Mhe. Tundu Lissu, Please Acha Kumsulubu Spika Wetu! Unammaliza Kabisa Hadi Ameshindwa Kazi!

Mhe. Tundu Lissu, Please Acha Kumsulubu Spika Wetu! Unammaliza Kabisa Hadi Ameshindwa Kazi!

Pasco acha akome sialiona bwana six anafaidi!Na bado mpaka 2015 ataiona joto yake.
 
Pasco siasa mchezo mchafu! Jioni utawakuta hivi!

IMG_4291.JPG


Ha ha haaaaa!!!,nimecheka mpaka basi kweli kikulacho kipo nguoni mwako.
 
Bunge halina kazi waondoke tu watusamehe hizo kodi zetu wanazotafuna kila siku kwa kukaa bila kazi, ndio maana Zitto ameamua aende zake kigoma kufanya shughuli za chama! Shame on them! Bunge linaogopa kuisimamia serikali sasa kazi yake ninini hasa?


hata Lema The same namuona huku Arusha anapiga kazi za chama nikajiuliza mbona ameacha Bonge kumbe ameona hawapewi nafasi ngoja watumie nafasi nyingine katika kuuambia umma wa watanzaniani jinsi rasilimali za nchi zinavyokeketwa kama mwanamke wa kimaasai. hata Mh. wa mwanza naye nilisikia swali laki likiulizwa na Nasari.

Sasa kuzuihia hoja binafsi ndio haki hiyo.

WATANZANIA TUNAZIJUA MBIVU NA MBICHI.

WE pasco leta tu hoja za kijinsia kwani yeye alivyopendekezwa na akakubali si alijua anaenda kuwaongoza jinsia zote sasa iweje utake Tindo Lisu amchukulie kama mkewe wakati mkewe kamwacha nyumbani??
NA MBADO NATAMANI ANGEMWAGA CHOZI AU KOJO KABISA KAMA MWENZAKE MWINZI MKUU ALIVYOLILIA MAALBINO
 
ha ha haaaaa!!!,nimecheka mpaka basi kweli kikulacho kipo nguoni mwako.
hakuna kitu alifikiri kujichezesha na tindo ndio kubembeleza urafiki wa kaisari tindo inabomoa miamba migumu hadi inatoa dhahabu na almasi uliza machali watakuambia jinsi ya kupata tanzanite lazima uwe na tindo lisu kali iliyonolewa
 
Heshima mbele sana GT, Natoa angalizo kwa MAT Kumchunguza kwa makini huyu HAMISI KIGWANGWALA kwa kauli yake Kuhusu Mh .Tundu Lissu , kama kwa upuuzi aliouwasilisha Bungeni bado ana sifa za kuwa member wa MEDICAL ASSOCIATION OF TANZANIA , Dr Namala Mkopi najua umo humu Jf , bila shaka maadili yamevunjwa , tunaomba Avuliwe uanachama ili Kulinda heshima ya Taaluma .
 
Uspika sio viti maalum kupewa,alichaguliwa na viazi wenzake wacha ale joto ya jiwe
 
Wanabodi,

Leo nimepata fursa ya kuliangalia bunge live asubuhi hii kupitia TBC-1,
Spika wa Bunge, Mhe. Anne Makinda ameshindwa kabisa kuliendesha bunge!, amepwaya sana na ameendesha kika bila confidence kabisa na mwisho wa maelezo yake, akamtaja Mhe. Tundu Lissu kama ndiye mbunge anayeongoza kwa kuleta vurugu bungeni, na Lissu aliponyanyuka kuomba muongozo wa Spika, akamvurumishia tena Spika Makombora mazito, na kama angeendela kidogo tuu!, Spika Makinda ange break down kwa machozi!. (Naamini akifika ofisini kwake, atajifungia kidogo na kuimalizia hasira yake the same way wanawake wote wanamalizaga hasira zao!.

Kwa kuzingatia sifa kuu iliyomfanya Mhe. Mama Makinda kuchaguliwa kuwa spika, huku Mhe. Tundu Lissu akiujua fika uwezo wa Madam Spika, kwanini anaendelea kumsulubisha kila apatapo fursa?!. This is not fair!.

Kwa vile Mama Makinda amepewa uspika because she is a lady, kwa uzi huu, namuomba Mhe. Tundu Lissu na wabunge wengine wa Kambi ya Upinzani, wanapokuwa na hoja za msingi, wamuaddress Madam Spika with courtesy of addressing a lady, ili ku restore confidence yake kuliendesha bunge ambapo kwa sasa, ameshindwa kabisa, amezuia hoja zote binafsi, hivyo leo bunge limekutana asubuhi tuu kwa kipindi cha maswali na majibu na kuahirishwa, natumaini kesho na keshokutwa itakuwa vivyo hivyo!, huu ni ufujaji bure wa rasilimali za Taifa!.

Nawauliza wajameni, hivi hiki anachofanya Mhe. Lissu na wabunge wengine wa upinzani, kumsubulu Madam Spika ambaye ni mwanamke bila huruma, ni sawa kweli?!.

Kiafrika, wanawanake ni ni watu wa kubembelezwa na kuonewa huruma!, hivi hawa wabunge wa upinzani ni watu wa aina gani wasio hata na huruma kwa wanawake?!, leo ilibakia kidogo tuu madam spika angelia!, jee hiki wanachofanya ni sawa kweli?!. Ni haki?!.

Nawaombeni tumtendee haki Spika wetu aendesha bunge kwa haki na kujiamini!.

Pasco.


Huruma huruma huku nchi inateketea,kama vipi hajalazimishwa chochote kuendelea kukalia kaa la moto.Aachie kiti hicho habari ya huruma labda akaonewe huruma na mumewe lakini katika masuala yanayohusu nchi atupishe tu,hii kasi hata maji ya kunywa anatakiwa ayaone machungu.
 
Huyo ndiye Tundu Lissu bana. Mpiganaji asiyeogopa lolote. Nchi hii inahitaji akina Tundu Lissu wengi zaidi ili iweze kunyooka. Kuna mambo mengi ya kipuuzi yanapaswa kukemewa in public.
 
Kiroboto leo alikua mdogo jamani!Nahisi jasho lilimtoka hadi kwenye kijiji!...
 
Tatizo ni uwasilishaji wa mada hapa JF...Mtu unaandika as if wote tumeona...Mkuu Pasco, hadi sasa sijajuwa nini kimetokea!!!!
 
Last edited by a moderator:
Asepe kule hatupo hapa kutetea ujinga wa watu wasiojua kuongoza mambo...spika ni mtu mkubwa sana nchini na anatakiwa kuwa mtu credible sana katika mambo ya management sasa hyu mama hajui lolote lile huwa yupo pale kutetea ujinga tu
 
Nadhani wabunge wa upinzani wakiwa wanachangia bunge, wasiseme tena Mheshimiwa spika wala naibu spika, wawataje kwa majina tu na ubunge wao basi
 
Back
Top Bottom