Mjadala mpya: Ni nani aliwaokoa abiria 24 wa ndege ya Precision Air?

Mjadala mpya: Ni nani aliwaokoa abiria 24 wa ndege ya Precision Air?

Hili tukio la huyu mtoto kusakamwa litafanya ajali zingine waokoaji wabaki kuangalia na kurekodi kwa simu zao tu maana kuna post nyingine wameishia kumtukana mtoto wa watu kumwita wa mchongo mara tapeli. Yani mtu nusura apoteze maisha kuokoa ila leo anakua kituko.
 
Hili tukio la huyu mtoto kusakamwa litafanya ajali zingine waokoaji wabaki kuangalia na kurekodi kwa simu zao tu maana kuna post nyingine wameishia kumtukana mtoto wa watu kumwita wa mchongo mara tapeli. Yani mtu nusura apoteze maisha kuokoa ila leo anakua kituko.
Kwenye uzi wangu ni wapi nimemsakama au kumtukana?
 
Kwa hayo ulizungumza nakanusha inaonyesha yakua huna uchambuzi sahihi juu ya hili..

CHAMBUZI MAKINI JUU YA AJALI YA NDEGE ZIWA VICTORIA MWANZA.
1: Huenda wengi wetu tulibaki na taharuki kubwa baada ya ajali kutokea.
2: Vyombo vingi vya habari vimechangia kutopata taarifa kwa usahihi kulingana na uwasilishwaji wa taarifa.
3: Tukumbuke Tanzania haijawahi kutokea ajali ya ndege yenye kubeba abiri wengi au ndege yenye ukubwa kama hiyo iliyoanguka.
4: Vyombo na vikosi vya uokozi kutofanya kazi kwa ufanisi na kutofika eneo husika kwa wakati.
5: Asilimia ya mashuhuda wa tukio walitokea eneo la kanda ya ziwa na baadae kuwa waokoaji na watoa msaada kwa wahanga wa ajali.

KWA NINI MAJALIWA ALIPASWA KUPONGEZWA NA SERIKALI.
Huyu kijana alijitoa kwa asilimia 100% kwenye swala zima la uokoaji na ukisikiliza baadhi ya mahojiano alifanyiwa na baadhi ya media’s utakundua sio yeye alifungua mlango ila alisaidiana na yule mhudumu wa ndege, Kwani inasemekana kuwa mhudumu alikua akihangaika kufanya kila jitihada kuufungua mlango ukaunamshinda ila baada ya majaliwa kufika na wenzake akasogea kwenye mlango na kuanza kusaidiana na mhudumu kwa kuelewana yule dada aliusuma kuja nje yeye majaliwa anauvuta baada ya kupata mwanya kidogo aliomba kasia kwa mwenzie na kuanza kuugonga ule mlango kisha kuupachua kwakua ulikua umejiloki kwa ndani ghafla kwenye hizo jitihada mlango ulifunguka na hapo ndipo shughuli ya uokozi wa abiria kutoka ndani ya ndege ilipo anza kwa kuwatoa na kuwaweka kwenye ngalawa na kuwavusha ng’ambo wakati huo hayo yanaendelea ilikua ni kundi la majaliwa likifanya hivyo pamoja na majaaliwa mwenyewe, Kilichompa credits ni baada ya kuzirahi kwenye tukio lkn kama sio hivyo angekuwa amebaki kama wenzie tu kwa walifanya shughuli ya uokoaji pamoja na ilipofika taarifa kwa PM ni kunakijana aliefanya kitendo cha ushujaa cha kuokoa abiria kwenye ndege iliyopata ajali na anafanana jina na yeye hicho kilichokua kigezo kikubwa cha Majaliwa kuendelea kupata credits nyingine nyingi kutoka kwa MH. WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA.
Na kwa yule dada mhudumu wa ndege kwa upande wake nadhani huwa tunafahamu kwamba kila kampuni inayokuaji huwa kuna zawadi na tuzo mbalimbali hutolewa kwa mfanyakazi au wafanyakazi bora kila mwaka pale kampuni inapokua ikifanya sherehe zake kwa kuongeza mwaka mwingine hivyo huyu dada yeye credits zake atapewa na kampuni anafanyia kazi na hata ikiwezekana bodi ya usimamizi wa safari za anga Tanzania kumtunuku TUZO kwa ujasiri aliufanya kwenye hilo tukio.
Na uzi ufungwe
 
Na uzi ufungwe
Na waufutilie mbali kwani naona huyu ndugu Mshana Jr hajafanya research ya aina yoyote bali ni njozi alizo nazo ameziandika akidhani yupo sahihi juu ya maono yake kwenye siasa..

Ushauri: YA NGOSWE AMWACHIE NGOSWE MWENYEWE..Hii siasa ya Tanzania imekwisha elemewa na vitu hadi kufikia hapa na wanachofanya chama tawala kwa sasa ni kutengeneza wapiga wapya kwani bado wana amini mabolizozo wapo wengi na watapata kura iwe isiwe na wapiga kura wenyewe ni wamama sisi wanaume ni wengi wa porojo kwenye magenge yetu ya kahawa na bao.
 
Wameshasema hao wadada kuwa walisaidiana na Majaliwa kufungua mlango sasa huko ku risk tu kwa huyo kijana ni jambo la kishujaa.
 
Aliyeokoa wengi kwaushapu wake ni majaliwa ila hakuwa pekee yake so mtajibeba
 
NGUVU ya JF ... 53 minutes ago

"Serikali inawaomba wananchi wote kuendelea kuwa watulivu wakati uchunguzi huu unafanyika na baada ya uchunguzi kukamilika watajulishwa. Aidha, Baraza linawashukuru na kuwapongeza wote waliohusika katika uokozi baada ya ajali hii kutokea" @MsigwaGerson
Screenshots_2022-11-14-17-59-54.jpg
 
Cha kushangaza hata Pilot na mwenzake waliopambana kuhakikisha wanapunguza maafa yasiwe makubwa zaidi, hawatambuliki!
Tena penyewe wamepoteza mpaka maisha!

Badala take kabwana mdogo kamoja pekee ndiyo kanapewa kiki za kutosha, kana kwamba kalikuwa peke yake kwenye hilo zoezi la uokoaji!

Viongozi wa hii nchi hawapo serious hata kidogo.
 
Kikubwa kuna waliotoka salama ilo tunashukuru. Kila mmoja aliyeshiriki ata kusogeza mtumbwi akifanya jambo la maana.

Tusubiri ripoti ya ajali. Ila vifo vilivyotokea kwa wale watu 19 ni uzembe wa serikali ilo hatuwezi pindisha wala kubadili
Word.
 
Back
Top Bottom