Mjadala kwa wanaokubali kuoa (Ndoa)
y

Maana ya Ndoa​

Ndoa ni muunganiko kati ya mwanamume na mwanamke, walio amua kwa ridhaa yao wenyewe kuishi pamoja kama mke na mume mpaka mwisho wa maisha yao ya ndoa.

Aina za ndoa kwa mujibu wa sheria
Kuna aina mbili tu za ndoa zinazotambulika na sheria ya ndoa Tanzania
  • Ndoa ya mke mmoja na mume mmoja tu.
  • Ndoa ya wake wengi.
Ndoa hizo zinaweza kusheherekewa kufuatana na misingi na taratibu za kidini, kimila au kiserekali, kushuhudiwa na watu wasiopungua wawili na kusajiliwa kwa mujibu wa sheria.

Hatua za kuchukua kabla ya ndoa kufungwa
  • Lazima taarifa ya nia ya kufunga ndoa itolewe siku 21 kabla ya ndoa kufungwa, kama kutakuwa na mwenye pingamizi budi litolewe itoe kabla ya ndoa kufungwa
  • Majina ya wale wanaotarajia kufunga ndoa, umri, majina ya wazazi wao na mahali wanapoishi yatajwe.
  • Tamko kwamba wanaotarajia kufunga ndoa hawana uhusiano unaokatazwa kisheria kufunga ndoa
KUSAJILI NDOA
Ndoa inaweza kufungwa Kiserikali au kwa madhehebu ya Kikristo au Kiislam au kufuatana na mila na desturi za wale wanaofunga ndoa.

Msajili wa ndoa atatoa cheti cha ndoa. Kila Ndoa inapofungwa lazima iwe na mashahidi wawili

Mambo ambayo sheria ya ndoa inakataza katika suala zima la kuoa au kuolewa
  • Mwanamke na au mwanaume kuolewa/kuoa bila ridhaa yake mwenyewe
  • Mwanamke na mwanaume wenye undugu wa damu kuoana
  • Mwanamke na mwanaume kuoana kabla ya kutimiza umri unaoruhusiwa kisheria (kwa mwanaume miaka 18 na kwa mwanamke miaka 18 au 15 kwa idhini ya wazazi/mlezi wake)
  • Kuoana watu wa jinsia moja
  • Mwanamke na mwanaume kutaka kuoana kwa mkataba wa kipindi maalum.
Haki za mume na mke katika ndoa
  • Wote wana haki ya kumiliki mali kama nyumba, shamba n.k. kwa majina yao binafsi;
  • Wote wana haki ya kutoa idhini katika uuzaji au kwa pamoja kuweka dhamana mali yoyote ya familia;
  • Wote wana haki ya kuishi katika nyumba ya familia iwapo mume/mke amemkimbia;
  • Mke ana haki ya kupewa matunzo yake na ya watoto wakati wa ndoa au iwapo mume amemkimbia, wameachana kwa amri ya mahakama. Na mume ana haki ya kupewa matunzo iwapo ana ulemavu hawezi kujiingizia kipato kutokana na ulemavu au ugonjwa wake;
  • Wote wana haki ya kutokupigwa na au kufanyiwa ukatili wa aina yoyote;
  • Wote wana haki ya kupeana unyumba;
  • Wote wana haki ya kutumia mali ya ndoa;
  • Wote wana haki kuomba amri ya talaka.
Ukomo wa ndoa Ukomo wa ndoa uko wa aina mbili:
  • Kifo cha mwanandoa mmoja wapo
  • Talaka ambayo imetolewa na Mahakama pekee pale inapojiridhisha kwamba kuna sababu ya msingi kufanya hivyo.
Baraza la usuluhishi la Ndoa
Baraza la usuluhishi la Ndoa, ni baraza lililoanzisha na kifungu 102 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, sura ya 29 kama sheria zilizopitiwa mwaka 2002, kwa madhumuni ya kusuluhisha wanandoa ambao wanaingia kwenye migogoro ya Ndoa. Kazi za Baraza la Usuluhishi la Ndoa:-
  • Kusuluhisha Wanandoa walioko kwenye Ndoa baada ya kupokea lalamiko toka kwa mmoja wapo wa Wanandoa
  • Kutoa hati maalum kuthibitisha kuwa suluhu imeshindikana na kuelekeza wanandoa kwenda Mahakamani kwa amri zaidi.
MUHIMU: Mahakama peke yake ndiyo ina mamlaka ya kutoa amri ya kutengana au talaka
Sababu zinazopelekea au kuishawishi mahakama kuvunja ndoa:-
  • Uzinzi kati ya wanandoa
  • Ukatili kati ya wanandoa au watoto wa ndoa
  • Dharau au kupuuza kulikokidhiri dhidi ya mwenzi
  • Kumtelekeza mwenzi kwa zaidi ya miaka mitatu Pale mwenzi anapofungwa kifungo cha maisha au kwa kipindi kisicho pungua miaka miaka mitano
  • Ikiwa mwenzi ameugua ugonjwa wa akili na imedhibitishwa na daktari kwamba hakuna uwezekano wa kupona.
  • Kubadili dini baada ya ndoa kufungwa pale wanandoa wote walikuwa wakifuata imani ya dini moja.
Haki za wanandoa zinazoambatana na amri ya talaka
  • Mgawanyo wa mali za ndoa /familia
  • Matunzo ya mke Hifadhi na matunzo ya watoto
  • Kizuizi cha kutobugudhiwa
  • Kuoa/Kuolewa tena
  • Fidia ya uzinzi
  • Gharama za kuendesha Shauri la Talaka
Haki ya Mgawanyo wa mali za familia/ ndoa Mali yoyote ambayo imepatikana wakati wa uhai wa ndoa na kwa nguvu na au machango wa pamoja wa wanandoa.

Iwapo mali iliyopatikana na mwanandoa mmoja wapo kabla ya ndoa au kwa nguvu zake mwenyewe lakini imeboresha/imetunzwa na mwanandoa mwingine mali hiyo itatambulika kama mali ya ndoa.

Lakini kama kuna mali yoyote ambayo mwanandoa mmoja amempa mwanandoa mwenzake kama zawadi, mali hiyo itakuwa ya yule aliyepewa pekee.

Aina za mchango
Kutekeleza kazi nyumbani hasa kutunza familia; mfano kuosha vyombo, kupika, kufua nguo, kubeba maji na kazi zingine zinazofanana na hizo kwa maslahi ya familia.

Kutunza mali za ndoa: mfano kufyeka, kulima, kuvuna shamba, kufanya marekebisho ya mali za ndoa kwa maslahi ya familia.

Mchango wa fedha wa mwanandoa katika kununua mali.

Haki ya Matunzo ya mwanandoa
Jukumu la kutoa matunzo kwa mke na watoto ni la mume, jukumu hilo litatekelezwa wakati wa uhai wa ndoa na baada ya talaka.

Haki ya Hifadhi na matunzo ya watoto
Hifadhi ya watoto hutolewa kwa mume au mke au mtu baki (mlezi) hasa kwa kuzingatia ustawi na maslahi ya wale watoto. Zaidi ya hayo, mahakama pia inaweza kuzingatia yafuatayo:

Umri wa wale watoto, mfano, watoto walio chini ya miaka saba kipaumbele cha hifadhi hupewa mama mzazi; labda kama kutakuwa na sababu za msingi za kuto fanya hivyo. Mfano kama mama mzazi ana matatizo ya kiakili, anaishi katika mazingira hatarishi.

Mazingira ya mahali watakapoishi watoto, mfano, kama mazingira ya upande mmoja ni hatarishi kwa ustawi wa mtoto, basi haki ya hifadhi atapewa mzazi mwingine bila kujali umri.

Matakwa ya wazazi wa mtoto nani kati yao angependa kupewa hifadhi ya watoto. Mila na desturi za jamii ambayo wanandoa wametokea.

Kama mtoto anaumri zaidi ya miaka saba na ana uelewa wa kutoa mapendekezo yake, basi matakwa/maoni yake yatasikilizwa zaidi.

Haki ya hifadhi ya mtoto haimnyimi mzazi mwenza haki ya kumuona na au kumtembelea mtoto/watoto. Haki ya hifadhi ya mtoto haiondowi jukumu la baba kutoa matunzo.

images
--------

Baadhi ya hoja za wanaokubali ndoa
  • Ndoa ni heshima kwa binadamu
  • Ndoa husababisha malezi bora kwa watoto
  • Ndoa huonyesha ukomavu wa akali
  • Ndoa ndio chanzo cha Taifa imara
  • Ndoa chanzo cha maadili mema kwa Taifa
  • Ndoa hutunza mali za famili
=======
Nimeona kuna nyuzi nyingi sana hapa JF zikihamasisha vijana kupinga masuala ya ndoa. Mtu kakurupuka huko kaona familia moja ina matatizo yao basi moja kwa moja analeta uzi kuwa ndoa haifai. Ndoa zimekuwepo toka enzi na enzi na changamoto kwenye familia hazikosi lakini leo mtu anakwambia kirahisi tu eti kataa ndoa.

Ndoa ni muhimu sana kwa mwanamume na mwanamke, ile hali ya kukaa pamoja kama familia inakufanya ujihisi tofauti na kipindi kile ukiwa peke yako. Matatizo kwenye ndoa hayakosekani ila hiyo sio sababu ya kufanya kuepuka ndoa.

Hawa watu wanaopinga ndoa naona ni wakwepa majuku, vijana mnaogopa majuku ya kifamilia? Inasikitisha sana. Ewe kijana ingia kwenye ndoa ukiwa tayari umekoamaa kiakili haswa acha kupumbazwa na maneno ya watu.

Changamoto ama majukumu huwezi kuyakimbia kamwe, za kuambiwa changanya na zako.

Pia soma: Mjadala kwa wanaokataa Kuoa (Ndoa)
oote uliyosema ni ukweli,lakini tatizo wanawake wa leowanataka wawapande waume zao kichwani!!!!,,,,,dunia ya leo sio ya jana!!!!!,,,wewe unaenda kazini na mkeo anaenda kazini watoto wanalelewa na house girl sasa ndoa ya nini,manake mama akae na watoto mwanzo mwisho asimamie mifugo ya familia na miradi ya familia iliyo karibu na nyumbani au hapo nyumbani{wachagga wanatumia sana huu mfumo] sasa wewe unaenda job,nae anajipodoa anaenda kazini kwake nahuko anakutana na wajanja wanamyandua mpaka akili ichanganyikiwa na kumwona mumewe boya na hapo tatizo linaanza
 
Habari wakuu

Jambo lolote zuri hupambaniwa(earned)...kuna sadaka kulipata.Watu wanaoshindwa kutoa sadaka kupata jambo zuri,huwa na tabia ya kuwaaminisha kuwa jambo hilo ni gumu haliwezekani na kubaki katika Hali ya kushindwa ndio mazingira sahihi...utawasikia watu wenye ufukara wa kujitakia wakisema ...uwe na Mali usiwe nayo utakufa tuu...au hakuna utajiri halali na blah blah

Wakati mwingine wale walioshindwa masomo ya sayansi au hisabati nao wangekuja na hoja zao ooh kwanza siasa ndo kila kitu nk

Nirudi katika ndoa...ndoa msingi wake ni jambo linalohitaji uadilifu wa half ya juu na kuaminiana,hali hii inahitaji kumshirikisha Mungu kwa sababu yote haya kuwezekana inahitajika IMANI...mfano unajua A Ana mapungufu haya lakini B nitadumu nae kama mume /mke baba/mama wa watoto wangu

Wengi hasa vijana hawawezi kujidhibiti miili kwa tamaa mbaya,starehe na anasa...anataka alale na kila mtu...ale hovyo hovyo na kunywa kwa sababu tuu Ana pesa,anajiona yuko huru lakini kwa kweli hayuko huru,ndio maana baadae hali kama addiction zinatuumbua...mfano wa mtu alie huru...akikuta hot pot limejaa nyama akiambiwa ajipakulie,atachukua finyango chache tuu!sio kwa sababu nyama ni tamu basi apakue zote

Silika hiyo ndio inatutofautisha na wanyama...mnyama akishikwa na ashki,anampanda yeyote na popote....anaweza mpanda hata mama yake au dada yake...ndio sifa ya kijana ambaye hawezi kuhimili hisia na mwenendo wake,ni kama mnyama ...huyu hafai wala ndoa haiwezi...atafanya harusi baadae atakwambia ndoa haifai

Msichana au dada anaeingia kwenye ndoa kama fursa ya kutoboa maisha,akikutana na changamoto ndogo ndogo za maisha ,atakwambia hayo hayo

Watu hawa kwa sababu wanadaiwa uadilifu,kumcha Mungu ...mambo ambayo sio rahisi yanahitaji kujisadaka mpaka kuyazoea kama mfumo wa maisha wa kawaida wa mtu...nao hawako tayari kuyafanya...mfano...kwenda kanisani/msikitini,kufunga kwaresma au Ramadan nk...kusaidia wengine...watakwambia ndoa ni ngumu

Hii haindoi ukweli kuwa wakati mwingine watu wamejikuta katika matatizo makubwa kwenye ndoa,lakini ni mara chache sana,ndio kusema gari kwa sababu zinapata ajali kila siku na kugharimu maisha ya watu...ndio tufanye safari zetu kwa mguu...kutoka Dar es Salaam hadi Njombe....au Kigoma?

Msingi wa jamii yoyote njema ni familia ya baba na mama,ndoa ndio taasisi bora kutupa haya...NDOA NI JAMBO JEMA LIMETOKA KWA MUNGU MWENYEWE NA LIHESHIMIWE NA KILA MTU
 
Kweli ndoa ni jambo jema, ila kwa kizazi hiki tunachoishi sasa Mungu aturehemu tu.
 
Habari wakuu

Jambo lolote zuri hupambaniwa(earned)...kuna sadaka kulipata.Watu wanaoshindwa kutoa sadaka kupata jambo zuri,huwa na tabia ya kuwaaminisha kuwa jambo hilo ni gumu haliwezekani na kubaki katika Hali ya kushindwa ndio mazingira sahihi...utawasikia watu wenye ufukara wa kujitakia wakisema ...uwe na Mali usiwe nayo utakufa tuu...au hakuna utajiri halali na blah blah
Wakati mwingine wale walioshindwa masomo ya sayansi au hisabati nao wangekuja na hoja zao ooh kwanza siasa ndo kila kitu nk

Nirudi katika ndoa...ndoa msingi wake ni jambo linalohitaji uadilifu wa half ya juu na kuaminiana,hali hii inahitaji kumshirikisha Mungu kwa sababu yote haya kuwezekana inahitajika IMANI...mfano unajua A Ana mapungufu haya lakini B nitadumu nae kama mume /mke baba/mama wa watoto wangu

Wengi hasa vijana hawawezi kujidhibiti miili kwa tamaa mbaya,starehe na anasa...anataka alale na kila mtu...ale hovyo hovyo na kunywa kwa sababu tuu Ana pesa,anajiona yuko huru lakini kwa kweli hayuko huru,ndio maana baadae hali kama addiction zinatuumbua...mfano wa mtu alie huru...akikuta hot pot limejaa nyama akiambiwa ajipakulie,atachukua finyango chache tuu!sio kwa sababu nyama ni tamu basi apakue zote

Silika hiyo ndio inatutofautisha na wanyama...mnyama akishikwa na ashki,anampanda yeyote na popote....anaweza mpanda hata mama yake au dada yake...ndio sifa ya kijana ambaye hawezi kuhimili hisia na mwenendo wake,ni kama mnyama ...huyu hafai wala ndoa haiwezi...atafanya harusi baadae atakwambia ndoa haifai

Msichana au dada anaeingia kwenye ndoa kama fursa ya kutoboa maisha,akikutana na changamoto ndogo ndogo za maisha ,atakwambia hayo hayo

Watu hawa kwa sababu wanadaiwa uadilifu,kumcha Mungu ...mambo ambayo sio rahisi yanahitaji kujisadaka mpaka kuyazoea kama mfumo wa maisha wa kawaida wa mtu...nao hawako tayari kuyafanya...mfano...kwenda kanisani/msikitini,kufunga kwaresma au Ramadan nk...kusaidia wengine...watakwambia ndoa ni ngumu

Hii haindoi ukweli kuwa wakati mwingine watu wamejikuta katika matatizo makubwa kwenye ndoa,lakini ni mara chache sana,ndio kusema gari kwa sababu zinapata ajali kila siku na kugharimu maisha ya watu...ndio tufanye safari zetu kwa mguu...kutoka Dar es Salaam hadi Njombe....au Kigoma?

Msingi wa jamii yoyote njema ni familia ya baba na mama,ndoa ndio taasisi bora kutupa haya...NDOA NI JAMBO JEMA LIMETOKA KWA MUNGU MWENYEWE NA LIHESHIMIWE NA KILA MTU
Ndoa na mahusiano ya kimapenzi ya muda mrefu ni maigizo tu.
 
  • Thanks
Reactions: M45
Wale vijana waliozaliwa na michepuko a.k.a wale wa kataa ndoa watakuja muda sio mrefu kukukashifu.
 
Ndoa ni jambo jema sana, wanadamu kusaidiana ... Inshallah Mungu atuwezeshe tupate wenza maana umri umeenda sana.
 
Tatizo la ndoa lilianzia pale mkutano wa beiging ulipofanyika haki sawa ...zikimpendelea mwanamke..mf kugawqna Mali linapotokea mmeachana hata akisababisha yeye mgawane..upendo kugeuka fedha na maisha Bora...wimbi la wanawake kutegemea mwenza badala ya kijishughulisha...wanawake kutegemea child support ...mkiachana anapewa jukumu la kibali na watoto...wanawake wanainchi kwenye ndoa wakifocus kuwa mwanaume atakufa mapema na la sivyo wanafocus kwenye retirement plan akiona Ana watoto na wewe huna Cha kumuachia au faidi kumshinda anakuacha na kuondoka na watoto inabaki mpweke na kujifia...ndoa NI nzuri ukibahatisha NI swa na bet ukila unaisifu Ila wengi wanatumia umizwa ..asilimia kubwa ndoa zinawaumiza lakini wamo tu...
 
Habari wakuu

Jambo lolote zuri hupambaniwa(earned)...kuna sadaka kulipata.Watu wanaoshindwa kutoa sadaka kupata jambo zuri,huwa na tabia ya kuwaaminisha kuwa jambo hilo ni gumu haliwezekani na kubaki katika Hali ya kushindwa ndio mazingira sahihi...utawasikia watu wenye ufukara wa kujitakia wakisema ...uwe na Mali usiwe nayo utakufa tuu...au hakuna utajiri halali na blah blah
Wakati mwingine wale walioshindwa masomo ya sayansi au hisabati nao wangekuja na hoja zao ooh kwanza siasa ndo kila kitu nk

Nirudi katika ndoa...ndoa msingi wake ni jambo linalohitaji uadilifu wa half ya juu na kuaminiana,hali hii inahitaji kumshirikisha Mungu kwa sababu yote haya kuwezekana inahitajika IMANI...mfano unajua A Ana mapungufu haya lakini B nitadumu nae kama mume /mke baba/mama wa watoto wangu

Wengi hasa vijana hawawezi kujidhibiti miili kwa tamaa mbaya,starehe na anasa...anataka alale na kila mtu...ale hovyo hovyo na kunywa kwa sababu tuu Ana pesa,anajiona yuko huru lakini kwa kweli hayuko huru,ndio maana baadae hali kama addiction zinatuumbua...mfano wa mtu alie huru...akikuta hot pot limejaa nyama akiambiwa ajipakulie,atachukua finyango chache tuu!sio kwa sababu nyama ni tamu basi apakue zote

Silika hiyo ndio inatutofautisha na wanyama...mnyama akishikwa na ashki,anampanda yeyote na popote....anaweza mpanda hata mama yake au dada yake...ndio sifa ya kijana ambaye hawezi kuhimili hisia na mwenendo wake,ni kama mnyama ...huyu hafai wala ndoa haiwezi...atafanya harusi baadae atakwambia ndoa haifai

Msichana au dada anaeingia kwenye ndoa kama fursa ya kutoboa maisha,akikutana na changamoto ndogo ndogo za maisha ,atakwambia hayo hayo

Watu hawa kwa sababu wanadaiwa uadilifu,kumcha Mungu ...mambo ambayo sio rahisi yanahitaji kujisadaka mpaka kuyazoea kama mfumo wa maisha wa kawaida wa mtu...nao hawako tayari kuyafanya...mfano...kwenda kanisani/msikitini,kufunga kwaresma au Ramadan nk...kusaidia wengine...watakwambia ndoa ni ngumu

Hii haindoi ukweli kuwa wakati mwingine watu wamejikuta katika matatizo makubwa kwenye ndoa,lakini ni mara chache sana,ndio kusema gari kwa sababu zinapata ajali kila siku na kugharimu maisha ya watu...ndio tufanye safari zetu kwa mguu...kutoka Dar es Salaam hadi Njombe....au Kigoma?

Msingi wa jamii yoyote njema ni familia ya baba na mama,ndoa ndio taasisi bora kutupa haya...NDOA NI JAMBO JEMA LIMETOKA KWA MUNGU MWENYEWE NA LIHESHIMIWE NA KILA MTU
Mna miaka mingapi ya ndoa na shemeji/wifi yetu?
 
Mwanamke kama utii na heshima kwako ni msamiati sababu ya malezi usiingie kwenye ndoa
 
Kweli ndoa ni jambo jema, ila kwa kizazi hiki tunachoishi sasa Mungu aturehemu tu.
Kila kizazi huwa na changamoto...lakini familia ndio sehemu sahihi ya kuzishinda changamoto...pamoja na kubebeana mapungufu ya kibinadamu,tunaunganisha nguvu kushinda changamoto...NDOA ni msingi wa familia thabiti
 
Mungu ni mwema atusaidie
Biblia yenyewe inasema bora usioe/kuolewa ila sababu ya tamaa za ngono uwe na mke/mume wako mwenyewe
ni kana kwamba ndoa sio jambo zuri ni vile tu kuna genye
 
Back
Top Bottom