Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Sawa kabisa, nawaunga mkono waliogoma kwa 100%

TRA kumejaa ufisadi na uonevu kwa wafanyabiashara wa Kariakoo.


Nashauri Kariakoo iwe free trade zone, yenye flat rate ya ushuru na unaolipwa mara moja tu, ili kama nchi tunufaike na soko la nchi zinazotuzunguka.
Ebu project hiyo flat rate iwe bei gani kwa mfano???
Kodi inalipwa kwenye faida.....wanatengeneza faida zisizolingana unataka utoe flat rate?

Kkoo Kuna watu wanatoa makadirio mil 100 kwa mwaka? Je hiyo rate ndio itumike?
 
Mzigo mmoja kukata Kodi Mara mbili ni double taxations tu ndio maana mfanyabiashara mchuuzi ni ngumu kutoboa lkn pia ndio maana wafanyabiashara wakubwa wanakwepa Kodi.
Haukatwi mzigo mara mbili!
Wanakatwa wamiliki wa hiyo biashara mara Moja Moja
Kama mzigo umepita mikono wamiliki wanne utakatwa mara nne Kwan umeuzwa mara nne na Kila stage umetengeneza faida
 
Bidhaa nyingi za dar es salaam zinategemea bandari kwa 90%
Najuwa hilo nilijibu tu kwa hoja ya mtu kusema kuna mipaka lakini shida kubwa hapa watu wa TRA wanajuwa kuwa kukiwa na mfumo usioingilika utaziba mianya ya rushwa watakufa njaa wanataka tubaki na hii analog mtu aweze tu kuamua kuna nini ndani ya container na gharama waamue nadhani kuna wakala wa kufanya clearance hawa wanatakiwa kuonesha 100% kuna nini na gharama zake ni zipi na viwango vya kodi viko kisheria ukiweka number kodi ni hii sasa kuwe na hali kuweka kiwango kuambatane na doc ku support gharama japo najuwa kuna ujanja mwingi mzigo wa mil 1 wanaweza kuweka laki moja hapa ndio tunatakiwa tutafute tech kuziba hii mianya kama shida kodi ni kubwa hilo na la kisera na serikali ina wajibu kuangalia. Mbona magari hakuna shida hizi, unaleta gari unaingiza model inakupa kodi hii wala huwezi kuchezea ndio maana ukija huku mitaani kwa wauza magari bei zinafanana sana.
 
Una Ungumzia mafuta ya wapi? Au yale ya vichupa? Mafuta nenda sheli uone lisiti zinazo mwagika alafu usome kodi yako kwa mafuta uliyopimiwa

Nunua muda wa maongozi upate kuletewa kodi uliyolipa

Kodi Kila mtu ana takiwa kulipa kwa namna yoyote inayofaa na sio kuikwepa
Hivi kweli hatuwezi kuja na mfumo mmoja tu TRA pale bandarini kuchukuwa kodi mara moja ili mzigo ukitoka basi watu wasisumbuane? mbona kwenye mafuta wameweza mzigo kwenye meli unakatwa kila kitu basi unaingia sokoni. Kuna nini hii kila siku kukimbizana wakati Tech imekuwa sana kuna njia za kuchukuwa mapato kwa njia ya kisasa tu badala ya haya mambo ya double taxation watu hakuna kuaminiana kwanini lakini? kodi kulipa ni haki basi tuweke mfumo utakaonekana ni wa haki.
 
Ebu project hiyo flat rate iwe bei gani kwa mfano???
Kodi inalipwa kwenye faida.....wanatengeneza faida zisizolingana unataka utoe flat rate?

Kkoo Kuna watu wanatoa makadirio mil 100 kwa mwaka? Je hiyo rate ndio itumike?
Flat rate ya 10% itasaidia kuwa na mzunguko mkubwa sana wa pesa.
 
Sijawahi na pengine sitakuja kuwahi kuelewa hizi kodi zinavyokatwa
Mzigo ukifika bandarini unatokutana na tra
Mzigo huohuo ukifika dukani unakutana tena na tra

Sasa najiulizaga yule tra wa bandarini ni tofauti na huyu wa dukani????
Na km wote ni TRA, hizi kodi za mara mbilimbili zinalenga nini????
Yule ni tofauti...! Nazani yawezekana majukumu pia nitofauti

Costume officer (wa forodha- bandari, airport na mipakani)

Tax Officer (hawa ndio tunao ishi nao humu ndani katika majukumu yetu ya kila siku)
 
Hivi kweli hatuwezi kuja na mfumo mmoja tu TRA pale bandarini kuchukuwa kodi mara moja ili mzigo ukitoka basi watu wasisumbuane? mbona kwenye mafuta wameweza mzigo kwenye meli unakatwa kila kitu basi unaingia sokoni. Kuna nini hii kila siku kukimbizana wakati Tech imekuwa sana kuna njia za kuchukuwa mapato kwa njia ya kisasa tu badala ya haya mambo ya double taxation watu hakuna kuaminiana kwanini lakini? kodi kulipa ni haki basi tuweke mfumo utakaonekana ni wa haki.
Wakiweka mfumo wa kodi haki na uwazi hao wezi wa TRA wanaolazimisha rushwa wakatajirikie wapi?
 
Kuna mtu humu jf aliwahi kusema kuna wafanyabiashara wanaopitisha mizigo kutoka stoo na kuwauzia wamachinga bila kupitia dukani kwahiyo serikali imeona kuna pesa inapotea hapo.
Hizo pesa wanazokusanya kwa nguvu hivyo mbona matumizi yake huwa ni ya kifisadi sana? Yani mtu apewe jukumu adokoe hela mchana kweupe na asiguswe. Kutii mamlaka katika mazingira haya ni ngumu mno
 
Kuna ubaya gani TRA kuwataka muorodheshe store zenu mnazohifadhia mali, wanataka wazifahamu ili wakazikague, kwasababu huko Kariakoo kuna ukwepaji mkubwa sana wa kodi.

Hata kama hizo kodi zinatumika hovyo serikalini, vyema store zenu zifahamike, ili mkiwatoroka bandarini mkakutane nao store, anyway niwapongeze hao wafanyabiashara kwa uthubutu wao, hata kama sikubaliani na madai yao.
Umakini wakufuatilia wangeweka kwenye pesa ambazo zinaliwa na mafisadi tungefika mbali kama nchi.

Kuna muda mwingine unajiuliza nilipe kodi halafu zinaliwa kiholela na watu wale wale kila siku bila ya kuchukuliwa hatua.
 
Tunadanganywa sana kuhusu Demokrasia na mambo mengine mengi tu na madhara yake tunakua wakaidi bila sababu za msingi au?

Urasimu Bandarini:Kama hii ndio sababu wameweza kutoa mbadala upi-- kuwaelewesha Serikali au TRA kutatua kero hii?
Huo Urasimu umeanzia wapi? Katika mfumo huo wa Bandarini? Kero hii ilianza lini manake toka najua Bandarini na kujua mizigo inapitia bandarini nimekuwa nasikia kodi hailipwi na rushwa inatokea, ikiwa ina maana wafanya biashara ndio wanaofaidika na mchezo wote wa ukwepaji kodi na kuifanya Serikali kukosa mapato; na watu kunenepeana matumbo kwa rushwa wanayokula....huo ndi Urasimu?

Hakuna nchi iliyoendelea ambayo wananchi au wafanyabiashara wanagoma kulipa kodi kwa sababu ya Urasimu. Nipo tayari kusahihishwa.

Kamata Kamata au amata Kamata: Kwa vyovyote vile kuna sababu TRA wanatoa ikiwa wanafanya mazoezi hayo mitaani, swali la kujiuliza, kama una store, kwanini uuze tena mitaani? Yaani una leseni ya Duka na Uchuuzi at the same time? Sielewi hapa.Isitoshe hata kuhariri haukufanyika na unaonyesha , kwa maoni yangu, hawakujianda vizuri...naona kana Wachuuzi kufanya Siasa vile Haijalishi kwani sio kinachowakwaza, nafikiri.

Usajiri wa Stoo au Sheria mpya ya Usajiri wa Stoo. Hakika Wananchi tunataka kujua bidhaa zinatoka wapi, na kama ni bidhaa zinazohitaji kuwepo kwenye maeneo muhimu, kama vile firiji, chumba kisicho kuwa na joto kati ya nyuzi, mathalani 20°c na 28°c n.k au Chumba kisicho kuwa na mvuke au humidity, au Chumba kisichokuwa na bidhaa za kuulia panya ikachanganywa na Biskuti au pipi za Watoto, n.k yaani Usalama mzima wa Binadamu na Afya ya Jamii kwa Ujumla Watumiaji wa Bidhaa tunataka tujue!

Unakataa vipi?

Walakin, TRA inafanya ukaguzi wa Ubora wa Store? Sidhani....nani ni Mdhibiti wa au mratibu wa Bidhaa za Kibinadamu na Zingine km Vipuri vya magari .n.k? Je, TRA wangeweza pata anuani au taarifa zingine, labda kutoka TBS au Wizara ya Afya au hata kutoka Halmashauri? -Halafu wawafuatilie?
Sasa kwaavile sijui Sheria hiyo mpya Inataka nini, nitagota hapo....nilicho kidadavua ni kuwa kuna mchongo wa Kisiasa hapo, kwani katika Dhamira yao wametaja Rushwa. Inachekesha na inasikitisha kuwa wanakubali na kukiri kuwa Wanatoa rushwa wakati wakilipa Kodi Aisee

Kuna Mchongo, na kama kuna Chama au Vyama vya kisiasa au Uharakati vimetumika, Aisee ni lazima wapelekwe kwenye Uhujumu Uchumi.... tutajua TISS-Uchumi watafanya nini, labda?

Kuna wachafuzi wapya, washugulikiwe haraka.
Au geresha toto hili
Ngoja ninywe Uji kabisa...na safari.......
 
Hakuna mantiki yoyote ya kupiga Kodi dukani tena unapiga Kodi stoo kwenye bidhaa zile zile. Huo ni wizi siyo kodi

Ingekuwa awamu ya 5 waandaaji wa mgomo wangetekwa jana kabla ya mgomo kuanza leo..
Yani ww una matatizo..Tatizo limetokea May 2023, kitu cha kwanza unachofikiria ingetokea awamu ile wangeshatekwa.. kwani kipindi kile walikuwa wanadai kodi ya stoo? Badilika
 
Najuwa hilo nilijibu tu kwa hoja ya mtu kusema kuna mipaka lakini shida kubwa hapa watu wa TRA wanajuwa kuwa kukiwa na mfumo usioingilika utaziba mianya ya rushwa watakufa njaa wanataka tubaki na hii analog mtu aweze tu kuamua kuna nini ndani ya container na gharama waamue nadhani kuna wakala wa kufanya clearance hawa wanatakiwa kuonesha 100% kuna nini na gharama zake ni zipi na viwango vya kodi viko kisheria ukiweka number kodi ni hii sasa kuwe na hali kuweka kiwango kuambatane na doc ku support gharama japo najuwa kuna ujanja mwingi mzigo wa mil 1 wanaweza kuweka laki moja hapa ndio tunatakiwa tutafute tech kuziba hii mianya kama shida kodi ni kubwa hilo na la kisera na serikali ina wajibu kuangalia. Mbona magari hakuna shida hizi, unaleta gari unaingiza model inakupa kodi hii wala huwezi kuchezea ndio maana ukija huku mitaani kwa wauza magari bei zinafanana sana.
Ulishawahi sikia kesi nyingi za Kontena za mitumba alafu ndani kuna Range Rover?
 
Kuna ubaya gani TRA kuwataka muorodheshe store zenu mnazohifadhia mali, mnaficha kitu gani, wanataka wazifahamu ili wakazikague, kwasababu huko Kariakoo kuna ukwepaji mkubwa sana wa kodi.

Hata kama hizo kodi zinatumika hovyo serikalini, vyema store zenu zifahamike, ili mkiwatoroka bandarini mkakutane nao store, anyway niwapongeze hao wafanyabiashara kwa uthubutu wao, hata kama sikubaliani na madai yao.
Je wewe ungeweza kulipia bidhaa ikiwa stoo na bidhaa hiyohiyo ulipie tena ikiwa dukani?
 
Kodi lazima mlipe mnatabia ya kuficha Mali kwenye stoo harafu mnapeleka kiduchu dukani Ili mkadiriwe Kodi..

Mkigoma tunawafutia leseni na wote waliogoma hayo maduka tunayafunga marufuku kufungua.

Very simple hii mbona.Tanzania ni kubwa hapo Kariakoo ni sehemu.ndogo sana mapato yake kwa.mwka hayafiki hata Bil.500
Unakemeaga matrillioni ya fedha yanayopotea serikalini hivihivi??
 
Kuna mtu humu jf aliwahi kusema kuna wafanyabiashara wanaopitisha mizigo kutoka stoo na kuwauzia wamachinga bila kupitia dukani kwahiyo serikali imeona kuna pesa inapotea hapo.
Wao si wameshalipia kodi walipoingiza hizo bidhaa. Wauze tu.
 
Wanaanza kupata Akili.Huu Mgomo Ulitakiwa uitishwe wakati hii sheria ilipotungwa Mwaka Jana?Hasa wakati inajadiliwa Bungeni.Sasa hivi Kelele zao wanampigia Asiyehusika. TRA wao ni watekelezaji tu wa sheria.Non-Compliance=Offence=Legal Action.

Watagoma Kisha Njaa zitawarudisha barabarani maana Mambo yatakuwa Magumu.

Ushauri wangu.Watulize wenge wajipange ili waweze kuweka mambo sawa.Lakini cha muhimu zaidi ni waende wakaisome Hiyo Sheria Vizuri kabla ya kupiga kelele
 
Back
Top Bottom