Mgomo wa Wafanyabiashara: Biashara zafungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024
Nyie gomeni wote , ila watu wa karume nsiwakwaze !
Wakigoma tunafanyaje sasa wakati huko ndo angalau tunaweza kupata Gucci na Versace kwa bei nafuu !
Karume wanalipa kodi?
Wale si wanalipa 500 za meza?
Wanalipa service levy?
Wamachunga wa Karume wana TIN number?
wana OSHA?
Wana NSSF?
Wana annual return za TRA?
Kama hawana hivi vyote basi hawa mgomo hauwahusu.
Karume ni gulio na siyo soko kama Kariakoo!
 
Kweli machinga wamefungua....mgomo huu hauwahusu.
Nipo K.Koo muda huu..

Machinga wana umoja wao...na kero zao.
Machinga hawana hata EFD...
Machinga hawalipi Service levy...
Machinga hawasumbuliwi na TRA...

Wamefungua na wanafanya biashara kama kawaida.

Walio funga hadi muda huu ni wamiliki wa maduka
Well narrated,wamachinga watagomea vitambulisho na mengi eyo .
 
Safi, nakwingineko pia watu wagome tu.

watawala hawawezi kufikiri nje ya box ili mapato yawe mengi baadala yake wanachukua njia rahisi ya kumkamua ng'ombe mwenye njaa huku wao wakiishi maisha expensive na kutapanya kwa kumkamua masikini.

Angalizo: Wanasiasa kaeni mbali na hii movie ya wafanyabiashara, msijihusishe nayo na kujitafutia umaarufu na kuharibu kile kilichokusudiwa na wafanyabiashara.
 
Chry

Hakuna mgawanyiko yaani kumuona fred, Martin na Hamis sehemu fulani pamoja na muhindi mmoja mkubwa hiyo ni ishara Kwanini hata barua haikuwa na jina.

Haiitaji degree kuelewa nini kimefanyika hapa.
Mkuu kwa hiyo viongozi ni kama hawakua tayari kugoma ? Au walihamasisha kugoma ila baadae wamewasaliti wenzao ? Au wametishiwa na serikali ?
 
Back
Top Bottom