Mjamzito afariki kwa kukosa pesa ya mafuta gari la wagonjwa, wakati Mama ananunua magoli

Mjamzito afariki kwa kukosa pesa ya mafuta gari la wagonjwa, wakati Mama ananunua magoli

Hatuwezi kulaumu serikali kwa kila kosa linalofanywa na watu huku chini!,sio kwamba hawakuweza kumuwahisha hospital huyo mama mambo mengine sie wananchi wenyewe hatuna uwajibikaji huyo dereva alishindwa nini kuwasaidia mafuta ya 180000! hata nauli mwanza dar haifiki hiyo hii ni rushwa sasa!..
huo si uzembe wa rais ni uwajibikaji wa dereva ama hiyo sehemu anayofanyia kazi,mwananchi hawezi kulipia pesa yote hiyo et mafuta huo ni uzandiki!.

watanzania tubadilike kwanini tutumie shida za mwengine kama sehemu yakupatia fedha,kwani kila mtu akifanya wajibu wake nini kitaharibika!!.
uchunguzi ufanyike na wanaotakiwa kuwajibishwa wawajibishwe hatuwezi kulea huu upuuzi kiasi hichi,hizi ni tamaa za watu binafsi!.
Masikini wa aina hiyo wanaohitaji msaada wa aina hiyo wako wengi sana nchini sasa dereva atasaidia wangapi??
 
Walishaambiwa wafyatue tu, huduma ziko bwerere na mapori bado yako makubwa hayana watu na wanyama.
Poor Tanzanians.
Kuzaana sio shida ikiwa rasilimali zinamfikia kila mtoto anayezaliwa. Lakini sio kila mja mzito anayeaga dunia lawama zipelekwe kwa Rais, hana jukumu la moja kwa moja la kushughulika na kila shida ya kila mtanzania.
 
Kuna mbunge wa huyo mama kuna mkuu wa wilaya anayotoka huyo mama, kuna mkuu wa mkoa. kuna serikali nzima kabla hujamhusisha SSH.

Wote hao wanahusika na wanawajibika kumsaidia huyo mama. Kuna zahanati zinazojengwa kwa pesa za kodi na huko Morogoro zipo nyingi tu.

Magoli yatanunuliwa tu kwani Simba na Yanga ni walipa kodi wakubwa kuliko taasisi nyingi zilizopo nchini. Wanao mchango mkubwa wa kukuza jina la Tanzania kimataifa.

Kila wanapofuzu makundi au robo fainali kuna pesa nyingi wanazoingiza kwenye akaunti za vilabu vyao na kuna kodi nyingi inayoingia serikali kuu.

Serikali haiwezi kumsaidia moja kwa moja kila mwanamke mjamzito, tupunguze hizi nongwa za kipuuzi.
Sasa mbona kituo cha afya au hata choo tu kikijengwa huko kijijini kwa kodi za raia sifa zote zinaenda kwa mama??
 
Baba yako angetumia condom tu, mwananchi wa kijijini anaweza kulipa sh 180,000? Umeona posho wanazolipana maofisa wa serikali?
Umeona magari ya thamani yanayonunuliwa serikali kila mwaka?
Unajua kuna halmashauri huwa zinarudisha pesa serikalini kwa kukosa matumizi?
Unajua wastani wa kipato cha mwananchi wa kijijini?

Ubinafsi wa kichawi huu kushindwa kuwaonea wengine wasio na kipato. Hebu tuambie serikali imefanya juhudi gani za kimkakati ili kuinua maisha ya watanzania vijijini?
Kweli wewe ni kiazi kwa kutetea upande mmoja na kushindwa kuona upande wa pili usiowajibika! Kuwa na wewe kiongozi upande mkokoteni tukuone unajali sana!
hivi unajua ni vijijini ( wengi wao) ndio wanakoongoza kwa kutopenda maendeleo kwa kukumbatia imani za kishirikina, ulevi na uvivu.
Ni mara ngapi umesikia wazazi wakizuia watoto wao wasiende shule kupelekea serikali kuwatafuta kwa gharama kubwa kuwarudisha shule.
Ni mara ngapi umesikia watu wa vijijini wakijivunia kuzaa kila mwaka bila kujali atajifungua vipi na atamlea vipi akiamini kila mtoto huja na bahati yake.
Vijiji vingi ni changamoto na wanatakiwa kuambia ukweli au la waendelee kujifunza in a hard way na kwamba hamna cha bure.Wawajibike na serikali iwajibike, Hakuna anayependa kuona mama mjamzito anafariki ila penye mapungufu lazima pasemwe kwa pande zote.
 
Kweli wewe ni kiazi kwa kutetea upande mmoja na kushindwa kuona upande wa pili usiowajibika! Kuwa na wewe kiongozi upande mkokoteni tukuone unajali sana!
hivi unajua ni vijijini ( wengi wao) ndio wanakoongoza kwa kutopenda maendeleo kwa kukumbatia imani za kishirikina, ulevi na uvivu.
Ni mara ngapi umesikia wazazi wakizuia watoto wao wasiende shule kupelekea serikali kuwatafuta kwa gharama kubwa kuwarudisha shule.
Ni mara ngapi umesikia watu wa vijijini wakijivunia kuzaa kila mwaka bila kujali atajifungua vipi na atamlea vipi akiamini kila mtoto huja na bahati yake.
Vijiji vingi ni changamoto na wanatakiwa kuambia ukweli au la waendelee kujifunza in a hard way na kwamba hamna cha bure.Wawajibike na serikali iwajibike, Hakuna anayependa kuona mama mjamzito anafariki ila penye mapungufu lazima pasemwe kwa pande zote.
Mleta mada bado anatumia njia ya kujenga hoja kwa nia ya kuvuta hisia za huruma kwa msomaji. Ni njia iliyopitwa na wakati ya kujenga hoja.

Karibu kila mkoa kuna magari ya wagonjwa wanagawiwa kila siku na wizara ya afya, huko Morogoro anapotoka huyo Mjamzito aliyefariki halijafika gari la wagonjwa?.

Pia kuna serikali nzima ya Mkoa yenye kuwajibika moja kwa moja na shida za wananchi, huyo Mama walishindwa kumuona na kumsaidia?.
 
Back
Top Bottom