Mimi naona dunia iachane na mfumo dume na rasmi 50/50 ishike hatamu

Mimi naona dunia iachane na mfumo dume na rasmi 50/50 ishike hatamu

Hiyo 50/50 unayotaka Mjukuu mtaweza majukumu yake?

Kwamba Mume atoe Kodi ya miezi 6 ya nyumba na Mke alipie miezi 6 iliyobaki ya Kodi.

Wanawake wenyewe ndiyo hawa ambao wanasema mshahara wao ni wao pekee ila wa Mshahara wa Mume ndiyo wa kutumika ndani ya nyumba?

Nina rafiki yangu ni Mzungu, wao ndiyo wanaiishi hiyo 50/50 ambapo wamegawana majukumu sawa sawa na Mume wake.

Ana watoto 2 na Mume wake, mtoto mmoja ana msomesha na kumgharamia yeye matibabu/mavazi na Kila kitu kuanzia alipozaliwa hadi Chuo Kikuu na mtoto mwingine ana gharamiwa yote hayo na Mume wake.

Nieleze kama Kuna Mwanamke Bongo hii ataweza kuyafanya hayo.

Ubunge wenyewe mnapewa bure bure na Chama
Watoe wazungu apa,wazungu hawana habari ya kutaka kuheshimiwa kama miungu mtu wanaume wa Tz ,wao wanaishi sawa wote wanajukumu la kuheshimiana.

Hapa anaongelewa mbongo asiyefanya majukumu yake kama mume alafu anataka aheshimiwe ni ngumu sana.
 
Watoe wazungu apa,wazungu hawana habari ya kutaka kuheshimiwa kama miungu mtu wanaume wa Tz ,wao wanaishi sawa wote wanajukumu la kuheshimiana.

Hapa anaongelewa mbongo asiyefanya majukumu yake kama mume alafu anataka aheshimiwe ni ngumu sana.
Hao Wanaume wasiowajibika mmewatolea wapi?

Yaani Mwanaume ambaye halipi Kodi/toa hela ya chakula/mavazi Kwa mke na Watoto wake/Asiyelipa ada ya watoto/kulipia gharama za hospitali n.k

Nawe Mwanamke unaendelea kukaa na huyo Mwanaume anakupiga mimba ya kwanza, unapigwa ya pili n.k

Basi nawe utakuwa haujitambui

Hiyo 50/50 haifanyi kazi Tanzania labda Kwa Wazungu huko
 
Nyie ndo mnaopendaga mserereko/kitonga hamtakagi kujituma, Dunia ya Sasa ukipenda mserereko au kitonga utaishia kupakuliwa kwenye sahani, utafirwa wewe shauri zako watakuingilia njia zote marinda yatatuliwe uanze kujinyea ovyo na ndo skuiz wanavofanyiwa wanawake kama wewe wapenda vitonga.
Nasikia wanakufanya vibaya hadi unavaa diper, huyo ni wewe na chaguzi zako, mimi nimechagua kuheshimu utu wangu.
 
Tumia hesabu ya uwiano kila tajiri mwanaume ana mke kaoa na wengi ufa na kuwaachia mabilioni ila baada ya hapo ni chini ya asilimia 1 ya hao wanawake ndiyo wanaweza japo kulinda huo utajiri kidogo tu wote walio salia utajiri unapukutika usijulikane ulipo tokomea ...tutizame kwa samia na jpm tu ...jpm ameacha mambo yapo kwenye mstari chanya ila kwa sasa samia katutoa na kutudumbukiza kwenye giza kila kitu kinasambaratika...huwezo wa akili wa mwanamke ni robo tu ya mwaname kwa wastani
Bado hujajibu swali langu je kwa wanaume hakuna ambao wanaachiwa mali na wazazi au ndugu zao na wanashindwa kuziendeleza hadi wanafirisika, hii nchi ina miaka zaidi ya 60 tangu imepata uhuru na imekuwa ikiongozwa na wanaume je wamefanya nini la maana ikiwa hadi leo mambo muhimu kama maji, umeme, afya, elimu, uchumi na teknolojia bado ni tatizo, na mbona umetolea mfano wa Tanzania tu je hakuna nchi ambazo zimeongozwa na wanawake na zinafanya vizuri au hata tukija kwenye kampuni je hakuna ambazo zimeongozwa na wanaume zikafanya vibaya na je hakuna ambazo zimeongozwa na wanawake zikafanya vizuri
 
"Mwanaume ni mtafutaji/mtoaji na kiongizi.Mwanamke ni mpokeaji na mtumiaji wa alichotafuta mwanaume.Sasa,wanawake wanataka kuwa watoaji.Kitu ambacho hakiwezekani!Hata ukifikiria,mwanaume mzima umekaa nyumbani unalea watoto,utajisikiaje?Haiingii akilini kabisa.Kizazi hiki bwana![emoji1787][emoji1787][emoji1787]".
Mkuu kama unahudumia mke wako na unasimamia huduma zote za nyumbani basi hapo mke lazima afanye majukumu yake mkuu, shida ni wale wanaume wanaotaka mke wa kusaidiana naye maisha ila yeye hataki kumsaidia mkewe majukumu, na bado anataka mke wake ampe heshima na utii kama mume wake
 
Mkuu kama unahudumia mke wako na unasimamia huduma zote za nyumbani basi hapo mke lazima afanye majukumu yake mkuu, shida ni wale wanaume wanaotaka mke wa kusaidiana naye maisha ila yeye hataki kumsaidia mkewe majukumu, na bado anataka mke wake ampe heshima na utii kama mume wake
Mwanaume/mume anataka mke amsaidie majukumu ya kutunza na kuongoza familia?Afungwe kengele mbili za shule(rims za scania)na kutoswa ziwa lolote lenye moto mwingi.
 
After God the only thing I fear ni feminist

Hayo ni maneno ya Khaligraph Jones kwenye ngoma yake ya Tuma Kitu
Maneno yake si biblia wala msaafu hayo ni mawazo yake binafsi tu, nafikiri wanao make sense ni wale wanaosema "after god fear technology", otherwise kila mtu aweza amua kusema lake hata wanawake nao wanaweza kuamua kusema "after god fear men" na wakawa sahihi vile vile
 
Watoe wazungu apa,wazungu hawana habari ya kutaka kuheshimiwa kama miungu mtu wanaume wa Tz ,wao wanaishi sawa wote wanajukumu la kuheshimiana.

Hapa anaongelewa mbongo asiyefanya majukumu yake kama mume alafu anataka aheshimiwe ni ngumu sana.
Wewe umenielewa mkuu
 
Hao Wanaume wasiowajibika mmewatolea wapi?

Yaani Mwanaume ambaye halipi Kodi/toa hela ya chakula/mavazi Kwa mke na Watoto wake/Asiyelipa ada ya watoto/kulipia gharama za hospitali n.k

Nawe Mwanamke unaendelea kukaa na huyo Mwanaume anakupiga mimba ya kwanza, unapigwa ya pili n.k

Basi nawe utakuwa haujitambui

Hiyo 50/50 haifanyi kazi Tanzania labda Kwa Wazungu huko
Sasa ukimuacha si ndio utasikia kelele za oo wanawake hawana uvumilivu, mume akiyumba au akifirisika wanakimbia, yani hata kama mume aliyumba au alifirisika kwa ujinga wake wanataka mke avumilie
 
Mwanaume/mume anataka mke amsaidie majukumu ya kutunza na kuongoza familia?Afungwe kengele mbili za shule(rims za scania)na kutoswa ziwa lolote lenye moto mwingi.
Yeah wapo kabisa wanakuambia eti hawataki wanawake magolikipa na ombaomba, ukimuambia sawa basi kama unataka mwanamke akusaidie majukumu yako kubaliana na matokeo yake, sikilizia hayo majina utakayoitwa asee
 
Yeah wapo kabisa wanakuambia eti hawataki wanawake magolikipa na ombaomba, ukimuambia sawa basi kama unataka mwanamke akusaidie majukumu yako kubaliana na matokeo yake, sikilizia hayo majina utakayoitwa asee
Mzembe na mjinga huyo.Anayakatibisha matatizo kwa uvivu wa kutafakari habari.
 
Sasa ukimuacha si ndio utasikia kelele za oo wanawake hawana uvumilivu, mume akiyumba au akifirisika wanakimbia, yani hata kama mume aliyumba au alifirisika kwa ujinga wake wanataka mke avumilie
Hiyo ni case tofauti Mjukuu, kama ameyumba Kiuchumi Kwa kukosa ajira n.k na alikuwa anahudumia familia yake kabla hajapata hiyo shida ya ajira anastahili kuvumiliwa.

Sifa ya Mwanaume ni kuwajibika Kwa familia atakayoianzisha, hayo ni mafunzo tuliyopewa tukiwa jandoni miaka ile ya Ujana.
 
Nasikia wanakufanya vibaya hadi unavaa diper, huyo ni wewe na chaguzi zako, mimi nimechagua kuheshimu utu wangu.
Sasa wewe endelea kutaka vya wanaume vya Bure Bure ndo ukubali na kupakuliwa, usipende kitonga mtoto wa kike jitume shauri zako watakukula pande zote ka samaki.
 
Hiyo ni case tofauti Mjukuu, kama ameyumba Kiuchumi Kwa kukosa ajira n.k na alikuwa anahudumia familia yake kabla hajapata hiyo shida ya ajira anastahili kuvumiliwa.

Sifa ya Mwanaume ni kuwajibika Kwa familia atakayoianzisha, hayo ni mafunzo tuliyopewa tukiwa jandoni miaka ile ya Ujana.
Sahihi kabisa babu, ila kuna wale wanaume pia wanaojijua hawana uwezo wa kuhudumia familia ila nao wanataka waoe, na wanalalamika kwamba wanawake wa siku hizi wanapenda pesa
 
Maneno yake si biblia wala msaafu hayo ni mawazo yake binafsi tu, nafikiri wanao make sense ni wale wanaosema "after god fear technology", otherwise kila mtu aweza amua kusema lake hata wanawake nao wanaweza kuamua kusema "after god fear men" na wakawa sahihi vile vile
When I get a time to waste, I'll comeback to you. Stay there
 
Ndio, kuna msemo unasema "with great authority comes great responsibility" yani kila mamlaka makubwa huambatana na majukumu makubwa, lakini jambo la kushangaza ni kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanayataka hayo mamlaka tu ila majukumu hawayataki

Mimi naona ifike pahala dunia iachane rasmi na mfumo dume na haki sawa ishike hatamu, kwa sababu wanaume hawataki tena majukumu hivyo hata hayo mamlaka hayawafai, wanaume wengi hawataki haki sawa ila wanataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke ndio afanye zaidi ya mwanaume

MImi naona kusiwe tena na mgawanyo wa majukumu yani hata kazi za nyumbani zifanywe na wote kama ambavyo kutafuta pesa limekuwa ni jukumu la wote, majukumu ya mwanamke yabaki yale ya asili na ya kimaumbile tu ambayo ni kubeba ujauzito, kuzaa na kunyonyesha, hayo tu ndio ambayo mwanaume hawezi kuyafanya ila majukumu mengine yote ya nyumbani kama kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, kulea watoto tangu wakiwa wachanga mfano kuwasafisha, kuwauguza wakiumwa, nk yafanywe na wote kwa usawa kabisa

Na vile vile kwa mfano mume akiweka laki mezani na mke naye aweke laki mezani mahitaji yote ya nyumbani wanunue kwa usawa bills zote walipe kwa usawa, na watoto wao wawahudumie kwa usawa ikiwemo kuwalipia ada na mahitaji yao mengine yote kwa usawa, hiyo ndio maana halisi ya 50 50 siyo mmoja anamtegea mwenzie eti mtu anataka pesa mtafute wote na bills mlipe wote, ila kazi za nyumbani na kulea watoto afanye mmoja na bado huyo mmoja amtii mwenzie na amlee kama anavyowalea watoto wake, what kind of cockamamie logic is this

Na jambo jingine naona pia tuachane na suala la mwanaume kumtawala mwanamke kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na habari za kichwa cha familia, yani hakuna tena kusema kwamba mwanamke anatakiwa amtii mumewe kila mtu awe na maamuzi juu ya maisha yake mwenyewe, kusiwe na wa kumuongoza mwenzake na pia kusiwe na habari za kuoa wala kuolewa tena bali iwe ni kuoana

Mnawalaumu wanawake kuwa wanadai haki sawa halafu hawataki majukumu lakini mnasahau kwamba sababu ya wao kukataa hayo majukumu ni kwa sababu mnataka wafanye yale ya kwenu tu, ila ya kwao bado mmewaachia wenyewe hamtaki kuyafanya yani huwezi kumuambia mwanamke ajitafutie pesa zake na akusaidie majukumu, halafu hapo hapo bado unataka huyo mwanamke akufanyie majukumu ya nyumbani na bado akupe heshima na utii

Kwanza hapo huyo mke anakuwa siyo msaidizi tena bali ni kama business partner tu hivyo ondoa kichwani suala la kumlazimisha akutii, hivi mnadhani mwanamke aliambiwa amtii mwanaume kwa misingi gani kama siyo kuhudumiwa maana huwezi kukitawala kiumbe usichokihudumia, hakuna binadamu mwenye akili timamu anayefurahia kutawaliwa na binadamu mwenzie asiyewajibika kwa lolote juu yake na kiuhalisia ukitoa huduma zinazohusisha pesa hakuna wajibu mwingine mwanaume alionao juu ya mwanamke

Kama ikiwa mtoto anamtii mzazi wake kwa sababu amemzaa na amemlea, watu wa dini wanaitii miungu yao kwa sababu wanaamini imewaumba na inawapa uhai, je mwanamke anapaswa amtii mumewe kwa sababu gani, tena hata mtoto mwenyewe akishatoka kwao akaanza kujitegemea kinachobaki kwa mzazi wake ni ile heshima tu kuwa amemzaa, lakini huyo mzazi anakuwa hana mamlaka tena ya kumpangia mtoto maisha yake mfano afanye kazi gani au arudi nyumbani muda gani kwa sababu hamhudumii tena

Sasa inashangaza pale mwanaume anapotaka mkewe atafute pesa wasaidiane maisha kwa kisingizio kwamba mke naye ana mikono miwili na miguu miwili, ila huyo huyo mwanaume haoni ajabu kumtawala huyo mke mwenye mikono miwili na miguu miwili kama yeye, yani imefikia hatua wanaume wanaona uchungu kugawana mali na wake zao na wengine ndio kabisa hawataki kuoa kwa kisingizio kwamba eti wakishafanikiwa wake zao watadai talaka ili wagawane mali

Yani hawaconsider tena yale majukumu yote ambayo wake zao wanawafanyia pamoja na utii ambao wake zao wanawapa, siku hizi wanadai kwamba kila mtu ajitafutie pesa zake na ikitokea wameachana kila mtu aondoke na chake, lakini cha kushangaza kwenye majukumu mengine hawasemi kila mtu afanye kwa usawa na kwenye suala la mamlaka hawasemi kila mtu ajitawale mwenyewe

Wale waumini wa ukristo hasa wanaume kama mmeamua kufuata maandiko basi fuateni yote, na kama mmeamua kuyapuuzia basi yapuuzieni yote msichague yale yanayowanufaisha ninyi tu halafu mengine mnajifanya hamyaoni, kwa sababu maandiko yanasema mume ndio atakula kwa jasho na si mke, halafu mbele ndio yanaendelea kwamba mwanaume atamtawala mwanamke, yule mke mnayemuota wa Mithali 31 yalikuwa mawazo binafsi ya mfalme Suleiman na si maagizo ya muumba

Hivo basi ifike pahala wanaume mchague moja kati ya mwanamke mfanyakazi/mfanyabiashara au mama wa nyumbani, na aina yoyote utakayochagua hapo lazima ukubaliane na sifa zinazoambatana na aina hiyo ya mwanamke siyo unachagua mfanyakazi/mfanyabiashara mnasaidiana majukumu, halafu hapo hapo unataka awe kama mama wa nyumbani au unachagua mama wa nyumbani halafu hutaki kumhudumia unaanza kumuona golikipa
Kama wanawake wanaweza kutukunja na kutugeuzageuza wanaume kama tunavyo wageuza sawa
 
Mtoa mada Kama vile keshapigwa na kitu kizito na marioo wa mjini[emoji4]
 
Back
Top Bottom