Mjadala kwa wanaokubali kuoa (Ndoa)
Bila ndoa unakuwa haujaishi bado!
Ndoa ina raha yaks bhana!
Ndoa inaheshimisha!
Kuna milango mingine ya riziki haiwezi funguka mpaka single kwenye ndoa!
Ambao hawako kwenye ndoa wanajiita kataa ndoa wanajifariji tu! huenda wajabahatika kupata machaguo sahihi!😊
Wenye makasiriko yao watauponda huu uzi hasa wanawake kurumbembe ambao wanatamani wholesale ila wamekosa watu sahihi wameamaua kujiita kataa ndoa
Wameamua kuiskashifu ndoa
Wan maneno yao ya mkosaji et "walioko kwenye ndoa wanatamani watoke" au wanaionja shubiri"
Hayo ni maneno wanayojipoza nayo!😆
Nways
musicarlito uzi mzuri sana huu umeongea point tupu
Wengi wamekosea lakini hawataki kujisahihisha ngali uwezekano upo...jeuri...ndoa inahitaji unyenyekevu


Wengine bado hawajakomaa hata kwa mahusiano...only a single heartbreak 💔 analia kataa ndoa...

Hao hao ndo usiku wanalia upweke na kuoshia kuwinda wame wake za watu...na wengine kuangukia katika ulevi na magonjwa ya akili
 
Kama ndoa ni jambo jema, Mbona huyo Mungu hakujiumbia mke wake wafunge ndoa?
Yeye ni Mungu amekamilika haitaji kitu au mtu kujikamilisha...wewe huwezi kupata mtoto bila mke,Yeye anaweza pata mtoto kwa namna yoyote apendavyo

Mke anamkamilisha mume
 
Asante...wanaoponda kuna vacuum kisaikolojia kwa sababu walipaswa kuwa kwenye ndoa

Vile isivyobahati,wengine wamekosea ,badala ya kujirekebisha au kurudi nyuma kuangalia wapi wamekosea...wanabaki wanaponda wakidhani itaponya maumivu yao...ikifika usiku wanakuwa na upweke mbaya unaopelekea wengine kwenye ulevi uliopitiliza au magonjwa ya akili

Wengine ni hawa ambao bado hawajakomaa sawasawa hata kuingia kwenye mahusiano serious...so a single heartbreak tayari ananyanyua mdomo ndoa haifai wakati hata mahusiano yenyewe kuingia hayuko illegible...Ana miaka 17 au 19 can you imagine
Wanajifariji hapa ili kusogeza masaa! Ila
Kuna muda mioyo yao inabubujikwa na simanzi kwa kukosa familia stable(ndoa)
Wanaume wanaishia kuzaa na wanawake tofauti tofauti Wanatamani wangekuwa na familia moja iliyo stable ambayo haijasambaratika!
Wadada wanaishia kuzalishwa! Wanakosa soko wanaleta makasiriko yao hapa! Wengine ndoa zimewashinda kwa sababu ya ujinga wao na wao wanaleta makasiriko hapa!
Wanaponda umri wa ndoa ikiwa ndoa ina ina muda mchache wanasema bado hujaoyaona yaliyoko kwenye ndoa!yani wanaaminishana ujinga! Wanafikiri kila mtu yupo kama wao! Kama hawakupata machaguo sahihi ni bora wamuombe tu mungu mungu hashindwi na jambo anaweza kurudisha furaha ya mioyo yao iliyopotea ila sio kupinda ndoa

Wengine wanaponda ndoa ilhali wako chuo third year ,wanapambania course work wengine wamegraduate lao mpaka sasa hivi hawalijui..hawaelewi wanachosema wanafata mkumbo!
 
Yeye ni Mungu amekamilika haitaji kitu au mtu kujikamilisha...wewe huwezi kupata mtoto bila mke,Yeye anaweza pata mtoto kwa namna yoyote apendavyo

Mke anamkamilisha mume
Kupata mtoto bila mke inawezekana.

Mbona kuna watoto wa kupandikiza
Sio lazima uwe na mke au ndoa.
 
Wanajifariji hapa ili kusogeza masaa! Ila
Kuna muda mioyo yao inabubujikwa na simanzi kwa kukosa familia stable(ndoa)
Wanaume wanaishia kuzaa na wanawake tofauti tofauti Wanatamani wangekuwa na familia moja iliyo stable ambayo haijasambaratika!
Wadada wanaishia kuzalishwa! Wanakosa soko wanaleta makasiriko yao hapa! Wengine ndoa zimewashinda kwa sababu ya ujinga wao na wao wanaleta makasiriko hapa!
Wanaponda umri wa ndoa ikiwa ndoa ina ina muda mchache wanasema bado hujaoyaona yaliyoko kwenye ndoa!yani wanaaminishana ujinga! Wanafikiri kila mtu yupo kama wao! Kama hawakupata machaguo sahihi ni bora wamuombe tu mungu mungu hashindwi na jambo anaweza kurudisha furaha ya mioyo yao iliyopotea ila sio kupinda ndoa

Wengine wanaponda ndoa ilhali wako chuo third year ,wanapambania course work wengine wamegraduate lao mpaka sasa hivi hawalijui..hawaelewi wanachosema wanafata mkumbo!
Well said ...wachache wangekuwa na sababu ya kuchukia kwa sababu ya changamoto fulani kubwa au bahati mbaya....ambayo nayo ukute ina ufumbuzi

Wengine watu wazima,lakini kwa kweli ki maadili hawajakomaa...mfano mtu humu anajivuna kuwa na mchepuko hali yuko katika ndoa ,na anaona ni jambo la kawaida,mtu huyo huyo kesho ataanzisha uzi hapa amekuta sijui sms za usaliti kwenye simu ya mke wake anaomba ushauri afanye nini...
Au mwingine dada yeye ni balozi wa u"feminism" Like ni 50 kwa 50...nae undhani ataifurahia ndoa?thubutu

Wengine ni hawa Generation Z ...anataka mwanaume aliejiriwa tena sio mwalimu,mwenye gari yake ,mwenye mvuto...na mahari familia yao wamesha set standard ni Mil 5...huyu akiangukia kwa matapeli anamlalamikia nani
 
Unaweza kupata mtoto bila ndoa.

Hakuna ulazima wa ndoa.
Unahitaji mtoto wa nini...mtoto pia ni matunda ya ndoa...kuondoa hawa mnaowataka wa kwenye maabara ambao baadae mnalalamika wakija kuwa mahogany mna apa kuwapiga risasi
 
Kila kizazi huwa na changamoto...lakini familia ndio sehemu sahihi ya kuzishinda changamoto...pamoja na kubebeana mapungufu ya kibinadamu,tunaunganisha nguvu kushinda changamoto...NDOA ni msingi wa familia thabiti
Nakubalia na wewe.
 
Unahitaji mtoto wa nini...mtoto pia ni matunda ya ndoa...kuondoa hawa mnaowataka wa kwenye maabara ambao baadae mnalalamika wakija kuwa mahogany mna apa kuwapiga risasi
Hata watoto wa ndoa wanaweza kuwa mahogany vilevile.
 
Habari wakuu

Jambo lolote zuri hupambaniwa(earned)...kuna sadaka kulipata.Watu wanaoshindwa kutoa sadaka kupata jambo zuri,huwa na tabia ya kuwaaminisha kuwa jambo hilo ni gumu haliwezekani na kubaki katika Hali ya kushindwa ndio mazingira sahihi...utawasikia watu wenye ufukara wa kujitakia wakisema ...uwe na Mali usiwe nayo utakufa tuu...au hakuna utajiri halali na blah blah

Wakati mwingine wale walioshindwa masomo ya sayansi au hisabati nao wangekuja na hoja zao ooh kwanza siasa ndo kila kitu nk

Nirudi katika ndoa...ndoa msingi wake ni jambo linalohitaji uadilifu wa half ya juu na kuaminiana,hali hii inahitaji kumshirikisha Mungu kwa sababu yote haya kuwezekana inahitajika IMANI...mfano unajua A Ana mapungufu haya lakini B nitadumu nae kama mume /mke baba/mama wa watoto wangu

Wengi hasa vijana hawawezi kujidhibiti miili kwa tamaa mbaya,starehe na anasa...anataka alale na kila mtu...ale hovyo hovyo na kunywa kwa sababu tuu Ana pesa,anajiona yuko huru lakini kwa kweli hayuko huru,ndio maana baadae hali kama addiction zinatuumbua...mfano wa mtu alie huru...akikuta hot pot limejaa nyama akiambiwa ajipakulie,atachukua finyango chache tuu!sio kwa sababu nyama ni tamu basi apakue zote

Silika hiyo ndio inatutofautisha na wanyama...mnyama akishikwa na ashki,anampanda yeyote na popote....anaweza mpanda hata mama yake au dada yake...ndio sifa ya kijana ambaye hawezi kuhimili hisia na mwenendo wake,ni kama mnyama ...huyu hafai wala ndoa haiwezi...atafanya harusi baadae atakwambia ndoa haifai

Msichana au dada anaeingia kwenye ndoa kama fursa ya kutoboa maisha,akikutana na changamoto ndogo ndogo za maisha ,atakwambia hayo hayo

Watu hawa kwa sababu wanadaiwa uadilifu,kumcha Mungu ...mambo ambayo sio rahisi yanahitaji kujisadaka mpaka kuyazoea kama mfumo wa maisha wa kawaida wa mtu...nao hawako tayari kuyafanya...mfano...kwenda kanisani/msikitini,kufunga kwaresma au Ramadan nk...kusaidia wengine...watakwambia ndoa ni ngumu

Hii haindoi ukweli kuwa wakati mwingine watu wamejikuta katika matatizo makubwa kwenye ndoa,lakini ni mara chache sana,ndio kusema gari kwa sababu zinapata ajali kila siku na kugharimu maisha ya watu...ndio tufanye safari zetu kwa mguu...kutoka Dar es Salaam hadi Njombe....au Kigoma?

Msingi wa jamii yoyote njema ni familia ya baba na mama,ndoa ndio taasisi bora kutupa haya...NDOA NI JAMBO JEMA LIMETOKA KWA MUNGU MWENYEWE NA LIHESHIMIWE NA KILA MTU
ndoa nzuri miaka ya zamani sio sasa
 
Ndoa halijawahi kuwa jambo la kiimani bali la kijamii ndo maana hata huko kuibariki kanisani Wakatoliki ndo waliliingiza miaka 1600 baadaye..
 
Wewe jamaa kiboko nilijua unapinga kuhusu Mungu kumbe hadi ndoa!!!
Ndoa ni mkataba wa hisia.

Hisia zikiisha ndoa imeisha.

Mnaanza kuparangana.

Sasa kwa nini uingie mkataba wa hisia, ambazo muda wowote zinaweza kubadilika?

Halafu zikibadilika, unaminywa na kufilisiwa mwanaume.

Mimi sikatai watu wafunge ndoa.

Mimi napinga ndoa, imekaa kitapeli na kiunyonyaji.
 
Ndoa halijawahi kuwa jambo la kiimani bali la kijamii ndo maana hata huko kuibariki kanisani Wakatoliki ndo waliliingiza miaka 1600 baadaye..
Mark 10:9

Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.

Hilo ni la wakatoliki?
 
Ndoa ni mkataba wa hisia.

Hisia zikiisha ndoa imeisha.

Mnaanza kuparangana.

Sasa kwa nini uingie mkataba wa hisia, ambazo muda wowote zinaweza kubadilika?

Halafu zikibadilika, unaminywa na kufilisiwa mwanaume.

Mimi sikatai watu wafunge ndoa.

Mimi napinga ndoa, imekaa kitapeli na kiunyonyaji.
Kwa hoyo unapinga kabisa uwepo wa familia?
 
Ndoa ni mkataba wa hisia.

Hisia zikiisha ndoa imeisha.

Mnaanza kuparangana.

Sasa kwa nini uingie mkataba wa hisia, ambazo muda wowote zinaweza kubadilika?

Halafu zikibadilika, unaminywa na kufilisiwa mwanaume.

Mimi sikatai watu wafunge ndoa.

Mimi napinga ndoa, imekaa kitapeli na kiunyonyaji.
Kwahiyo hutaoa ?
 
Back
Top Bottom