Mjini Mipango: Unaweza kuanza hii biashara hata kwa mtaji usiozidi bei ya iPhone moja latest

Mjini Mipango: Unaweza kuanza hii biashara hata kwa mtaji usiozidi bei ya iPhone moja latest

Isanga family wewe ni wapi huko tunasifika kwa uchapakazi?🙃
Mkuu hili la kusema watanzania ni wachapakazi mara nyingi ni bla bla zilizopo mitaani ukiwa Tanzania. Na linatokana na watu kukosa expusure ili wajue watu nchi nyingine wanafanyaje kazi. Hata mimi kbla sijatoa tongotongo nilikuwa nadhani nchi kama za Ulaya au hata India watu hawawezi kazi za ''maguvu'' hata kidogo. Kila kwa mfano nikiona wahindi au wazungu naona kama ni walaini na hawawezi shuruba. Kumbe nilikuwa nakosea. Isanga family yeye nadhani ana-compare zaidi na South Africa ambako nao nasikia ni wavivu kweli kweli. Nasema hivi kwa sababu amekuwa anatoa michango mingi inayoonyesha kuwa yuko familiar sana na South.
 
Wewe umeamua tu kufanya ligi na mwanzisha uzi, kimsingi alichoeleza kiko wazi na amejibu accordingly. Few sips of water can do
Jamaa ana majibu mabovu tu sijaelewa na wengi hawajaelewa nilitaka anieleweshe lakini matokeo ndiyo hayo majibu ligi me ya nini mkuu
 
Mkuu hili la kusema watanzania ni wachapakazi mara nyingi ni bla bla zilizopo mitaani ukiwa Tanzania. Na linatokana na watu kukosa expusure ili wajue watu nchi nyingine wanafanyaje kazi. Hata mimi kbla sijatoa tongotongo nilikuwa nadhani nchi kama za Ulaya au hata India watu hawawezi kazi za ''maguvu'' hata kidogo. Kila kwa mfano nikiona wahindi au wazungu naona kama ni walaini na hawawezi shuruba. Kumbe nilikuwa nakosea. Isanga family yeye nadhani ana-compare zaidi na South Africa ambako nao nasikia ni wavivu kweli kweli. Nasema hivi kwa sababu amekuwa anatoa michango mingi inayoonyesha kuwa yuko familiar sana na South.
Hapo sawa nakuelewa!
 
Leo nimeenda kukodisha mbao. Yule jamaa nimemuachia 30,000/- kwa mbao 20! Jamaa ana mbao nyingi tu Kwa ajili ya kukodisha. Nimefikiria unaweza kuanza hii biashara hata Kwa mtaji usiozidi bei ya iPhone moja latest. Imagine huyu mtu akipata wateja wawili tu kama mimi anatengeneza 60,000/- haina kodi wala nini maanake mbao ziko uwani kwake. Vijana amkeni fursa zipo zinasubiri uthubutu.
Vijana wamebweteka sana, wanasubiri kuajiriwa
 
Naishi mbali kidogo na eneo husika, sasa hapo site kuna jamaa yangu pia amejenga akaniambia tuchukue kwake, ili kuokoa muda nikamtuma fundi akaziangalie kama zinafaa akasema hazifai kabisa
Na eti anajifanya fundi mwaminifu anasema hawezi kutumia mbao mbovu maana kazi zake yeye huwa hataki kuharibu
Basi nikawa sina namna ila kununua tu,

Hata hivyo umenipa somo, tunakoendelea bora ionekane nabishana na mtaalamu
Inawezekana pia fundi alikuwa sawa na alichokiona maana kama mbao zimetumika muda mrefu na zimepinda ama kupasuka zingemsumbua fundi na pengine kuharibu kazi.
 
Jombaa wapo ambao Iphone pia ndio mtaji na ofisi yao kiasi cha kuingiza zaidi ya hata 100K kwa siku...nakubaliana pia wapo ambao wanamiliki Iphone kwa kuchat tu facebook, whatsap nk huku hata techno ya 60k ikiweza kufanya hizo kazi..

tukirudi kwenye maada yako, hiyo biashara ni nzuri sana kwenye maeneo ambayo yako active kwenye ujenzi kama Goba, madale, bunju nk..zipo nyingine kama concrete mixer, plate compactor ndogo, roller compactor ndogo..nk.

Nakubaliana na wewe, mjini fursa ziko nyingi kuna wakati kinahitajika kichwa chako tu na kama una uwezo wa kuwa na hela kuanzia 1m to 5m zinachezaga na wewe basi umiza kichwa kila siku nini ufanye zilete matokeo na sio kwenda kuzichoma kidimbwi au juliana....
 
Ujenzi gani huo unakodi mbao kisha zinarudi bila kuwa na matundu ya misumali?
 
Mkuu unachosema ni sahihi mno! WATANZANIA NI WAVIVU
Uko sahihi nkoi. Sio WaTZ tu, ni karibu Wafrika wote ni wavivu, hatupendi kazi, tuna visingizio sana na si waaminifu. Nimeona hii kwa nchi kadhaa za Afrika nilizofika.

Ukienda nchi zilizoendelea ndio utajua sisi ni wavivu na hakuna wakati tutawafikia wenzetu. Hata tubadilishane wahamie Afrika, twende kwao, baada ya miaka michache watatupita tena.

Hii jamii yetu ya wavivu wengi pia inakwamisha wachache wenye bidii. Unaajiri vijana, wanakusumbua hadi uwasimamie hasa. Na ukiwasimamia wanakimbia. Huwezi fungua biashara ukasafiri au ukashinda kwenye majukumu mengine inakufa.

Ndio maana matajiri wengi Afrika wenye makampuni makubwa wasimamizi wao wa kazi ni Wazungu au wa-Asia. Tazama Mo, Bakhresa, Mengi, Dangote, Patel na hata makampuni mengi yanayokuwa.
 
Back
Top Bottom