Unapenda sana kujisifu.Peaky...
Watu wengi wananifahamu sana si wewe peke yako.
Nami nakufahamisha kuwa ningekuwa naandika dini kitabu cha Abdul Sykes nilichoandika kisingefanyiwa ''review'' na mabingwa wa African History: John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan na review zao tatu zote zikachapwa katika Cambridge Journal of African History.
Naamini unajua maana ya mimi kutajwa ndani ya Cambridge Journal yoyote iwayo ile hata kama itakuwa ni ya kujifunza kupanga maua mezani.
Peaky...Unaukataaje udini wakati machapisho yako yote yamejaa udini?
-The question of Muslim stagnation in Ed. In Tz
-The plight of Tanzanian Muslims
-Islam and politics in Tz
Kama mwanahistoria, ni article gani uliongelea dini zingine? Au zenyewe hazina historia?
Unafaa kuandika historia ya uislam, huwezi andika kitu bila kutaja uislam.
Peaky...Unapenda sana kujisifu.
Kwa leo inatosha.Peaky...
Majisufu si uungwana.
Nakujibu sijisifu na kama ningetaka kujisifu ningekueleza mengine kabisa.
Tony,ni ukweli historia ya tanganyika ina walakini mfano kuna sehemu wanaelezea Chifu Mkwawa alikuwa anajua kusoma nakuandika kiarabu, je alijifunzia wapi?
Kuna mambo mengi hapo yamefichwa au kupotoshwa.
Peaky...Kwa leo inatosha.
Naona hatutamaliza. Nikutakie jioni njema
Kwani tulikuwa tunashindana?Tony,
Mkwawa aliingizwa Uislam na Abushiri bin Salim na ndiye aliyemfunza kuandika na kusoma.
Fika Mkwawa Museum utaikuta historia yote ya Mkwawa imewekwa pale na utaelezwa kuwa baada ya kuingia Uislam jina alilochagua ni Abdallah (Mtumishi wa Allah).
Utaziona na barua alizokuwa akiandika.
Peaky...
Wengi wameshindwa kunishinda katika historia ya wazee wangu kwa kuwa haikunitaka mimi kuingia maktaba yoyote kujua kuwa babu zangu waliunda African Association mwaka wa 1929 alijenga kwa mikono yao ofisi ya African Association kati ya 1929 - 1933 nk. nk.
Wewe huna historia hii na sikulaumu kwani si chaguo lako kama ilivyokuwa mimi si chaguo langu kuwa babu yangu ni Salum Abdallah aliyekuwa mwanachama wa African Association, Al Jamiatul Islamaiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) hadi kuwa mwanachama wa TANU 1954, kuasisi TRAU 1955 na kashiriki katika mapambano yote dhidi ya ukoloni hadi uhuru ukapatikana 1961.
Mwaka wa 1964 akawekwa kizuizini Jela ya Uyui.
Historia hii isingeweza kuwapo kwa mtu mwingine yeyote.
View attachment 2972083
Kulia ni Kassanga Tumbo na anefuatia ni Salum Abdallah na viongozi wa TRAU Tabora kavishwa mgolole kama alama ya kiongozi katika mapambano
Peaky...Kwani tulikuwa tunashindana?
Tatizo lako ni udini pekee.
Cambridge wanaijua historia ya Tanzania kuliko Watanzania?Peaky...
Nami nakujibu kuwa ningekuwa naandika dini nisingekuwa mmoja kati ya waandisi 500 kutoka kila pembe ya dunia walioandika Dictionary of African Biography (DAB).
Volume sita na ulikuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press New York.
Mwenye tatizo ni wewe unachomwa na kuandikwa historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika ambayo imepokelewa vyema na Cambridge Journal of African History, Dictionary of African Biography (DAB)na vyuo vyote duniani vinavyosomesha historia ya Afrika.
Iweje hawa hawaoni Uislam katika kalamu yangu?
Na mwandishi wa historia hii ni mimi.
Peaky...Cambridge wanaijua historia ya Tanzania kuliko Watanzania?
Niliwajua kitambo.Peaky...
Mimi siwezi kuwajibia ila nitakuuliza wewe je uliwajua waasisi wa historia African Association kabla ya mimi kuandika majina yao hapa?
Kitabu kichapwe wasomaji wataamua wenyewe kama historia ilivurugwa au la.Kitabu kichapwe kwa madhumuni ya kuonyesha yaliyochangiwa na wasomaji ili kudhihirisha jinsi historia ya uhuru ilivyokuwa imevurugwa.
Kuchapwa mjadala ule kama ulivyokuwa utabainisha ukweli.
Peaky...Niliwajua kitambo.
Chief,Kitabu kichapwe wasomaji wataamua wenyewe kama historia ilivurugwa au la.
Je, Elimu Hii umepanga kuirithisha kwa watu?Nyiokunda,
Nazingumzia historia ya uhuru wa Tanganyika kama ilivyohifadhiwa.
Sizungumzi kuhusu kurejesha hisani wala majina ya mitaa mfano Mtaa wa Bibi Titi Mohamed.
Nimesoma kama undergraduate Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam Political Science na kulikuwa na kozi ikisomeshwa: Government and Politics in East Africa.
Katika kozi hii tulikuwa tunafundishwa historia ya nationalist politics Kenya, Uganda na Tanganyika na Zanzibar.
Mwalimu alikuwa wakisomesha historia ya TANU na kumtaja Nyerere peke yake.
Sikupata kumsikia akimtaja Abdul Sykes na wazalendo wengine hata siku moja.
Katika semina za somo hili ndipo mwalimu wangu aliponipenda sana kwani nilikuwa nikichangamsha mijadala kwa kuibomoa historia tuliyosomeshwa darasani.
Mwalimu akinisikiliza na kunitia moyo nieleze ninayoyajua na hasa nilipoeleza kuwa African Association imeasisiwa na babu zangu.
Siku hiyo darasa zima liliangua kicheko.
Mwisho wa siku niliyecheka nilikuwa mimi na wanafunzi wenzangu wakawa wameduwaa.
Mwalimu wangu huyu Mashaallah akinipa alama za juu.
Kozi nyingine ambayo mwalimu alinipenda ni The Rising of the Working Class tukifunzww siasa za watu wa tabaka la chini walivyopigania haki zao duniani kote.
Fikiria ndani ya semina mwalimu ananipa nafasi ya kueleza historia ya babu yangu Salum Abdallah mwanachama wa African Association Dar-es-Salaam kuanzia 1929 na Tabora kuanzia 1948 alipoongoza migomo mitatu ya wafanyakazi (General Strike) 1947, 1949 na 1960.
Migomo yote hii ipo katika historia ya Tanganyika lakini hakuna popote jina la babu yangu limetajwa katika vitabu vya rejea tulivyokuwa tukisoma.
Mwalimu wangu huyu na yeye alinipenda na akipenda kuniita kwa majina yangu matatu: Mohamed Said Salum.
Kisa ni kirefu.
Ndipo nilipoamua kuandika kitabu na nilianza utafiti katika Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam nikiwa mwanafunzi.
Mswada wa kitabu changu ulisomwa kwa mara ya kwanza na walimu wangu wa historia Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.
Napenda kusema kuwa baadhi walitumia katika paper zao katika journals na vitabu waliyosoma na kujifunza kutoka mswada wangu.
Bahati mbaya hakuna aliyefanya "acknowledgement" kwangu.
The rest is history.
Dr. M...Je, Elimu Hii umepanga kuirithisha kwa watu?
Ili kupatikane Isnad safi na mnyororo Uliofaa?
Kama umechapwa kwenye Cambridge journal of African history, wewe tayari ni mshindiDr. Mambo...
Si kama nataka kujisifu ila nataka kukueleza ukweli.
Hakuna wa kunishinda katika historia ya uhuru wa Tanganyika.
Na sababu yake ni moja tu.
Mimi nimeandika historia ya wazee wangu ambao ndiyo walioasisi African Association 1929 na wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika 1933), wakampokea Julius Nyerere 1952 na wakaunda chama cha TANU 1954.
Niliyoandika hakuna aliyekuwa anayajua katika hao wote watu milioni moja ila wachache sana.
Kuwa na watu wengi wanaokuunga mkono si ushindi.
Ushindi ni kuwa na historia ambayo hakuna aliyekuwa anaijua.
Vipi Yericko anishinde mimi?
Wala hao unaowaita manguli wa historia hawakuwa wameandika lolote katika si paper wala kitabu.
Mimi nimeingia katika mjadala nikiwa na "track record," nzito.
Nimeandika vitabu kadhaa, nimezungumza vyuo vikuu kadhaa Afrika, Ulaya na Marekani na nimechapwa katika Cambridge Journal of African History na nikiwa mmoja wa waandishi 500 walioandika Dictionary of African Biography (DAB).
Naamini umeelewa.
Bale...Kama umechapwa kwenye Cambridge journal of African history, wewe tayari ni mshindi
MohamedPeaky...
Uliwajuaje?
Peaky...Mohamed
-Inamaana kabla yako kuja na hii historia ya upande mmoja hakuna historia zingine zimeandikwa?
-Wewe unaongelea historia ya kuanzia 1950's je kabla ya hapo Tanganyika haikuwa na historia?
-Hao unaowaita wazee wako wakati wanafanya hizo harakati za uhuru, hakukuwa na watu wengine walioshuhudia?
-Kwa nini unahisi ni wewe tu unaeijua historia ya kweli na si wengine pia?
-Unahisi ukiandika historia na wengine wakaamua kunyamaza wasikukosoe utakuwa umeonge ukweli ndio maana wakanyamaza?Peaky...
Kitabu cha Abdul Sykes si historia ya upande mmoja.
Kuna historia ya wazalendo wengi waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Wazalendo hawa huwasomi popote katika vitabu vilivyotangulia ila katika kitabu cha Abdul Sykes.
Unaweza ikiwa kitabu unacho ukaangalia Faharasa (Index) utakuta majina yao.
Mimi naongelea historia ya uhuru wa Tanganyika kuanzia 1924 Dr. Kwegyr Aggrey alipokutana na Kleist Sykes na Dr. Aggrey akamshauri Kleist kuasisi African Association.
Sikuanza historia ya uhuru katika miaka ya 1950.
Wengine waliokuwapo wakati huo nimewataja mfano Martin Kayamba, Erica Fiah, Ali Jumbe Kiro, Juma Mwindadi kwa kuwataja wachache.
Mimi naijua historia ya kweli kwa sababu nimeiandika na hakuna mtafiti mwingine aliyeipinga kwa kuja na kitabu chenye historia inayopingana na historia niliyoandika.
Kitabu sasa kina umri wa miaka 25.
Lakini kubwa hii ni historia ya watu ambao wengi wao mimi niliwafahamu udogoni kwangu.
View attachment 2972736
Juma Mwindadi Mwalimu Mkuu wa shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika
Mwafrika wa Kwanza Mjumbe katika Bodi ya Dar es Salaam Municipal Council
Mwafrika wa pili ni Kleist Sykes
View attachment 2972739
Erica Fiah
Mwafrika wa kwanza kuwa na gazeti ''Kwetu.''