Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Hii ni kkoo sio biashara yako ya kitumbua
Kitendo cha kkoo kugoma hta masaa mawili serikali yako ya ccm inapishana na kodi sio chini 1b
Hajui kodi inayo kusanywa hapo kkoo pekeyake, kuna wilaya nzima haifiki makusanyo yake yote ya kodii yanokusanywa kkoo

Sent from my Q2 using JamiiForums mobile app
 
ChoiceVariable mambo ya dokta wa uchumi haya au siyo?

Taratibu nchi inaelekea shimoni
Kodi lazima mlipe mnatabia ya kuficha Mali kwenye stoo harafu mnapeleka kiduchu dukani Ili mkadiriwe Kodi..

Mkigoma tunawafutia leseni na wote waliogoma hayo maduka tunayafunga marufuku kufungua.

Very simple hii mbona.Tanzania ni kubwa hapo Kariakoo ni sehemu.ndogo sana mapato yake kwa.mwka hayafiki hata Bil.500
 
Kwanini unasema kulipa kodi ni kuviziana, unaviziwa nini? Kama unalipa kodi sawasawa wanakuvizia kitu gani. Unataka wasije kukagua kwako unaficha nini?

Kwahiyo na wauza madawa muhimu wasiwe wanakaguliwa kwa sababu wanaviziwa. Wazalishaji viwandani wasiwe wanakaguliwa ubora kisa washapewa leseni hivyo wasiviziwe. Mahospitali binafsi yasiwe yanafanyiwa ukaguzi, watu wauziwe madawa yasiyo na ubora na madaktari wasio na vigezo kisa hospitali zisiviziwe.

Sheria ya kodi inasema kodi ikusanywe kila mnyororo wa thamani unapoongezeka. Na wewe unanunua kitu kwa 800, unakiuza kwa 1500 tiyari kuna thamani imeongezeka wanakuja kuchukua % kadhaa. Wakikusanya kodi kupitia mpakani na bandarini pekee Hyatt Regency, The Kilimanjaro italipaje kodi? Maana hainunui nyanya na kabeji nje, haipitishi nyama bandarini wala mpakani?

Nchi zenye mifumo mizuri ya kodi huwa zinavizia vizuri sana na ole wako ukutwe umekwepa kodi, jera nje nje.
Umejichanganya kweli ngoja nijibu hoja zako, kama una TRA imara mzigo hautoki ila uwe umelipiwa kila kitu mbona mafuta wameweza? wanachukuwa mpaka VAT huko huko nenda kituo chochote cha mafuta utapata risiti lakini hukuti makato sababu wameshachukuwa. Mungizaji mali anatakiwa kulipa kila kitu mpaka VAT halafu akifanya mauzo yeye ana deal na TRA anaweza ku claim tax refund akiwa na vielelezo kilichoingia ingia kinalingana na alichouza. Hivi hujawahi kwenda nje ukanunua hata simu tu hapo Dubai unalipa VAT ila kama sio mkazi ukifika airport una claim VAT na ukionesha risiti unalipwa sababu mfumo umewekwa wa haki. Unaongelea nyanya hivi toka lini TRA wakakusanya kodi za nyanya hizo ni kodi zinalipwa sokoni na manispaa ndio wanakusanya kodi hizo. ukija mfano mdogo mafuta yakitoka bandarini yanakuwa yameshalipiwa kila kitu lakini mafuta hayo yanapita mikononi kwa wengi kabla kumfikia mlaji ila hukuti kodi tena inaongezeka kuna wale wanachukuwa mzigo jumla wanaweka kwenye tank zao na wao wanauza kwa wenye vituo na bei hizi zinatofautiana sehemu na sehemu lakini makato same na yameshakatwa. Kuvizia ni ujinga ndio sababu container linatoka bandarini halafu linaanza kufukuzwa mitaani kama TRA hawaaminiki kule bandarini badilisha mfumo kuondoa mianya ya udanganyifu ukiondoa urasimu unapunguza mianya ya rushwa. Kariakoo nzima hawawezi kuwa waizi ukiona kijiji kinalalamika ujue kuna shida.
 
Kodi lazima mlipe mnatabia ya kuficha Mali kwenye stoo harafu mnapeleka kiduchu dukani Ili mkadiriwe Kodi..

Mkigoma tunawafutia leseni na wote waliogoma hayo maduka tunayafunga marufuku kufungua.

Very simple hii mbona.Tanzania ni kubwa hapo Kariakoo ni sehemu.ndogo sana mapato yake kwa.mwka hayafiki hata Bil.500
Kwa kuwa mna maduka yenu siyo?

Kama kidume kweli jaribu kufanya huo utopolo.

TRA inanuka rushwa halafu mnawanyanyasa walipakodi. Kwani tumesahau tozo ya kipuuzi ilivyotuumiza wananchi?


Try it and you will test your own borth
 
Sijawahi na pengine sitakuja kuwahi kuelewa hizi kodi zinavyokatwa
Mzigo ukifika bandarini unatokutana na tra
Mzigo huohuo ukifika dukani unakutana tena na tra

Sasa najiulizaga yule tra wa bandarini ni tofauti na huyu wa dukani????
Na km wote ni TRA, hizi kodi za mara mbilimbili zinalenga nini????
Ni mifumo ya kiunyonyaji tu,, Hiyo ni double taxations. Mfano mwingine ni huu Mimi nikienda dukani kariakoo kuchukua mzigo na Kisha kupewa risiti yangu huwa Kuna Kodi nailipia..lkn mzigo huohuo nikileta dukani kwangu kuuza nakutana na TRA Tena ...kwhy ni mwendo wa kukamuana tu
 
Muilize Dr. Ulimboka awamu ya nne alifanywa nini alipokuwa kiongozi wa mgomo wa madaktari.
Unapokuwa unapigania haki au kupambana na majitu madhalimu hautakiwi kuwazia vitisho vyao wakiteka wa kwenu wakamtesa na nyie mnateka wa kwao mnamtesa na kuwapa taarifa wajue kuwa mnalipiza.
 
Kwa kuwa mna maduka yenu siyo?

Kama kidume kweli jaribu kufanya huo utopolo.

TRA inanuka rushwa halafu mnawanyanyasa walipakodi. Kwani tumesahau tozo ya kipuuzi ilivyotuumiza wananchi?


Try it and you will test your own broth
Maduka yetu wapi? Endeleeni Kigoma.uone kama hatujafuta leseni na mnaanza upya na funawasaka..

Kama TRA inanuka Rushwa na nyie mnakutana na hao waomba Rushwa na sio Waziri Kwa nini hamuwaripoti Kwa mamlaka husika?

Hakuna kuleana Kwa washenzi kama.nyie,watu wenyewe hata sio manufacturer Bali wachuuzi tuu.

Mnaficha bidhaa stoo kukwepa Kodi harafu mnasemaje?
 
Ni kweli zina shida, ila hazijatungwa na TRA. Yani matatizo yetu makubwa ni kuongozwa na vilaza na watu wasioelewa, tatizo mara nyingi sio watekelezaji. Wafanyabishara watatumia TRA kukataa matakwa ya serikali ila serikali ndio ina shida wala sio TRA ambao ni mtekelezaji.

Serikali ikitaka kuwakataa na kuwaonyesha wanadai mambo yasiyowezekana itatafuta makosa kwenye madai yao. Waandae muswada mzuri wagome wakiwa na kauli nzito, sasa hivi ukiwatafuta utakuta kila mmoja anaongea la kwake sasa mgomo gani unafanikiwa hivyo
Shida ni kutafuta mchawi , watanzania ndio tunakwama hapo ndio sababu hatuwezi kutatua matatizo yetu.
Malalamiko yooote hapo ni kwa Tra, lakini kama kulikuwa na mtu wa kwanza kuwa tagged na hizi lawama alitakiwa kuwa ni mbunge ambaye anaidhinisha hizi sheria .
Anatajwa aingilie Rais ambaye hata hakuwepo bungeni hii miswada ikijadiliwa .
 
Hamuwezi kugoma wiki nyie[emoji1787][emoji1787]kesho njaa na marejesho yatawarudisha kufungua hizo frem zenu[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kwan wamesema hawauzi. Ndugu ungejua huu mgomo una faida mara mbili kwa wafanyabiashara usingesema hapa. Sasa usianze kunichimba nikupe Siri za ndani ndani boss. Am sorry.
 
Sheria za ongezeko la kodi kutokana na mnyororo wa thamani , tumekurupuka , hizi ni system za kibepari hazifanyi kazi vizuri kwenye nchi zaa kijamaa .leo hii vat kwa kuepuka ugomvi na mamlaka wafanyabiashara wameziweka kama gharama ya biashara , maana ili ulipwe vat ni lazima ufanye biashara na kiwanda.
Tanzania sio nchi ya kijamaa, ni ya kibepari zaidi
 
Back
Top Bottom