Mhasibu wa Benki atekwa, achomwa petroli porini

Mhasibu wa Benki atekwa, achomwa petroli porini

I'm doing my home-work.
Kwanini wamchome moto akiwa hai?
Aliwezaje kufanikiwa kuwatoroka?
Je walipomteka walimtoa fahamu kwanza, wakaamini wameshamuua ndipo wakaenda kumchoma moto, na kuondoka? na hivyo moto ukamzindua na kuanza kukimbia?

Au, walimchoma moto akiwa hai na kumuacha afanikiwe kutoroka ili aweze kuongea maneno yatakayopelekea upeleleza kuhama mbali kabisa na sababu ya tukio hilo na kuwaelemea wengine?

Waliofanya tukio hili are very professional events planners and killers, nawwza nikathubutu kusema waliofanya tukio hili hawatokei ndani ya mipaka ya nchi yetu.
"walimchoma moto akiwa hai na kumuacha afanikiwe kutoroka ili aweze kuongea maneno yatakayopelekea upeleleza kuhama mbali kabisa na sababu ya tukio hilo"

Unaweza kuelezea kidogo hapa mkuu. Kitu gani kingelisababisha aongee maneno yanayoweza kuondoa ushahidi wa tukio baada ya kufanikiwa kupona kifo?
 
UNKNOWN SOURCES/SIJATHIBITISHA

Inasemekana alinayehisishwa na kifo chake ni Boss wake …

Aliaambiwa afoji check ya 1B isemekane imeandikwa kimakosa ili hiyo hela isionekane Bank .. Lakin Binti alikataa..

Boss alimsumbua akakosa amani akaomba ruhusa kuja Kibaha kuisalimia familia yake .. Lakin alikuwa akiwasiliana na Mchumba wake nakumpa taarifa hizo..

Alipokuja Kibaha alimshirikisha Baba yake Mzazi ambaye ni Doctor Mkuu Mwimbili Dar. Siku chache kurudi nyumban Boss wake alimpigia Baba yake huyo Binti kumtaka amwambie mwanaye aache kazi ndani ya masaa 24 . Baba ake akahoji kwakosa gani mwanangu alilolifanya?

Lakin siku ya pili alipigiwa simu na mmoja wa wafanyakazi wenzake Kahama kumjulisha wamekuja Dar kikazi wanapita kibaha wamsalimie… According to that .. Alipokea simu kwamba wamefika wakutane alipotoka ndyo hakurudi tena ..

Kupelekwa porini na kuchomwa moto na sindano za sumu .. Alijitahidi kujikongoja mpka eneo la makazi ya watu .. Nakuonba msaada apigiwe simu Baba ake .. Toka hapo alikata kauli na kukimbizwa Mwimbili.. na siku chache kuaga dunia..

Inasemekana Boss wake ameshakamatwa sheria itafata mkondo wake ..

Mungu ailaze roho ya marehemu Martha [emoji17].

Sent from my CPH2239 using JamiiForums mobile app
Kwenye pesa binadamu yuko tayari kufanya chochote kile mradi tu aipate,so sad...
 
"walimchoma moto akiwa hai na kumuacha afanikiwe kutoroka ili aweze kuongea maneno yatakayopelekea upeleleza kuhama mbali kabisa na sababu ya tukio hilo"

Unaweza kuelezea kidogo hapa mkuu. Kitu gani kingelisababisha aongee maneno yanayoweza kuondoa ushahidi wa tukio baada ya kufanikiwa kupona kifo?
Kuna uwezekano wauaji walimfuatilia mienendo yake na kumfahamu na kum mark vya kutosha.
Inawezekana, baada ya kumteka wakawa wanampiga biti kwamba siku nyingine iwe fundisho kwa wanaopenda kuingilia either mahusiano ya watu au mambo yasiyomhusu kitu ambacho kinakuwa rahisi kwa marehemu ku connect dots na kujua watu hawa watakua ni akina fulani au wametumwa na fulani (hapo wauaji wanazidi kujijengea kinga ya kutohisiwa)
Kitu ambacho kitapelekea vyombo vya uchunguzi vilivyomhoji kuelekeza nguvu zao ambako maelezo ya marehem yameelekeza.

Wakati kiuhalisia kifo cha marehemu kitakua kinahusiana na tukio la yofauti kabisa na maelezo ya marehemu.

Cha kufanya, wajaribu kufanya tracking katika biashara za marehemu tangu akiwa Babati hadi alipohamia Kahama.

Waangalie manunuzi aliyowahi kuyafanya na malipo yake yalikuaje.

Waangalie mazingira ya kuacha kazi yalikuwaje, na mahusiano aliyokua nayo na wateja wa bank kote alipowahi kufanyia kazi.

Waangalie mahusiano na wafanyakazi wenzake, hasa wale wafanya kazi wenzake ambao ni 'Partners in Crime' ambao huku uswahili huwa tunapenda kuwaita 'Pika pakua', pia bosi wake. Lazima kuna issue ya mgao iwe inahusika hapo.

Nina uhakika mpaka sasa wana taarifa za kutosha kuhusiana na jinsi alivyoondoka kanisani.
Pale Kahama lazima kutakua na eneo pendwa ambalo marehemu alikua akipenda kutembelea akiwa na watu fulani, ni muhimu sana kuipitia nayo.
 
Kama kuna jambo ambalo unatakiwa uwe unaliombea sana katika maisha ya kila siku ni kuepuka kuishi na uadui na watu wanaokuzunguka,ni ngumu kuepuka lakini kwa uwezo wa Mungu inawezekana,na mbaya sana katika hao maadui uogope yule ambaye ana tabia ya kulipiza kisasi,maana kuna watu wao ni 'do me i do you',hawa ni hatari sana.Hapa ukiangalia kuna mambo matatu yanaweza kuhusika Kisasi,kupoteza ushahidi au kumuadabisha...,
 
Huyu sio binti wa Dr. Towo? Ila binadamu tuna roho mbaya sana! Hivi kweli unaamua kumuua mwenzako kwa kumwagia petrol na kuwasha kiberiti hadi afe?! Kosa alilofanya halikuwa na adhabu mbadala? Pole familia ya Towo. RIP dada yetu.
 
Mtaalamu wa akili ni mtu anayedai kutumia utambuzi wa ziada (ESP) kutambua taarifa iliyofichwa kutoka kwa hisi za kawaida, hasa zinazohusisha telepathy au clairvoyance, au ambaye anafanya vitendo ambavyo havielezeki na sheria za asili, kama vile psychokinesis au teleportation.
 
Jeshi la polisi liliwa kumfuata au kumpa wito wa kisheria Lissu akatoe maelezo kuhusu kupigwa kwake risasi?
Watu wanaoshambuliwa na kuuwawa uchunguzi wao haufanyiki kwa sababu wamekufa??
Lissu hakutoa ushirikiano na jeshi la polisi sio siri
 
MPAKA WATU WANAIGIZA SAUTI YA BOYFRIEND NA KUMWITA NNJE YA KANISA AISEE YANGU MACHO KAMA ATASHIKWA MTU HAWA NI PROFESSIONAL KILLERS AMBAO HAWAJAWAHI SHUHUDIWA KATIKA NCHI YA TANZANIA TOKA UHURU
 
Kama kuna jambo ambalo unatakiwa uwe unaliombea sana katika maisha ya kila siku ni kuepuka kuishi na uadui na watu wanaokuzunguka,ni ngumu kuepuka lakini kwa uwezo wa Mungu inawezekana,na mbaya sana katika hao maadui uogope yule ambaye ana tabia ya kulipiza kisasi,maana kuna watu wao ni 'do me i do you',hawa ni hatari sana.Hapa ukiangalia kuna mambo matatu yanaweza kuhusika Kisasi,kupoteza ushahidi au kumuadabisha...,
Wengine ni rohoo mbayaa tuu yani Ukishakuwa mtu mzima mkuu utakutana na vioja vingi sanaa.. unaedhani ni jirani yako kumbe ndo Mtu anaekuchukia na kukufanyia mabaya sirini kila sikuu yani BINADAMU ACHANA NAO. Sio wote wanaotendwa ubaya walifanya ubayaa.
 
Back
Top Bottom