Mgawo mkali wa umeme na maji unaoendelea nchini ni wazi kabisa watendaji wa Serikali mnaihujumu Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan

Mgawo mkali wa umeme na maji unaoendelea nchini ni wazi kabisa watendaji wa Serikali mnaihujumu Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan

Ukiona mawaziri husika hawatumbuliwi basi ujue kuwa hakuna hujuma zozote.

Isipokuwa Kuna matatizo ambayo mawaziri wa wizara na Mh. RAIS wanayajua na hivyo hakuna mtu anayeweza kutatua tatizo lililo nje ya human resources( Mfano: ukame).
 
Nchi toka 1961 bado viongozi w serikali wanatoa tamko MVUA hamna.... wamekaa nao wanasubiri mvua.. swali la ziada ni mbona haya makali kuna kipindi hayakuwapo?? Licha ya hali ya mvua kuwa 'duni'?
 
Hiki kinachoendelea kimyakimya ni mchakato wa kuturudisha kuleee miaka ilee ya 2005, 2006, 2007...... miaka ambayo Dar Es Salaam na Tanzania kwa ujumla ilikua imepambwa na mikokoteni ilishosheheni madumu ya korie yaliyobeba maji na magari yenye matank ya maji kila kona.

Kwa kasi ya ajabu tunarudi miaka Ile ambayo mazingira yalikua yamepambwa kwa sauti za majenereta usiku na mchana

Au ndio ule mkakati wa kuutaka urais umeanza!? Acheni mambo yenu buana. Mama Samia yupo sana bado, ndio kwanza kumekucha

Hali ni mbaya sana na hatari kwa afya kwa jiji lenye wakazi wengi zaidi nchini, Dar Es Salaam. Watu tumepona kwenye corona lakini sasa mnataka kutulazimisha tufe kwa kipindupindu

Watendaji mnaohusika kwenye haya maeneo fanyeni kile kilichokua kinafanyika miaka mitano iliyopita hadi tukasahau kabisa kero ya umeme na maji. Kupewa nafasi ya kuhudumia wananchi kwa huduma muhimu kama umeme na maji halafu hao wananchi wakakosa hizo huduma ni wazi kabisa kwamba kufanya imeshindikana. Bora kuiacha office kuliko kukaa kwenye office halafu huduma asipatikane

Tanesco na idara za maji sisi wananchi tunamuamini rais wetu na yeye amewaamini nyie. Mnapopewa dhamana ya kutuhudumia halafu mnaamua kutuhujumu tutapaza sauti kwamba kazi imewashinda. Heri kuteua na kutumbua kuliko wananchi kuteseka kwa kukosa huduma za msingi tena ambazo wanazichangia kwa kodi zao wenyewe

Mungu ibariki Tanzania
Mungu mbariki Rais wetu Samia Suluhu Hasan
Kazi iendelee

Cc Wizara ya Afya Tanzania


Asante TANESCO kwa majibu mazuri ya mipango ya kupambana na shida ya umeme ya muda mfupi na muda mrefu.
Sisi wananchi tunafarijika sana mnaposikia sauti zetu na kutujibu kama hivi
Ila sasa mjitahidi kwenda na hiyo mipango kwa wakati ili mwakani muda kama huu kukawa na tatizo hilihili na majibu yakawa hayahaya

Plan nzuri bila utekelezaji makini na kwa wakati inakua mbaya zaidi kwa wananchi waliokua na subra, Rais amewaamini abajua nyie ni wataalamu mnaoweza kumsaidia kuwahudumia watu wake. Basi msiipoteze imani ya watanzania kwa serikali yao

Tanesco Kazi iendelee 👍
Wanaihujimu vipi? Wao ndio wameleta Ukame?
 
Acheni USANII nyie wababaishaji tu hamna lolote.

Taasisi zote ziko chini ya Rais na serikali yake! Kama kweli anahujumiwa kwanini asiwawajibishe hao wahujumu?

Urongo mtupu! Mwambieni ukweli huyo mama kwamba hajiwezi, acheni kulaghai watu eti anahujumiwa!

Anajihujumu mwenyewe na udhaifu wake!
Nashangaa mtu anaesema anahujumiwa wakati taasisi zote zipo chini ya rais.

How insane.
 
Tuchepushe maji ya ziwa victoria yaende kwenye mabwawa ya umeme watu wapate umeme muda wote na mto Ruvu watu wapate maji muda wote!
 
Huu ukame na kupungua kwa kina cha maji ungekua umeanza mwaka huu wangeleweka kidogo japo bado wangelaumiwa kwa kuwa na mipango isiyoangalia dharura
Suala hili ni la kidunia,, kikubwa ni kuwa na chanzo mbadala cha nishati, mfano gesi ambayo tunayo ya kutosha, trilions zilizoenda nyerere hydroelectric power project, zingeenda kwenye mradi wa gesi , tatizo la nishati lingepungua sana
 
Huu ukame na kupungua kwa kina cha maji ungekua umeanza mwaka huu wangeleweka kidogo japo bado wangelaumiwa kwa kuwa na mipango isiyoangalia dharura
Mipango ipo na ndio maana Rais Samia anajenga mabwawa na kidunda nk..

Mwendazake ndio wa kulaumiwa hakuna kitu alifanya kwenye sekta ya Maji.
 
Mipango ipo na ndio maana Rais Samia anajenga mabwawa na kidunda nk..

Mwendazake ndio wa kulaumiwa hakuna kitu alifanya kwenye sekta ya Maji.
Mwendazake ndio kakausha maji mto ruvu?

Semeni ukweli kuongoza nchi kama Tanzania kila anayepewa cheo anataka kuwa mpigaji bila kiongozi wa juu kuwa madhubuti msahau maendeleo.

Watanzania tumezoea kusukumwa ndio mambo yaende bila hivyo business as usual.
 
Nakumbuka ya huko ughaibuni...mama mtu kashika usukani kwa siku 45! Akajipima akaona hatoshi na hivyo akachukua hatua ya kiungwana, akajiwajibisha na kuachia huo usukani.

Hapa kwetu ni kung'ang'ania tu, hajiuzulu mtu hapa. Kuna nyakati hata inabidi Mungu kuingilia kati. Lakini hapa akina mama D ndio huingilia kati...utawasikia mara oh, anahujumiwa! Ebo!
 
Kwa ugumu huu wa maisha nakuelewa sana, kwa sisi tunaotegemea kutumia umeme ndio tuweze kupata kipato cha kuendesha maisha yetu tunaelewa nini kinatupata tunaposhindwa kuingiza siku ati sababu hamna umeme

Nadhani hawawezi kukuacha uvae chup kichwani mkuu
Sisi tunaotengeneza ice cream na kuzigandisha mambo hayaendi [emoji1]

Ova
 
Back
Top Bottom