Mjadala wa Wachangiaji M1 JF Jukwaa la Historia 2013

Mjadala wa Wachangiaji M1 JF Jukwaa la Historia 2013

Kleyst na wanawe mchango wao tumeusoma, unafahamika. Sijawahi kuusikia mchango wa baba yake Dossa kwenye harakati za kupigania uhuru, hakupenda kujihusisha na siasa?

Jingine, wazee waliojitoa kwa hali na mali tunawafahamu. Hata kwenye vitabu vya historia shule ya msingi tuliwasoma, japo si wote kama unavyoeleza kuwa kulikuwa na upotoshaji wa historia.

Kwenye jukwaa la siasa humu, kuna mtu anatajwa sana kuisaidia TANU, na anavyokuzwa utafikiri aliisaidia kuliko kina mzee Rupia.

Mtu huyo anatajwa kwa jina la Aikaeli Mbowe, wewe katika tafiti zako umewahi kukutana na mchango wa huyu mtu kwa TANU?
 
Kleyst na wanawe mchango wao tumeusoma, unafahamika. Sijawahi kuusikia mchango wa baba yake Dossa kwenye harakati za kupigania uhuru, hakupenda kujihusisha na siasa?

Jingine, wazee waliojitoa kwa hali na mali tunawafahamu. Hata kwenye vitabu vya historia shule ya msingi tuliwasoma, japo si wote kama unavyoeleza kuwa kulikuwa na upotoshaji wa historia.

Kwenye jukwaa la siasa humu, kuna mtu anatajwa sana kuisaidia TANU, na anavyokuzwa utafikiri aliisaidia kuliko kina mzee Rupia.

Mtu huyo anatajwa kwa jina la Aikaeli Mbowe, wewe katika tafiti zako umewahi kukutana na mchango wa huyu mtu kwa TANU?
Gagnija,
Azizi Ali baba yake Dossa alifariki mwaka wa 1951 muda mfupi baada ya kutoka Hijja.

Aziz Ali hakuwahi harakati za TANU.
In Shaa Allah nitakuwekea link hapo chini usome maisha yake.

Aikaeli Mbowe alisaidia kuiingiza TANU Kilimanjaro na alitoa nyumba yake moja kuwa ofisi ya TANU.

Thread 'Historia ya Aziz Ali' Historia ya Aziz Ali
 
Kabisa kamaliza kila kitu.
Suala la historia ya Tanzania madhaifu yapo na yanahitaji marekebisho sasa mzeee Said anatumia Ile gap kupenyeza agenda yake ya udini na kubeza yaliyofanywa na waasisi wengine ambao sio wa dini yake
 
Hao wachangiaji milioni moja umewahesabu vipi
 
Mzee wangu,
Kinachokuondolea heshima hapa Jf sio kwamba husemi ukweli au huoneshi mchango wa dini yako katika kupatikana kwa uhuru.

Ila shida ni kushupalia "udini" kitu ambacho hakifungamani na mshikamano na ujenzi wa taifa hili.kiasi kwamba inakuja to the maximum unataka uonekane kama ni victim.
Hakuna asiyejua mchango wa waislamu lakini nina uhakika laiti wewe ungekuwa kiongozi mkuu wa kisiasa katika nafsi yoyote hapa nchini aisee ungeleta mambo ya udini sana
 
Itakuwa jumla ya watu waliochangia na walioupitia uzi kwa kusoma tu.
Juzi niliongelea suala moja mtu anapoandika UZI tena kwenye Heading alafu kuna ambiguity kuhusu facts anapunguza credibility ya kilichoongolewa

Moja nimecheki UZI Husika katika page ya 900; post ya mwisho ni namba 17,991 mpaka dakika hii kwahio posts zote ni hizo....

Mbili tukija suala la kuvunja rekodi.... kwa haraka tu nimecheki huu UZI
una pages 20,015 na posts 400,282 mpaka sasa (Na hapo wala sijafanya upembuzi yakinifu ni top of my mind nimecheki tu posts husika....

Sasa kama tu uchunguzi / umakini wa kufanya jambo hili dogo unakuwa na uwalakini / ambiguity tutaamini vipi uchunguzi wake katika hivyo vitabu / historia kwamba napo hakujafanyika makosa madogo madogo kama haya ?
 
MJADALA WA WACHANGIAJI M1 JF Jukwaa la Historia 2013

Yericko Nyerere (pichani) miaka 11 iliyopita alifungua uzi JF kwa nia ya kupinga historia ya uhuru wa Tanganyika kama nilivyoieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

Huu ukawa mjadala mkali, mrefu uliokwenda kwa miezi sita mfululizo bila ya kusimama, uliopitiwa na wasomaji milioni moja.

Wasomaji waliosimama kama kundi moja wakimuunga mkono Yericko Nyerere walikataa kuwa Waislam na Uislam hauna cha kujivunia katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hawa walikuwa wakali kwa lugha na wakati mwingine walitoa vitisho na matusi.

Wachangiaji wachache hawajai kiganjani waliniunga mkono wakishikilia kuwa nimeandika historia ya kweli ambayo imefuta historia iliyokuwa haina ithibati.

Mimi nilisimama kwenye ukweli kuwa historia niliyoandika ndiyo historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika na historia ya kweli ya Julius Kambarage Nyerere katika uhusiano wake na wenyeji wa Dar es Salaam.

Mjadala kama huu haujapata kutokea tena na umeweka rekodi ya pekee sasa muongo mmoja umefika.

Leo nimeshangaa kuona uzi huu umewekwa JF Jukwaa la Historia na mwanachama anaejiita "Ubongokid," akiomba mnakasha ule wa watu milioni moja ufanywe kitabu.

Mjadala huu ulikuja kuzaa kitabu cha Ujasusi kilichokuja kujibu upotoshaji wa Historia ya Tanganyika na Historia ya Zanzibar, Kitabu hiki kimenipa tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu Barani Afrika 2023 na sasa nimeingia kwenye kinyang’anyiro cha kuwania tuzo ya mwandishi bora barani Afrika inayotolewa Lagos nchini Nigeria

IMG_1446.jpeg
IMG_1430.png
IMG_0120.jpeg
IMG_0054.jpeg
d279a6d1-0830-4337-85bd-d1faa574d801.jpeg
 
Suala la historia ya Tanzania madhaifu yapo na yanahitaji marekebisho sasa mzeee Said anatumia Ile gap kupenyeza agenda yake ya udini na kubeza yaliyofanywa na waasisi wengine ambao sio wa dini yake
Mpaji...
Sithubutu kufanya kitu kama hicho kwani hakuna angeinigusa.

Vyuo vyote nilivyoalikwa kuzungumza wangenipuuza kwani hakuna chuo kinamtaka mpuuzi.

Kumwalika mtu kuzungumza kwenye chuo ni mlolongo mrefu kutafuta umakini wa mwalikwaji.

Angalia picha hizo hapo chini:

1713784578097.jpeg

1713784700946.jpeg

BBC Swahili Service, Dar es Salaam
1713784833025.jpeg

AZAM TV

Halikadhalika wachapaji vitabu wasingechapa vitabu vyangu na halikadhalika vyombo vya habari visingetaka kuhojiana na mimi.
 
Mjadala huu ulikuja kuzaa kitabu cha Ujasusi kilichokuja kujibu upotoshaji wa Historia ya Tanganyika na Historia ya Zanzibar, Kitabu hiki kimenipa tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu Barani Afrika 2023 na sasa nimeingia kwenye kinyang’anyiro cha kuwania tuzo ya mwandishi bora barani Afrika inayotolewa Lagos nchini Nigeria

View attachment 2970925View attachment 2970926View attachment 2970927View attachment 2970928View attachment 2970929
Safi sana mwamba sio mtu anawapamba wazee wake tu kana kwamba wananchi wengine walikuwa hawajui umuhimu wa Uhuru!
 
Safi sana mwamba sio mtu anawapamba wazee wake tu kana kwamba wananchi wengine walikuwa hawajui umuhimu wa Uhuru!
Nyio...
Unao wazalendo wasiokuwa hawa waliopigania uhuru wa Tanganyika kisha wakafutwa katika historia ya uhuru?

Hakuna binadamu asiyetamani kuwa mtu huru lakini kujua umuhimu wa uhuru kuna maana gani kama hawakusimama kupigania uhuru wao?

Tafadhali weka hapa historia za hao unaodhani mimi sìjawatambua tuzisome.
 
Hahahaaaa... Mzee Said kipenzi cha mtume Muhammad (s.a.w). Mtetezi wa uislam. Usie na mswalie mtume dhidi ya makafir. Mfia dini mmoja. Mwarabu wa roho. Mwanahistoria isiyotamatika bila kuchomekea uislam na mchango wake chanya. Mwandishi na mwanaharakati nguli wa historia ya Tanganyika. Unalianzisha tena? Kitu pekee nakusifu, huna mihemko. Huna majibu mabaya kwa mtu.
mbona unamkejeli Mohammed Said kiaina? Sidhani kama hiyo ni sahihi.
Hayo ya kipenzi cha Mtume na muarabu wa roho yamehusu nini na historia aliyoeleza yeye?

Wacheni kejeli zungumzeni facts. Na wewe ukiandika mchango wa wakristo kwenye uhuru wa Tanganyika pia tutasoma na kutoa comments zetu, alimradi taarifa ziwe za ukweli.
 
mbona unamkejeli Mohammed Said kiaina? Sidhani kama hiyo ni sahihi.
Hayo ya kipenzi cha Mtume na muarabu wa roho yamehusu nini na historia aliyoeleza yeye?

Wacheni kejeli zungumzeni facts. Na wewe ukiandika mchango wa wakristo kwenye uhuru wa Tanganyika pia tutasoma na kutoa comments zetu, alimradi taarifa ziwe za ukweli.
Biti...
Hakuna historia ya uhuru wa Tanganyika zaidi ya hii tunayojadili hapa.

Kimeandikwa kitabu cha maisha ya Mwalimu Nyerere na waandishi wake wamenihoji mara mbili nyumbani kwangu.

Nimewaeleza haya mnayosoma hapa na nimewapa picha na nyaraka.

Kitabu hiki ni volume tatu.
Wasome kitabu hiki.

Wangekuwa wanacho cha kuandika wangeshafanya hivyo miaka mingi.
 
Nyio...
Unao wazalendo wasiokuwa hawa waliopigania uhuru wa Tanganyika kisha wakafutwa katika historia ya uhuru?

Hakuna binadamu asiyetamani kuwa mtu huru lakini kujua umuhimu wa uhuru kuna maana gani kama hawakusimama kupigania uhuru wao?

Tafadhali weka hapa historia za hao unaodhani mimi sìjawatambua tuzisome.
Watu wamepewa mitaa hadi barabara hao wengine watoto wao wamekuwa na wadhifa mkubwa hapa Tanzania ! ni nini ambacho hawajakumbukwa?
 
Watu wamepewa mitaa hadi barabara hao wengine watoto wao wamekuwa na wadhifa mkubwa hapa Tanzania ! ni nini ambacho hawajakumbukwa?
Nyiokunda,
Nazingumzia historia ya uhuru wa Tanganyika kama ilivyohifadhiwa.

Sizungumzi kuhusu kurejesha hisani wala majina ya mitaa mfano Mtaa wa Bibi Titi Mohamed.

Nimesoma kama undergraduate Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam Political Science na kulikuwa na kozi ikisomeshwa: Government and Politics in East Africa.

Katika kozi hii tulikuwa tunafundishwa historia ya nationalist politics Kenya, Uganda na Tanganyika na Zanzibar.

Mwalimu alikuwa wakisomesha historia ya TANU na kumtaja Nyerere peke yake.

Sikupata kumsikia akimtaja Abdul Sykes na wazalendo wengine hata siku moja.

Katika semina za somo hili ndipo mwalimu wangu aliponipenda sana kwani nilikuwa nikichangamsha mijadala kwa kuibomoa historia tuliyosomeshwa darasani.

Mwalimu akinisikiliza na kunitia moyo nieleze ninayoyajua na hasa nilipoeleza kuwa African Association imeasisiwa na babu zangu.

Siku hiyo darasa zima liliangua kicheko.

Mwisho wa siku niliyecheka nilikuwa mimi na wanafunzi wenzangu wakawa wameduwaa.

Mwalimu wangu huyu Mashaallah akinipa alama za juu.

Kozi nyingine ambayo mwalimu alinipenda ni The Rising of the Working Class tukifunzww siasa za watu wa tabaka la chini walivyopigania haki zao duniani kote.

Fikiria ndani ya semina mwalimu ananipa nafasi ya kueleza historia ya babu yangu Salum Abdallah mwanachama wa African Association Dar-es-Salaam kuanzia 1929 na Tabora kuanzia 1948 alipoongoza migomo mitatu ya wafanyakazi (General Strike) 1947, 1949 na 1960.

Migomo yote hii ipo katika historia ya Tanganyika lakini hakuna popote jina la babu yangu limetajwa katika vitabu vya rejea tulivyokuwa tukisoma.

Mwalimu wangu huyu na yeye alinipenda na akipenda kuniita kwa majina yangu matatu: Mohamed Said Salum.

Kisa ni kirefu.

Ndipo nilipoamua kuandika kitabu na nilianza utafiti katika Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam nikiwa mwanafunzi.

Mswada wa kitabu changu ulisomwa kwa mara ya kwanza na walimu wangu wa historia Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Napenda kusema kuwa baadhi walitumia katika paper zao katika journals na vitabu waliyosoma na kujifunza kutoka mswada wangu.

Bahati mbaya hakuna aliyefanya "acknowledgement" kwangu.

The rest is history.
 
Nyiokunda,
Nazingumzia historia ya uhuru wa Tanganyika kama ilivyohifadhiwa.

Nimesoma kama undergraduate Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam Political Science na kulikuwa na kozi ikisomeshwa Government and Politics in East Africa.

Katika kozi hii tulikuwa tunafundishwa historia ya nationalist politics Kenya, Uganda na Tanganyika na Zanzibar.

Mwalimu alikuwa wakisomesha historia ya TANU na kumtaja Nyerere peke yake.

Sikupata kumsikia akimtaja Abdul Sykes na wazalendo wengine hata siku moja.

Katika semina za somo hili ndipo mwalimu wangu aliponipenda sana kwani nilikuwa nikichangamsha mijadala kwa kuibomoa historia tuliyosomeshwa darasani.

Mwalimu akinisikiliza na kunitia moyo nieleze ninayoyajua na hasa nilipoeleza kuwa African Association imeasisiwa na babu zangu.

Siku hiyo darasa zima liliangua kicheko.

Mwisho wa siku niliyecheka nilikuwa mimi na wanafunzi wenzangu wakawa wameduwaa.

Mwalimu wangu huyu Mashaallah akinipa alama za juu.

Ndipo nilipoamua kuandika kitabu na nilianza utafiti nikiwa mwanafunzi.

The rest is history.
Mzee tulia sasa. Una madini mengi lakini udini unakufanya ukose heshima unayostahili.
 
Nilipata muda wa kupitia machapisho yote hakika kila mtu alifanya kwa nafasi yake. Hongereni sana
 
Mzee tulia sasa. Una madini mengi lakini udini unakufanya ukose heshima unayostahiki.
Peaky...
Nashukuru naheshimika.

Wala sijaandika Uislam ambao wewe unataja dini.

Hili nimelieleza mara nyingi hapa na kwa ushahidi nikionyesha vitabu vyangu nilivyoandika na kuchapwa ns wachapaji wakubwa ulimwenguni kama Oxford University Press.

Nimepokea tuzo kadhaa kwa uandishi wangu.

Nimealikwa kuzungumza na kutoa mada kwenye vyuo vingi: University of Johannesburg, Kenyatta University, University of Ibadan, University of Iowa, Northwestern University nk.

Hapa nyumbani nimezungumza: Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam, State University of Zanzibar, Sokoine na hadi shule za sekondari.

Ikitokea niko katika mji kote duniani ninapopita na jamaa wakajua niko mjini kwao hawakosi kunikaribisha hata kwa kikombe cha chai tuzungumze mawili machache.

Nimeshirikishwa katika miradi ya kuandika historia ya Afrika hapa nyumbani na nje.

Chombo.gani cha habari ambacho hakijafanya mahojiano na mimi?

TBC Taifa, TBC 1, AZAM, ITV, BBC, VoA, DW achilia mbali Online TV.

Huku ndiyo kukosa heshima?
 
Back
Top Bottom