TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Kigamboni

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Kigamboni

Watu wa kisota tunateseka na kukatikakatika kwa umeme kuliko maeneo mengine ya Kigamboni. Hivi sasa ni wiki moja tuna shida ya umeme kuwa mdogo (Low Voltage) kiasi cha kushindwa hata kuzungusha feni kwa spidi. Vitu vikiungua TANESCO wakiburuzwa mahakamani watalipa?
 
Pia barabara za Kisota ni mbaya sana. Toka zichongwe hazijawahi kufanyiwa ukarabati. Halmashauri tunaomba mtuangalie.

Nadhani Kisota ni katika maeneo ya kigamboni lililosahaulika sana. Au labda kisota iko chini ya wilaya nyengine na Sio Kigamboni ?
 
Hata Mizimbini kuna same problem umeme na barabara, nimeshaongea mpaka na mbunge sijaona hata action atlist mkuu ungesema una follow up.sasa hata kwenda kwa mguu madibwi ni kama bahari.

Tulishawahi kutengeneza wenyewe tukaweka kifusi ila hali ni ile ile. Nilijua hapa atlist someone will take action Mkuu mbona umenyamazia issue yetu??

Kifurukwe street, barabara haifai.
 
35768714eddad7766a3711e2162ce7a2.jpg
c4a2d940aad95bfcc96dab7bbf7a0529.jpg
d3676f75fd8d8d6ed02fa2f1902dde09.jpg
7843ccdc10dc1e9d60279cb7be1f14e4.jpg

Hii ndo Kifurukwe Street, Magari ya kwenda Darajani yanapita hapa.
 
Niwaombe wana Kigamboni mnapotoa ripoti Tanesco kuhusu tatizo la umeme kuwataka watoa huduma wawape namba ya kumbukumbu (Reference number) kwa ajili ya kufuatilia. Usikubali majibu ya mdomo bila ya ushahidi. Majibu ya "suala hili tunalijua na tunafuatilia" hayakubaliki.

Aidha, ni vyema kumuuliza jina la anayekuhudumia na kuweka kumbukumbu ya muda uliofanya mawasiliano.

Nimewasiliana na Meneja wa Tanesco (W) na kumtaka kufanya maboresho ya huduma kwa wateja kupitia Emergency line yao.

Dkt Faustine Ndugulile Mb
Mbunge Kigamboni
27.03 2017
 
Kigamboni tuna barabara za aina mbili. Zile zinazosimamiwa na Serikali Kuu kupitia Tanroads na zile za mitaa zilizo chini ya Halmashauri.

Niwaombe kuwasiliana na waheshimiwa kwa changamoto zinazohusu barabara za mitaa.

Changamoto za barabara za Tanroads ninawajibika nazo moja kwa moja kama Mbunge.

Asanteni

Dkt Faustine Ndugulile Mb
Mbunge Kigamboni
27.03 2017
 
Pale Kigamboni kuna viwanja vya miradi vimepimwa kama Geza Ulole, Kibada, Muongozo nk, ni wakati muafaka huduma za jamii kama barabara, Umeme na Maji vikafikishwa haraka ili maeneo hayo yaendelezwe. Inakuwa haina maana wala motivation kama maeneo ya miradi ya serikali yanakuwa sawa na squatter.

Kuna tatizo lingine sugu la kuchelewesha vibali vya ujenzi. Yaani pale Temeke Luna watu wameomba vibali vya ujenzi hawajapata kwa zaidi ya miezi sita, kila ukienda eti Baraza la Madiwani halijakaa kupitisha vibali. Sasa sijui kati ya Madiwani na Engineers nani anatakiwa kutoa kibali?? Na ukianza ujenzi utawaona manispaa hao wamefika wanakutaka u-stop ujenzi. Rushwa tupu.

Sasa unajiuliza, kwa nini ukanunue Kiwanja kilichopimwa halafu kupata kibali cha ujenzi upate usumbufu kiasi hiki?? Why not opt for squatter?? Unajenga bila kumfuata mtu. Ndio maana nasema hakuna motivation, its very discouraging

dah hili suala wamefanya mradi kabisa, yaani inakera, ishu ya umeme na miundo mbinu maeneo yaliyopimwa nalo ni tatizo sugu. ishu ya miundombinu ikiwemo ya umeme ndio inasababisha hata wizi kwa maeneo ya kule maana giza limejaa alafu watu wanaogopa kuhamia kwenye mabanda yako sababu ya usalama kuwa mdogo.
 
Mh: Dr faustine ndugulile (Mbunge) tanesco ni wasunbufu na wana majibu yasiyomlidhisha mteja..mfano sisi tunamalalamiko zaidi ya miezi kadhaa eneo la mpakani mwa mkwajuni na vijibweni...eneo hili umeme ni mdogo sana kiasi kwamba unaunguza mpaka vitu kwa kukosa nguvu ya kutosha, inafika muda mpaka mtu unaona ni bora usiwe na umeme kuliko kuwa na umeme ambao hauwezi kuwasha vitu vya ndani..na tumeenda mara nyingi lakini hakuna msaada wowote tunaopewa zaidi ya kuambiwa subirini foreni mtarekebishiwa..dakika ya mwisho juzi mwenzangu ameenda akaambiwa kila siku anakuja kusumbua utafikiri tatizo ni la peke yake
 
Nmealipia umeme toka mwaka jana mwez wa tisa..mpka leo cjawekewa umeme...nkienda Tanesco nnaambiwa tatizo n nguzo zimeisha... Mh tusaidie sisi wakaz wa tuangoma tuepukane na hili pale yombo kuna nguzo zaid ya 2000 kwanini wasichukue kule nasisi tukapata mwanga?
 
Mkuu Vedasto Prosper kuna hili suala la namna ya kudispose taka hapa kigamboni. Inasikitisha sana maeneo yaliyo surveyed kama kibada ,mikwambe mpaka Tuangoma; pamoja na mitaa kupangika vyema na kila nyumba kuwa inafikika kirahisi lakini hakuna huduma wala mpango wowote wa ukusanyaji wa taka. Mara kadhaa nimejaribu kwenda ofisi za serikali za mitaa lakini nao unakuta hawana majibu ya maana zaidi ya kukwambia "unajua manispaa haijatupatia gari la taka".
Matokeo yake watu either wanakua na mashimo ya taka kwenye majumba yao (njia ya kijima kabisa ya waste disposal) au wale wenzangu na mie wanavizia usiku na kutupa taka barabarani( pathetic!).
Nauliza tu, japo halipo katika vipaumbele hapo juu, lakini hivi kweli tumeshindwa hata kuorganize huduma hii ipatikane kwa kulipia kwa kila kaya? Naamini kabisa watu watakua tayari kulipia huduma hii kama ingekua available.
Kazi njema!
 
MBUNGE wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile ametoa mwito kwa wanahabari kuitangaza wilaya hiyo ambayo bado ni mpya kwa kuelezea vivutio na fursa zinazopatikana katika wilaya hiyo ili ikue kwa kasi.

Dk Ndugulile aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano wake na waandishi wa habari wanaoishi Kigamboni ambapo pia uliwashirikisha viongozi wa wilaya hiyo lengo likiwa ni kujenga ukaribu, uhusiano na mfumo wa mawasiliano.

“Tuna kazi kubwa sana ya kuitangaza wilaya yetu, tunapaswa kuelezea umma ni fursa zipi zinapatikana Kigamboni na vivutio gani vipo… hii itasaidia kukuza wilaya yetu,” alisema mbunge huyo wa Kigamboni.

Aidha, alisema amedhamiria kuhakikisha wilaya hiyo inakuwa katika kila sekta ambapo kwa upande wa sekta ya elimu amedhamiria kuweka umeme katika shule zote za sekondari ambazo hazina umeme kwa kupitia fedha za mfuko wa jimbo lengo likiwa ni kukuza kiwango cha elimu.

Alisema kwa upande wa huduma za afya alisema wamehakikisha kwamba dawa zinapatikana katika zahanati, vituo vya afya na hospitali huku wakiendelea na mikakati ya kujenga hospitali ya wilaya hiyo.

Mkuu wa wilaya hiyo, Hashim Mgandilwa alisema wameandaa dokumentari ambayo itabeba fursa zote zilizopo Kigamboni lengo likiwa ni kuitangaza wilaya hiyo.

Mgandilwa alisema kuna changamoto kubwa ya elimu lakini kwa sasa wanazishughulikia ili kuhakikisha wilaya hiyo inaongoza katika mitihani ya Taifa.

Mapema Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Rahel Mhando aliwaasa wanahabari kuzingatia maadili na misingi ya taaluma sanjari na kuimarisha ushirikiano ili kuleta matokeo chanya katika kuitangaza Kigamboni, moja ya wilaya mpya nchini zilizoanzishwa hivi karibuni
 
MBUNGE wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile ametoa mwito kwa wanahabari kuitangaza wilaya hiyo ambayo bado ni mpya kwa kuelezea vivutio na fursa zinazopatikana katika wilaya hiyo ili ikue kwa kasi.

Dk Ndugulile aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano wake na waandishi wa habari wanaoishi Kigamboni ambapo pia uliwashirikisha viongozi wa wilaya hiyo lengo likiwa ni kujenga ukaribu, uhusiano na mfumo wa mawasiliano.

“Tuna kazi kubwa sana ya kuitangaza wilaya yetu, tunapaswa kuelezea umma ni fursa zipi zinapatikana Kigamboni na vivutio gani vipo… hii itasaidia kukuza wilaya yetu,” alisema mbunge huyo wa Kigamboni.

Aidha, alisema amedhamiria kuhakikisha wilaya hiyo inakuwa katika kila sekta ambapo kwa upande wa sekta ya elimu amedhamiria kuweka umeme katika shule zote za sekondari ambazo hazina umeme kwa kupitia fedha za mfuko wa jimbo lengo likiwa ni kukuza kiwango cha elimu.

Alisema kwa upande wa huduma za afya alisema wamehakikisha kwamba dawa zinapatikana katika zahanati, vituo vya afya na hospitali huku wakiendelea na mikakati ya kujenga hospitali ya wilaya hiyo.

Mkuu wa wilaya hiyo, Hashim Mgandilwa alisema wameandaa dokumentari ambayo itabeba fursa zote zilizopo Kigamboni lengo likiwa ni kuitangaza wilaya hiyo.

Mgandilwa alisema kuna changamoto kubwa ya elimu lakini kwa sasa wanazishughulikia ili kuhakikisha wilaya hiyo inaongoza katika mitihani ya Taifa.

Mapema Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Rahel Mhando aliwaasa wanahabari kuzingatia maadili na misingi ya taaluma sanjari na kuimarisha ushirikiano ili kuleta matokeo chanya katika kuitangaza Kigamboni, moja ya wilaya mpya nchini zilizoanzishwa hivi karibuni
mbona hunipi jibu kuhusu suala la nguzo Tanesco?
 
Wakuu, Kile kipande cha barabara kutoka Mwisho wa Lami darajani hadi Njia panda ya Ferry -Kisiwani Kibada, Muda wowote inaweza anza kujengwa. Tayari Mkandalasi yupo Tayari.
ba5ace65-4593-435a-9b53-62b557c83c2a (1).jpg
 
TAARIFA YA MBUNGE WA KIGAMBONI DKT FAUSTINE NDUGULILE KUHUSU MIRADI YA MAENDELEO KIGAMBONI
Napenda kutoa taarifa ya wapi tulipofikia kwenye utekelezaji wa miradi tuliyokubaliana kwenye kikao chetu.

1. Barabara ya kutoka Darajani hadi kwa Msomali

Mkandarasi ameshapatikana kazi ya ujenzi kuanza muda wowote kuanzia sasa.

2. Upatikanaji wa nguzo za umeme

Kumekuwa na changamoto wa upatikanaji wa nguzo za moto mdogo (Low Tension-LT) toka Tanesco Makao Makuu. Nguzo za umeme mkubwa (High Tension-HT) zipo. Kazi ya usambazaji wa umeme mkubwa unaendelea. Kazi ya kuunganisha umeme majumbani unasuasua kutokana na uhaba wa nguzo. Mara ya mwisho Wilaya ya Kigamboni ilipata nguzo 50 wakati mahitaji no zaidi ya nguzo 500. Ninaendelea kufuatilia ili mgawo wa nguzo uongezeke.

3. Barabara ya Feri-Tungi-Kisiwani-Kibada

Zabuni ya barabara hii ilitangazwa mapema mwaka huu. Hadi zabuni zinafunguliwa ni kampuni moja ilijitokeza na gharama zake zilikuwa juu sana.

Gharama zimekuwa juu kutokana na hali ya upatikanaji wa kifusi kutokuwa na uhakika baada ya kuzuia machimbo katika Wilaya Mpya ya Kigamboni.

Hata hivyo, kama Uongozi wa Wilaya tumeshakubaliana kuhusu kuwa na maeneo mahsusi ya uchimbaji kifusi ambayo yatasimamiwa na Halmashauri na kwa ajili ya miundombinu ya Halmashauri na ile ya Tanroads.
Baada ya maafikiano haya, ninatarajia zabuni hii itatangazwa tena baada ya kupata uhakika wa upatikanaji wa kifusi.

4. Barabara ya Feri-Mjimwema-Kimbiji-P'Mnazi

Barabara hii itaendelea kujengwa. Makisio ya gharama yapo kwenye bajeti itakayowasilishwa Bungeni hivi karibuni.

5. Barabara ya Kibada-Mwasonga-Kimbiji

Kazi ya usanifu na upembuzi yakinifu unaendelea kwa saaa. Hakuna maoteo ya kujenga barabara hii kwa mwaka wa fedha 2017/18. Tunajaribu kuangalia wapi tunaweza kupata hela ya kujenga barabara yote kwa mpigo.

6. Suala la Kituo kidogo cha umeme

Ununuzi wa eneo umekamilika. Bajeti ya ujenzi wa kituo iko kwenye bajeti ya mwaka 2017/18 ambayo utekelezaji wake unaanza Julai 2017.

Aidha, maeneo ambayo hayana umeme tumeyaingiza kwenye mradi wa REA awamu ya Tatu. Tunasubiri utekelezaji baada ya kuzinduliwa.

Aidha, tunatarajia kukatika katika kwa umeme kutapungua sana baada ya vituo cha kupoozea umeme cha Mbagala na Kurasini vitakapokamilika.

Umeme tunaopata unaanzia Kipawa na unahudumia baadhi ya maeneo ya Ilala, Temeke, Mbagala yote, Mkuranga yote na Kigamboni yoye.

Mfano, jana umeme ulikatika jana usiku kutokana na tatizo lililotokea huko Tazara.
Ujenzi wa kituo cha Kigamboni ndio suluhu ya kudumu.

Suala la utitiri wa leseni, wavuvi kupewa nyenzo na uvuvi haramu nililifikisha kwa Waziri wa Sekta. Nikiri sijapata mrejesho wa kutosheleza kuleta majibu. Ninaendelea kufuatilia.

Dkt Faustine Ndugulile Mb
Mbunge
15.04.2017
 
TAARIFA YA MBUNGE WA KIGAMBONI DKT FAUSTINE NDUGULILE KUHUSU MIRADI YA MAENDELEO KIGAMBONI
Napenda kutoa taarifa ya wapi tulipofikia kwenye utekelezaji wa miradi tuliyokubaliana kwenye kikao chetu.

1. Barabara ya kutoka Darajani hadi kwa Msomali

Mkandarasi ameshapatikana kazi ya ujenzi kuanza muda wowote kuanzia sasa.

2. Upatikanaji wa nguzo za umeme

Kumekuwa na changamoto wa upatikanaji wa nguzo za moto mdogo (Low Tension-LT) toka Tanesco Makao Makuu. Nguzo za umeme mkubwa (High Tension-HT) zipo. Kazi ya usambazaji wa umeme mkubwa unaendelea. Kazi ya kuunganisha umeme majumbani unasuasua kutokana na uhaba wa nguzo. Mara ya mwisho Wilaya ya Kigamboni ilipata nguzo 50 wakati mahitaji no zaidi ya nguzo 500. Ninaendelea kufuatilia ili mgawo wa nguzo uongezeke.

3. Barabara ya Feri-Tungi-Kisiwani-Kibada

Zabuni ya barabara hii ilitangazwa mapema mwaka huu. Hadi zabuni zinafunguliwa ni kampuni moja ilijitokeza na gharama zake zilikuwa juu sana.

Gharama zimekuwa juu kutokana na hali ya upatikanaji wa kifusi kutokuwa na uhakika baada ya kuzuia machimbo katika Wilaya Mpya ya Kigamboni.

Hata hivyo, kama Uongozi wa Wilaya tumeshakubaliana kuhusu kuwa na maeneo mahsusi ya uchimbaji kifusi ambayo yatasimamiwa na Halmashauri na kwa ajili ya miundombinu ya Halmashauri na ile ya Tanroads.
Baada ya maafikiano haya, ninatarajia zabuni hii itatangazwa tena baada ya kupata uhakika wa upatikanaji wa kifusi.

4. Barabara ya Feri-Mjimwema-Kimbiji-P'Mnazi

Barabara hii itaendelea kujengwa. Makisio ya gharama yapo kwenye bajeti itakayowasilishwa Bungeni hivi karibuni.

5. Barabara ya Kibada-Mwasonga-Kimbiji

Kazi ya usanifu na upembuzi yakinifu unaendelea kwa saaa. Hakuna maoteo ya kujenga barabara hii kwa mwaka wa fedha 2017/18. Tunajaribu kuangalia wapi tunaweza kupata hela ya kujenga barabara yote kwa mpigo.

6. Suala la Kituo kidogo cha umeme

Ununuzi wa eneo umekamilika. Bajeti ya ujenzi wa kituo iko kwenye bajeti ya mwaka 2017/18 ambayo utekelezaji wake unaanza Julai 2017.

Aidha, maeneo ambayo hayana umeme tumeyaingiza kwenye mradi wa REA awamu ya Tatu. Tunasubiri utekelezaji baada ya kuzinduliwa.

Aidha, tunatarajia kukatika katika kwa umeme kutapungua sana baada ya vituo cha kupoozea umeme cha Mbagala na Kurasini vitakapokamilika.

Umeme tunaopata unaanzia Kipawa na unahudumia baadhi ya maeneo ya Ilala, Temeke, Mbagala yote, Mkuranga yote na Kigamboni yoye.

Mfano, jana umeme ulikatika jana usiku kutokana na tatizo lililotokea huko Tazara.
Ujenzi wa kituo cha Kigamboni ndio suluhu ya kudumu.

Suala la utitiri wa leseni, wavuvi kupewa nyenzo na uvuvi haramu nililifikisha kwa Waziri wa Sekta. Nikiri sijapata mrejesho wa kutosheleza kuleta majibu. Ninaendelea kufuatilia.

Dkt Faustine Ndugulile Mb
Mbunge
15.04.2017
Hiyo barabara ya pembamnazi inajengwa wapi?????????
 
Makisio ya gharama yapo kwenye bajeti itakayowasilishwa Bungeni hivi karibuni. Kwa sasa Wabunge wapo Bungeni, hivyo itajengwa usiwe na shaka.
Haya.....

Na tusubiri itengwe

Ingawa kitengwa ni jambo moja kitolewa ni jambo la pili

Lakini mbunge kajitahidi kuliwakilisha
 
Mshimiwa sasa nguzo 50 kati ya nguzo 500 ndo nini? Ukienda tanesco kule buza kuna nguzo zaid ya 2000 zipo pale uwanjan huu mwez wa 4 sasa
 
Kero kubwa Kigamboni ni tozo ya kivuko cha daraja jipya Mheshimiwa umefikia wapi na huu ndio msimu wa bunge la bajeti
 
Back
Top Bottom