Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Kwanini unasema kulipa kodi ni kuviziana, unaviziwa nini? Kama unalipa kodi sawasawa wanakuvizia kitu gani. Unataka wasije kukagua kwako unaficha nini?

Kwahiyo na wauza madawa muhimu wasiwe wanakaguliwa kwa sababu wanaviziwa. Wazalishaji viwandani wasiwe wanakaguliwa ubora kisa washapewa leseni hivyo wasiviziwe. Mahospitali binafsi yasiwe yanafanyiwa ukaguzi, watu wauziwe madawa yasiyo na ubora na madaktari wasio na vigezo kisa hospitali zisiviziwe.

Sheria ya kodi inasema kodi ikusanywe kila mnyororo wa thamani unapoongezeka. Na wewe unanunua kitu kwa 800, unakiuza kwa 1500 tiyari kuna thamani imeongezeka wanakuja kuchukua % kadhaa. Wakikusanya kodi kupitia mpakani na bandarini pekee Hyatt Regency, The Kilimanjaro italipaje kodi? Maana hainunui nyanya na kabeji nje, haipitishi nyama bandarini wala mpakani?

Nchi zenye mifumo mizuri ya kodi huwa zinavizia vizuri sana na ole wako ukutwe umekwepa kodi, jera nje nje.
Sheria za ongezeko la kodi kutokana na mnyororo wa thamani , tumekurupuka , hizi ni system za kibepari hazifanyi kazi vizuri kwenye nchi zaa kijamaa .leo hii vat kwa kuepuka ugomvi na mamlaka wafanyabiashara wameziweka kama gharama ya biashara , maana ili ulipwe vat ni lazima ufanye biashara na kiwanda.
 
Punguza makasiriko
Kodi inayokadiriea na TRA ni kuwakomoa wafanyabiashara bila kujali sisi walaji.

Naunga mkono mgomo

Najua sasa wanasakwa viongozi wa mgomo kwa udi na uvumba ili wahasiwe kama walivyomfanyia unyama Ulimboka
Sina makasiriko, mgomo hauandaliwi na mawazo ya kijinga yanayopingwa kirahisi. Weka mawazo yaliyonyooka na sababu zisizo na shaka ili mamlaka ibanwe kutoa suluhisho. Sio sababu uchwara za kudai kodi ikatwe bandarini na mipakani, TRA wasiviziwe. Kwa sababu hizi hamna popote mgomo unafika.

Sababu za kugoma zipo nyingi sana na kuumiza kichwa serikali, ila wanaogoma hawana kauli nzito za kusimamisha.
 
Hivi kweli hatuwezi kuja na mfumo mmoja tu TRA pale bandarini kuchukuwa kodi mara moja ili mzigo ukitoka basi watu wasisumbuane? mbona kwenye mafuta wameweza mzigo kwenye meli unakatwa kila kitu basi unaingia sokoni. Kuna nini hii kila siku kukimbizana wakati Tech imekuwa sana kuna njia za kuchukuwa mapato kwa njia ya kisasa tu badala ya haya mambo ya double taxation watu hakuna kuaminiana kwanini lakini? kodi kulipa ni haki basi tuweke mfumo utakaonekana ni wa haki.
Nani kakuambia petrol station hazilipi kodi za ndani?
 
Sijawahi na pengine sitakuja kuwahi kuelewa hizi kodi zinavyokatwa
Mzigo ukifika bandarini unatokutana na tra
Mzigo huohuo ukifika dukani unakutana tena na tra

Sasa najiulizaga yule tra wa bandarini ni tofauti na huyu wa dukani????
Na km wote ni TRA, hizi kodi za mara mbilimbili zinalenga nini????
Kodi za bandarini na dukani ni tofauti
 
Hivi kweli hatuwezi kuja na mfumo mmoja tu TRA pale bandarini kuchukuwa kodi mara moja ili mzigo ukitoka basi watu wasisumbuane? mbona kwenye mafuta wameweza mzigo kwenye meli unakatwa kila kitu basi unaingia sokoni. Kuna nini hii kila siku kukimbizana wakati Tech imekuwa sana kuna njia za kuchukuwa mapato kwa njia ya kisasa tu badala ya haya mambo ya double taxation watu hakuna kuaminiana kwanini lakini? kodi kulipa ni haki basi tuweke mfumo utakaonekana ni wa haki.
Acha uongo. Kodi za mafuta ziko nyingi na hazitozwi bandarini tu. Kodi za mapato, ushurunwa halamashauri, PAYE, SDL n.k. vinatozwa nje ya bandari.
 
Sina makasiriko, mgomo hauandaliwi na mawazo ya kijinga yanayopingwa kirahisi. Weka mawazo yaliyonyooka na sababu zisizo na shaka ili mamlaka ibanwe kutoa suluhisho. Sio sababu uchwara za kudai kodi ikatwe bandarini na mipakani, TRA wasiviziwe. Kwa sababu hizi hamna popote mgomo unafika.

Sababu za kugoma zipo nyingi sana na kuumiza kichwa serikali, ila wanaogoma hawana kauli nzito za kusimamisha.
Sasa ndo wamegoma na hauna la kuwafanya.

Tuma askari wakawatwange hadi wafungue maduka
 
Punguza makasiriko
Kodi inayokadiriea na TRA ni kuwakomoa wafanyabiashara bila kujali sisi walaji.

Naunga mkono mgomo

Najua sasa wanasakwa viongozi wa mgomo kwa udi na uvumba ili wahasiwe kama walivyomfanyia unyama Ulimboka
Mkuu labda twende sawa , Tra ni watch dog tu , watunga sera (wabunge )ndio wenye shida , na tupo kwenye migogoro hii kutokana na sheria mbovu zilizotungwa na bunge letu tukufu.
Mapendekezo ya Tra kwenda bungeni kwa wakati fulani yanakuwa makali kutokana na usumbufu wanaoupata wakiwa kazini, ila bunge lingekuwa imara kuna baadhi ya vitu havikutakiwa kabisa kuwa sheria kama vingejadiliwa kiufasaha.
 
"Bandarini ni mpakani..." nani kakwambia hivyo? Wewe ukiona bandari pale Dar es Salaam, Mtwara na Tanga unaona ile ni mipaka. Ukitoka bandarini kuna exclusive economic zone ya Tanzania ina mamia ya kilomita majini, kule ndio kuna mpaka na international waters.

Alafu mpaka ni lazima upakane na nchi, pale Dar es Salaam bandari inapakana na nchi gani. Taratibu za kimamlaka hazibadilishi maana, mkoa wa ki-TANESCO haulifanyi eneo kuwa mkoa wa kiutawala wa TAMISEMI.

Hapo Kariakoo muuza furniture inavyotengeneza nchini atalipaje kodi kama mnataka walipishwe wanaotumia bandari na borders pekee?
This is a challenge kwenu, nishaona nchi wana mfumo mzuri sana wa kodi na unakata kodi ndani
Bure kabisa wewe. Kwa hiyo meli ikiwa baharin ikiingia tu kwenye maji ya TANZANIA ya tanzania kwenyebahari ya hindi TRA wanapanda kwenye meli kuanza kutoza kodi
 
Waache wakae na hela zao. Watu walipe kodi ili mabwanyenye na ma'mwinyi wakazitapanye na kuzila kwa kununua Mashangingi mapya ya 2023 na kujiongeza mishahara na marupurupu.

Wacha raia watumie hela zao wenyewe. Kodi kodi kodi .... Mxiem [emoji19] kodi ya nyoko.
Wanaohimiza kulipa kodi,,wao hawalipi kodi sasa si usenge huu!!!
 
Sheria za ongezeko la kodi kutokana na mnyororo wa thamani , tumekurupuka , hizi ni system za kibepari hazifanyi kazi vizuri kwenye nchi zaa kijamaa .leo hii vat kwa kuepuka ugomvi na mamlaka wafanyabiashara wameziweka kama gharama ya biashara , maana ili ulipwe vat ni lazima ufanye biashara na kiwanda.
Ni kweli zina shida, ila hazijatungwa na TRA. Yani matatizo yetu makubwa ni kuongozwa na vilaza na watu wasioelewa, tatizo mara nyingi sio watekelezaji. Wafanyabishara watatumia TRA kukataa matakwa ya serikali ila serikali ndio ina shida wala sio TRA ambao ni mtekelezaji.

Serikali ikitaka kuwakataa na kuwaonyesha wanadai mambo yasiyowezekana itatafuta makosa kwenye madai yao. Waandae muswada mzuri wagome wakiwa na kauli nzito, sasa hivi ukiwatafuta utakuta kila mmoja anaongea la kwake sasa mgomo gani unafanikiwa hivyo
 
Mamlaka ya TRA haina uzi humu tuitag ione malalamiko ya wananchi? au ikiwezekana tukatoe malalamiko kwenye uzi wao.
Tuanze na bungeni , ndio kunakozaliwa matatizo yote haya. Siasa mbovu huzalisha sheria mbovu
Sheria ya uhujumu uchumi kwa mfano imetumika vibaya sana awamu ya tano ,kuadhibu wanasiasa na walioupinga utawala ule na hata hii leo Tra wakitaka kukukomoa wanakupa kesi ya uhujumu uchumi,
 
Back
Top Bottom