Mjane wa Mrema atoswa, familia yapinga wosia uliachwa na Mrema. Mjane apokonywa nyumba ya Salasala

Tukiacha hili wazo lako liendeleee vikongwe wengi wenye pesa watavamia na viduduwasha dakika za mwisho ili warithi mali.

Hili halipo!!
 
Mrema hakuwa mzee kihivyo
Sema kisukari tu kimempelekesha
Na kumdhohofisha mwili

Ova
 
Wanazuwia mali za mjane lakini hawaja mzuwia Mrema kuoa wakati wa uhai wake. Ama kweli tukifa wajane na watoto wetu wanapitia wakati mgumu sana.
Mimi nadhani sheria zibadilike ili kuangalia ''hali halisi''. Nakwazika kukubali mwanamke anayeolewa na mtu mgonjwa na mzee kama alivyokuwa Mrema, na wakaishi kwa muda mfupi kabisa na hana mtoto yeyote eti anastahili kurithi mali ya marehemu.
 
Kinachowauma ndugu ni shemeji yao kuja kula mali za ndugu yao na wanaume wengine.

Mrema karata zake hakuzichanga vyema, kwa umri wake na maradhi yaliyokuwa yanamuandama angetafuta mjane mwenye hata 55+ amsaidie afe nae hapo kusingekuwa na purukushani hizi.
 
teh teh teh teh -- fursa mzee hiyo wacha wazee waliwe si wanayataka wenyewe !!
 
Ndo mkome kuoa uzeeni, ukifika miaka kuanzia 70 upo Saa ya jioni jiweke karibu na Mola wako ujiandae safari ya kuondoka duniani, ni kipindi cha kutengeneza na Mola wako
 
Kimsingi unapokabiliana na maradhi yenye kuonesha kupona ni kudra za Mungu haina haja ya kuoa kama huna mke, maana ukioa ni muda mfupi tu unaweza kuaga dunia ukamuachia mtoto wa watu sintofahamu kwenye kumiliki mali kama mke halali wa ndoa.

Hili nalo liwe funzo kwa mabinti kukimbilia mali kwa wazee waliowazidi umri mkubwa watapata fedheha wakifiwa na hao wenzi wao endapo watadumu muda mfupi.
 
Umeongea kwa busara sana mkuu, hongera
 
Shida ni wao kushindwa kumshauri mzee wao asioe au asifunge ndoa Kanisani! Hapa ndipo mwanadada alipocheza kete muhimu!

Sheria ya ndoa na sheria ya mirathi ni vitu viwili tofauti! Kwenye sheria ya ndoa sifa ya mtu kupewa mgao wa mali inategemea na namna alivochangia katika upatikanaji wake, hapo kama ingetokea huyo mke wa Mrema angepeana TALAKA leo hii na Mrema basi asingepata mgao wowote wa mali kwakua ndani hiki kipindi walichooana (March to August) hakuna mali yoyote waliyochuma pamoja na hata kama ingekuwepo basi ingekuwa kidogo sana!

Kwa Upande wa sheria ya mirathi inaangalia tu nani na nani wana sifa ya kurithi mali za Marehemu?
Katika kundi hili wenye sifa ni pamoja na mjane wa Marehemu bila kujali aliolewa nae jana au leo! Kikubwa ni awe tu na sifa ya kutambulika kama mke halali na hapo kitambulisho ndoa halali tu!

Hivyo kwa muktadha huo mjane wa Mrema ana sifa ya kuwa mmoja wa warithi wa mali za Mrema hata kama hajazaa nae mtoto hata mmoja kwakua hakuna sheria ya ndoa au ya mirathi inayomlazimisha kuwa na mtoto!
 
Upo sahihi lakini inategemea na aina ya ndoa iliyofungwa. Kama ni customary marriage hawezi kurithi.

Pia sheria ya mirathi inaangalia wanandoa waliishi maisha gani kipindi cha uhai wake/wao. Mfano kama waliishi kimila mali itagawanywa kulingana na sheria za mila.

Vivyo hivyo kama waliishi katika imani za dini mfano kiislamu basi itatumika Islamic law kwenye suala la mirathi.
 
Ngoja tusikilize Wosia wa marehemu Mrema alisemaje!
Your browser is not able to display this video.
 
Inakuaje mtu anaambiwa hakua na akili timamu wakati anaandika wosia wakati huo huo hawasemi akili haikua sawa wakati anafunga ndoa? Ikiwa ni hivyo waseme hata ndoa sio Halali Kwa sababu akili haikua sawa pia.
Ukifika miaka 70, kisheria kuna baadhi ya maamuzi yako yanaweza kupingwa mahakamani either ukiwa bado hai ama mfu sababu kuu ni kwamba afya ya akili inakuwa ishaanza kuzorota katika umri huo.
 
ukifika miaka 70, kisheria kuna baadhi ya maamuzi yako yanaweza kupingwa mahakamani either ukiwa bado hai ama mfu sababu kuu ni kwamba afya ya akili inakuwa ishaanza kuzolota katika umri huo.

Huko kote Sina ubishi, Sasa kama ni hivyo, siwarahisishe mambo kwa kuanza kutengua maamuzi yake ya kuoa? Kwamba hata ndoa yenyewe ni batili. Baada ya hapo haya mengine yote yatakua Batili pia, kesi inaisha.

Nje ya mada, hivi Rais wa USA wa Sasa na aliyepita Wana umri Gani? Tuangazie na spika wa bunge Peloci pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…