Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Nilimuahidi mfano whiteskunk lakini nadhani utaleta mwanga pia kwa akina Kiranga na masdinero masproblemas mfano wenyewe ni;

Imagine dunia au ulimwengu mwingine ambapo wao kutokana na miale ya jua lao kuwa hafifu [au kuwa na spectrum nyembamba] wanaona vitu kama gizanigizani tu kwa hiyo wanaonaga vitu bila rangi yaani black&white tu.

Bahati nzuri mtu kutoka duniani akafanikiwa kuwatembelea akafika akataka kuwaelekeza hii idea ya 'rangi' atawaelekezaje wamuelewe? Akiwaambia kuna nyekundu/bluu/kijani watamuona anazingua tu. Hata kama yeye anaweza kuwa anaziona kihafifuhafifu kutokana na kuishi sana duniani. Kwa watu wa kule ambao hawajawahi kuona rangi atapata tabu tu. Wabishi watakataa tu na akizidi watampiga mawe. Na wanasayansi wao wenye nia njema ya kuthibitisha watamtaka awapelekee ushahidi na hayo maelezo yatoshe katika black and white[B&W] tu! Imagine kuielezea nyekundu katika lugha yenye B&W tu. Huyu jamaa akirudi duniani akachukua maua mekundu na ya njano akapeleka akiyafikisha wakayatazama watacheka halafu watasema. Hii unayosema nyekundu ni kwamba ina weusi zaidi ya hili unalosema la njano hakuna cha rangi wala nini hapo. Na hilo neno njano na nyekundu umetunga tu.

Ili aweze labda amchukue mtu wa huko amlete duniani azione rangi halafu akirudi naye anaweza kuanza kuappreciate idea ya rangi na kuwaelekeza wengine. Sio lazima aje duniani lakini akiwa na imani akakubali kujifunza na akaelewa anaweza naye kuappreciate idea ya rangi. Ndugu zangu huu ndio ugumu wa kuleta uthibitisho wa uwepo wa mambo ya kiroho kwa watu ambao wanachukulia haya material ndio halisi na ndio kitu pekee kilichopo, black and white.
Nikikwambia kuna rangi ambayo haipo utakubali ipo?

Mfano wako wa rangi hautusaidii kitu.

Kwa sababu unatuambia kuna uwezekano wa kuwepo vitu tusivyovijua.

Hautuambii jinsi ya kutenganisha vitu ambavyo vipo kiuhalisia na vile ambavyo ni vya kufikirika tu havipo nje ya ulimwengu wa kufikirika tu.
 
Safi sasaa ni hivi:

Mimi ninasema kuwa lugha yako ni material kwa sababu hata maswali unayouliza yanajionesha na mambo unavyoyaona inajionesha mfano; Mfano unaposema 'wazo ni kitu kilichopo na mimi nimeeleza namna ya kulipima'! inashangaza maana mimi binafsi nilichowahi kutype ni nimeassert kwamba wazo ni kitu kilichopo na kuonesha namna ya kulihisi.

Kupima ni kwa ajili ya vitu material vitu vya kimawazo havipimiki, ni hivyo viko lakini hilo halituzuii kutuathiri, kuvitumia, kuvienjoi na kuviishi au kuvifuata. Hauhitaji kumleta Mungu au roho katika material ndio umuishi. Tunauishi ufalme wa Mungu katika hali hiyohiyo ya kiroho.

Sasa fanya zoezi moja, kama siku zote umekuwa ni wewe unayewaza mawazo yako, au kutumia mawazo ya wengine. Basi jaribu kuyakinisha wazo ambalo sio la mtu bali hilo wazo liwe lipo kama lilivyo na linajiendesha na kutuendesha. Au fikiria wazo la ulimwengu mzima wote. Kwanza imeandikwa tutamuabudu katika roho na kweli. Kwa hiyo Kiranga hata kama ukibaki kusema ni hadithi tu elewa kwamba ni hadithi ambayo unaweza kuiishi maana ipo.
 
Hautuambii jinsi ya kutenganisha vitu ambavyo vipo kiuhalisia na vile ambavyo ni vya kufikirika tu havipo nje ya ulimwengu wa kufikirika tu.
Hii sentensi inaonesha wazi kuwa tafsiri yako ya uhalisia bado ipo limited na material tu. Ukiongeza msamiati utakuta kuna vitu vinavyoonekana na visivyoonekana na vyote ni halisi.

Najua hata hii vinavyoonekana na visivyoonekana bado utaitafsiri kimaterial🤦‍♂️😂🤣. Nakazia visivyoonekana simaanishi upepo, au oksijeni hapana. Namaanisha vitu kama wazo, hisia
 
Nimeuliza hivyo kujibu hoja ya kuwa kila kitu kina lengo mahsusi kwa sisi binadamu. Sio kweli. Kuna mambo hutokea bila kupangwa na kubadili kabisa kila kitu. Mtu mwenye nia njema hatasimama na kusema hizo turning points ambazo zingedondokea upande wowote na kuleta matokeo tofauti nazo zilipangwa kwa malengo fulani. Unpredictability unaipeleka wapi? Nina imani umepitia chaos theory na suala la butterfly effect.
Tukiifuata chaos theory vizuri itabidi hadi leo kuwe tu na vumbivumbi mchanganyiko/supu ya elementi badala ya uhai. Inahitajika akili ili kupangilia vitu katika hali inayoweza kuleta sense. Vinginevyo kukiwa na kani tu bila akili mwisho wa siku ni kusambaratika kwa kila kitu na kujichanganyachanganya bila maana yoyote. Kanuni za thermodynamics zinasema hivyo.

Kama wewe upo leo na unasema kuwa vitu vyote havina maana ina maana tayari umeshakubali kwamba unachokisema ndio kinaleta maana. Kwa hiyo 'vya maana' tayari vinakuwa vipo na visivyo na maana vinakuwa vipo. Tofauti na hivyo basi wewe mwenyewe unayesema havina maana ndio haupo jambo ambalo linakuwa halina maana tena kwa sababu tunakubaliana kwamba wewe upo na upo unabisha hapo😂🤣🤣.

Ndugu yangu logically ukianza na premise ya chaos itabidi uende na chaos mpaka mwisho ambapo ndio unarealize hapana bwana hakuna cha chaos wala unpredictability bali kuna mchango wa effect nyingi nyingi zenye malengo tofautitofauti. The fact that only living things resist natural tendency to dissociate proves that there is something in the living that the non living do not have.
 
Hiyo nimetumia kama mfano tu wa vita na matatizo mengi ambayo binadamu anayapata hapa duniani ila Mungu mwenye huruma na upendo kakaa kimya bila hata kuingilia.
Ulitaka atoe msaada wa jeshi au silaha? Mungu hahusiki na maovu hapa duniani...Binadamu alitaka ayajue mabaya hamna haja ya kulalamika.
 
Tukiifuata chaos theory vizuri itabidi hadi leo kuwe tu na vumbivumbi mchanganyiko/supu ya elementi badala ya uhai. Inahitajika akili ili kupangilia vitu katika hali inayoweza kuleta sense. Vinginevyo kukiwa na kani tu bila akili mwisho wa siku ni kusambaratika kwa kila kitu na kujichanganyachanganya bila maana yoyote. Kanuni za thermodynamics zinasema hivyo.

Kama wewe upo leo na unasema kuwa vitu vyote havina maana ina maana tayari umeshakubali kwamba unachokisema ndio kinaleta maana. Kwa hiyo 'vya maana' tayari vinakuwa vipo na visivyo na maana vinakuwa vipo. Tofauti na hivyo basi wewe mwenyewe unayesema havina maana ndio haupo jambo ambalo linakuwa halina maana tena kwa sababu tunakubaliana kwamba wewe upo na upo unabisha hapo[emoji23][emoji1787][emoji1787].

Ndugu yangu logically ukianza na premise ya chaos itabidi uende na chaos mpaka mwisho ambapo ndio unarealize hapana bwana hakuna cha chaos wala unpredictability bali kuna mchango wa effect nyingi nyingi zenye malengo tofautitofauti. The fact that only living things resist natural tendency to dissociate proves that there is something in the living that the non living do not have.
Kwenda na chaos mpaka mwisho? Hauko serious Uhakika Bro. Kila unachoona kina order sasa kilianza kwenye mvurugano. Chaos ni sehemu ya muendelezo wa vitu vyote. Case in point, ukielewa vyanzo na matokeo ya hizo chaos zinazoibuka mida fulani utaona hamna nafasi ya mkono wa nje zaidi ya vilivyopo ulimwenguni.
 
Sayansi na udadisi haujawahi kuwa rafiki wa mambo ya kiimani ambayo ndio msingi wa dhana "roho". Mtaalamu wa baiolojia lazima aelewe kujitambua, hulka, mawazo, mtazamo, utu na tabia ya binadamu vyote ni matokeo ya muundo wa ubongo na si kitu kingine.
Sayansi imeendelea sana kutokana na kuzidadisi hizo imani na filosofi zilizokuwapo, vyote imaginations na ideas za kutungatunga zimekuwa stimulant kubwa sana za scientific progress.

Mfano hiyo dhana yako ya hayo mambo ya 'kiutambuzi' kuwa ni matokeo ya muundo wa ubongo hata sasa haijastahimili chunguzi za kisayansi. Kuendelea kuishikilia kama ndiyo sababu pekee ya personality zetu nayo inakuwa ni imani yabhuyo mwanasayansi binafsi. Binafsi sipati shida kwa kuwa mchango wa umbo na kemikali vya ubongo pamoja na nafsi/roho/fikra vyote ninavitambua. I regard this as a broader view of reality.
 
Kwenda na chaos mpaka mwisho? Hauko serious Uhakika Bro. Kila unachoona kina order sasa kilianza kwenye mvurugano. Chaos ni sehemu ya muendelezo wa vitu vyote. Case in point, ukielewa vyanzo na matokeo ya hizo chaos zinazoibuka mida fulani utaona hamna nafasi ya mkono wa nje zaidi ya vilivyopo ulimwenguni.
Seriously? chaos itengeneze kitu ambacho kinamake sense halafu kisha tena kiharibike baada ya hapo. Sasa hiyo order ilitengenezwa kwa ajili ya nini? Tena order yenyewe sio ya kitoto order inayotokeza hadi akina sisi [mimi na wewe] tunaofikiria na kujadili. Braza ebu jiappreciate kwanza utata ulionao ndipo uanze kumtafuta Mungu mtata zaidi yako

Mimi nitakubali kuwa kweli hapo mwanzo wa dunia kulikuwa na chaos tu hadi 'akili' fulani ya juu ilipoamua kuzipanga hizo fujo katika mipangilio yenye potential ya kutokeza maana huko mbele. Akili ilihusika na kila kiumbe anayeishi anayo share ya hii akili. Akikufa anakuwa amepoteza akili kwa hiyo chaos ndo inatake over tena.

Swali kama ubongo ndio chanzo cha utambuzi, na umaana unaweza kuniambia tumboni wakati bado kiumbe kinatokezwa kutoka katika bonge la seli, kabla ya ubongo kutengenezwa ni kipi kinakuwa kinaelekeza hayo matukio yafanyike? Ivi bro nikisema kuwa hapo ni nafsi ya mtoto ipo bize kujiandalia mazingira ya kuinteract na kuiexperience dunia na mazingira una maoni gani?.

Mazingira ya dunia yatainteract na mwili, mwili utainteract na ubongo, ubongo utainteract na akili na akili itainteract na roho so roho itakuwa imeiexperience dunia kupitia mlolongo wooote huo. Sina hakika kama roho na nafsi vipo steji moja lakini kuna uwezekano roho yupo juu, ni baba yake na nafsi.
 
Sayansi imeendelea sana kutokana na kuzidadisi hizo imani na filosofi zilizokuwapo, vyote imaginations na ideas za kutungatunga zimekuwa stimulant kubwa sana za scientific progress.

Mfano hiyo dhana yako ya hayo mambo ya 'kiutambuzi' kuwa ni matokeo ya muundo wa ubongo hata sasa haijastahimili chunguzi za kisayansi. Kuendelea kuishikilia kama ndiyo sababu pekee ya personality zetu nayo inakuwa ni imani yabhuyo mwanasayansi binafsi. Binafsi sipati shida kwa kuwa mchango wa umbo na kemikali vya ubongo pamoja na nafsi/roho/fikra vyote ninavitambua. I regard this as a broader view of reality.
Roho [emoji28] dah... kuhusu muundo wa ubongo sio imani, imeshathibitishwa! Mwanabailojia anayebaki na mitazamo ya kizamani kuhusu vitu vilivyo wazi sasahivi lazima aendelee kushikilia imani za roho na vishirikishi vyake potofu.
 
Seriously? chaos itengeneze kitu ambacho kinamake sense halafu kisha tena kiharibike baada ya hapo. Sasa hiyo order ilitengenezwa kwa ajili ya nini? Tena order yenyewe sio ya kitoto order inayotokeza hadi akina sisi [mimi na wewe] tunaofikiria na kujadili. Braza ebu jiappreciate kwanza utata ulionao ndipo uanze kumtafuta Mungu mtata zaidi yako

Mimi nitakubali kuwa kweli hapo mwanzo wa dunia kulikuwa na chaos tu hadi 'akili' fulani ya juu ilipoamua kuzipanga hizo fujo katika mipangilio yenye potential ya kutokeza maana huko mbele. Akili ilihusika na kila kiumbe anayeishi anayo share ya hii akili. Akikufa anakuwa amepoteza akili kwa hiyo chaos ndo inatake over tena.

Swali kama ubongo ndio chanzo cha utambuzi, na umaana unaweza kuniambia tumboni wakati bado kiumbe kinatokezwa kutoka katika bonge la seli, kabla ya ubongo kutengenezwa ni kipi kinakuwa kinaelekeza hayo matukio yafanyike? Ivi bro nikisema kuwa hapo ni nafsi ya mtoto ipo bize kujiandalia mazingira ya kuinteract na kuiexperience dunia na mazingira una maoni gani?.

Mazingira ya dunia yatainteract na mwili, mwili utainteract na ubongo, ubongo utainteract na akili na akili itainteract na roho so roho itakuwa imeiexperience dunia kupitia mlolongo wooote huo. Sina hakika kama roho na nafsi vipo steji moja lakini kuna uwezekano roho yupo juu, ni baba yake na nafsi.
Kinachofanya kazi ni genes. Dna za wazazi husika zinakuwa na kibarua cha kuwasha sifa za mtoto ajae. Hizo huelekeza kila kitu. Awe na rangi gani, jinsia ipi, viungo vikae wapi n.k.

Ni hizi genes ndio chanzo cha uhai uonavyo leo. Kila kiumbe hai kina genes. Kapitie "genome project" na matokeo yake yaliyofanikisha kuleta catalog ya viumbe vyote dunian na utambuzi wa genes kwa kila kiumbe kilichofanyiwa utafiti... mwanabaiolojia unatoa wapi roho hapa? Yai tangu liko kwenye mirija au mbegu kwenye mmea hai tayari lina chembe za uhai. Uhai upo hata pale macho yetu yasipoweza kuona. Hakuna nafasi ya kitu unachodai mungu.

Kuhusu chaos usishangae inawezaje kuleta order. Naomba ufatilie zaidi. Utagundua dhana ya chochote unachoona kiko complex lazima kiumbwe na kitu kingine complex zaidi au vinginevyo ni dhaifu mno.

Bado najiuliza mwanabaiolojia wa kweli unaaminije wizardry ya eti tumeumbwa na mungu huku ukijua kabisa sisi tumetokana na mabadiliko ya muda mrefu. Hata leo ukiangalia mwili wa binadamu bado una mapungufu na vitu vingi visivyohitajika au kuleta madhara. Chukulia mfano mdogo tu shepu na utendaji wa jicho. Mwanga unapata tabu kuleta fahamu kwa sababu ya mpangilio mbovu wa mishipa na lens. Hakuna uumbaji hapa. Muumbaji asingefungafunga mishipa hovyo kwenye viumbe. Design ya viumbe vingi ina shida kibao. Utagundua huwezi kulaumu sana kwa sababu evolution ni utaratibu unaochukua muda mrefu ili ku fine tune viumbe through natural selection.

Haya mambo sio rahisi. Tunaendelea kujifunza kwa shida. Vingi kuelewa sio rahisi kwa sababu ile ile ya namna bongo zetu zilivyo. Zimeundwa kustahimili maisha fulani ambayo sio ya kufikiria sana. Ndio maana mazoezi ya kufikiria sana, au kusoma, au logic yanatupiga chenga wengi wetu. Simple explanations ndio favorite input ya bongo zetu. Lakini uhalisia sio hivyo. Kusema tu tumeumbwa na mungu sio suluhisho hata kidogo kwa vile hiyo kauli haitoi mantiki wala majibu kamili. Sana sana utaongezea uongo kusapoti dhana hiyo isiyo na mashiko yenye uhakika.
 
Kinachofanya kazi ni genes. Dna za wazazi husika zinakuwa na kibarua cha kuwasha sifa za mtoto ajae. Hizo huelekeza kila kitu. Awe na rangi gani, jinsia ipi, viungo vikae wapi n.k.

Ni hizi genes ndio chanzo cha uhai uonavyo leo. Kila kiumbe hai kina genes. Kapitie "genome project" na matokeo yake yaliyofanikisha kuleta catalog ya viumbe vyote dunian na utambuzi wa genes kwa kila kiumbe kilichofanyiwa utafiti... mwanabaiolojia unatoa wapi roho hapa? Yai tangu liko kwenye mirija au mbegu kwenye mmea hai tayari lina chembe za uhai. Uhai upo hata pale macho yetu yasipoweza kuona. Hakuna nafasi ya kitu unachodai mungu.
Moja kati ya kitu kulichosisimua katika genome project ni kukuta kuwa mpunga/mchele uko na vinasaba vingi kuliko binadamu! Je mpunga ni mtata kuliko sisi? Kwamba sisi tunajiona tu ila aliyeendelea ni mpunga na sio sisi?

Ikiwa genes ndiyo zinazoamua kiumbe aweje mbona ziko nyingi sana na hatupati sifa zote bila mpangilio? mfano nimerithi vinasaba vya ufupi kwa mama na urefu kwa baba kwa nini nisiwe mrefu na mfupi [sielewi hata ndo nitakuwajewaje!?] bali nichague kuwa aidha mrefu au mfupi. Nikisema kuwa hiyo ni uthibitisho kuwa busara/akili tayari imeshaanza kuchagua mema na yasiyo mema kwake utasemaje? Mfano mwingine watoto wazaliwe na wazazi wanene na watoto wengine wawe wanene wengine wembamba. Nikuibie siri ukiamua kuchunguza hao watoto namna wanavyofikiri [personality zao] utagundua mchango wa nafsi binafsi ya mtu, mawazo binafsi ya huyo mtoto ulivyo mkubwa kuliko hata hizo genes. Vinasaba vinaleta kila kitu [chaos] ni mtu ndiyo anayejichagulia vya kufata na vya kuacha [order]. Natumai umeshapitiapitia watu wa epigenetics. Watu wa epigenetics wanajaribu kui'materialize' idea kufanya kama kuicrystalize. Lakini kama ulishasikiaga 'mind over matter' huo ni mfano mzuri haya mawazo tunayokuwa nayo tunayoyaishi kila siku ndiyo yanaongoza kinasaba gani kifunguliwe kipi kifungwe kama hujan'gamua
 
Hata leo ukiangalia mwili wa binadamu bado una mapungufu na vitu vingi visivyohitajika au kuleta madhara. Chukulia mfano mdogo tu shepu na utendaji wa jicho. Mwanga unapata tabu kuleta fahamu kwa sababu ya mpangilio mbovu wa mishipa na lens. Hakuna uumbaji hapa. Muumbaji asingefungafunga mishipa hovyo kwenye viumbe. Design ya viumbe vingi ina shida kibao. Utagundua huwezi kulaumu sana kwa sababu evolution ni utaratibu unaochukua muda mrefu ili ku fine tune viumbe through natural selection.
Daah! hiviii?! basi jaribu kidogo kuwa na ule ukubali ushukurani kwa vitu vilivyopo. Jicho kwa hatua lilipofikia na kazi kubwa linayofanya linastahili pongezi. Kung'an'gana tu na kuliboresha jicho bila kujali mifumo mingine utakuwa unafanya kazi sawa na kupakua muvi kali 8k UHD halafu una TV ya chogo. Kipindi tupo primitive [hata sasa] ilitosha sana tukubali. Jicho liwe na kasi zaidi liingize taarifa zaidi likaone kakitu saizi ya bakteria na saizi ya mlima kwa wakati mmoja! Lione mbalii na hapa karibu kwa wakati mmoja halafu lipeleke kwenye ubongo. Unataka ubongo uzidiwe upigwe shoti au? na hata kama utaweza kuzichakata hizo taarifa then what for? Anyway tunazidi kuboresha kadri mambo yanavyobadilika sikatai. Sikatai evolution mimi. Kila siku ninaona chura akitoka kiluwiluwi hadi chura mzima -ni sehemu ya dizaini inayofanya kazi vizuri mno.

Hata kama evolution bado inaendelea itaendelea kwa akili sio tu kukimbilia kisicho na manufaa yoyote. Na nikwambie kitu tu; unapokubali kwamba kuna mapungufu na tupo katika mchakato wa kuuelekea ukamilifu ujue kisirisiri unamtukuza Mungu aliye mkamilifu katika vyote!🤭.
 
Moja kati ya kitu kulichosisimua katika genome project ni kukuta kuwa mpunga/mchele uko na vinasaba vingi kuliko binadamu! Je mpunga ni mtata kuliko sisi? Kwamba sisi tunajiona tu ila aliyeendelea ni mpunga na sio sisi?

Ikiwa genes ndiyo zinazoamua kiumbe aweje mbona ziko nyingi sana na hatupati sifa zote bila mpangilio? mfano nimerithi vinasaba vya ufupi kwa mama na urefu kwa baba kwa nini nisiwe mrefu na mfupi [sielewi hata ndo nitakuwajewaje!?] bali nichague kuwa aidha mrefu au mfupi. Nikisema kuwa hiyo ni uthibitisho kuwa busara/akili tayari imeshaanza kuchagua mema na yasiyo mema kwake utasemaje? Mfano mwingine watoto wazaliwe na wazazi wanene na watoto wengine wawe wanene wengine wembamba. Nikuibie siri ukiamua kuchunguza hao watoto namna wanavyofikiri [personality zao] utagundua mchango wa nafsi binafsi ya mtu, mawazo binafsi ya huyo mtoto ulivyo mkubwa kuliko hata hizo genes. Vinasaba vinaleta kila kitu [chaos] ni mtu ndiyo anayejichagulia vya kufata na vya kuacha [order]. Natumai umeshapitiapitia watu wa epigenetics. Watu wa epigenetics wanajaribu kui'materialize' idea kufanya kama kuicrystalize. Lakini kama ulishasikiaga 'mind over matter' huo ni mfano mzuri haya mawazo tunayokuwa nayo tunayoyaishi kila siku ndiyo yanaongoza kinasaba gani kifunguliwe kipi kifungwe kama hujan'gamua
Sielewi una maana gani kwa utata lakini sio ajabu kwa mimea kuwa na complications zaidi ya sisi. Sisi na wanyama wengne hatujizalishii chakula wenyewe. Tunategemea vyanzo vya nje. Kwa msingi huo lazima tuwe tofauti sana na mimea. Sisi hatuwezi hata kuvuna nguvu ya jua kama mimea!

Genes ziko nyingi sana lakini huwezi kuactivate zote kwa kiumbe mmoja. Kitakufa au kukosa balance. Dna huongoza sifa zipi ziwake na zipi zisizi... ni kama kwenye suala la genetics mtoto ana 50% ya kupata aina ya sifa za mzazi mmoja, 25% ya kila bibi na babu,12.5% ya za kila baba na mama wa mabibi na mababu n.k.... kila sehemu mtoto akiwa tumboni anaokoteza chembe, sio zote. Kipimo sio akili wala ufahamu (bado hamna hivyo vitu kwa hatua hii) bali ni vimelea tu ndio vinavyoshindania kubebwa. Ikishinda kwenye urefu, itapoteza kwenye rangi n.k., n.k.... akili inajengwa na mazingira ya nje, mtu azaliwi tu Akawa na akili tayari!

"Mind over matter" ni fiction. Hakuna memory isiyo na physical attributes whilst Kuna mindless matter, au sio sawa? Unaweza kupata Jerusalem la kichwa ukabaki kama kabichi. Mindless lakin alive. Hebu waza akili ni nini kama sio kupokea, kuelewa, kuhifadhi, na hata kuendeleza ufahamu. Utapokeaje tarifa bila milango ya fahamu(physical)‽ utaelewaje bila ubongo kuwa sawa(physical)? Utahifadhi wapi kumbukumbu? Matter is the grand daddy of mind. Tujaribu kuweka imani pembeni na tukazane na taaluma. Tusiingie kwenye zone ya udadisi na conclusions za kiimani mfukoni, tutakuwa tunajizunguka tu. This analogy is misleading: "Kwa vile hiki kipo basi Kuna kingine kilichofanya uundaji" Madini ardhini yanaundwa na kiumbe gani? Mimea ilivyo imeundwa na nani? Sio mungu. Chukua hata mifano midogo ya uumbaji wa binadamu ambao wengi wetu huchukulia kama vilikuwepo tu kwa uchache wanyama tunaokula, mimea tunayolima... ng'ombe, kuku, mbuzi, mahindi, ngano, mchele n.k... Ukihoji vizuri kibaiolojia au kwa matawi mengine ya sayansi japo kwa uchache utagundua hamna nafasi ya hizo imani za mungu. Jaribu tu.
 
Daah! hiviii?! basi jaribu kidogo kuwa na ule ukubali ushukurani kwa vitu vilivyopo. Jicho kwa hatua lilipofikia na kazi kubwa linayofanya linastahili pongezi. Kung'an'gana tu na kuliboresha jicho bila kujali mifumo mingine utakuwa unafanya kazi sawa na kupakua muvi kali 8k UHD halafu una TV ya chogo. Kipindi tupo primitive [hata sasa] ilitosha sana tukubali. Jicho liwe na kasi zaidi liingize taarifa zaidi likaone kakitu saizi ya bakteria na saizi ya mlima kwa wakati mmoja! Lione mbalii na hapa karibu kwa wakati mmoja halafu lipeleke kwenye ubongo. Unataka ubongo uzidiwe upigwe shoti au? na hata kama utaweza kuzichakata hizo taarifa then what for? Anyway tunazidi kuboresha kadri mambo yanavyobadilika sikatai. Sikatai evolution mimi. Kila siku ninaona chura akitoka kiluwiluwi hadi chura mzima -ni sehemu ya dizaini inayofanya kazi vizuri mno.

Hata kama evolution bado inaendelea itaendelea kwa akili sio tu kukimbilia kisicho na manufaa yoyote. Na nikwambie kitu tu; unapokubali kwamba kuna mapungufu na tupo katika mchakato wa kuuelekea ukamilifu ujue kisirisiri unamtukuza Mungu aliye mkamilifu katika vyote![emoji2960].
Nimecheka sana [emoji1]hiyo shoti kwenye ubongo. Mbona kitu kinachotokea au seizures huwa ni nini? Kimsingi ubongo unaweza sana kupokea taarifa zaidi, tatizo liko kwenye jicho. Huyo mungu mnasingizia kaunda mfumo hovyo hivi? Let's be serious. Hii ni kazi ya muundo usio na consciousness wala plan yoyote. There's is no meaning to life in beliefs. Tuhoji, tusome, tujadili tuupate ukweli. Sio hizi neno nyepesi kwamba tuliumbwa. Tusipojua tukiri hatujui. Sio kuanza kuchonga uongo.
 
Daah! hiviii?! basi jaribu kidogo kuwa na ule ukubali ushukurani kwa vitu vilivyopo. Jicho kwa hatua lilipofikia na kazi kubwa linayofanya linastahili pongezi. Kung'an'gana tu na kuliboresha jicho bila kujali mifumo mingine utakuwa unafanya kazi sawa na kupakua muvi kali 8k UHD halafu una TV ya chogo. Kipindi tupo primitive [hata sasa] ilitosha sana tukubali. Jicho liwe na kasi zaidi liingize taarifa zaidi likaone kakitu saizi ya bakteria na saizi ya mlima kwa wakati mmoja! Lione mbalii na hapa karibu kwa wakati mmoja halafu lipeleke kwenye ubongo. Unataka ubongo uzidiwe upigwe shoti au? na hata kama utaweza kuzichakata hizo taarifa then what for? Anyway tunazidi kuboresha kadri mambo yanavyobadilika sikatai. Sikatai evolution mimi. Kila siku ninaona chura akitoka kiluwiluwi hadi chura mzima -ni sehemu ya dizaini inayofanya kazi vizuri mno.

Hata kama evolution bado inaendelea itaendelea kwa akili sio tu kukimbilia kisicho na manufaa yoyote. Na nikwambie kitu tu; unapokubali kwamba kuna mapungufu na tupo katika mchakato wa kuuelekea ukamilifu ujue kisirisiri unamtukuza Mungu aliye mkamilifu katika vyote![emoji2960].
Paragraph ya mwisho umeandika kwa misingi ipi? Elezea huo ukamilifu kwa vigezo vya msingi.
 
Paragraph ya mwisho umeandika kwa misingi ipi? Elezea huo ukamilifu kwa vigezo vya msingi.
Nimezungumzia kwamba, evolution inaendelea kwa malengo fulani ni tukio linaloongozwa na akili kubwa sio fujofujo tu.

Kama jicho kwa sasa halijatimia basi linabadilika kuuelekea utimilifu zaidi ili kuweza kuchakata vitu visivyoshikika zaidi. Mwili, ubongo na viungo vyote na jamii kwa ujumla huandaliwa kabla ya kupewa jukumu kubwa zaidi vililoletwa kufanya.

Akili nayo inabadilika kuuelekea ukamilifu pia, kila siku kadri unavyopambana na changamoto/taarifa mpya unajijenga. Kwenye akili hapo fikiria mwanzoni ilikuwa labda na uwezo wa kutambua milima, mawe na wanyama wengine [primitive]. Baadaye ikaanza kutambua na kuvalue vitu kama serikali, jamii na ustaarabu, baadaye ikiendelea zaidi utaona inatambua na kuvipa umuhimu wa kwanza vitu vya kiroho. Evolution inaendelea!
 
"Mind over matter" ni fiction. Hakuna memory isiyo na physical attributes whilst Kuna mindless matter, au sio sawa? Unaweza kupata Jerusalem la kichwa ukabaki kama kabichi. Mindless lakin alive. Hebu waza akili ni nini kama sio kupokea, kuelewa, kuhifadhi, na hata kuendeleza ufahamu. Utapokeaje tarifa bila milango ya fahamu(physical)‽ utaelewaje bila ubongo kuwa sawa(physical)? Utahifadhi wapi kumbukumbu? Matter is the grand daddy of mind. Tujaribu kuweka imani pembeni na tukazane na taaluma. Tusiingie kwenye zone ya udadisi na conclusions za kiimani mfukoni, tutakuwa tunajizunguka tu. This analogy is misleading: "Kwa vile hiki kipo basi Kuna kingine kilichofanya uundaji" Madini ardhini yanaundwa na kiumbe gani? Mimea ilivyo imeundwa na nani? Sio mungu. Chukua hata mifano midogo ya uumbaji wa binadamu ambao wengi wetu huchukulia kama vilikuwepo tu kwa uchache wanyama tunaokula, mimea tunayolima... ng'ombe, kuku, mbuzi, mahindi, ngano, mchele n.k... Ukihoji vizuri kibaiolojia au kwa matawi mengine ya sayansi japo kwa uchache utagundua hamna nafasi ya hizo imani za mungu. Jaribu tu
Kama ambavyo nyasi ni nyingi kuliko swala na ngombe, na swala ni wengi kuliko simba ndivyo ambavyo matter ni nyingi kuliko mind. Akili inaitumia maada ndiyo maana matter inaonekana kuwezekana kuwepo bila akili. Lakini ndio nishakuambia bila akili [ya juu] tegemea kusambaratika tu kwa huo mfumo husika. Fikiria kiasili mgonjwa vegetative angeishije bila akili ya hao wanaomhudumia?

Tukibaki kutambua na kufanyia kazi vitu vinavyoshikika tu tutapata ugumu sana kufanya maendeleo[akili primitive inatambua na kuchambua vitu concrete]. Lakini tukivichambua hivyo vitu tukatambua kani zinazoviathiri sifa na tabia zao tukavumbua formula tukatatua matatizo yake kihivyo tukirudi kwenye umaterial tunavitawala na kuviendeleza bila wasiwasi [akili iliyoendelea inatambua na kuchambua vitu abstract]. Sasa huoni tukienda mbele zaidi tukatambua vitu spiritual [kwako utasema imaginary] tunaweza kuwa na nguvu juu hata ya viti abstract?. Kwa hiyo inaonesha vitu visivyoshikika ndio vinavyotawala hivi vinavyoshikika.

Cha msingi tu hapo ni ukweli, maana kama unachora grafu ukapiga mstari ile slope yake itakuwa ya kweli uchukulie pointi juu, au chinichini hata huku kwenye negative kama ni kweli ni kweli. Kama formula ya kiroho ni ya kweli ukaifanyia kazi uthibitisho utauona dhahiri kwa matokeo yake katika akili na matokeo makubwa zaidi katika maada. Na isipofanya kazi kuna mawili; labda formula ni ya uongo au kuna vitu vingine hujavitambua kumbe navyo vinaathiri. Havipingani

Basi kadiri kitu kinavyozidi kuwa mbali na maada ndiyo kinazidi kuwa na nguvu juu ya maada kikubwa tu kiwe na akili kubwa na kivielewe hivi vya chini yake na kuvitambua. Spiritual - Abstract - Concrete in order of precedence
 
Nimezungumzia kwamba, evolution inaendelea kwa malengo fulani ni tukio linaloongozwa na akili kubwa sio fujofujo tu.

Kama jicho kwa sasa halijatimia basi linabadilika kuuelekea utimilifu zaidi ili kuweza kuchakata vitu visivyoshikika zaidi. Mwili, ubongo na viungo vyote na jamii kwa ujumla huandaliwa kabla ya kupewa jukumu kubwa zaidi vililoletwa kufanya.

Akili nayo inabadilika kuuelekea ukamilifu pia, kila siku kadri unavyopambana na changamoto/taarifa mpya unajijenga. Kwenye akili hapo fikiria mwanzoni ilikuwa labda na uwezo wa kutambua milima, mawe na wanyama wengine [primitive]. Baadaye ikaanza kutambua na kuvalue vitu kama serikali, jamii na ustaarabu, baadaye ikiendelea zaidi utaona inatambua na kuvipa umuhimu wa kwanza vitu vya kiroho. Evolution inaendelea!
Ndio, inaendelea hapo tuko pamoja. Mutations zinatokea kila leo. Corona virus alivyosumbua dunia na variations zake ni exhibition nzuri sana ya evolution.

Umeeleza vizuri sana sema hapo kwenye "akili kubwa na sio fujofujo" usijeteleza ukaenda kwenye ule mfereji wa kuipa hiyo "akili" subject yako ile ya deity. Ni bora useme akili kubwa ni natural selection. Wewe ni msomi una wajibu wa kukataa imani potofu.
 
Kama ambavyo nyasi ni nyingi kuliko swala na ngombe, na swala ni wengi kuliko simba ndivyo ambavyo matter ni nyingi kuliko mind. Akili inaitumia maada ndiyo maana matter inaonekana kuwezekana kuwepo bila akili. Lakini ndio nishakuambia bila akili [ya juu] tegemea kusambaratika tu kwa huo mfumo husika. Fikiria kiasili mgonjwa vegetative angeishije bila akili ya hao wanaomhudumia?

Tukibaki kutambua na kufanyia kazi vitu vinavyoshikika tu tutapata ugumu sana kufanya maendeleo[akili primitive inatambua na kuchambua vitu concrete]. Lakini tukivichambua hivyo vitu tukatambua kani zinazoviathiri sifa na tabia zao tukavumbua formula tukatatua matatizo yake kihivyo tukirudi kwenye umaterial tunavitawala na kuviendeleza bila wasiwasi [akili iliyoendelea inatambua na kuchambua vitu abstract]. Sasa huoni tukienda mbele zaidi tukatambua vitu spiritual [kwako utasema imaginary] tunaweza kuwa na nguvu juu hata ya viti abstract?. Kwa hiyo inaonesha vitu visivyoshikika ndio vinavyotawala hivi vinavyoshikika.

Cha msingi tu hapo ni ukweli, maana kama unachora grafu ukapiga mstari ile slope yake itakuwa ya kweli uchukulie pointi juu, au chinichini hata huku kwenye negative kama ni kweli ni kweli. Kama formula ya kiroho ni ya kweli ukaifanyia kazi uthibitisho utauona dhahiri kwa matokeo yake katika akili na matokeo makubwa zaidi katika maada. Na isipofanya kazi kuna mawili; labda formula ni ya uongo au kuna vitu vingine hujavitambua kumbe navyo vinaathiri. Havipingani

Basi kadiri kitu kinavyozidi kuwa mbali na maada ndiyo kinazidi kuwa na nguvu juu ya maada kikubwa tu kiwe na akili kubwa na kivielewe hivi vya chini yake na kuvitambua. Spiritual - Abstract - Concrete in order of precedence
Spiritual thinking ni mythical exercise. Myths hazina kazi kwenye taaluma za ushahidi na matokeo halisi.

Ondoa lugha ya kushikika. Phenomenon inaweza isishikike au kuonekana lakini ikawa na athari inayopimika kama dark matter, heavenly forces kama weak force, au g force. Sasa hizo roho ziko wapi? Ulizipimaje? Uliwezaje kutenga athari mahsusi ya uwepo roho? Namaanisha elezea kazi ya roho. Kama zinaishia kwenye abstracts tu bila theory kamili na application nazo ni myths.
 
Back
Top Bottom