ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,753
- 9,575
kwani harusi yako iilikuwaje the bossMimi kinachonishangaza ni huu utaratibu unaosema eti ukichangia elfu hamsini unakwenda na mpenzi wako,,,,lakini ukichangia elfu 25 unenda peke yako na kadi imeandikwa kabisa ni single.....
Utasema concert....
Wabongo bana.....
Yaani huwezi kupata date ukaamua kwenda nae kwenye harusi
kwa kuwa ulitoa mchango wa single.....aghhhh...
Na bila mchango hualikwi....
[emoji2] [emoji2] [emoji2]NAOMBA WENYE USHAWISHI HASA MLIOPO DSM,MTUPE MBINU NA TECNIQUES ZA KUMALIZA HII KERO "ONCE AND FOR ALL".JAMANI WATU TUNAUMIZWA SANA NA HII MICHANGO,SIO SIRI.MHESHIMIWA MAKOND(RC WA DSM) TUNAOMBA MCHANGO WAKO WA MAWAZO WA JINSI KUMALIZA HII KERO HASA KWA WANANCHI WAKO WA DAR.MAANA NAKUAMINIA KWA UBUNIFU MKUU.
NAOMBA WENYE USHAWISHI HASA MLIOPO DSM,MTUPE MBINU NA TECNIQUES ZA KUMALIZA HII KERO "ONCE AND FOR ALL".JAMANI WATU TUNAUMIZWA SANA NA HII MICHANGO,SIO SIRI.MHESHIMIWA MAKOND(RC WA DSM) TUNAOMBA MCHANGO WAKO WA MAWAZO WA JINSI KUMALIZA HII KERO HASA KWA WANANCHI WAKO WA DAR.MAANA NAKUAMINIA KWA UBUNIFU MKUU.
Sio siri hii michango ya sherehe inaudhi sana na kibaya zaidi siku hz sherehe zimeongezeka...kitchen party, bachelor party, spinster party, engagement party, wring party, send off party, main party, cooking party, furniture party, kipaimara, kwaresma, ubatizo, birthday party, etc. Hizi sherehe zinaudhi sana. Kuna siku nililala na kadi za harusi zaidi ya 20. Nilijaribu kizichambua ili nichangie baadhi na nyingine niziache lakini nikashindwa. Kila kadi ilikuwa na kima cha michango kisichopungua 50,000, yaani 50,000 x 20 = 1,000,000. Jamani mtatuua na hii michango yenu ya harusi!
Nini kifanyike?
1. Serikali ianze kukata kodi kwenye michango ya harusi na kodi iwe kubwa (zaidi ya 60% ya michango yote) ili liwe fundisho kwa wachangishaji wote wa michango hiyo.
2. Serikali ipige marufuku harusi kufanyikia kwenye kumbi za sherehe....ielekeze sherehe zote kufanyikia nyumbani kwa bwana/bibi harusi na zifanyike kati ya saa 6 mchana hadi saa 12 jioni ili kutoa nafasi kwa wananchi kurudi makwao mapema pasipo kuchoshana.
3. Serikali ipige marufuku matumizi ya watoto wadogo kwenye sherehe ili kuwazuia kushuhudia mambo makubwa yafanyikayo kwenye sherehe hizo na kuwadhulumu haki yao ya kulala mapema.
4. Yeyote atakayekiuka makatazo haya afungwe jela sio chini ya miaka 30 (kama wabakaji wanavyofungwa).
Nawasilisha.
Unataka kumtega mkuu wa mikoa, ee..!!??NAOMBA WENYE USHAWISHI HASA MLIOPO DSM,MTUPE MBINU NA TECNIQUES ZA KUMALIZA HII KERO "ONCE AND FOR ALL".JAMANI WATU TUNAUMIZWA SANA NA HII MICHANGO,SIO SIRI.MHESHIMIWA MAKOND(RC WA DSM) TUNAOMBA MCHANGO WAKO WA MAWAZO WA JINSI KUMALIZA HII KERO HASA KWA WANANCHI WAKO WA DAR.MAANA NAKUAMINIA KWA UBUNIFU MKUU.
Wenye fedha halafu wanachangiana?Huu si utakuwa ujinga?Kama una fedha unachangiwa nini tena?Si ugharimie halafu utakaowaalika ndio wakupe tu zawadi!Waache wenye uwezo wa kifedha waendelee kuchangiana,wewe kama huna shauri yako,binadamu hawafanani usiwasemee watu,usisema twafa sema nafa,mtu anaeingiza sh mil 3 kwa mwezi simi kama ni tatizo kwake kuchangia harusi kiwango chochote,tatizo letu tu wavivu na waoga wakuchangamkia fursa,kazi kubwa ni kubet mda wote.
hii nimeipenda watanzania yufungue macho katika hiloHaya majadiliano kuhusu michango ya harusi ni mwanzo mzuri wa mwisho wa jambo hili. Ingawa nia ya kuchangiana ni kujenga mshikamano katika jamii na miongoni mwa wanajamii, hali inavyoendelea michango itachukua sura nyingine haswa pale wengio wanaochanga watakapogundua kuwa wanaokuza mila hii mpya ni wanaofaidika kibiashara na michango hii. Nionavyo mimi michango ya harusi ni chain ya business ya wale wote wanaohusika na huduma mbali mbali za harusi- wenye kumbiza harusi, wapika keki, vinywaji , washona nguo, wenye salon, magari, ma MC etc, . Hawa watapigana sana michango isiishe. Wakati mwingine nawafanansisha hawa na ngariba wa tohara kwa watoto wa kike. Wamejizatiti kuhakikisha haiachwi maana wanafadikika. Matumaini yangu ni kuwa hali ngumu ya maisha itaanza kutunyorosha tuanze kufikiri mambo yaliyo ya msingi na kuacha yasiyo ya msingi. Kikubwa vipaumbele vyetu ni vya ajabu sana. Jaribu kuomba michango ya mgonjwa hakuna watu wengi wa kujitolea omba michango ya harusi wengi watakuchangia. Hivi inaleta akili harusi za million 100 wakati kuna watoto wandugu, jamaa, jirani hawaendi shule hivi hii sio kufuru?Mbona tunaiga sana mambo mengi toka mataifa ya nje ila la harusi ndogo na gharama nafuu hatuigi? mfano kwa Australia, sherehe ya harusi ni swala la mtu binafsi na haizidi watu 20 wanaolikwa hotelini na kujilipia wenyewe. Wataliano na wagiriki wanatabia kama zetu waafrica, harusi kubwa, majumba na magari makubwa ni mawazo ya kiajabau sana. Cha ajabu watu hatuelewi kuwa mtoto mmoja wa jirani ama ndugu asipoenda shule na kukua bila kusoma na kuandika ni mzigo kwetu sisi sote na utatuumiza katika kodi maana mtoto huyu hataweza kuchangia uchumi wa taifa ipasavyo. WaTanzania tubadilike. Hata mimi sichangii harusi badala yake ninatoa elimu kwanini si lazima ingawa unakuwa very unppular na sometimes hat andugu wanakukimbia ninachangia misiba na elimu lakini harusi nimeacha sisi tulio kwenye mapambano ya kupiga vita harusi kubwa na michango ya harusi tuanze kuonyesha mfano kwa kuwa na harusi ndogo pale inapohusu watoto ama ndugu zetu. makanisa na misikiti ingiliane kati na mhamasishe harusi zifungwe kanisani/misikitini na sherehe zifanywe za jumla misikitini. yyako makanisa yameanza vipaimara vinafanywa pamojo na kwa gaharma nafuu.
Kwani kuna mtu hushikiwa panga akilazimishwa achangie Harusi?Ifike mahali kila mtu agharamie harusi yake au ya ndugu yake bila kushirikisha watu wengi kama ilivyosasa, Kwa kweli tuige mfano wa wenzetu kenya maharusi wanagharamia shughuli yao kwa msaada wa ndugu na marafiki wakaribu,lakini pia sherere za mchana zinapunguza mambo mengi jioni kila mtu kwake hakuna habari ya kukesha, mnapata chakula cha mchana na vinywaji laini visivyo na pombe, Maharusi kama wana uwezo basi watafanya tafrija fupi usiku ya watu wachache.
Hapa bongo usipo mchangia mtu unashangaa anakununia kabisa kwa kweli inabidi tubadilike
Ukienda kuomba msaada wa kuchangiwa ada hakuna ambaye atakusaidia ila peleka kadi ya mchango wa harusi watachanga hata kama wengine hawamjui muhusika.
Umewahi kushikiwa bunduki uchangie?NAOMBA WENYE USHAWISHI HASA MLIOPO DSM,MTUPE MBINU NA TECNIQUES ZA KUMALIZA HII KERO "ONCE AND FOR ALL".JAMANI WATU TUNAUMIZWA SANA NA HII MICHANGO,SIO SIRI.MHESHIMIWA MAKOND(RC WA DSM) TUNAOMBA MCHANGO WAKO WA MAWAZO WA JINSI KUMALIZA HII KERO HASA KWA WANANCHI WAKO WA DAR.MAANA NAKUAMINIA KWA UBUNIFU MKUU.
Umesahau hii:-sherehe zote ziwe na pombeHii Kitu nilitaka kuipost hapa miezi kadhaa iliyopita sema nikasahau, leo kuna jamaa kanipigia anataka nimtumie dolali za mchango wa harusi ya binamu yake ambaye hata simjui wala sijawahi msikia.
Tuendelee:-
Wakuu hii kitu bado bongo ipo tena siku hizi ni project kubwa na za garama ya juu.
Watu wanakutana kila wiki mara moja kwenye baadhi ya bar, wanakunywa na kusaza katika hivyo vikao vya maandalizi, vikao hivyo huchukua miezi miwili hadi mitatu. Na katika vikao hivyo watu hutoa ahadi ya kiasi cha fedha watakachotoa kwa ajili ya harasi, wanaume hutoa michango ya bachela parti na harusi kuu, na kina dada hutoa michango ya sendi off, bridoshawa, kichenipati, na harusi kuu.
Kwa kifupi zoezi hili linakula hela nyingi sana, nimeambiwa sometimes you can be asked to contribute to more than 10 wedding a year, na ukitoa chini ya laki moja unaonekana mtu wa hovyo hovyo.
Jamani ndugu zangu naombeni mwongozo mimi naona kama hii ni too much.
Badala ya michango ya vikao vya harusi basi tuihamishie kwenye Elimu na Matibabu.
MJ
====================
NAOMBA WENYE USHAWISHI HASA MLIOPO DSM,MTUPE MBINU NA TECNIQUES ZA KUMALIZA HII KERO "ONCE AND FOR ALL".JAMANI WATU TUNAUMIZWA SANA NA HII MICHANGO,SIO SIRI.MHESHIMIWA MAKOND(RC WA DSM) TUNAOMBA MCHANGO WAKO WA MAWAZO WA JINSI KUMALIZA HII KERO HASA KWA WANANCHI WAKO WA DAR.MAANA NAKUAMINIA KWA UBUNIFU MKUU.
nenoMhubiri wa "Hatimaye maisha"yanayorushwa mubashara kutoka Mbeya alisikika akizungumzia kidogo suala la kujiepusha na gharama za arusi na kuangalia suala la elimu zaidi.
Nampongeza kama kiongozi wa kiroho kuzungumzia hilo,lakini alisema kidogo sana kuhusu aina hiyo ya "ujinga" ambao umekuwa ugonjwa wa wa Tanzania hasa wa imani ya kikristo.
Arusi zimekuwa ni kitu cha kuoneshana ufahari na mashindano ya matumizi makubwa ya pesa kwa ulevi na fahari za muda tofauti kabisa na uhalisia wa maisha ya walio wengi wanaoshiriki arusi hizi.
Ujinga unakuwa mkubwa zaidi pale mtu anapokuwa tayari kuchangia zaidi ya laki saba hadi milioni kwa mwaka kwa ajili ya arusi halafu anakataa kuchangia matibabu ama elimu kwa watoto wenye uhitaji.
Nawapongeza wakenya tangu enzi zile za mwl.Nyerere utasikia matangazo radioni "mbunge wa nyeri anaalika harambee ya kuchangia wanafunzi siku ya jumamosi"...
Matangazo hayo nikikumbuka japo nilikuwa mdogo,yanaonesha umakini wa wakenya katika suala la elimu.
Nilipokuwa mdogo nikisikia salamu katika vipindi vya watoto walikuwa na msemo " na maziwaa..ya watoto wa nyayo"
Viongozi waliona umuhimu wa lishe kwa watoto ili wawe makini na elimu.
Vipi suala la gharama hizi za arusi lisijadiliwe kwa kina na kubadilisha mind set za wa Tanzania kutoka kuchangia arusi na kufikiria kusaidia katika suala la elimu.
Bahati mbaya baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wanahimiza matumizi mabovu ya arusi za kifahari na wakati huo ndoa zinazofungwa nyingine hazidumu.
Imefika wakati wa kila mmoja wetu aanze kuangalia upya iwapo tunahitaji arusi za kifahari wakati tunakabikiwa na umaskini na ujinga ambao hatuungani kuutokomeza kama tunavyoungana wakati wa arusi.
kuna mtu aliniletea kadi ya mchango, aisee jibu langu lilikuwa moja tu kuwa mim huwa sichangii sherehe, nachangia misiba na matibabu na matatizo mengine. Kiasi fulani hakupendezwa na jibu langu na hakuamini kama nipo serious. Mi saiv kwenye harusi nachangia ndugu zangu tu na si vinginevyo. Ila kwenye matatizo nachangia bila kujali uduguIfike mahali kila mtu agharamie harusi yake au ya ndugu yake bila kushirikisha watu wengi kama ilivyosasa, Kwa kweli tuige mfano wa wenzetu kenya maharusi wanagharamia shughuli yao kwa msaada wa ndugu na marafiki wakaribu,lakini pia sherere za mchana zinapunguza mambo mengi jioni kila mtu kwake hakuna habari ya kukesha, mnapata chakula cha mchana na vinywaji laini visivyo na pombe, Maharusi kama wana uwezo basi watafanya tafrija fupi usiku ya watu wachache.
Hapa bongo usipo mchangia mtu unashangaa anakununia kabisa kwa kweli inabidi tubadilike
Ukienda kuomba msaada wa kuchangiwa ada hakuna ambaye atakusaidia ila peleka kadi ya mchango wa harusi watachanga hata kama wengine hawamjui muhusika.