Mitandao ya kijamii siku hizi imekuwa chanzo kikubwa cha stress na msongo wa mawazo kwa vijana

Mitandao ya kijamii siku hizi imekuwa chanzo kikubwa cha stress na msongo wa mawazo kwa vijana

Wakuu habari zenu,leo kidogo tuzungumzie kuhusu hili la mitandao ya kijamii.

Siku hizi maisha yamegeuka sana,ni ngumu sana kudeal na stress na msongo wa mawazo hasa pale unapokuwa unapitia kipindi kigumu katika maisha.

~Umeachana na mpenzi wako uliyempenda sana,kesho unamuona facebook,instagram or WhatsApp anakula maisha na mpenzi mpya tena aliyekuzidi viwango.

~Unaperuzi facebook mara unakutana na picha za jamaa uliowaacha shule tena wale vilaza kabisa wanakula good time,wakati huo wewe upo tu nyumbani kwa shemeji na vyeti vyako vya chuo havina kazi.

~Hujabahatika kupata mtoto, unapita mitandaoni watu wanapost picha za birthday za watoto wao, huku upande wako mawifi wanakusakama kila kukicha kwamba unakula tu na kujaza choo.

~Au unapitia chats kwenye group unakutana na mapicha wenzako wote uliosoma nao wanaolewa huku wewe upo nyumbani umezalishwa huna mbele wala nyuma.

~Ni ngumu sana kukutana na hizo mambo ukapotezea,lazima zitakuathiri kwa kiasi flani, na mara nyingi husababisha watu kupata hali ya upweke, mfadhaiko,wivu uliopindukia au kumfanya mtu awe depressed na mara chache watu huishia kujiuwa kabisa.

______________________________________
Youngblood
Sasa mtu umeshaachana nae unamfatilia wa nini??

Ukiona mtu mmeachana nae ila we bado unamfatilia kwa kila anachofanya basi we bado unamtaka wakati ye ameshakusahau na anaendelea na maisha yake

Kwahiyo stress za hivi ni za kujitakia tu wala hazina mantiki
 
Sasa mtu umeshaachana nae unamfatilia wa nini??

Ukiona mtu mmeachana nae ila we bado unamfatilia kwa kila anachofanya basi we bado unamtaka wakati ye ameshakusahau na anaendelea na maisha yake

Kwahiyo stress za hivi ni za kujitakia tu wala hazina mantiki
Inatokea sana tu hasa pale ambapo wewe ndiye ambaye umeachwa?

BTW habari yako Jimena .
 
Kanuni 10 za kushinda sononeko katika mitandao ya jamii.

1. Usijilinganishe na watu wengine. Jilinganishe na wewe mwenyewe wa kabla. Kuna mtu mwanamme alimzidi mshahara mwanamke kazini, akashangaa huyu mwanamke mbona anavaa nguo za fahari, ana gari la fahari, wakati namzidi mshahara? Kumbe mwenzake anahudumiwa na mumewe.

2. Furahia mafanikio ya wenzako. Kuwa na kijiba cha roho kwa sababu mwingine kafanikiwa si tabia mbaya tu, ni tabia inayokupa sononeko lisilo na sababu.

3. Badala ya kusononeka watu wengine wanapofanikiwa, jaribu kutafuta sababu za mafanikio yao. Kuna watu wengine wanaonekana wamefanikiwa lakini wamefanya mambo ya aibu kama umalaya na kuuza madawa ya kulevya. Kwangu kupata hela kwa njia hizo si mafanikio.

4. Tambua si kila anayeonekana kafanikiwa amefanikiwa kweli, na si kila anayeonekana hajafanikiwa hajafanikiwa. Waingereza wanasema "everything that glitters, is not gold". Kuna watu wanajua kujiweka kama wamefanikiwa katika mitandao ya jamii, wakati hawana lolote. Halafu kuna kina Said Bakhressa kuwaona mitandao ya jamii wanajitapa ni kazi sana.

5. Tumia muda mwingi zaidi katika kufanya shughuli za maendeleo, kusoma, kufanya kazi, kufanya biashara na kadhalika, zaidi ya kuangalia mitandao ya jamii.

6. Pambana na hali yako. Kama unataka mambo makubwa, fanya utafiti wa kitu kipi kitakutoa na kukupa kipato na nafasi ufanye makubwa.

7. Ukishindwa kabisa kubadili hali yako, kubali ukweli na kubali maisha yako. Ukiwa na tamaa kamwe huwezi kutosheka hata uwe mfalme wa dunia utataka utawale na Mars. Ukiwa mtu wa kuridhika unaweza kuwa na amani kwa shamba lako dogo tu. Inawezekana mwenye kidogo akaishi kwa amani kuliko mwenye kingi.

8. Elewa kwamba kujionesha sana mitandao ya jamii kuna ku expose kwa mengi. Kuna wezi wanaangalia nani ana mali gani tumuibie, kuna madanga yanataka kufuatilia watu, kuna ma hackers wanataka ku hack na ku blackmail. Wanaojionesha sana mitandaoni wana ji expose kwa wote hao.

9. Tambua mitandao ya jamii ni chanzo cha wivu na magomvi mengi katika jamii. Wanaojinadi sana wanapata magomvi sana.

10. Tambua watu wengi huheshimika sana mpaka wanapoonekana upumbavu wao kwenye mitandao ya jamii. Unavyozidi kutumia muda kwenye hii mitandao na kuipa nguvu, ndivyo unavyozidi kuanika upumbavu wako.
Kula supu ya kongoro nakuja kulipa
 
Kama hapa jf ndo kiboko unaeza kuta unatoleana povu na mkeo,mmeo au x wako bila kujua na mkikutana home una kile kinyongo cha mtandaon bila kujua aliekupa hiko kinyongo ndo huyo unalala nae usiku🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kuna watu ukiwaona mitandaoni unaweza kusema dah..mbona mie nimechelewa..Lakini sasa kutana nae Live hahahahahah utabaki unajichekea tuu..🤣🤣
 
That's the spirit my man.

Zile colognes kwa sasa zimezidi mara mbili.

Nilikuta watu wanaongelea perfumes na colognes, na mimi kama kawaida yangu si mgumu wa kuchangia kwenye hoja ninayoipenda.

Na tangu siku ile sijawahi tena kupost zile picha.

Maana ilikuwa mpaka Nyani Ngabu mtu wa ma cologne hajaamini kama picha ya kwangu, alifikiri nimeiokota kwenye internet.

Na mimi nilijua watakuwapo watu wa kuhoji, kwa hiyo nilivyopiga picha niliweka kikaratasi nimeandika "Kiranga".

Nikamwambia Nyani Ngabi hebu zoom katikati ya picha chini utaona salamu zako hapo.

Mwenyewe alizima fegi, alimeza moshi na kuutolea masikioni.

Jivin'.
Hahahahaha
 
Niliteseka sana mwaka miaka ya nyuma enzi za JK nikiona watu wanapost wako kwenye ndege siti ya dirishani. Nikasema ee Mungu niwezeshe na mimi siku moja nipande ndege ila kwa mara ya kwanza isiwe Bombardier wala hizi ndogo za kina Coastal aviation (nilikuwa specific kwenye maombi)... na pia niliomba ikiwezekana iwe nje ya nchi. Miaka kadhaa mbele siku ikafika baada ya majaribio kadhaa ya kutaka kukata tiketi fastjet kutofanikiwa. Siku hiyo nakumbuka nilikata tiketi ya fastjet kutoka Dar - KIA nililipia Tsh 77,000/= taslimu. Ndege ya saa moja jioni. Kuanzia saa 8 mchana nilianza kuaga watu wangu wote muhimu pia kuwajulisha wenyeji wangu kwamba nitatua na mwewe. Nikafika JNIA mapema kabisa ila kilichotokea kilinisikitisha sana.. nilidhani ndege ni unapanda tu kama basi. Nikajiambia nitaenda kupanda dakika 15 kabla ya ndege kuondoka. Huo muda mwingine nikawa bize kuchukua selfie na video clip maeneo ya airport kwa kumbukumbu. Sikuamini nilivyoambiwa muda ushapita hata milango ya ndege ishafungwa kwahiyo nikate tu tiketi nyingine ya kesho saa 4. Ilibidi nifanye hivyo. Bahati nzuri baada ya hapo nikaanza kusafiri nchi mbalimbali. Kwa kifupi picha za mitandao zilinisaidia kunipa machungu na kufanya kazi kwa bidii zaidi
 
Ni kweli kabisa...Ila kitu cha muhimu, maisha yanayooneshwa kwenye Facebook siyo halisi... Kwanini nasema siyo halisi..? Siyo halisi kwasababu watu wanaonesha side moja ya maisha yao...yani ule upande wa raha, na kula bata...lakini maisha hayapo hivyo...kuna upande mwingine...kuna magonjwa, misuko suko, njaa, kiu, masumbuko,, mabalaa...hivi watu hawataki kuvionesha...

Sasa mkuu ukiwa na njaa utaiyoneshaji fb nikitu ambacho nikama Imani unais ni njaa ambayo mtu hawez kuiyona utawezaje kupost njaa fb[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Niliteseka sana mwaka miaka ya nyuma enzi za JK nikiona watu wanapost wako kwenye ndege siti ya dirishani. Nikasema ee Mungu niwezeshe na mimi siku moja nipande ndege ila kwa mara ya kwanza isiwe Bombardier wala hizi ndogo za kina Coastal aviation (nilikuwa specific kwenye maombi)... na pia niliomba ikiwezekana iwe nje ya nchi. Miaka kadhaa mbele siku ikafika baada ya majaribio kadhaa ya kutaka kukata tiketi fastjet kutofanikiwa. Siku hiyo nakumbuka nilikata tiketi ya fastjet kutoka Dar - KIA nililipia Tsh 77,000/= taslimu. Ndege ya saa moja jioni. Kuanzia saa 8 mchana nilianza kuaga watu wangu wote muhimu pia kuwajulisha wenyeji wangu kwamba nitatua na mwewe. Nikafika JNIA mapema kabisa ila kilichotokea kilinisikitisha sana.. nilidhani ndege ni unapanda tu kama basi. Nikajiambia nitaenda kupanda dakika 15 kabla ya ndege kuondoka. Huo muda mwingine nikawa bize kuchukua selfie na video clip maeneo ya airport kwa kumbukumbu. Sikuamini nilivyoambiwa muda ushapita hata milango ya ndege ishafungwa kwahiyo nikate tu tiketi nyingine ya kesho saa 4. Ilibidi nifanye hivyo. Bahati nzuri baada ya hapo nikaanza kusafiri nchi mbalimbali. Kwa kifupi picha za mitandao zilinisaidia kunipa machungu na kufanya kazi kwa bidii zaidi
Kuna siku nilitaka kujipindua hivyo hivyo hapo Dar.Nilikuwa nakwenda Mwanza.

Nimekaa nasikiliza mziki mkubwa kwenye headphones, nikajisahau.Kuja kustuka dakika chache tu zimebaki milango ya ndege ifungwe.

Ilibidi niharakishe kuingia kwenye ndege, nafikiri nilikuwa mtu wa mwisho.

Sasa kuingia kwenye ndege, air hostess alikuwa kashatoa matangazo watu wazime simu, mimi sikusikia, kwa sababu yalitolewa kabla sijapanda nafikiri.

Nikawa nawapigia simu wenyeji wangu Mwanza kuwajulisha nitatua muda gani.

Huo mzozo uliozuk hapo ilibidi mpaka mzee mmoja wa usalama aingilie.Maana hatukuelewana na air hostess, yeye alifikiri mimi nimesikia tangazo nafanya ukaidi tu, wakati tangazo lilitolewa kabla mimi sijaingia kwenye ndege.

Habari hii inatufundisha tuwahi kupanda kwenye vyombo vya usafiri kuepuka usumbufu.
 
Mkuu umenigusa sana nikionaga watu na watoto nahisi kama wao ni special sana aisee..[emoji22]
Unachokisema ni kweli wakati mwingine unamu unfollow mtu maana anachangia hoja kubwa ya kukunyanyasa kifikra bila yeye kujua
Kuna watu yani since day 1 wao mambo yao hayajawahi kupinda ..bora Jf hatuonani aisee
😂😂😂😂
 
Kuna watu ukiwaona mitandaoni unaweza kusema dah..mbona mie nimechelewa..Lakini sasa kutana nae Live hahahahahah utabaki unajichekea tuu..[emoji1787][emoji1787]
[emoji23]ni kweli kabisa mkuu,kuna watu wanajua kweli kuigiza
 
Wakuu habari zenu, leo kidogo tuzungumzie kuhusu hili la mitandao ya kijamii.

Siku hizi maisha yamegeuka sana, ni ngumu sana kudeal na stress na msongo wa mawazo hasa pale unapokuwa unapitia kipindi kigumu katika maisha.

~Umeachana na mpenzi wako uliyempenda sana, kesho unamuona facebook, instagram or WhatsApp anakula maisha na mpenzi mpya tena aliyekuzidi viwango.

~Unaperuzi facebook mara unakutana na picha za jamaa uliowaacha shule tena wale vilaza kabisa wanakula good time, wakati huo wewe upo tu nyumbani kwa shemeji na vyeti vyako vya chuo havina kazi.

~Hujabahatika kupata mtoto, unapita mitandaoni watu wanapost picha za birthday za watoto wao, huku upande wako mawifi wanakusakama kila kukicha kwamba unakula tu na kujaza choo.

~Au unapitia chats kwenye group unakutana na mapicha wenzako wote uliosoma nao wanaolewa huku wewe upo nyumbani umezalishwa huna mbele wala nyuma.

~Ni ngumu sana kukutana na hizo mambo ukapotezea, lazima zitakuathiri kwa kiasi flani na mara nyingi husababisha watu kupata hali ya upweke, mfadhaiko, wivu uliopindukia au kumfanya mtu awe depressed na mara chache watu huishia kujiua kabisa.

______________________________________
Youngblood
Kikubwa kujikubali, kuna best friend wangu nilisoma nae primary na maisha kiasi ya o level nilipata kukaa kwao, hakunahatika kupata nafasi ya kwenda high school. Nipo mwaka wa tatu ndio kaenda chuo cha ualimu. January kanipigia alipata nafasi ya ualimu na Mungu kamjaalia mtoto.
I mean, kila jambo lina wakati wake. Hakuna maisha ya “group “ binafsi sipendi kushika life theories za life begins at 40s etc, hakuna fixed guarantee ya kuwa pahala kutokana na level ya elimu au umri ulonao au jamii/ matafiki walokuzunguka
 
Back
Top Bottom