TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

Ujenzi wa Nyumba ya Daktari katika kituo cha Afya Nhobora

Maendeleo ya mpango huu Jana, Siku ya tarehe 10/10/2016 mtendaji kata wa kata ya Mbogwe, kapewa barua na mkurugenzi wa mji nzega, kuhakikisha mtendaji wa kijiji cha Nhobola aliyesimamishwa kazi kutokana na kukataliwa na wanakijiji wa kijiji cha Nhobola kuwa mtendaji wa kijiji hicho, ahakikishe anakabizi ofisi ndani ya Siku saba na kuruhusu mambo mengine yaendelee kuhusu maendeleo ya ujenzi wa nyumba ya Daktari.
 
Leo tarehe 11.10.2016 Mheshimiwa mbunge wa jimbo la Nzega mjini ameendelea na ziara yake ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ndani ya jimbo lake ambayo imeanzishwa na nguvu za wananchi sambamba na kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Kituo cha kwanza kilikua kwenye kijiji cha Undomo Kata ya Uchama. Hapa Mheshimiwa mbunge alikagua zahanati ya Undomo na kuchangia Tsh millioni moja kwaajili ya kufanya wiring na kuvuta umeme. Ikumbukwe kwamba zahanati hii ilikua bado haina umeme.

Kituo cha pili kilikua kijiji cha Idala ambapo napo kuna changamoto kubwa ya maji. Hapa Mheshimiwa mbunge amechangia Shillingi laki tano (500000) kwaajili ya kuchimba Bwawa la Idala na kuliongezea kina. Mheshimiwa mbunge pia amechangia matofali 10000 kwaajili ya ujenzi wa zahanati ya Idala.
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa kikundi cha Umoja Mining Group kinachochimba kwenye mgodi wa namba 7 halisi ameahidi matofali 1000 na kujenga msingi wa zahanati.

Kituo cha tatu na cha mwisho kilikua kijiji cha Uchama. Kijiji hiki kina changamoto kubwa ya huduma ya afya kupatikana kwa mbali. Mheshimiwa mbunge amechangia tofali 10000 na mifuko 50 ya cement.
Katika hatua nyingine kikundi cha Umoja Mining Group katika jitihada za kumuunga mbunge kwenye shughuli za kimaendeleo, nao wamehaidi shillingi lako tano (500000 ) na Matofali 1000.

Imetolewa na Katibu Ofisi ya Mbunge.
 
Leo katika ziara ya Mheshimiwa Mbunge katika kijiji cha Undomo kuna ubadhirifu mkubwa sana umegundulika katika zahanati ya kijiji cha Undomo.

Wananchi wamekua hawapati dawa wanapokwenda hapo mida ya mchana na wagonjwa ambao kisera wanatakiwa kupata matibabu kukosa matibabu.

Baada ya kuuliza wananchi mh mbunge aligundua ;

1: Madawa yanayopelekwa na MSD mganga wa kituo hicho huhamishia katika duka lake binafsi.

2: Kamati ya Afya ya kijiji kutoshirikishwa ktk upokeaji wa madawa na kushiriki katika kufunga taarifa madawa yanapoisha.

3: Watu wenye kadi za CHF badala ya kutibiwa watu 6 badale yake wanatibiwa wawili

4: Wagonjwa kukosa huduma kila baada ya saa 6 mchana na kuambiwa wamechelewa.

Hatua alizochukua mbunge;

Mbunge aliamua kwenda kwenye duka na kukuta madawa ambayo yangetakiwa kwenda zahanati.

Mbunge aliunda kamati ya afya mpya katika mkutano huo wa hadhara.

Kuwaomba wananchi kutoa taarifa zozote zile za ubadhirifu Halmashauri au ofisini kwake.

Aidha Mheshimiwa mbunge aligundua ubadhirifu wa zaidi ya milioni 7 na kuagiza wiki ijayo mkutano wa kijiji uitwe chini ya Usimamizi wa sungusungu mapato yasomwe na mtendaji asipofanya hivo sungusungu wamkamate mtendaji na kuitaarifu jeshi la polisi.

imetolewa na Katibu wa Mbunge Nzega
 
Yupo vizuri na ana harufu ya mabadiliko kiongozi huyu.
 
Airtel Tanzania kupitia mpango wake wa Airtel FURSA “Tunakuwezesha” kwa kushirikiana na Nzega Urban Trust Fund asasi iliyoundwa kimkakati na Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini Mhe. Hussein Bashe ili kumaliza tatizo la umasikini wa kipato Jimbo la Nzega Mjini leo imezindua programu maalumu ya kuwezesha vijana iliyopewa jina la WanaNzengo Airtel FURSA.

Programu hii itawawezesha zaidi ya wajasiriamali 350 kunufaika na mikopo kupitia huduma ya Airtel Money. Mikopo hii itatolewa kwa kikundi kilichoundwa na vijana watano ambao watapewa mtaji kati ya shilingi Shs.100,000 hadi 1,000,000 kulingana na mahitaji yao.
 
Kiukweli Mala ya kwanza nilikuwa sina imani na Mh Bashe nilijua uyu mbunge sawa na wale wale waliotangulia kina seleli na Kigwangala ila sasa nimeanza kuona utofauti bashe ni mbunge wa kipekee, ila sifa tunazokupa usijisahau wananzega tunataka maendeleo hasa tatizo la maji ufumbuzi wa haraka unaitajika
 

Kukamilisha mabweni na madarasa ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondaro Bulunde


MAENDELEO YA MRADI

Leo tarehe 13/10/ 2016 naibu Waziri wa TAMISEMI bwana Selemani Jaffo akiongozana na Mh Mbunge Hussein bashe wametembelea katika shule ya sekondari Bulunde, kuangalia maendeleo ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha tano na cha sita ambapo madarasa mawili tayali ujenzi wake umekamilika, vile vile kuangalia maendeleo ya ujenzi wa mabweni ambao mpaka sasa bado unaendelea
 
ikiwa ni mwendelezo wa ziara za Mh Mbunge kuonana na wakazi wa Jimbo la Nzega Mjini kwa lengo la kukagua mipango ya maendeleo ya jimbo, na kusikiliza changamoto za wanaichi, maoni, ushauri, pamoja na kuwapa mrejesho wa changamoto mbali mbali ambazo Mh Mbunge Hussein bashe amezishuguliakia na ambazo bado anaendelea zishugurikia

Leo tarehe 13 /10 /2016 Mh Mbunge alikuwa katika kata ya Nzega magharibi katika mtaa wa majengo, Mh Mbunge kasema kuanzia mwaka wa masomo 2017, wanafunzi wote watakao chaguliwa kujiunga na kidato cha tano haijalishi umechaguliwa shule iyopo ndani ya mji wa Nzega, au nje ya Nzega kinachoangaliwa tu mwanafunzi aliyechaguliwa kujiunga na kidato cha tano awe anatoka ndani ya Jimbo la Nzega Mjini, na shule aliyomaliza kidato cha nne iwe ipo ndani ya Jimbo la Nzega Mjini, Mh Mbunge kasema atawalipia ada mpaka pale watakapo maliza masomo yao ya kidato cha tano na cha sita, jambo hili ni endelevu mpaka pale mda wake walitumikia Jimbo la Nzega Mjini ni kuisha

Hii inatokana na ahadi alizo ahidi kipindi cha uchaguzi kuwa endapo atakuwa Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini, basi elimu ya kidato cha kwanza mpaka cha sita itakuwa bure, kwakua ahadi yake ili endana na moja wapo ya ahadi ya chama chake cha mapinduzi (CCM) kuwa endapo chama cha mapinduzi kitaongoza inchi elimu ya msingi itakuwa bure (kuanzia darasa la awali mpaka kidato cha nne) hivyo baada ya chama cha mapinduzi kushinda na kuongoza inchi ahadi ya elimu bure inatekelezwa

Kwa maana hiyo elimu ya kidato cha tano na cha sita kwa sasa siyo bure, ni ya kulipia hivyo basi ili kutimiza ahadi yake Mh Mbunge aliyo ahidi kipindi cha kampeni zake leo katamka kuwa garama hizo zote za kusoma kidato cha tano na cha sita Mbunge ata garamia endapo mwanafunzi atafauru kuendelea na masomo ya kidato cha tano na cha sita.
 
Hilo suala la kusomesha wanafunzi watakao chaguliwa kujiunga kidato ha tano na cha sita nampongeza Mbunge cha muhimu asikabidhi suala hili mikononi mwa watu vijana watapata shida uko mashuleni waendapo suala hili asimamei yeye kama yeye Mbunge
 
>Kukamilisha ujenzi wa kituo cha mabasi Nzega

MAENDELEO YA MRADI

Halmashauri ya mji nzega kuanzia kesho juma tatu ya tarehe 17/10/2016 itaanza kutoa fomu za maombi ya zabuni kwa mtu au kikundi kinachoitaji kujenga banda au vibanda vya biashara katika kituo kipya cha mabasi Nzega

Gharama za uchukuaji fomu ya maombi ni shilingi laki moja (100,000/=)
 
Ombi hapa kwenye ugawaji wa zabuni isije kutokea Mbunge, au madiwani wakachukua maeneo kwa kigezo cha wameshinda zabuni nzega tunaijua siye yani mkurugenzi hapo chonde chonde tunakuomba hilo uzingatitie isije hayo maeneo wapewe wafanya biashara tu ikiwezekana wanapokuja kuomba zabuni muweke na kipengere ili ushinde zabuni inabidi uwe na tin namba na leseni ya biashara ambayo ins zaidi ya mwaka maaana watu wa halmashauri watatumia watu kushika maeneo mfano hata Mbunge uyu asije jimilikisha maeneo kwa kutumia vijana wake
 
>ujenzi wa nyumba ya Daktari katika kituo cha afya Nhobora

MAENDELEO YA MPANGO

Mtendaji wa kata ya Mbogwe, leo tarehe
17/10/2016, amekabidhi ofisi ya afisa mtendaji wa kijiji cha Nhobola, kwa mwenyekiti wa kijiji cha Nhobola, akiwa pamoja na wenyeviti wa vitongoji wa kijiji cha Nhobola, ili mwenyekiti wa kijiji aweze kuitisha kamati ya kijiji ikae na kukubaliana ili wachague kaimu mtendaji wa kijiji wa mda na kwenda benki kuchukua pesa ili ujenzi wa nyumba ya Daktari katika kituo cha Afya Nhobora uweze kuendelea

Hatua hii imekuja baada ya mtendaji wa kijiji cha Nhobola kusimishwa kazi na mkurugenzi wa mji nzega na kuombwa akabidhi ofisi ndani ya Siku saba

Hivyo Siku ya ijumaa ya tarehe 14/10/2016 mtendaji wa kijiji cha Nhobola amekabidhi ofisi kwa mtendaji wa kata ya Mbogwe
 
Miye naombi kwa Mbunge, mkurugenzi, afisa habari na Katibu jamani mda waliotoa tuchukue fomu za zabuni ni mdogo yani Siku tatu leo juma tatu mpaka juma tano alafu jambo lenyewe tumetangaziwa jana ombi ebu wambie watuachie huu mwezi wote hii haraka haraka inaibua maswali kwanini haraka hivi au tayali wamekwisha gawia viwanja wao kwa wao ili ni ombi
 

Mkuu hii stendi inajengwa sehemu gani?
 
Mkuu hii stendi inajengwa sehemu gani?
Kama mwenyeji wa nzega hiki kituo kinajengwa maeneo ya uswilu ila sasa kumepata umarufu kama maeneo ya stendi eneo hili lipo jirani na njia panda kati ya barabara inayokuja nzega mjini kutoka kitangiri, na bara bara iendayo shinyanga watu wa nzega wanaita barabara ya Uchama .
 
Umeandika vizuri mkuu ila kuna shirika moja World Vision limejitoa sana ktk wilaya hyo kutoa michango ya maendeleo ya jamii,nimejisikia vibaya kutoona hata umelitaja kwa uchache.au mashirika binafsi ni mwiko kuyasifia?wapeni na wao hongera zao mkuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…