
Aaaaah....Kumbe ndivyo Auntie?
Basi nikajua ndiyo huyo wa kwa Millard...
Halafu huyo wa Vitenge Kariakoo ni maarufu sana..
Sanaaaa kuna kipindi mwaka jana nahisi alikamatwa na kupewa kesi ya kuhujumu uchumi
 
Ismal Masoud Tanga: Walioiba fedha za Umma wasomewe Albadir!!!!!
 
Umeshaagiza mzigo kupitia mtu wa tatu ukafanya hiyo prorata?
Mkuu embu tuachane na hili hatutaelewana sababu unasema jambo ambalo ni nadharia maana moja ya tatizo la mfumo ambalo hata W/mkuu kalikubali leo ni hili.

Tukubali kutokukubaliana kuwa ukiwa na mzigo bila risiti wewe ni mhujumu uchumi kama unavyosema.
kwani hapa tunaongelea tatizo au tunaongelea way forward zitakazo tatua tatizo la waagizaji wa mizigo kwa less than container?
 
kwani hapa tunaongelea tatizo au tunaongelea way forward zitakazo tatua tatizo la waagizaji wa mizigo kwa less than container?
Sio ww uliyesema kuwa ukiwa na mzigo bila risiti ni mkwepa kodi? Kama ndiye na unajua kuwa inawezekana kuwa na mzigo bila risiti sababu ya mfumo basi hukupaswa kusema hivyo.

Anyways kama ni way foward unaongelea upo sawa. Inawezekana kabisa kutatua hilo na litatatulika. Kuna kamati imeundwa naamini watalitazama.
 
Mmoja kaomba namba ya waziri mkuu...
Kwa mara ya kwanza leo ndo nimejua
Muongeaji anasema au wakadange ?sasa hawa ndo waongeaji wao??
Unafanya kazi TRA.


HIVI TUKIWAPIMA MAENDELEO MLIYONAYO NA MISHAHARA YENU VINALINGANA??

KUWENI NA HURUMA, BIHASHARA NI NGUMU.

JUST IMAGINE MTU ANASHINDIA UKOKO DUKANI THEN UNAKUJA KUMWOMBA RUSHWA YA MILIONI 4 KISA KASAHAU, AU KAACHA MAKSUDI KUTOA RISITI YA AFU TATU??

ANYWAY MTAKUFA VIBAYA NYIE
 
Mwigulu ni arrogant sana.Vile alianzisha betting company,alifuta kodi kwenye betting company. Mwigulu hafai kuwa waziri.
Tuache
 

Attachments

  • IMG-20230517-WA0002.jpg
    IMG-20230517-WA0002.jpg
    49.5 KB · Views: 1
Back
Top Bottom