Mizengo Pinda: Tuanze mchakato wa kuwa na Tume huru ya Uchaguzi
Binafsi napenda tupate katiba mpya ila inahitaji mchakato mrefu, tuanze na jambo muhimu ambalo utekelezaji wa kuwa na Tume huru, na iwe huru kweli kweli, muswada wa marekebisho ya katiba unaweza andaliwa na kupelekwa bungeni NOW!
Wenzio hawataki, wanataka Katiba Mpya kwanza
 
Mazingaombwe......Baada ya kubanwa na mabeberu ndio mnaona umuhimu ya Tume huru ya uchaguzi? ...... CCM mnatia aibu sana kwa hihi tibia zenu.

Tunasubiria na katiba mpya !
Hapana!! Suala la Tume huru ya uchaguzi ni Muhimu sana na ni takwa la wananchi na sio mabeberu ili kukidhi haki ya kuchagua na kuchaguliwa!

Hapo hamna ubeberu hapo
 
Mh!! Hata shetani akizeeka anakuwa Malaika......

Halafu Pinda ukimrudisha madarakani leo, hayo maneno atayakana mchana kweupe.

Hata Mama Samia siku akitoka madarakani utasikia tumechelewa sana kupata katiba mpya.
 
"Kuna mambo ambayo sisi CCM kama chama tawala lazima tubebe dhima. Tutoe uongozi. Kwa, mfano hili la Tume Huru ya Uchaguzi kizuizi ni nini? Hili ni jambo ambalo lazima tukubaliane na wenzetu wa upinzani na tuanze mchakato wa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi"

Chanzo: Darmpya
Hili suala la tume huru ya uchaguzi ni suala la msingi sana.

Kilichotokea 2020 hakikuwa na afya kwa nchi yetu ipo siku kutaiangamiza nchi.

2008 kenya waliuana law sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

2010 Zimbabwe wakauana kwa sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

Ivory coast waliuana kwa sababu ya tume ya uchaguzi.

Tunataka mpaka nini kitokee ndiyo tujue umuhimu wa tume ya uchaguzi.
 
Endeleeni kushupaza shingo, hamjifunzi, huku kushupaza shingo kwenu ndiyo kulisababisha tukose katiba mpya 2014
Hivi wewe unadhani kila Kitabu kutoka BMK ilikuwa Katiba! Tanganyika bado kuna tatizo kubwa sana!
 
Pinda anasema iundwe tume huru ya uchaguzi lakini baadhi ya wana CCM wanadai tume iliyopo ni huru.Kwa kweli karibu anguko la shetani linakaribia,maana ni vigumu shetani kushindana na Mungu.
 
Kwa nini mnapenda kupinga, kukashfu na kubeza kila kitu, as long as kinatoka upande ambao hamkubaliani nao? Kwa style hii itachukua muda mrefu sana wapinzani kutoboa
Kwa nini mwachukia sana kupingwa? Kwa nini mnaogopa sana maoni tofauti? Ugonjwa gani huu mlionao?
Nadhani hamjiamini HASA kwa vile huwa hamna majibu ya hoja kinzani.
 
Hili suala la tume huru ya uchaguzi ni suala la msingi sana.

Kilichotokea 2020 hakikuwa na afya kwa nchi yetu ipo siku kutaiangamiza nchi.

2008 kenya waliuana law sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

2010 Zimbabwe wakauana kwa sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

Ivory coast waliuana kwa sababu ya tume ya uchaguzi.

Tunataka mpaka nini kitokee ndiyo tujue umuhimu wa tume ya uchaguzi.
Umenena point tupu mkuu!
Na sisi kwa mtazamo wa mzee huyu imepaswa tuongoze gia ili tukoleze mwendo wa kuipata Tume huru ya uchaguzi
 
Endeleeni kushupaza shingo, hamjifunzi, huku kushupaza shingo kwenu ndiyo kulisababisha tukose katiba mpya 2014
CCM si mliendelea na Bunge la Katiba mpya na mkapigisha kura Hadi watu waliokuwa mahututi huko India Ili column ienee!
Na tukabiwa Katiba pendekezwa imepitishwa na kilichobaki ni kupeleka Kwa wananchi ikapigiwe kura!!!

Sasa swali:Kushupaza shingo kulizuia Nini CCM/Serikali kuipeleka Katiba pendekezwa Kwa wananchi ikapigiwe kura???

Acheni ujinga!
 
Tume huru ya uchaguzi lazima ianze na katiba, uwezi kutunga Sheria iliyo kinyume cha katiba. Mzee Pinda atusaidie yeye hiyo tume huru inaundwaje endapo katiba inabaki ileile?

Je hiyo tume itatokana na wananchi au itatokana na wanasiasa? Nadhani kujadili kuwa na tume huru ni makosa na nimchongo wa TCD kupunguza Kasi ya mambo yanayoendelea Sasa. Tumekwama na tumekuwa watu wakulumbana Kwa miaka Sasa, malumbano yalianza baina ya viongozi lakini Sasa yamekwenda Hadi Kwa wananchi wa chini, hakuna mwenye Imani na mfumo wa kisiasa na hata waliopitishwa na mfumo uliopo wa siasa hakuna mwenye uwezo wakusimama mbele ya wananchi kusema walimchagua.

Hoja ibaki moja TU ya katiba mpya, ndani ya katiba mpya mengine yote yatapata ufumbuzi. TCD waache agenda za michongo, wasimame kuhesabiwa kwa kudai Kati mpya SIYO kuitia Katiba viraka.

Mwisho, wanapojadili Tum huru wajiulize bunge lakupitisha hiyo sheria ya kuunda tume huru ni lipi? Bing la Sasa linaweza kupitisha sheria ya Tume huru? Bunge la chama kimoja lipitishe sheria ya kuunda tume huru.....labda wapewe maelekezo.

Tukitaka tume huru tutengeneze bunge jipya la katiba , la sivyo hata bunge la kubadili sheria Kwa sasa halikidhi vigezo vya mabunge ya kidemokrasia
 
Back
Top Bottom