LGE2024 Mimi na familia yangu tumeshajiandikisha kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

LGE2024 Mimi na familia yangu tumeshajiandikisha kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Leo tarehe 11 Oktoba, 2024 mimi na mume wangu Advocate Gwajima na watoto wetu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea, tumefika kituo cha Serikali ya Mtaa wetu wa Salasala, Kata ya Wazo kujiandikisha na kuboresha taarifa zetu kwenye daftari la mpiga kura wa serikali za mitaa kama maandalizi kuelekea kupiga kura ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa utakaofanyika 27 Novemba, 2024 nchini kote.

Hatua hii ni kufuatia uzinduzi rasmi kitaifa wa kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura wa serikali za mitaa uliofanywa tarehe 11 Oktoba , 2024 huko Chamwino, Dodoma na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan.

PONGEZI kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wetu wa Salasala, Kata ya Wazo Ndugu Robert Ally Massawe kwa maandalizi mazuri ya utaratibu wa kujiandikisha na wepesi na umahiri wa maafisa waandikishaji kwenye kutoa huduma husika.

Mimi na familia yangu tunawahamasisha watanzania wote wenye sifa ya kupiga kura kujitokeza kwa wingi kwenda kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwenye serikali za mitaa yao zoezi litakalofanyika kuanzia tarehe 11-20 Oktoba, 2024.

Viongozi wenye sifa za kutumikia jamii ni matokeo ya kura yako mtanzania mwenye sifa ya kupiga kura hivyo, jitokeze jiandikishe. Mimi na familia yangu, tayari tumetimiza wajibu wetu.

Tunawatakia uandikishaji na uboreshaji mwema wa taarifa zenu kwenye daftari husika.

MWISHO.

View attachment 3121584View attachment 3121585View attachment 3121586View attachment 3121587View attachment 3121588View attachment 3121589
View attachment 3121590
Hongera Dr. Gwajima , ila kungekuwa na options ya kuwafuata watu majumbani/ makazini ingependeza zaidi
 
Maendeleo ndio yanapaswa kuhamasisha watu kujiandikisha, kupiga kura na kuchagua viongozi na wala sio kampeni kama za kutokomeza surua, mabusha na matende...
 
Leo tarehe 11 Oktoba, 2024 mimi na mume wangu Advocate Gwajima na watoto wetu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea, tumefika kituo cha Serikali ya Mtaa wetu wa Salasala, Kata ya Wazo kujiandikisha na kuboresha taarifa zetu kwenye daftari la mpiga kura wa serikali za mitaa kama maandalizi kuelekea kupiga kura ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa utakaofanyika 27 Novemba, 2024 nchini kote.

Hatua hii ni kufuatia uzinduzi rasmi kitaifa wa kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura wa serikali za mitaa uliofanywa tarehe 11 Oktoba , 2024 huko Chamwino, Dodoma na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan.

PONGEZI kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wetu wa Salasala, Kata ya Wazo Ndugu Robert Ally Massawe kwa maandalizi mazuri ya utaratibu wa kujiandikisha na wepesi na umahiri wa maafisa waandikishaji kwenye kutoa huduma husika.

Mimi na familia yangu tunawahamasisha watanzania wote wenye sifa ya kupiga kura kujitokeza kwa wingi kwenda kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwenye serikali za mitaa yao zoezi litakalofanyika kuanzia tarehe 11-20 Oktoba, 2024.

Viongozi wenye sifa za kutumikia jamii ni matokeo ya kura yako mtanzania mwenye sifa ya kupiga kura hivyo, jitokeze jiandikishe. Mimi na familia yangu, tayari tumetimiza wajibu wetu.

Tunawatakia uandikishaji na uboreshaji mwema wa taarifa zenu kwenye daftari husika.

MWISHO.

View attachment 3121584View attachment 3121585View attachment 3121586View attachment 3121587View attachment 3121588View attachment 3121589
View attachment 3121590
Wewe ni kati ya mawaziri uliye karibu na Watanzania. Kila Waziri, Waziri, mkuu, Rais, Makamu wa Rais, NW, makatibu wakuu, Mkuu wa Mkoa, Wakurugenzi, wakuu wa wilaya, kata, vijiji, mitaa, watumishi wote wa umma wangekuwa kama wewe tungepiga hatua. Mtu kama wewe,Jerry Slaa, Lukuvi mtaishia kutumbuliwa na serikali hii.
 
Maendeleo ndio yanapaswa kuhamasisha watu kujiandikisha, kupiga kura na kuchagua viongozi na wala sio kampeni kama za kutokomeza surua, mabusha na matende...
Mkwe kajiandikishe.
 
Mheshimiwa, mimi hapa kijana shupavu nimefanikiwa kumuona mwanao.
Nauliza tu, je itapendeza na mimi nikiwasiliana nae ili siku moja mimi pia nikae nae kwenye dawati la kuboresha taarifa za uchaguzi kama wewe na advocate hapo..?
 
Dah! Sasa sisi wengine tukiacha kwenda kazini siku hiyo tumelala njaa, endeleeni kutuwakilisha kwanza hata sijui faida ya kupiga kura.
 
Kwa wateule wa rais lazima wajiandikishe Kwa sababu ndiyo sehemu Yao inayowapatia kula Yao na maisha Bora .Sasa Mimi ambaye siyo mteule ambaye miaka mingi nimepiga kura lakini Kuna hujuma ambazo zinaonekana wazi kabisa kuwa Kuna chama kinasaidiwa na polisi kuiba kura ili kishinde Sasa hapo Kuna faida gani ya kujiandikisha ili kupiga kura?
 
nimejiandikisha leo,ila ntapga kura ya ya mwenyekiti tu huko kwingine sina habari maana hakuna haki.
 
Hongereni ila washauri viongozi wenzako wenye dhamana ya kusimamia uchaguzi watende haki ,nchi inatumia fedha nyingi sana kwenye uchaguzi kuanzia uandikishaji hadi upigaji kura ,matendo ya kuiba kura au kuaanda kura za maruhani mapema ni bora kusifanyike uchaguzi muwe mnajichagua wenyewe ili hizo fedha ziende kutumika kwenye huduma za jamii.
Je ? Umejiandikisha?
 
Tusidanganyane, nyie mmeboresha taarifa zipi zaidi ya kuandikisha jina lako na umri basi. Mimi mtaani kwangu wanaandika jina na umri tu, hakuna taarifa za ziada wanazochukua. Machawa msituchanganye wananchi tuone kuwa tulichoandikishwa si sahihi.
Ndiyo kuboresha mwenyewe huko, umefanya vema
 
Back
Top Bottom