Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania


Nairobi huwa kuna sherehe? Pesa yote wanaimalizia kwenye kupamba garden na keki inayokatwa mnalishwa ukumbi mzima na umma moja? May hiyo nido sherehe kwa Nai @ Nyamayao
 
Yaan unakuta mtu mlisoma nae na mlikuwa hamuwasiliani ila akikaribia kuoa au kuolewa, salam kama dozi ya maleria kutwa mara tatu, mwisho wa siku kumbe anataka michango
 

Juzi hapa nilialikwa kuhudhuria kikao cha harusi, hiyo harusi ni ya ndugu yake na girl friend wangu,huyo ndugu wa mpenzi wangu hana kazi, anakaa na huyo bwana wake na wamezaa mtoto mmoja.

Mume wake hana kazi ya kueleweka, wakataka wafunge ndoa,garama za ndoa zikatakiwa zibebwe na upande wa mke.

Bajeti ikapangwa milioni tisa, bwana harusi hana hata mia, yote hiyo ikatakiwa itoke kwa watu kwa njia ya michango, hao wanandoa wanaishi nyumba ya kupanga.

Nikauliza watu kwenye kikao kwa nini hiyo pesa tusiwape hata wakafungua fremu kuliko kwenda kuiunguza kwa siku moja alafu hawa watu waendelee kuishi maisha magumu, sikueleweka,pesa ikataftwa hadi ikapatikana na ndoa ikafungwa.

Huu ni uharibifu mkubwa wa rasilimali fedha na mipango mibovu, kufanya maonyesho ya ndoa huku kesho watu wanarudi kuishi maisha yale yale ya siku zote.
 

Mkuu, watanzania hatuchangii maendeleo ya mtu. Ndiyo maana hukueleweka kikaoni.
Ni rahisi mtu kuchangia usafiri wa marehemu fedha nyingi kuliko kumpa hela ndogo ya dawa akiwa mgonjwa!
Jirani zetu Kenya wanachangiana kupeleka watoto shule / vyuoni. Sisi michango yetu ni arusi, sendoff,birthday, kupaimara nk.
Tuna safari ndefu kupata maendeleo.
 
Nina kadi za michango saba, nimeshachangia tatu bado nne nimekasirikiwa na wahusika yani haya mambo ni shida sana.
 
mi nilishatoa tangazo ofisini kwetu kuwa wasinipe card sitachanga... kwenye budget yangu siweki na boss wangu haniongezei fungu la michango...
 
Mmh naona Kila mtu amechoshwa na michango humu, sijui hao wanaochangisha hawamo humu? Afu hivi kati yetu Hamna ambao walifanya harusi kwa kuchangisha watu, it's payback time eti, ulitolewa michango na wewe utoe sasa hivi.

Hako ni kaustaarabu ketu waafrika for years now. Ingawa kameanza kutupiliwa mbali, watu budget zetu kali. Ukiona hakuna umuhimu wa kuchanga wala kuchangiwa basi usimchangie mtu. Ila kama unategemea siku moja kuja kuchangiwa basi changa tu kwanza kabla hujachangiwa. Afu kama hutaki kumchangia mtu usimchangie tu, mwambie sina hela full stop. Hamna haja ya kujinung'unisha
 
Inakera sana hii michango....hapa Nina kadi zaidi ya tano, zinagongana tarehe...kichwa chanipasuka...
 
Kwa kweli hii michango ni janga la taifa imenifilisi vya kutosha,jana usiku nilikaa kutathmini yani toka january nimetoa hela nyingi kwa ajili ya harusi ambazo in actual sense zingefanya kazi nyingine ya maana sana,leo asubuhi nimeamka salamu ya kwanza mezani nakuta kadi nyingine nikauliza ya nan naambiwa mchango wa harusi eti anataka laki moja jirani yangu kaleta,hivi wanaume wenzangu mkichukuana mkawekana ndani kama mke na mume mtapungukiwa nini? mbona sisi tumefanya hvyo na bdo tunaishi?
Kuanzia leo sitoi tena mchango wa harusi....
 
Haya mambo ya kuchangia harusi niliacha siku nyingi na nina amani ile mbaya. Lililosababisha hasa nikaacha ni baada ya mfanyakazi mwenzangu kunisema maneno machafu kisa nilimwambia anisamehe sina mchango kwa wakati huo ila nitatafuta zawadi mambo yangu yakiwa mazuri niwapelekee nyumbani kwake akiwa tayari ameshaoa. Lah! ilikuwa balaa, jamaa akasema mpaka jasho linamtoka. Ahhh, hapo nikaamua isiwe shida, toka kipindi hicho, no mchango wa sherehe yeyote, period. Tena mtu akinifata namwambia wazi, 'tafadhali sichangii sherehe yoyote' na kadi huwa sitaki kuchukua kabisaaaa!.Ila kwenye matatizo ndio nipo roho nyeupe kuchangia.

Pia inatakiwa uwe makini maana isije we hutaki kutoa kwa wenzio halafu vya kwako unaomba michango!. Hapo utakosea sana. Cha maana ni kuwa neutral tu, we huombi wala pia hutoi. Huwa inakuwa ngumu watu kukuelewa mwanzoni ila wakishakuzoea hata kadi hawaleti tena wanabaki kukwambia kwa mdomo tu huku wanatabasam, hahahhahah!.
 

That was perfect.... ugonjwa mtu hachangii halafu harusi ndo wanaipa kipaumbele..watu mtu hata ukiwa na mgonjwa hakuna msaada..utashangaa huyo mgonjwa akifariki michango ya msiba itakavyotiririka..aibu yetu watanzania
 
Moja ya kero kubwa na ambayo kwa mtizamo wangu inaweza kuwa kikwazo kwa wananchi wa kawaida kuendana na kaulimbiu ya hapa kazi tu, ni namna tunavyoendesha sherehe mbalimbali za kijamii, kama vile harusi, send-off party, kitchern party na sasa imeongezeka sherehe zingine kama ubatizo, kipaimara, graduation na engagement party.

Raia maskini hulazimika kuchanga pesa nyingi na wengi hulazimika kuingia kwenye mikopo ambayo huwatesa mno, mtu hulazimika kuchangia hata kama hana pesa kwa kuogopa kutengwa na jamii.

Tatizo la pili ni muda ambao sherehe hufanyika. Nyingi huisha usiku sana, "sherehe inaisha saa saba usiku au saa nane, unafika nyumbani saa tisa usiku, kupata usingizi saa kumi alfajiri, asubuhi unatakiwa uwepo kazini saa moja asubuhi. Hivi hapo ufanisi utakuwepo kweli?"

Tatizo la tatu ni siku za sherehe, ukiondoa harusi, sehemu kubwa ya sherehe zilizobakia hufanyika katikati ya wiki, jambo ambalo hupunguza kwa kiasi kikubwa utendaji kazini na wakati fulani huathiri mahudhurio ya wafanyakazi.

Ili kuendana na kauli mbiu ya hapa kazi tu, napendekeza wizara inayohusika na ustawi wa jamii ifanye yafuatayo;

  • Ipige marufuku michango yote ya sherehe, na atakayechangisha aadhibiwe vikali
  • Sherehe zote zifanyike weekend au siku za mapumziko
  • Mwisho wa sherehe zote uwe saa kumi na mbili jioni, adhabu kali itolewe kwa atakayezidisha muda

Familia ziendeshe sherehe kwa gharama zao wenyewe, wasiruhusiwe kuchangisha kwa mtu asiye mwana familia, nchi nyingine kama Zambia wameweza, kwanini sisi tushindwe. Kama nawe unakerwa na jambo hili, toa pendekezo, huenda wahusika nao wakapitia uzi huu.

Alamski!
 
Kwani watu hulazimishwa kutoa? Kwahiyo unataka uende kwenye harusi bila kutoa mchango? Umaskini hauishi kwa kutotoa michango ya jambo ka harusi, naona kila zigo mnamuangushia Magufuli.

Wewe usitoe mchango wako wengine watatoa.. Watu mnataka kuwa ka Yuda iskariote alivomwambia Yesu kuwa mwanamke anatumia mafuta ghali kumfuta miguu, kwanini yasiuzwe wapewe maskini. Yesu aka....... Umaskini mtakuwa nao siku zote
 
Kama kuna mtu analazimika kuchangia na kuhudhulia....sio mzima huyo akapime akili....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…