Mishahara kuchelewa, kipimo kingine cha uwezo wa Rais Samia

Mishahara kuchelewa, kipimo kingine cha uwezo wa Rais Samia

Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.

Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
serikali ina kz nyingi kwa taarifa za chini ya kapet mshahara utachelewa sbb kulipa malimbikizo na vyeo vipya wataanza kulipwa mwezi huu
 
24 unalalamika? kuna taasisi qamezoea kupitishwa hadi tarehe 2.

lakin kama pia unaona ni ishu. tafuta biashara kuliko kukaa unasubiria mshahara wa serikal.. halad ulichelewa unalalamika.
boss hanuniwi
Bosi hanuniwi? Pale tu kabebwa na katiba.
 
Kwa kweli nashangaa, kwani hata mwezi haujaisha! Afadhali ingekuwa tarehe 30 ndiyo ungeanza kulalamika.
Ikifika tarehe 30, itakuwa watumishi wamefanya kazi zaidi ya mwezi mmoja bila malipo. Maana mwezi Jana mishahara ilitoka tarehe 23 hadi 24.
 
Kati ya vitu JPM alifanikiwa sana ni kuweka predictability na consistency katika utawala wake, na kwake suala la mishahara ya wafanyakazi hakucheza nalo. Sikutegemea kabisa kama hili la mshahara lingeanza kuchezewa mapema hivi.
Sasa kama aliweka mishahara fixed, hakuna cha nyongeza wala madaraja kwa miaka 6 ni wazi kusingekuwa na marekebisho yoyote jambo ambalo lisingechelewesha mishahara.....
 
Kuna ka ujinga watu wengi wanako, eti mshahara umechelewa.

Mfano umepewa mshahara wako tarehe 25, na mshahara unaofuata unapokea tarehe 25. Sasa kuna tofauti gani na tarehe 30 hadi tarehe 30?

Idadi ya siku ni zile zile
 
Sasa kama aliweka mishahara fixed, hakuna cha nyongeza wala madaraja kwa miaka 6 ni wazi kusingekuwa na marekebisho yoyote jambo ambalo lisingechelewesha mishahara.....
Suala la kuchelewesha mishahara halina uhusiano wowote na kiwango cha mishahara inayolipwa. Mwajiri hulipa mshahara kwa kadri ya uwezo wake, lakini ulipwe kwa wakati. Fluctuation ya namna yoyote ile katika tarehe za kulipa mshahara hudhihirisha either huna cha kulipa au huna nidhamu/unapuuza tu wafanyakazi wako.
 
Kuna ka ujinga watu wengi wanako, eti mshahara umechelewa.

Mfano umepewa mshahara wako tarehe 25, na mshahara unaofuata unapokea tarehe 25. Sasa kuna tofauti gani na tarehe 30 hadi tarehe 30?

Idadi ya siku ni zile zile
Hii comment yako ni kutetea ujinga tu.
 
Watu ni walalamishi Sana,kuzidi siku moja tu tayari watu mshaanza kumtoa kasoro rais,Mimi mwenyewe ninaishi kwa kutegemea salary lakini simlaumu rais ,ni kawaida tu,tujifunze kuwa na vipato mbadala hii itatuondolea Hali za stress.mimi hapa hata Kama mshahara utachelewa siku kumi na tano mbele bado naweza ishi bila shida kwa sababu licha ya kuwa mtumishi bado Nina kazi nje ya utumishi ambayo nikiifanya siwezi kosa laki tatu kwa mwezi hapa lazima maisha yasonge.

Watumishi wenzangu tujitume tuache kukishi kwa kutegemea mshahara tutajikuta na tutaishia kuwa watu wa lawama tu.
 
Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.

Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
Badala ya kuja na wazo kwamba mishahara isitishwe ndani ya miaka mitatu, ilifedha hizo zikaelekezwe kwenye miradi itakayoweza kujenga ajila za watu million kumi, we we unatuletea mishahara kuchelewa mapema hiii.
 
Back
Top Bottom