Mizengo Pinda: Tuanze mchakato wa kuwa na Tume huru ya Uchaguzi
2531624_IMG-20200921-WA0009.jpg
 
Mh!! Hata shetani akizeeka anakuwa Malaika......

Halafu Pinda ukimrudisha madarakani leo, hayo maneno atayakana mchana kweupe.

Hata Mama Samia siku akitoka madarakani utasikia tumechelewa sana kupata katiba mpya.
Kabisa Mkuu. Utashangaa mpaka akili yako isielewe je Ni huyu huyu aliekubali kipindi kile au mwingine. Wanachungulia Sana maslai.
 
Misimamo iliyopitiliza kwenye dunia ya sasa ndiyo mambo ya "Kilongi" chief, siku hizi issues zinaisha kwa mazungumzo na "compromises", Ni mwendo wa kula na kuliwa, wewe ukitaka kula tu basi dunia ya sasa inakutema! Mambo ya akina Fidel castro, Che Guavara, Mugabe hayana nafasi kwenye ulimwengu wa sasa
Tulishatoka huko Zanzibar na muuafaka, Kikwete na katiba mpya na kualika upinzani Ikulu labda kama ulikua ujazaliwa.
Mwisho sasa, MaCCM yakapindua meza.
Katiba mpya ni lazima na ni sasa.
 
Kwa nini mnapenda kupinga, kukashfu na kubeza kila kitu, as long as kinatoka upande ambao hamkubaliani nao? Kwa style hii itachukua muda mrefu sana wapinzani kutoboa
Wapinzani sio kwamba wanataka kutoboa au usifikiri wanataka madaraka tu. Wanataka kuikomboa nchi kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi. Nchi iwe huru na mfumo unaoeleweka. Sio leo anakuja mpigaji anaanza kuzima zima umeme kuanzia asubuhi. Tunataka uhakika wa mambo mengi. Kama hawa mafisadi kupitia madowans katiba iseme tu piga risasi kama china. Mtu anapatikana na nyumba 100 wakati mshahara wake unajulikana twanga risasi.
 
Makada wenzangu wa ccm tutafute kazi za kufanya tuanze ujasiriamali mapema tujiandae kisaikoloji kuvaa vimini na kuuza Baa na kukata maumo, tuendako ni kugumu sana kwa upande wetu maisha yana kasi ya 5G tunapotea kwenye rama soon pesa ya umma inaenda kua mama mkwe,mambo ya kulala mbele na mabegi ya kura yanaenda kukomeshwa
Sijui watakuelewa?
 
Makada wenzangu wa ccm tutafute kazi za kufanya tuanze ujasiriamali mapema tujiandae kisaikoloji kuvaa vimini na kuuza Baa na kukata maumo, tuendako ni kugumu sana kwa upande wetu maisha yana kasi ya 5G tunapotea kwenye rama soon pesa ya umma inaenda kua mama mkwe,mambo ya kulala mbele na mabegi ya kura yanaenda kukomeshwa
Waliopo madarakani hawatakubali
 
"Kuna mambo ambayo sisi CCM kama chama tawala lazima tubebe dhima. Tutoe uongozi. Kwa, mfano hili la Tume Huru ya Uchaguzi kizuizi ni nini? Hili ni jambo ambalo lazima tukubaliane na wenzetu wa upinzani na tuanze mchakato wa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi"

Chanzo: Darmpya
Mmgghhff labda !!!.

Hata Nyerere aliuona udhaifu wa katiba, baada tu ya kutoka madarakani. Polepole naye , Sumaye naye, Lowasa pia na Mzee Warioba pia . Hivyo sishangazwi na Pinda
 
Wapinzani sio kwamba wanataka kutoboa au usifikiri wanataka madaraka tu. Wanataka kuikomboa nchi kutoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi. Nchi iwe huru na mfumo unaoeleweka. Sio leo anakuja mpigaji anaanza kuzima zima umeme kuanzia asubuhi. Tunataka uhakika wa mambo mengi. Kama hawa mafisadi kupitia madowans katiba iseme tu piga risasi kama china. Mtu anapatikana na nyumba 100 wakati mshahara wake unajulikana twanga risasi.
Aliyekuambia China wanapiga risasi mafisadi nani?
 
Sijui watakuelewa?
Watanielewa tu sina ubaya nimesoma upepo unavyovuma wasiponielewa muda utawaelewesha tu

Makada tuanzishe group letu la kikoba anatoka Moja Moja kila siku Mimi nitakuwa kijumbe sawa

inabidi tuanze kujifunza maisha ya uswahili mapema tujifunze kusalimia watu maviete yatabaki Historia
 
Back
Top Bottom