Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Ndio, inaendelea hapo tuko pamoja. Mutations zinatokea kila leo. Corona virus alivyosumbua dunia na variations zake ni exhibition nzuri sana ya evolution.

Umeeleza vizuri sana sema hapo kwenye "akili kubwa na sio fujofujo" usijeteleza ukaenda kwenye ule mfereji wa kuipa hiyo "akili" subject yako ile ya deity. Ni bora useme akili kubwa ni natural selection. Wewe ni msomi una wajibu wa kukataa imani potofu.
Moja kati ya sifa ya ma atheist ni kwamba yanakuwaga majitu yenye akili Na kufikiri sana, hilo ninalitambua. Ni watu ambao hawapendi maelezo sahili ya vitu vitata. Ndio maana mnayakataa maelezo rahisi kumhusu Mungu. Lakini msiishie kukataa kila kitu tafuteni maelezo ya uhalisia wa Mungu sasa.

Labda waliochukua jukumu la kutusambazia na kutuelekeza kuhusu Mungu na mambo ya kiroho enzi hizo waliwakuta watu simple minded ndio maana kila wakiwaelekeza hata kwa lugha nyepesi na vimifanomifano, wale watu wanaelewa kidogo uhalisia ila mifano ndio wanaikazia sasa!. Mfano vitu kama Bwana wa majeshi, mfalme mwenye nguvu vilitumika baadae kwa watu ambao akili yao iliwaza vita na ukombozi. Wa zamani zaidi wana vitu kama Ancient of days [hawa watamchukulia kama ana madevu meupe na baraghashia] sikumbuki vingine. Ni vile tu lile wazo la mungu linaeleweka kulingana na akili ya yule anayeambiwa. Inategemea na uelewa wake na imagination yake. Lakini Mungu mwenyewe alianza na kitu abstract tu moja kwa moja - IAM THAT IAM!

Moja ya lengo la hii mada ni kulithibitisha uhalali wa lile wazo la 'umungu' tuanze kwanza kwa kutambua kuwa hilo ni wazo halali halafu baada ya hapo ndio tutajadili na kuendelea kumtafuta na mambo yanayohusiana na yeye yapojepoje. So ukifanya kosa la kulikataa wazo mojakwa moja huwezi kulisoma zaidi wala kukua katika ufahamu wake. Kwa hiyo mimi leo nikikuambia; Ichukue hiyo natural selection, halafu badala ya kuiacha kama a 'mindless/purposeless phenomenon of nature', ikubali kwamba iko na inafanya machaguo yake kwa akili kulielekea lengo fulani. Natural selection sio mungu mind you, hiyo ni sehemu tu ya hekima yake Mwenyezi.
 
Phenomenon inaweza isishikike au kuonekana lakini ikawa na athari inayopimika kama dark matter, heavenly forces kama weak force, au g force. Sasa hizo roho ziko wapi? Ulizipimaje? Uliwezaje kutenga athari mahsusi ya uwepo roho? Namaanisha elezea kazi ya roho. Kama zinaishia kwenye abstracts tu bila theory kamili na application nazo ni myths.
Yaani we jamaa, ivi mfano ukienda huko kwenye ma dark matter ma dark energy. Unapoambiwa balance ya kani za expansion na contraction zilivyo bado tu unabaki na wazo la mindless chaos of matter. Tofauti ya kuzidi kwa atomu tano tu ingetosha kufanya ulimwengu ucollapse -gravity ingezidi. Na kama gravity ingepungua kwa kijisehemu kidoooooooogo sana kasi ya kusambaa ingezidi na tusingepata chochote! Bado tu hutaki kukiri kuwa haya mambo yanaongozwa? Kani zote zinaongozwa na akili ndio sababu mambo ya maana yanajitokeza baadae bro.

Hata hivyo mtaelewa tu maana meshaanza kuona vitu ambavyo lazima vitawapelekea kuwaza kuwa kuna kitu zaidi ya juu ya maada. Eti ooh ukichukua dark matter ukaweka kwenye kaboksi kadogo inakuwa na uzito mdogo, ukilikuza boksi marambili uzito unajidouble!! halafu eti ooh sayansi ni vitu vinavyoshikika tu. Mtaelewa tu. Mojawapo wa kazi za roho ni kudizaini, kufinyanga na kuongoza vitu kama ma bigbang. Kutunga kanuni zitakazouongoza ulimwengu kuanzia mwanzo leo na hadi mwisho na kupatia. Kwa lugha ya kawaida tunayoielewa tukaambiwa 'And let there be light' lakini kiukweli hapo utakuta ni maformula, ma kani mazitomazito na li akili likuuubwa sana, kubwa mno. Ni noma.
 
Na kabla hatujaendelea zaidi hii itawahusu wote masdinero masproblemas na Kiranga hivi mlishawahi kufanya zoezi la kutilia shaka kila kitu? Nalipendekeza maana naona kama linaweza kusaidia.

Jaribu kukaa mwenyewe na kutilia shaka kila kitu ulichoelekezwa kila elimu uliyopewa. Tilia shaka dini, tilia shaka Mungu, Sayansi, Philosophy kila kitu hadi cosmology. Kisha anza kuyakubali mambo kwa kupitia ushahidi wa vitu unavyothibitisha mwenyewe sio kusoma maandishi na picha.

Kwa faida ya wote nitatoa mfano wa ugunduzi/realization yangu mfano mimi; Nikizungumzia baiolojia mfano mimi ninao ushahidi ninawaona watu, wanyama, mimea. Nimeviona viseli kwenye hadubini, nimekaona ka plasimodiamu. Nikaamua kujenga ukweli kutokana na msingi huo mwisho nikafikia kwambaa;
Theory of everything (Nadharia [yangu] ya kila kitu)
We are of God and we live for mankind. (Sisi ni wa Mungu na tunaishi kwa ajili ya wanadamu). Anything done in that statement is right, anything contrary to this statement is left. Living and doing according to this statement is healthy and therefore right. Always healthy things are right.
'Shit happens' is the worst philosophy to live with. 'Shit happens for a reason' is healthy, w...jpg
 
Na kabla hatujaendelea zaidi hii itawahusu wote masdinero masproblemas na Kiranga hivi mlishawahi kufanya zoezi la kutilia shaka kila kitu? Nalipendekeza maana naona kama linaweza kusaidia.

Jaribu kukaa mwenyewe na kutilia shaka kila kitu ulichoelekezwa kila elimu uliyopewa. Tilia shaka dini, tilia shaka Mungu, Sayansi, Philosophy kila kitu hadi cosmology. Kisha anza kuyakubali mambo kwa kupitia ushahidi wa vitu unavyothibitisha mwenyewe sio kusoma maandishi na picha.

Kwa faida ya wote nitatoa mfano wa ugunduzi/realization yangu mfano mimi; Nikizungumzia baiolojia mfano mimi ninao ushahidi ninawaona watu, wanyama, mimea. Nimeviona viseli kwenye hadubini, nimekaona ka plasimodiamu. Nikaamua kujenga ukweli kutokana na msingi huo mwisho nikafikia kwambaa;
Theory of everything (Nadharia [yangu] ya kila kitu)
We are of God and we live for mankind. (Sisi ni wa Mungu na tunaishi kwa ajili ya wanadamu). Anything done in that statement is right, anything contrary to this statement is left. Living and doing according to this statement is healthy and therefore right. Always healthy things are right.View attachment 2200923
Natilia shaka kwamba wewe upo.
 
Natilia shaka kwamba wewe upo.
Hii haina afya, hivyo sio sahihi maana ukipelekwa kwa daktari wa akili ukaulizwa kuhusu statement 'Natilia shaka kwamba wewe upo' uliwezaje kumuambia huyo uliyemtilia shaka na bado ukategemea majibu toka kwake? Huoni unajichanganya imani yako na maneno yako? Atahitimisha you re incoherent and even seeing things, or unseeing things to be exact!

Sentensi yako ingekuwa sahihi kimantiki ungeiweka katika nafsi ya tatu kama unavyofanyaga kila siku kuhusu Mungu
ungesema ivii 'Masdinero natilia shaka kama Uhakika yupo' hapo sawa.
 
Ongea na Mungu mwambie kule Ukraine watu aliowaumba Putin anawaua kinyama bila huruma yoyote. Mbona Mungu kanyamaza!

Mwanzo 1:27, na Tuumbe Mtu kwa sura na mfano wetu akatawale duni, utawala wa duni alipewa Mwananadam na mwanadam anawajibika kwa kila uharibifu wa Dunia, ndo maana ilimcost Mungu kuwa mwanadam.

Sasa basi, katika maombi Yesu alifundisha, kuna sehemu inasema tuombe ufalme wake uje, kwa hiyo ni kwamba tuna mamlaka na kuamua nini kifanyike duniani, tunaweze kabisa mzuilia Mungu, Mungu anaweza kila kitu mpaka aseme vinginevyo, na ameamua kufanya kazi na wana damu.

Ubaya wowote unaofanyika duniani ni sababu ya mwanadamu, Mungu hausiki hata kidogo.
 
Hii haina afya, hivyo sio sahihi maana ukipelekwa kwa daktari wa akili ukaulizwa kuhusu statement 'Natilia shaka kwamba wewe upo' uliwezaje kumuambia huyo uliyemtilia shaka na bado ukategemea majibu toka kwake? Huoni unajichanganya imani yako na maneno yako? Atahitimisha you re incoherent and even seeing things, or unseeing things to be exact!

Sentensi yako ingekuwa sahihi kimantiki ungeiweka katika nafsi ya tatu kama unavyofanyaga kila siku kuhusu Mungu
ungesema ivii 'Masdinero natilia shaka kama Uhakika yupo' hapo sawa.
Kwani wapi nimesema nategemea majibu kutoka kwako?

Na hata nikitegemea jibu, kwani wewe hujui kwamba hata ma online bot yanaweza kujibizana na wewe?

Haiwezekani kupata autoreply from an online bot bila ya mtu kuwapo?

Na wewe si uliyeniambia nitilie shaka kila kitu?

Sasa mbona nafuata ushauri wako na kutilia shaka uwepo wako, halafu unanishangaa kwa kufuata ushauri wako mwenyewe?
 
Kuna mtindo wa kwenye social media watu kutosoma maelezo marefu sana. Hivyo basi nimeamua kuileta sehemu tu ya ile sehemu ya pili, enjoy;
View attachment 2174800
....................kukazia pointi kadhaa na kufunga;
Ndugu zangu, haidhuru mtu au mfumo kutokujua mwisho au mwanzo wake ili kuleta maana – ‘sense’. Maana inakuja pale kipande cha mfumo husika utakapokuwa unatenda kulingana na muelekeo sahihi ukiuchukulia mfumo mzima juu kabisa hadi chini kabisa. Sense ni ule tu uelekeo sahihi basi. Hata kama labda moyo unafahamu tu kwamba ‘ulimwengu mzima’ ni wenyewe tu na ukajijali wenyewe tu hautakuwa na maana tena mwilini. Lakini ukawa na akili ya kuelewa kwamba kuna mfumo mzima wa mishipa na kazi yake ni kuisambazia hiyo mishipa damu basi tayari utakuwa na maana na utaishi. Utaishi vizuri hata kama haujawahi kuiona mivitu migumu kama mifupa [damu yenyewe inatengenezwa huko]. Moyo ukasema wenyewe unajua kuna nyama tu na nyama ndiyo kila kitu kilichopo. Utaendelea kuishi huku ukilindwa na mifupa hiyohiyo uliyoikataa kwamba haipo na haina maana yoyote. Lakini ukitaka [ufe huo moyo] ni pale utakapofanya kitu ambacho ni non-sense yaani kinyume na ukweli wake. Mfano ukaamua kunyonya damu badala ya kuisukuma. Au kuji mwambafai na kujipa umuhimu wa kwanza badala ya kusambaza damu wenyewe ndiyo uitumie damu kukua na kuitumia zaidi. Kujitukuza kujipa umuhimu wa kwanza wewe badala ya vyote sio jambo zuri. Maana viungo vipo kwa ajili ya viungo wenzake na kwa ajili ya lengo la jumla la kuwepo kwa huo mfumo. Kwa hiyo tukirejea kwa mwili tutasema moyo ni kwa ajili ya mapafu, miguu, mikono, ubongo, moyo na mwiliwote na mtu mzima kwa ujumla. Kwa hiyo moyo unaweza kusema kuwa lile wazo la mtu ndiyo mungu. Mungu wake anaonekana kuwa tofauti kabisa na asili ya moyo wenyewe ulivyo kwanza haonekani wala hashikiki.

Mfano wa seli pia ni hivyohivyo mitochondria ipo kwa ajili ya ribosome, nucleus, membrane, mitochondria yenyewe na seli nzima kwa ujumla wake. Mitochondria akiongeza ujuzi wake atagundua kuwa hata ile idea nzima ya seli sio mwisho. Ni mungu wake kwa level fulani lakini sio mwisho. Atagundua kwamba zipo seli nyingine pia mwilini mamilioni na mamilioni nazo zina mitochondria zake na zoote zinafanya kazi kwa ajili ya kuuendeleza huu mwili mzima. Ndio zinaonekana kama zimaulisha ubongo wa mwili huo lakini ukitizama kwa makini utagundua kuwa hata ubongo unafanya kazi kwa ajili ya mtu ambaye ni jitu zima limalotawala seli zooote moja moja katika makundi. Lakini hapohapo ukipindisha kidogo kubadili mizania ya utazamaji unaweza kusema kuwa huyu mtu naye yupo kwa ajili ya kuvitumikia hivyo viseli [na vimitochondria] vyoote mwilini mwake ili viendelee kuishi. Nayo sio mbaya ukiamua hivyo kwa sababu huo pia ni ukweli na ni kitu kilekile tunachokisema kila siku. Na huyu mtu ameonesha kuwa yuko na upendo woote na kujali kote na uangalizi wote kwa viseli vyote vilivyo chininya uangalizi wake. Kwa hiyo kwa viseli vya mwili mtu ni Mungu wao.

Tukibakia hapohapo ona jinsi mambo yote yanavyopata majibu ya wazi kabisa. Tunaona ni sahihi kwa seli hai nyekundu za damu kufa kila zinapotimiza wastani wa siku 120. Sijui kama zinalalamika au zinaumia kufanya hivyo sijui. Lakini inaonesha kuwa zimezaliwa zimemtumikia mungu[mtu] na mwisho zimekufa zitaacha nyingine zikifanya kazi. Zitazaliwa seli nyingime. Haya ikatokea mwili umevamiwa na wadudu hatari. Tunaona rasilimali muhimu kwa matumizi ya seli nyingine zikibadilishwa njia na kupewa askari [chembe za kinga] ili zikapambane na wavamizi. Labda seli nyingine huwa zinanungunika na kuleta migomo ndio maana sababu tunaona mwili ukinyon’gonyea. Mfano ni kichwa ndio kinauma au ni damu ndiyo imeambukizwa maralia. Lakini misuli ya miguu, tumbo na viungo vya uzazi vyote vinalala, si hamu ya chakula wala ya kula inayobakia. Au mfano wa pale ambapo mwili unapoamua kuviua vipande vyake vinavyotaka kuleta shida kwa mwili mzima. Mfano; seli zilizokaidi kufa zenyewe zikaamua badala yake kukua tuu pasipo kujali zinaleta faida wala hasara kwa wenzie. Zenyewe zinachojua ni kula kunenepeana na kukua zaidi na zaidi. Kila aliye jirani nazo anaumia tena anachukizwa na uwepo wake. Muda utafika mwili utaamua kuziua japo kutokana na mapendo makubwa utafanya hivyo kwa maumivu makubwa sana. Ukisikia kansa inatesa jua kwamba kansa inatesa kweli kweli. Ni maumivu makali na ndio maana wanaoiugua huwa wanasemwa kuwa ‘they are battling cancer’ ni vita! Lakini hata yanapotokea haya tunapaswa tutambue kuwa yote ni katika upendo tu wa baba yao hizo seli mtu mwenyewe. Maana kwa upendo anaidhinisha seli mbaya ziuwawe hata kama zinazobaki zitayapata maumivu hakuna namna. Yote haya yangeepukika kama seli mbovu zitaamua kufa zenyewe kwa upendo kuwaachia wengine waishi. The key hapa ni upendo. Mungu ni pendo walishasema. Hata kama kwa upendo ataamua kwamba wacha tu vyote viishi [ambavyo mara nyingi hutokea] na mwishoni atauvunjavunja mwili wote huyu mtu katika kifo nao ni upendo. Sema tu namna hii ya pili itawaacha wale seli wengine na mateso makali hadi kufa kwao. Seli wazuri wamapoumia na mtu naye anaumia lakini kwa upendo anavumilia.

Panda hatua moja tuje kwa binadamu binadamu anaweza kujihisi kwamba yeye yupo na anajifanyia kazi kwa ajili yake kwa faida zake lakini hilo jambo haliwezekaniki. Kwanza tukianza tu kwenye kufanya kazi mara nyingi ni kuwatumikia wengine. Mfano umejiajiri unanyoa nywele unawanyoa wengine. Unapika mamantilie umawapikia wengine. Mganga anawatipu watu wenzake wanaomzunguka. Kwa kufanya hivyo unafanya kile ambacho Mungu anataka; kuwatumikia wengime na kumtumikia yeye. Na Mungu naye anajishughulisha na kuendelea kuwepo kwa sisi wote duniani pamoja na vyote vinavyotuzunguka ili tuendelee kuwepo kwa ujumla wake. Wanazaliwa wanadamu wengine wengine wanafariki. Wote tunapendezwa na kukua na maendeleonya kiuchumi. Mungu pia anayafurahia hayo ikiwa yanaleta hali nzuri kwa wote viumbe, wanadamu na mazingira. Wote wanadamu, majirani na Mungu huchukizwa pale mtu anapoamua kukua tuu hata kwa madhara kwa watu wengine. Mtu ambaye badala ya kuwatumikia watu ataamua kuwatumia watu kujikuza pasipo faida yoyote kwa watu na dunia kwa ujumla anaenda kinyume na mantiki senseless. Basi yanaweza kumpata mabaya kutokana na mifumo tuliyojiwekea labda mwizi atafungwa gerezani. Au kuugua kutokana na matumizi yaliyopitiliza ya chochote hadi akajiharibu. Au kwa upendo akaachwa aendelee kuishi japo hii itakuja kwa gharama ya maumivu ya wale wengine wote wenye kuwa wema machoni pa Mungu. Lakini mwisho wa siku utakuja na kila kitu kuvunjwavunjwa na hukumu kupitishwa.

Baada ya kufa sasa ndiyo kila kipengele kitajihukumu kutokana na kiwango kilichofuata hiyo mantiki. Kama kilifanya vyema ni furaha tuu milele na kama kilifanya visivyo ni shida tuu milele. Kama ambavyo sisi binafsi hufanya makosa na kuumia nafsini. Na wakati mwingine kutamani kurudi nyuma na kurekebisha makosa. Labda ni kweli huwa zinatolewa nafasi za pili ili kuja kurekebisha makosa hilo sina hakika japo uwezekano ni mkubwa wa ukweli huo. Au labda kile kilichotenda vibaya kinarudishwaga tena levo ya chini ili kikajifunze kutenda mema baadaye kitapandishwa. Kwa usemi huohuo na kile kilichotenda vema basi kitarudishwa katika levo ya juu yake maana kimeuthibitishia mfumo kwamba kinafahamu lengo lake. Aliye mwaminifu kwa kidogo tunaweza kumuongeza majukumu zaidi maana tunamuamini au sio? Wapo watu wanaoamini hivyo. Mfano labda kwenye ufufuo ile kuvikwa miili mipya itakuwa na zile taarifa za seli zilizofanya vizuri wakati wa uhai wake. Maana tofauti na kufanyiana kazi hapa duniani tupo pia kwa ajili ya kujifunza kitu fulani.

Basi ndugu zangu nahitimisha; kama ambavyo neutroni zipo kwa ajili ya protoni, nyutroni wenzake zenyewe na ulimwengu mzima kwa ujumla. Ndivyo ambavyo atomu nzima ipo kwa ajilinya atomu wenzake, lengo fulani la uwepo wa maada na ulimwengu mzima kwa ujumla. Ndivyo ambavyo seli zipo kwa ajili ya seli wenzake, viungo na tishu mtu na dunia na ulimwengu mzima kwa ujumla. Ndivyo ambavyo sayari zipo kwa ajili ya zayari nyingine, vimondo, jua na lengo zima la kuanzishwa kwa sayari na mfumo wa jua na ulimwengu mzima kwa ujumla. Ndivyo hivyohivyo ndugu zangu magalaksi yapo kwa ajili ya magalaksi mengine na gesi, na nafasi na ulimwengu mzima kwa ujumla. Basi kwa mfananisho huo mimi nasema wazo la Mungu ni wazo halali kabisa na linaleta mantiki kuliko ile kuwepowepo tu bila lengo lolote, bila jukumu lolote. [Ili unielewe basi rudia hii aya ya mwisho ukibadili [replace] neno ulimwengu mzima kwa ujumla na neno Mungu.] Mungu yupo ndugu zangu Mungu yupo. Nakubali kuwa anaweza kuwa katika muonekano tusioweza kuung’amua kisawasawa hadi inapelekea kuambizana sisi kwa sisi kuwa hachunguziki. Ni sawa lakini lile wazo la kwamba yupo linabaki palepale. Na sifa zake za kuwa na upendo wote na ujuzi wote ni sahihi kabisa. Kuwepo pote hiyo ndiyo haswaa imejionesha katika makala hii ndefu. Hata kama sayansi au watu wataamua kumficha mbali juu kabisa infinity au kumficha chini kabisa infinitesimall bado Mungu ataonekana tu kwa sababu yeye ni mwanzo na mwisho, hana mwanzo wala mwisho ni hamna na ndo kila kitu. Ukivichunguza vitu vikubwa juu kabisa yako utamkuta mungu. Na hata ukivichunguzwa vitu vidoogo vya wewe na chini yako utamkuta Mungu pale. Somo lolote ukilichukua ukalifafanua ukalisoma na ukalichunguza mpaka mwisho wake utamkuta Mungu. Kwa hiyo iwe ni baiolojia, fizikia, filosophia mwisho utamkuta Mungu. Nawasilisha.
View attachment 2174803
Who is God?

Does God exists in physical or spiritual world?
 
Mwanzo 1:27, na Tuumbe Mtu kwa sura na mfano wetu akatawale duni, utawala wa duni alipewa Mwananadam na mwanadam anawajibika kwa kila uharibifu wa Dunia, ndo maana ilimcost Mungu kuwa mwanadam.

Sasa basi, katika maombi Yesu alifundisha, kuna sehemu inasema tuombe ufalme wake uje, kwa hiyo ni kwamba tuna mamlaka na kuamua nini kifanyike duniani, tunaweze kabisa mzuilia Mungu, Mungu anaweza kila kitu mpaka aseme vinginevyo, na ameamua kufanya kazi na wana damu.

Ubaya wowote unaofanyika duniani ni sababu ya mwanadamu, Mungu hausiki hata kidogo.
Asante sana sana kumuelewesha. Exactly hiki ndicho tunachokimaanisha tukisema 'we make shit happens'. Tunayo nafasi ya kufanya mambo tunavyoamua na tutapambana na matokeo yake mbele kwa mbele.

Lakini tukijitiisha na kuamua kufanya mambo kulingana na mapenzi ya Mungu hiyo ndiyo itakuwa tumepatia. So utawala wa dunia tumepewa na uwezo wa kuamua tunajichagulia
 
Kwani wapi nimesema nategemea majibu kutoka kwako?

Na hata nikitegemea jibu, kwani wewe hujui kwamba hata ma online bot yanaweza kujibizana na wewe?

Haiwezekani kupata autoreply from an online bot bila ya mtu kuwapo?

Na wewe si uliyeniambia nitilie shaka kila kitu?

Sasa mbona nafuata ushauri wako na kutilia shaka uwepo wako, halafu unanishangaa kwa kufuata ushauri wako mwenyewe?
Poa bhana endelea halafu tafuta kuvikubali kwa uthibitisho.

Kwanza ukilinganisha na mimi wewe mashaka yako yameanzia mbali. Mimi nilianza kujitilia shaka mwenyewe kwanza kama nipo! nikaenda hadi nikaestablish kwamba nipo. Ndio maana ninawaza na ninajiuliza kama nipo. Na kwa kuwa mtu ni 'mawazo yake' kama alivyosema Munga Tehenan katika kitabu chake cha UCHAWI. Basi mimi nipo.

Ndo nikakua nikatilia shaka kama wengine wapo au kingine chochote kipo. Mfano nahisi ulishaskia lile swali kwamba 'How do you know that the moon is there, when no one is looking at it'. Kuna watu wana uwezo wa kukuaminisha kwamba watu wote duniani wakisahau wakaacha kufikiri kuhusu mwezi - mwezi utakuwa haupo! hadi formula watakuchorea!!. Watakuambia vyote unavyoona ni akili yako inavijenga muda huohuo paap!! Basi nikakataa huo ujingaa nikaestablish kwamba mimi nipo watu wengine wapo na vitu vipo. Basi nikaisoma miti na wanyama na mimi nikapata kwamba vinaishi kwa lengo, kazi na kanuni kadhaa ambazo hadi sasa bado najifunza. Nilianza na vinavyoshikika na mimi.

Sijawahi kuthibitisha galaxy nyingine zipo wala viatomu lakini kwa hivi nilivyovithibitisha sipati tabu kupokea maelezo ya vitu vingine kwa ukweli wake. Mfano huu ukweli wa kwamba mifumo inaundwa kwa lengo maalumu na inalitumikia hilo lengo. Hilo lengo ni kila kitu katika mfumo, ni zaidi ya mfumo, lipo juu katika mfumo na lipo pote katika mfumo at the centre and the circumference thereof. Lengo linaupenda mfumo. Lengo ndio mfumo lakini huwezi kusema mfumo ndio lengo na ukawa sahihi kwa asilimia mia.
 
Who is God?

Does God exists in physical or spiritual world?
God is what IS. Hafananishwi. Think of the highest concept of beauty, truth, life, light, love, intelligence, purity etc, those are some of the properties of God.

About being in spiritual or physical world. You know you are thinking in physical terms so your answer is a bit complicated. It is like this;
The spiritual realm is above the physical, but it is also before the physical. It is the centre and the circumference thereof. Meaning the spiritual world interpenetrates the whole physical world while being above and before. God is spiritual so is in the spiritual world and that is another way of saying EVERYWHERE.
 
Roho ni nini?

Thibitisha roho ipo kweli nje ya habari za kufikirika tu.
Leo umebanwa tena kwenye 18 hadi umetoka nnje ya mada ambavyo nilikubananishaga mimi hadi ukaishia mitini [emoji1787][emoji1732][emoji851]
 
Poa bhana endelea halafu tafuta kuvikubali kwa uthibitisho.

Kwanza ukilinganisha na mimi wewe mashaka yako yameanzia mbali. Mimi nilianza kujitilia shaka mwenyewe kwanza kama nipo! nikaenda hadi nikaestablish kwamba nipo. Ndio maana ninawaza na ninajiuliza kama nipo. Na kwa kuwa mtu ni 'mawazo yake' kama alivyosema Munga Tehenan katika kitabu chake cha UCHAWI. Basi mimi nipo.

Ndo nikakua nikatilia shaka kama wengine wapo au kingine chochote kipo. Mfano nahisi ulishaskia lile swali kwamba 'How do you know that the moon is there, when no one is looking at it'. Kuna watu wana uwezo wa kukuaminisha kwamba watu wote duniani wakisahau wakaacha kufikiri kuhusu mwezi - mwezi utakuwa haupo! hadi formula watakuchorea!!. Watakuambia vyote unavyoona ni akili yako inavijenga muda huohuo paap!! Basi nikakataa huo ujingaa nikaestablish kwamba mimi nipo watu wengine wapo na vitu vipo. Basi nikaisoma miti na wanyama na mimi nikapata kwamba vinaishi kwa lengo, kazi na kanuni kadhaa ambazo hadi sasa bado najifunza. Nilianza na vinavyoshikika na mimi.

Sijawahi kuthibitisha galaxy nyingine zipo wala viatomu lakini kwa hivi nilivyovithibitisha sipati tabu kupokea maelezo ya vitu vingine kwa ukweli wake. Mfano huu ukweli wa kwamba mifumo inaundwa kwa lengo maalumu na inalitumikia hilo lengo. Hilo lengo ni kila kitu katika mfumo, ni zaidi ya mfumo, lipo juu katika mfumo na lipo pote katika mfumo at the centre and the circumference thereof. Lengo linaupenda mfumo. Lengo ndio mfumo lakini huwezi kusema mfumo ndio lengo na ukawa sahihi kwa asilimia mia.
Umethibitisha vipi kwamba upo? Na una uhakika gani uthibitisho wako ni thabiti?
 
Leo umebanwa tena kwenye 18 hadi umetoka nnje ya mada ambavyo nilikubananishaga mimi hadi ukaishia mitini [emoji1787][emoji1732][emoji851]
Nje ya mada wapi? Na unajuaje hapa ni nje ya mada si wewe tu hujajua kutenganisha nje na ndani mpaka uko wapi?
 
Umethibitisha vipi kwamba upo? Na una uhakika gani uthibitisho wako ni thabiti?
Kwangu mimi ilikuwa rahisi tu kama nilivyosema inaanzia kwenye tafsiri ya 'mimi ni nani'. Kwa kuwa nilishadefine mapema kwamba mimi au ule umimi ni lile wazo la mimi, ule ufikiri wangu kwamba mimi ni. Ninazo sehemu mbalimbali za mwili ili niweze kuinteract na mazingira na watu wengine.

Yaani mtu kama mtu ni lile wazo la uyeye ule ufikiriaji wake au mawazo yake. Ndo maana utaskia 'tumuulize Kiranga tumsikie anasemaje' -Ujue tunalitaka wazo la kiranga ndio kiranga mwenyewe huyo.
Mdomo ni mdomo wako na unaweza kuwa kiranga bila mdomo tutayapata mawazo yako kwa namna nyingine utaandika.
Mikono ni mikono yako tutawasiliana na kiranga hata asipokuwa na mikono.
Kichwa ni kichwa cha kiranga hadi ubongo ni ubongo wa kiranga sasa kiranga mwenyewe ni nani? lile wazo hai la kiranga, ule ufikiri wake ndio kiranga mwenyewe.

Mimi sikupata tabu kujua kama nipo kwa sababu nilichukulia kule kukaa tu na kuwaza kama sipo au nipo tayari inaonesha nipo maana wazo la mimi ni hai na nipo nachanganua mambo hayo. Nilijua wengine wapo kwa sababu kuna mda unakutana na watu wabishi na tunakuwa na mawazo tofauti kabisa kuhusu uhalisia. So Kiranga yupo na Interlacustrine R yupo pia.
 
Kwangu mimi ilikuwa rahisi tu kama nilivyosema inaanzia kwenye tafsiri ya 'mimi ni nani'. Kwa kuwa nilishadefine mapema kwamba mimi au ule umimi ni lile wazo la mimi, ule ufikiri wangu kwamba mimi ni. Ninazo sehemu mbalimbali za mwili ili niweze kuinteract na mazingira na watu wengine.

Yaani mtu kama mtu ni lile wazo la uyeye ule ufikiriaji wake au mawazo yake. Ndo maana utaskia 'tumuulize Kiranga tumsikie anasemaje' -Ujue tunalitaka wazo la kiranga ndio kiranga mwenyewe huyo.
Mdomo ni mdomo wako na unaweza kuwa kiranga bila mdomo tutayapata mawazo yako kwa namna nyingine utaandika.
Mikono ni mikono yako tutawasiliana na kiranga hata asipokuwa na mikono.
Kichwa ni kichwa cha kiranga hadi ubongo ni ubongo wa kiranga sasa kiranga mwenyewe ni nani? lile wazo hai la kiranga, ule ufikiri wake ndio kiranga mwenyewe.

Mimi sikupata tabu kujua kama nipo kwa sababu nilichukulia kule kukaa tu na kuwaza kama sipo au nipo tayari inaonesha nipo maana wazo la mimi ni hai na nipo nachanganua mambo hayo. Nilijua wengine wapo kwa sababu kuna mda unakutana na watu wabishi na tunakuwa na mawazo tofauti kabisa kuhusu uhalisia. So Kiranga yupo na Interlacustrine R yupo pia.
Unajuaje kwamba wewe upo kweli na si wazo tu?
 
Unajuaje kwamba wewe upo kweli na si wazo tu?
Hahahahaaaah huhuhuuuuuh! amaa kweli basi tuanze na swali la mtu ni nani labda. Mtu ni nani bwana Kiranga.

Nimeona umepuuzia jinsi mimi nilivyomtafsiri mtu, hebu tukusikie na wewe unasemaje. Mtu ni nani au ni nini?
 
Au ndo tutarudi kulekule mwanzo kwenye swali la je? wazo kwako ni 'kitu halisi' kwa kiasi gani.
 
Hahahahaaaah huhuhuuuuuh! amaa kweli basi tuanze na swali la mtu ni nani labda. Mtu ni nani bwana Kiranga.

Nimeona umepuuzia jinsi mimi nilivyomtafsiri mtu, hebu tukusikie na wewe unasemaje. Mtu ni nani au ni nini?
Kwa nini unakuja kwa mtu kama hujaweza kujithibitisha wewe upo?
 
Back
Top Bottom