DOKEZO Mfanyabiashara maarufu Arusha aibiwa Tsh. Milioni 100 kwenye akaunti ya Benki ya NMB

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Benki ya posta wametembea na shekeli za faza yangu, Mungu anawaona
 
Alikuwa anapita mule-mule !!! Sema yeye alikuwa anapiga parefu !!!
Hushpuppi $4,000 angeona unamsumbua tu, hata hela ya kununua Champagne inakuwa haijafika bado.

Ila Wamarekani nuksi, walikuwa wanajua birthday yake real, kwa sababu alishawahi kuomba visa ya US wakamkatalia, lakini data zake walikuwa nazo.

Sasa, wakawa wanamshuku kuwa huyu anayepiga watu mitandaoni ndiye Hushpuppi, wakawa na ushahidi kibao, ila hawana uhakika.

Uhakika waliupata walivyomuona mitandaoni anasherehekea birthday yake siku ile ile aliyoiandika kama birthday yake kwenye kuomba visa ya US.

Wakamdaka. Ujanja wake wote Hushpuppi kaenda ku boogie kwenye kujionesha mitandaoni tu.

Angekuwa mtu wa kimyakimya huenda angewapiga sana tu.

Lakini sasa yeye labda point yake yote ya kuwapiga ni ili ajioneshe awatese watu wamuone ana hela.

In which case kupiga hela kubwa halafu kuishi maisha ya kujificha ingekuwa kama hakuna maana hivi.
 
Ujanja wake wote Hushpuppi kaenda ku boogie kwenye kujionesha mitandaoni tu..... (This was his GRAVE MISTAKE !!!)
 
Ujanja wake wote Hushpuppi kaenda ku boogie kwenye kujionesha mitandaoni tu..... (This was his GRAVE MISTAKE !!!)
Sasa yeye point yake kubwa ya kutaka kupiga ni ili aje kuwatambia nyie, kupiga bila kutamba mitandaoni aliona kama haina maana.

Mafiosi wanasema kuwa kupiga hela kubwa si kazi kubwa, kazi kubwa ni kuishi maisha ya kawaida baada ya kupiga hela kubwa.

Yani kuna vishawishi vingi sana vya kutaka ujioneshe kuwa na wewe unazo watu wakuheshimu, sasa ukijionesha tu, wazee wanakudaka hapohapo.
 
Hao air money ni majizi mpaka ya mabando unanunua mb 245 unashangaa unatumia mb 50 itakuwa hela
 
Walitakiwa waonyeshe mtririko wa hiyo acc yake bila hivyo hao ni wezi,ngewafungulia kesi
 
Utauliza wewe umepata wapi hii taarifa
 
Ni kweli ndugu yangu Dola 4000 wanaona ndogo
 
Huyu ombeni ni huyu mkazi wa kiboriloni juu ya kanisa au siyo yeye mkuu
 

Hahahaha Sasa ulicheka nn mkuu? Ukute ndugu yako alichukua salary advance kabisaaa na akafa bank hawajarudisha chao [emoji23][emoji23]
 
Unakuta Samuel alienda likizo ndio bomb likalipuka
Msiwe na tabia ya kutaka uhudumiwe na mtu mmoja tuu bank lazima akulize
Unakuta kila ukienda anakupokea na kukupa huduma
Balance anakupa yeye hiyo ni rahisi ktembea na carry-on ya Ile amount aliotia kwa acc yako
Mfano acc alivyokupa balance ya mwisho ilikuwa 10m akatoa 3m za matumizi yake
Ukija atakupa balance ya ten M plus zozote utakazokuwa umeongeza baada ya balance ya mwisho.
Utadanuka siku ambayo unaenda kukuta mwingine
 
Barclays pia kuna mwana aliikula milioni 300 alikuwa ameimaliza yote kwenye Bata alipokamatwa alikuwa hana hata hela ya mawakili.Tulimsaidia tulikuwa hatujui mwenzetu hela anapata wapi. Yaani tulishangaa hela yote huo hana hata kiwanja hata shamba.
 
Barclays pia kuna mwana aliikula milioni 300 alikuwa ameimaliza yote kwenye Bata alipokamatwa alikuwa hana hata hela ya mawakili.Tulimsaidia tulikuwa hatujui mwenzetu hela anapata wapi. Yaani tulishangaa hela yote huo hana hata kiwanja hata shamba.
Hahahaha balaa sana. Yaan ulimbukeni qa kupata pesa nyingi kwa ghafla lazima upagawr
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…