Mimi ni Muislamu. Nasema HAPANA kwa katiba pendekezwa

Mimi ni Muislamu. Nasema HAPANA kwa katiba pendekezwa

Mbna unachanganya frequency humu ndani wewe mambo yanshule wapi na wapi, mambo ya dini wapi na wapi?

utafiti uliofanyika humu jf unaonyesha kwamba wewe na dada yako Claudiaeliakim mnashabikia msichokijua, yamkini ninyi ni mapacha, ndugu wa damu au mtu mmoja mwenye i/d mbili, rais wa jmt kasalimu amri kwa tamko la maaskofu sembuse nyie watu wawili (2-in-1)?
 
Last edited by a moderator:
utafiti uliofanyika humu jf unaonyesha kwamba wewe na dada yako Claudiaeliakim mnashabikia msichokijua, yamkini ninyi ni mapacha, ndugu wa damu au mtu mmoja mwenye i/d mbili, rais wa jmt kasalimu amri kwa tamko la maaskofu sembuse nyie watu wawili (2-in-1)?

Unaonekana ulikimbia Milembe wewe, unazidi kubashiri, hivi tokea uanze kubashiri umeambulia nini zaidi ya kujaza server za JF humu ndani? jipange wewe chonga ndoi uje tena.
 
utafiti uliofanyika humu jf unaonyesha kwamba wewe na dada yako Claudiaeliakim mnashabikia msichokijua, yamkini ninyi ni mapacha, ndugu wa damu au mtu mmoja mwenye i/d mbili, rais wa jmt kasalimu amri kwa tamko la maaskofu sembuse nyie watu wawili (2-in-1)?

Huyo Eliakim kama unamtaka si umweleze awe demu wako naona unamtajayaja sana, hatuko kushabikia majina ya watu hapa wewe na yeye mna matatizo
 
Mie pia nasema hapana,mpaka tupate kadhi kwanza.

Hiyo Mahakama ya Kadhi mnayoitaka nyinyi ni tofauti na anayoijua Kikwete? Keshasema anzisheni tu na serikali haiwezi kuwaingilia. Sasa mnataka kipi tena?

Inawezekana hata wengine hawajui hiyo Mahakama ya Kadhi itakuja kufanya lipi hasa, lakini bado wanapiga yowe kwamba ije tu.
 
Rais Mtarajiwa wewe unaamka kwenye ndoto na kuanza kuulizia mambo ya ibada. Kwanza inawezekana hata ibadani hukwenda. Nakushauri usome Katiba Inayopendekezwa na uipigie kura ya ndiyo. Nafahamu saa nyingine huwa unakuwa muelewa. Kila kheri. Ukipata ugumu katika interpretation ya vifungu vya Katiba tafadhali tuwasiliane kwani nimegundua wewe ni mtu unayetaka kujifunza. Karibu sana.

teh...teh...teh.. na hii ni i/d yako ya tatu humu jf dada Claudiaeliakim kweli njia ya muongo fupi sana, hongera mtu 3-in-1 unayeshabikia usichokijua, hakika mwaka huu utaisoma namba na kujifunza nini maana halisi ya uzalendo!
 
Last edited by a moderator:
10402013_415267728640955_3246074672258301477_n.jpg
 
utafiti uliofanyika humu jf unaonyesha kwamba wewe na dada yako Claudiaeliakim mnashabikia msichokijua, yamkini ninyi ni mapacha, ndugu wa damu au mtu mmoja mwenye i/d mbili, rais wa jmt kasalimu amri kwa tamko la maaskofu sembuse nyie watu wawili (2-in-1)?


President elect umekwisha na umefirisika kifikra,unachokifanya wewe ni kutaka kunivunja nguvu nisiendelee kuchangia,kwa taarifa yako umekwama,hujielewi kwa akili zako za kushikiwa umeanza kufananisha watu mweee aka babu wee unikome na tena usinidharirishe kwa kunifananisha na hao unaowawaza wewe.
 
teh...teh...teh.. na hii ni i/d yako ya tatu humu jf dada Claudiaeliakim kweli njia ya muongo fupi sana, hongera mtu 3-in-1 unayeshabikia usichokijua, hakika mwaka huu utaisoma namba na kujifunza nini maana halisi ya uzalendo!

Wewe ndio utaisoma namba hunipati ng'ooo!usilazimishe mambo tena unikome kawaambie hao hao uliowazoea na kama unafikiri utanipata kwa kunitega umeliwa mie siwezi kuona unashabikia mishuzi yako nikakuacha nchi ni yetu sote lazima tuheshimu kama vipi kesho tuonane.
 
Hii nini sasa unataka tuipigie kura?hiyo kaipitisheni kwenye nyumba zenu za ibada mimi nasubiri katiba pendekezwa nipige kura na hicho kipengele chako hakipo endelea kusubiri.
No Kadhi Court is the bottom line.
 
Huyo Eliakim kama unamtaka si umweleze awe demu wako naona unamtajayaja sana, hatuko kushabikia majina ya watu hapa wewe na yeye mna matatizo


Ooohooo jamani nyie tuheshimiane ha ha ha mie najiheshimu na humu sina haja ya kumtaka huyo Elect atanipotezea muda wangu nmuona kama mwana JF mwenzangu ila akiniboa tu namwaga mboga, duuuu nyie mmewaza mbali ha ha ha ha acheni bhana.
 
Nimesikia Rais wetu Mhe Kikwete akisema akisema, serikali haitaanzisha Mahakama ya Kadhi na kwamba ni Jukumu la waislamu wenyewe kuianzisha na kuihudimia.

Waislamu tumekuwa tukiburuzwa na kugaragazwa katika mambo ya msingi hasa pale wenzetu wa dini nyingine wanapoweka ngumu.

Tuliomba sensa iwe na kipengele cha dini, tukashindwa baada ya usaliti wa BAKWATA. 2005 tulidanganywa ktk ilani ya CCM, tukawachagua. Lakini Hola.

Mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ulipoanza, tukaona ndipo pa kupatia Mahakama ya Kadhi. Rasimu ya Kwanza na ya pili, zikaja bila ya Mahakama ya kadhi.

Tulipokuja juu, Waziri Mkuu akaahidi Mswaada wa Mahakama ya Kadhi utapelekwa Bungeni februari. Kiini macho kikafanyika eti kupata ridhaa na muafaka na ndugu zetu wa upande wa pili.

Na katika Mchakato wa kuurudisha bungeni mswaada April hii, viongozi wa wenzetu wametia munda. Hawaitaki Mahakama ya Kadhi. Wamehamasisha waumini wao, wajiandikishe kwa wingi na muda ukifika, wapige kura ya HAPANA kwa Katiba Pendekezwa.

Serikali imeogopa nguvu ya wenzetu wakristo. Imesema HAPANA kwa Mahakama ya kadhi, licha ya Tafiti nyingi kuonesha, Mahakama ya kadhi haina madhara (Waziri Mkuu, Waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu) waliuthibitishia Umma.

Kutokana na kudharauliwa na kupuuzwa kunakofanywa na serikali mara kwa mara dhidi ya waislamu na Uislamu, binafsi nitapiga kura ya HAPANA KWA KATIBA PENDEKEZWA.

Ewe Muislamu na ndugu zangu wa dini nyingine, tuungane tupige kura ya HAPANA kwa katiba pendekezwa






Asante JK kwa kulionahilo shughuli za dini zibakie kuendeshwa na dini husika, mie sitaki kodi yangu ninayolipa itumike kugharamia mahakama ya kadhi.
 
Nimesikia Rais wetu Mhe Kikwete akisema akisema, serikali haitaanzisha Mahakama ya Kadhi na kwamba ni Jukumu la waislamu wenyewe kuianzisha na kuihudimia. Waislamu tumekuwa tukiburuzwa na kugaragazwa katika mambo ya msingi hasa pale wenzetu wa dini nyingine wanapoweka ngumu. Tuliomba sensa iwe na kipengele cha dini, tukashindwa baada ya usaliti wa BAKWATA. 2005 tulidanganywa ktk ilani ya CCM, tukawachagua. Lakini Hola. Mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ulipoanza, tukaona ndipo pa kupatia Mahakama ya Kadhi. Rasimu ya Kwanza na ya pili, zikaja bila ya Mahakama ya kadhi. Tulipokuja juu, Waziri Mkuu akaahidi Mswaada wa Mahakama ya Kadhi utapelekwa Bungeni februari. Kiini macho kikafanyika eti kupata ridhaa na muafaka na ndugu zetu wa upande wa pili. Na katika Mchakato wa kuurudisha bungeni mswaada April hii, viongozi wa wenzetu wametia munda. Hawaitaki Mahakama ya Kadhi. Wamehamasisha waumini wao, wajiandikishe kwa wingi na muda ukifika, wapige kura ya HAPANA kwa Katiba Pendekezwa. Serikali imeogopa nguvu ya wenzetu wakristo. Imesema HAPANA kwa Mahakama ya kadhi, licha ya Tafiti nyingi kuonesha, Mahakama ya kadhi haina madhara (Waziri Mkuu, Waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu) waliuthibitishia Umma. Kutokana na kudharauliwa na kupuuzwa kunakofanywa na serikali mara kwa mara dhidi ya waislamu na Uislamu, binafsi nitapiga kura ya HAPANA KWA KATIBA PENDEKEZWA. Ewe Muislamu na ndugu zangu wa dini nyingine, tuungane tupige kura ya HAPANA kwa katiba pendekezwa
Ni kweli kwamba kila mtu ana uhuru wa maoni,ila katika hili naona sio sahihi hata kidogo kuchanganya maslahi ya imani yako na maswala ya kitaifa kwa kuwa swala la katiba halina dini ni la watanzania wote,sasa unapotumia dini yako kusema hiki na kile hakijawekwa kwenye katiba pendekezwa na kina maslahi katika imani yako nadhani utakuea umepotoka ndg yangu kwa sababu hebu fikiria kila mtu kwa imani yake aseme kile chenye maslahi kwake na kiandikwe kwenye katiba,itakuwa katiba au kitu gani ?nadhani ujiunge na walio wengi na ukubaliane tu na katiba inayopendekezwa kwa kuwa imetokana na wananchi wenyewe,tafadhali sana kama una ajenda nyingine ndg yangu sema ila hilo watanzania hawaliungi mkono na hawataliunga mkono kamwe
 
Back
Top Bottom