Miradi mikubwa haikuanza kipindi cha Hayati Magufuli pekee

Miradi mikubwa haikuanza kipindi cha Hayati Magufuli pekee

Kama isingewezekana bila JPM imekuaje Sasa hao kina January na Samia tulioambiwa ni mafisadi wamemaliza bwawa na wanalijaza Maji? Au akifanya JPM pekee ndio anaweza wengine hawawezi chochote?
Hao wameanzisha mradi gani mpya
 
Werevu wanalazimisha kuwa wajinga zaidi pale wanapoambiwa JPM amejenga vituo vya afya nchi nzima, bwawa la JKNHP, SGR, flyover, barabara kubwa ya njia nane, meli kedekede, na mambo haya yako hadi makwao wanakoishi

Eti wanataka wawe vipofu na viziwi wasione wala kusikia alichofanya huyu mwamba!

Pumbavu sana mnaodhani ni wasomi na werevu halafu mnalazimisha kufunga masikikio na kuziba macho yenu kisa JPM kamwambia Mbowe alipe kodi blicanas akajidai eti yeye ni mpinzani atapiga kelele kwa mabeberu!

Acheni wehu basi nyinyi wasomi!

Mkifanya vema hata nyinyi tutawapongeza tuu!

Hapo ulipo huna lolote na ndiyo maana anazungumziwa JPM
Mbona uwanja wa ndege wa chato umeuficha ?
au huu siyo uwekezaji wa Magufuli ?
 
Habari za weekend wanajukwaa

Kumekuwa na kelele nyingi sana kutoka kwa wafuasi wa JPM kwamba miradi itakufa ama miradi haitofanyika sababu JPM hayupo. Na wengine wameenda mbali sana na kusema hakuna aliyewahi kufanya miradi kama ilivyofanyika awamu ya tano. Hapo chini nimeweka mifano tu ya miradi awamu ya nne kwa kuweka rekodi sawa kuwakilisha awamu zingine zilizopita kabla ya JPM.

1. Mradi wa Bomba la gesi ulicost matrilioni ya fedha na ulifanyika enzi za JK na Leo hii umeme wa Tanzania kwa 60% unategemea Bomba lile la gesi.

2. Barabara za lami zilijengwa almost Kila mkoa Ili kuunganisha mikoa jirani; pamoja na madaraja ya kumwaga kama Malagarasi n.k. So kama ni miundombinu ya barabara kikwete aliwekeza sana.

3. Mfumo wa Barabara za mwendokasi uliasisiwa kipindi hiki na serikali ya JK Ilimwaga mabilioni kujenga mwendokasi na kuagiza mabasi husika.

4. Airport ya J.K Nyerere Airport ilipanuliwa awamu ya nne. Leo hii tuna Airport yenye Hadhi ya kimataifa jambo ambalo halikufanyika tokea uhuru!!

5. Uzalishaji umeme ulipanuliwa kwa kujenga kituo Cha kufua umeme wa gesi pale Kinyerezi. Hatua hii iliongeza capacity ya uzalishaji umeme kuliko awamu zote zilizopita!!

6. Kulifanyika mradi mkubwa wa kutoa Maji ziwa Victoria kuelekea mikoa ya Kanda ya kati. Mradi ule umefika mpaka mkoa wa Tabora na Sasa unaelekea Singida!! Hayo ni mabilioni na ubunifu wa hali ya juu licha ya kelele kutoka kwa mataifa kama Misri yaliyopinga kabisa kuguswa Maji ya ziwa Victoria.

Hii ni mifano tu ya haraka haraka kwenye eneo la miundombinu. Kwahiyo tuache hizi propaganda kwamba miradi ilianza awamu ya 5 na imeisha awamu ya 5 ni uzembe tu wa kufikiri. Hiyo miradi tajwa hapo juu ingefanyika awamu ya 5 nadhani kelele zingekua nyingi mnoo.

Ni vizuri tuheshimiane Kila awamu, alipoishia Nyerere, mkapa aliendeleza and so on hata Mama Samia anaendeleza anapoweza so tusijikweze kweze na kelele nyingi as if JPM alikua Alpha na Omega.

Naomba kuwasilisha
Halafu yote haya yalifanyika bila kutekana, kuporana na kuuana
 
substandard unamaanisha nini. We hakuna unalojua kuhusu ujenzi. Kikwete miradi yake ni mingi ukianzia na huo wa UDOM kujenga chuo kikuu kikubwa kuliko vyote africa mashariki na kati. Mabarabara; Kuunganisha makao makuu ya mikoa karibu yote kwa lami, aliunganisha Dodoma na Iringa, Songea na Mtwara kupitia Tunduru, Nanyumbu na Masasi. Aliunganisha mikoa ya Arusha, Manyara, Singida na Dodoma. Aliunganisha Mbeya na Sumbawanga. Aliunganisha Sumbawanga na Katavi. Aliunganisha Shinyanga na Tabora kupitia Nzega. Aliunganisha Singida na Tabora kupitia Itigi na Uyui. Aliunganisha Mwanza, Geita na Kagera. Alijenga barabara ya lami kutokea Tinde(Shinyanga) kuipitia Kahama mpaka Karagwe mpakani mwa Nchi yetu na Rwanda.

Alijenga upya barabara kutoka Arusha-Makuyuni-Minjingu. Barabara za mipakani; Alijenga upya Barabara kutoka Arusha-Namanga. Alijenga barabara kutoka Njia panda ya Himo mpaka Tarakea. Alijenga Barabara kutoka Musoma mpaka Sirari. Alijenga barabara kutoka Tanga mpaka Horohoro. Alijenga barabara kutoka Songea mpaka Mbinga ambayo sahivi ndiyo inamaliziwa kuelekea Mbamba Bay wilaya ya Nyasa. Ongezea na wewe km ni mtanzania. Alipanua uwanja wa ndege wa JULIUS NYERERE. Kikwete ndiyo aliyejenga mradi wa mabasi yaendayo haraka Dar Es Salaam. Hiyo ni baadhi ya miradi na hatukuona makeke yoyote mtu wa watu ni mnyenyekevu mpaka leo.
Apo mwambia alikaa kipindi kimoja tu angemaliza viwili Yani ingekuwa hatari na nusu
 
Habari za weekend wanajukwaa

Kumekuwa na kelele nyingi sana kutoka kwa wafuasi wa JPM kwamba miradi itakufa ama miradi haitofanyika sababu JPM hayupo. Na wengine wameenda mbali sana na kusema hakuna aliyewahi kufanya miradi kama ilivyofanyika awamu ya tano. Hapo chini nimeweka mifano tu ya miradi awamu ya nne kwa kuweka rekodi sawa kuwakilisha awamu zingine zilizopita kabla ya JPM.

1. Mradi wa Bomba la gesi ulicost matrilioni ya fedha na ulifanyika enzi za JK na Leo hii umeme wa Tanzania kwa 60% unategemea Bomba lile la gesi.

2. Barabara za lami zilijengwa almost Kila mkoa Ili kuunganisha mikoa jirani; pamoja na madaraja ya kumwaga kama Malagarasi n.k. So kama ni miundombinu ya barabara kikwete aliwekeza sana.

3. Mfumo wa Barabara za mwendokasi uliasisiwa kipindi hiki na serikali ya JK Ilimwaga mabilioni kujenga mwendokasi na kuagiza mabasi husika.

4. Airport ya J.K Nyerere Airport ilipanuliwa awamu ya nne. Leo hii tuna Airport yenye Hadhi ya kimataifa jambo ambalo halikufanyika tokea uhuru!!

5. Uzalishaji umeme ulipanuliwa kwa kujenga kituo Cha kufua umeme wa gesi pale Kinyerezi. Hatua hii iliongeza capacity ya uzalishaji umeme kuliko awamu zote zilizopita!!

6. Kulifanyika mradi mkubwa wa kutoa Maji ziwa Victoria kuelekea mikoa ya Kanda ya kati. Mradi ule umefika mpaka mkoa wa Tabora na Sasa unaelekea Singida!! Hayo ni mabilioni na ubunifu wa hali ya juu licha ya kelele kutoka kwa mataifa kama Misri yaliyopinga kabisa kuguswa Maji ya ziwa Victoria.

Hii ni mifano tu ya haraka haraka kwenye eneo la miundombinu. Kwahiyo tuache hizi propaganda kwamba miradi ilianza awamu ya 5 na imeisha awamu ya 5 ni uzembe tu wa kufikiri. Hiyo miradi tajwa hapo juu ingefanyika awamu ya 5 nadhani kelele zingekua nyingi mnoo.

Ni vizuri tuheshimiane Kila awamu, alipoishia Nyerere, mkapa aliendeleza and so on hata Mama Samia anaendeleza anapoweza so tusijikweze kweze na kelele nyingi as if JPM alikua Alpha na Omega.

Naomba kuwasilisha
Unajisumbua na maelezo yako, Sukuma gang wote ni mazezeta wasiojielewa na watakupinga tu. Umepoteza muda na energy bure kuandika uzi wako.
Just imagine miradi yote ya awamu ya tano wanaita ya 'fedha za Mwendawazimu oops sorry za Mwendakuzimu' sasa wewe jaribu kuseme hiyo miradi uliyoiorodhesha ni ya fedha za JK kama watakubaliana nawe, yaani fedha za walipa kodi wanazigeuza kana kwamba ni zake binafsi.
NB: Kuweka records sawa ungeorodhesha miradi iliyofanywa katika awamu zote, isijekuwa nawe unacheza mchezo wa 'kichawa' kama wauchezao Sukuma gang.
 
Safi sana, malizia hata Udom alijenga Kikwete pia, kabla ya Kikwete kulikuwa hakuna Tanzania kila kilianzia kwa Kikwete, umemponda Magufuli na kumsifu Kikwete hauna tofauti na mashabiki wa Magufuli na uko subjective zaidi lkn unasahau Kikwete alichukuwa nchi kutoka kwa Mzee Mkapa na Mzee Mkapa kwa Mzee Mwinyi na Mzee kutoka kwa Mwalimu Nyerere, lkn wewe umeanzia kwa Kikwete you are no diffrent uko hapa kuendekeza ligi za kitoto.

Next time jaribu kuwa objective badala ya kuwa subjective na emotional.
[emoji106][emoji106][emoji106][emoji106][emoji106][emoji106][emoji106]
 
Mbona mnatumia nguvu kubwa sana kuonyesha JPM hakufanya kitu?..

Ni kweli inawezekana miradi mikubwa haikuanza kipindi cha JPM tu maana hata reli aliijenga mkoloni, Bandari alizijenga mkoloni nk... Ukiondoa mkoloni mtanzania pekee mweusi aliyekuja na maamuzi ya miradi mikubwa ambayo wengi tuliona haiwezekani ni JPM.

Nitajie Rais gani Tanzania ambaye alishafanya projects zinazofanana na hizi alizozianzisha JPM ....kuanzia Stieggler's, SGR, BUSISI bridge, Hospitali za rufaa kila mkoa, Ujenzi wa hizi meli za toka mkoloni ( pale Ziwa Victoria hakukuwahi kuwa meli ya kisasa toka JKN na mkoloni)....

Inawezekana JPM anamapungufu yake lakini naweza kusema ni aina ya RAIS ambaye angeifaa sana Tanzania..
 
Mbona uwanja wa ndege wa chato umeuficha ?
au huu siyo uwekezaji wa Magufuli ?
Bahati mbaya miradi yote ya Magufuli haina hati ya jina lake, ni juu yenu wasomi walalamishi kuamua, mufugie kuku ama muipotezee!

Wasomi wa tz mna wivu wa kipumbavu sana
 
Labda kama huna unalolijua kuhusu ilo bwawa, ila unabyomuona Samia na Janauary wanaubunifu wowote? Just be neutral! Samia anavyomuona ni mtu ambae anasumbua kichwa chake kutafuta taarifa? Kubuni vitu?
Umeongea ukweli kabisa samia hawezi jisumbua kamwe kuumiza kichawa kwanza wazanzibar sio watu wa kupenda shida huoni siku hizi ndo kwanza anapaka lipustiki anakuwa kama binti hivi
 
We m
We mjinga Sana tafuta hotuba ya mama wakati anaapishwa kuwa raisi akisema miradi yote iliyo achwa na magufuli ataikamilisha na kuanzisha mipya. Na ndoo anachofanya saivi .
Kisema ni kitu kimoja kutekeleza ni kitu kingine
 
Werevu wanalazimisha kuwa wajinga zaidi pale wanapoambiwa JPM amejenga vituo vya afya nchi nzima, bwawa la JKNHP, SGR, flyover, barabara kubwa ya njia nane, meli kedekede, na mambo haya yako hadi makwao wanakoishi

Eti wanataka wawe vipofu na viziwi wasione wala kusikia alichofanya huyu mwamba!

Pumbavu sana mnaodhani ni wasomi na werevu halafu mnalazimisha kufunga masikikio na kuziba macho yenu kisa JPM kamwambia Mbowe alipe kodi blicanas akajidai eti yeye ni mpinzani atapiga kelele kwa mabeberu!

Acheni wehu basi nyinyi wasomi!

Mkifanya vema hata nyinyi tutawapongeza tuu!

Hapo ulipo huna lolote na ndiyo maana anazungumziwa JPM
Ukiwa Rais muovu lazima uzungumziwe tu, sasa ulitaka uzingumziwe mtu kama wewe?
 
Back
Top Bottom