Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Kuna jamaa kila mwezi anaweka kibindoni kama milioni 3 hivi kama mshahara, lakini cha ajabu bwana huyo wakati anakaribia kuoa pasipo hata huruma akawa anasmbaza kadi za mchango hadi kwa watu wenye kipato cha chini kabisa.

Kwa kweli sikuweza kumkalia kimya bwana yule...mtu mwenye mshahara mkubwa kama huyo wala hatakiwi kuchangisha bali anachotakiwa ni kualika watu wakampe support kwenye hiyo sherehe yake.

Kuomba mchango ni tamaduni zetu jamani wala msilalame.

Mfano:
kijijini kwetu kukiwa na harusi majirani huja na mabeseni ya chakula, wenye kuleta wali sawa, ndizi sawa etc
kwahiyo ulitaka na hapa mjini watu waje na mabeseni ya chakula ukumbini? na kama sio mbadala ni nini?

Mfano 2.
Kuna watu wenye vipato vikubwa wakiamua kuoa bila kuomba michango, siku mtu akipelekewa invitation card anakataa kuhudhuria akidai hakushirikishwa kwenye kuchangia. hili nalo unalizungumziaje?

Mfano 3.
Hakuna kitu kibaya kama kubagua mtu wa kumpa kadi ya kuomba mchango wa harusi na mbaya zaidi mtu akijua hujampa kwasababu ya kipato chake kidogo.........nakuhakikishia utalaumiwa na hiyo jamii sana.

Sherehe ni watu bwana na ukiwahitaji sharti uwaombe mchango na usipowaomba mchango hata ukiwaarika hawaji ng'oooo kwa sababu tu eti hukuwashirikisha kwenye kuchangia

Finally, akili kukichwa ukiona huna senti ya kuchangia ww sepa kimyakimya
 
Uzuri wa michango ya harusi hulazimishwi kama huna hela mtu akikuletea kadi mwambie ukweli wakati mwingine tunatoa ahadi wenyewe na kwa kiasi kikubwa yanakuwa kama mashindano ya nani kaahidi nini. Kuna watu wana hela zao kuchangia elfu 50 au laki moja na yeye pamoja na mpenzi wake kwenda kufurahi ni jambo la kawaida maana angeweza kutumia kiasi hicho kwenye kumbi za starehe kama si kwenda harusini.

Sawa sawa
 
Juzi nilikuwa kwa kikao budget mil 25. Wakati wa maongezi ya chini kwa chini jamaa akadokeza budget ya fulani ilikuwa mil 40. Hela yote hii lazima iliwe yote iishe


Hapa Bwana/Bi anaishi nyumba ya kupanga, kwao kijijini hajajenga hata room mbili, za kupumzikia uendapo kuwasalimu wazazi/ndugu etc
 
Kuomba mchango ni tamaduni zetu jamani wala msilalame.

Mfano:
kijijini kwetu kukiwa na harusi majirani huja na mabeseni ya chakula, wenye kuleta wali sawa, ndizi sawa etc
kwahiyo ulitaka na hapa mjini watu waje na mabeseni ya chakula ukumbini? na kama sio mbadala ni nini?

Mfano 2.
Kuna watu wenye vipato vikubwa wakiamua kuoa bila kuomba michango, siku mtu akipelekewa invitation card anakataa kuhudhuria akidai hakushirikishwa kwenye kuchangia. hili nalo unalizungumziaje?

Mfano 3.
Hakuna kitu kibaya kama kubagua mtu wa kumpa kadi ya kuomba mchango wa harusi na mbaya zaidi mtu akijua hujampa kwasababu ya kipato chake kidogo.........nakuhakikishia utalaumiwa na hiyo jamii sana.

Sherehe ni watu bwana na ukiwahitaji sharti uwaombe mchango na usipowaomba mchango hata ukiwaarika hawaji ng'oooo kwa sababu tu eti hukuwashirikisha kwenye kuchangia

Finally, akili kukichwa ukiona huna senti ya kuchangia ww sepa kimyakimya

Watu walikuwa wanachangiswa hizo sinia za mchele, unga n.k kwa kupenda wenyewe leo hii mtu anakuletea kadi anakupangia na kiwango kabisa.Watu wanabagua kabisa asiyechangia hapati kadi hata kama ni jirani hayo mambo kwa mababu zetu na vijiji vingine kwa sasa hayapo.Kuna siku nilipokea kadi tano za harusi nichangia kwa mwezi mmoja basi nikaona ngoja niwagawie kila mtu 30,000 jumla ikawa 150,000. unajua walinipa kadi ya single halafu bado unaendelea kutetea uzezeta.Unajua 150,000. ni karo za wanafunzi wawili wa shule za selikali boarding kwa mwaka mmoja na change juu.
 
Kuna jamaa kila mwezi anaweka kibindoni kama milioni 3 hivi kama mshahara, lakini cha ajabu bwana huyo wakati anakaribia kuoa pasipo hata huruma akawa anasmbaza kadi za mchango hadi kwa watu wenye kipato cha chini kabisa.

Kwa kweli sikuweza kumkalia kimya bwana yule...mtu mwenye mshahara mkubwa kama huyo wala hatakiwi kuchangisha bali anachotakiwa ni kualika watu wakampe support kwenye hiyo sherehe yake.

word!!
 
Halafu sasa hao wachangishaji ni wasumbufu...kila siku lazima akuendee hewani kukumbushia...utadhani aliwekeza

mkuu watu8 nina mmoja kanipa kadi mchango sh 50,000/= yeye yupo Tanga (na harusi hukohuko) mimi nipo Mbeya na analijua hilo vema, lakini anavyonifatilia laaaaaah! yani kila sms yake mwishoni inakumbushia mchango! ngoja siku nijiboost nimwambie ukweli am not willing! huku ni kurudishana nyuma!
 
Uzuri wa michango ya harusi hulazimishwi kama huna hela mtu akikuletea kadi mwambie ukweli wakati mwingine tunatoa ahadi wenyewe na kwa kiasi kikubwa yanakuwa kama mashindano ya nani kaahidi nini. Kuna watu wana hela zao kuchangia elfu 50 au laki moja na yeye pamoja na mpenzi wake kwenda kufurahi ni jambo la kawaida maana angeweza kutumia kiasi hicho kwenye kumbi za starehe kama si kwenda harusini.
Ninachopinga mimi ni kuomba michango hata kwa mtu ambaye unajua hataweza kuhudhuria mfano uko Arusha unaomba mchango mtu wa Mbeya hii imekaaje? Labda kama huyo mtu uliwahi kumchangia au ni ndugu yako vinginevyo kama ni rafiki ni kiasi cha kumpa taarifa si kumuomba mchango.

Sio lazima wapi wakati usipochanga unazungumzwa vibaya. Inahitaji moyo mgumu kama wangu kukataa kuchangia harusi. Mimi wameshanijua, waseme weeeee, tutakutana kwenye misiba, harusi zenu mi za nini. Issue ni ndoa sio kukurukaara za miezi umi sababu ya siku moja.

Na ukiona mwanaume ni mshabiki sana wa sherehe, you just know he has got too much of his mother in him
 
Watu walikuwa wanachangiswa hizo sinia za mchele, unga n.k kwa kupenda wenyewe leo hii mtu anakuletea kadi anakupangia na kiwango kabisa.Watu wanabagua kabisa asiyechangia hapati kadi hata kama ni jirani hayo mambo kwa mababu zetu na vijiji vingine kwa sasa hayapo.Kuna siku nilipokea kadi tano za harusi nichangia kwa mwezi mmoja basi nikaona ngoja niwagawie kila mtu 30,000 jumla ikawa 150,000. unajua walinipa kadi ya single halafu bado unaendelea kutetea uzezeta.Unajua 150,000. ni karo za wanafunzi wawili wa shule za selikali boarding kwa mwaka mmoja na change juu.


Ninachojaribu kuelezea ni uhalisia ulivyo huko mtaani. Ni kweli michango imezidi hapa nilipo ninakadi zaidi ya saba sasa ni uamuzi wangu nichangie ama nisichangie. Tamaduni zetu za kitanzania ni kushirikisha watu katika Misiba, Harusi, Graduation ceremony nk. Sasa ni juu yako hawa watu utawashirikisha vipi ili watambue kuwa unajari uwepo wao
 
Hi!

Enzi za mababu zetu mtu akiolewa ng'ombe anachinjwa ndugu, jamaa na marafiki wanaalikwa tunamuaga bibi harusi na upande wa bwana harusi nao wanafanya hivyo na wanampokea mke wao mchezo unaishia hapo.Mpaka sasa vijijini watu bado wanaendelea na utaratibu huu na harusi zinafanywa bila hata kutumia gharama kubwa.

Jitu lina uwezo wa laki sita linaamua kuweka budget ya milioni 20 wakati hata kiwanja halina.Basi linaanza kuombaomba utafikiri omba omba wa mjini.Jifunzeni kujitegemea kama babu zetu.Cha ajabu zaidi wengi wanaoendekeza utamaduni huu ni wasomi badala ya kuchangia shughuli za maendeleo na kusomesha watoto wao wamekalia kuchangishana michango ya harusi kama mazezeta.Jamii inatarajia kujifunza kutoka kwa wasomi sasa kama wasomi ndiyo wanaibuka na haka kautamaduni ka kishamba nchi yetu kuendelea ni ndoto.

Ndoa ni makubaliano ya watu wawili hata kama mtafanya harusi ya kifahali namna gani haibadilishi kitu badilikeni tuendeleze familia zetu,jamii na nchi yetu kwa ujumla.

Huu upuuzi nilisha acha miaka 3 iliyopita pale mjinga mmoja aliponiletea kadi nakunipa masharti ukitoa elfu 50 utapata kadi ya mwaliko pamoja na kuhudhuria ukumbini ya MR&MRS, nikitoa elfu 30 nitapata kadi yakuhudhuria mm pekee nikitoa chini ya hapo nihudhurie kwenye ndoa tu sintoweza kwenda ukumbini.
 
Hi!

Enzi za mababu zetu mtu akiolewa ng'ombe anachinjwa ndugu, jamaa na marafiki wanaalikwa tunamuaga bibi harusi na upande wa bwana harusi nao wanafanya hivyo na wanampokea mke wao mchezo unaishia hapo.Mpaka sasa vijijini watu bado wanaendelea na utaratibu huu na harusi zinafanywa bila hata kutumia gharama kubwa.

Jitu lina uwezo wa laki sita linaamua kuweka budget ya milioni 20 wakati hata kiwanja halina.Basi linaanza kuombaomba utafikiri omba omba wa mjini.Jifunzeni kujitegemea kama babu zetu.Cha ajabu zaidi wengi wanaoendekeza utamaduni huu ni wasomi badala ya kuchangia shughuli za maendeleo na kusomesha watoto wao wamekalia kuchangishana michango ya harusi kama mazezeta.Jamii inatarajia kujifunza kutoka kwa wasomi sasa kama wasomi ndiyo wanaibuka na haka kautamaduni ka kishamba nchi yetu kuendelea ni ndoto.

Ndoa ni makubaliano ya watu wawili hata kama mtafanya harusi ya kifahali namna gani haibadilishi kitu badilikeni tuendeleze familia zetu,jamii na nchi yetu kwa ujumla.

Nakubaliana nawe 100%. Mie nilikwisha sema siku nikioa sitochangisha mtu hata mmoja. Na hata ndugu na jamaa wakiamua kunichangia basi itakuwa kwa hiari yao. Nitajiandaa kwa kadiri nitakavyo weza na kualika watu wachache. Sitaki ufahali wala kupoteza muda kwa kuomba watu michango. Na sasa hivi napendelea zaidi ndoa za kimila kama ilivyo kuwa asili yetu waafrika.Tumezidi kuiga mambo..mara kuvalishana pete na madikodiko mengine kibao. Napinga sana haya mambo. Wenzetu Nigeria wamefunguka kuhusu ndoa hizi za kizungu, wao wameanza kufunga kwa wingi ndoa za kimila. Afrika ya kusini nao vivyo hivyo. Bado sisi muzungu worshipers!!
 
Napata kadi za kuchangia harusi karibu kila mwezi naletewa karibu kadi 3, @50,000 approximately =150 , 000 .

Haya majanga sana ,mshahara wangu 550,000 , which means 30% michango harusi ,Ninaacha haya mambo ,mimi mwenyewe sitafanya hiyo mambo, yaani kila weekend tupo busy kuchangisha harusi.

Kama tunataka kutokomeza umasikini na wakati tunatiana umasikini ,siwezi tena.

Jamani kama huna uwezo usisumbue watu bwana ,funga ndoa ya kawaida tuache mambo ya kuiga.
 
Yangu nilipanga iwe na sherehe, wapambe wakapiga mahesabu ikafika 17 m. nikawahoji watachangia how much? wakapata 4.5 m. Then nikawaambia nachukua mkopo nimalizie gap. bahati sisi waislam hatuna ulazima wa sherehe, nikaongeza 1.5 m kwa bibi harusi wakafanikisha sherehe kubwa ya kawaida tu. then wapambe waliponifuata nikawaambia nimejkosa venue so hadi next weekend.. huu ni mwaka wa kumi next weekend haijafika. Namshukuru wife alinisihi nisichukue mkopo wa kipuuzi.
 
Napata kadi za kuchangia harusi karibu kila mwezi naletewa karibu kadi 3, @50,000 approximately =150 , 000 .
Haya majanga sana ,mshahara wangu 550,000 , which means 30% michango harusi ,Ninaacha haya mambo ,mimi mwenyewe sitafanya hiyo mambo, yaani kila weekend tupo busy kuchangisha harusi ,kama tunataka kutokomeza umasikini na wakati tunatiana umasikini ,siwezi tena.Jamani kama huna uwezo usisumbue watu bwana ,funga ndoa ya kawaida tuache mambo ya kuiga


bado unaishi nyumba ya kupanga au umerithi?
 
Back
Top Bottom