Mjue Judith Mhina, mwanamama aliyetaka kuinunua Vingunguti na Buguruni Mnyamani kabla hajazuiwa na Hayati Magufuli

Nikajiuliza alikuwa mfanyabiashara gani mkubwa tz huyu?bahresa at al washindwe kuwatoa maskin vingunguti na buguruni aje kufanikiwa huyu wa kuja kwa pesa za mirathi?😅ikiona nyani mjini ujue kaletwa huyo
Radio mbao yeye ni kivuli tu nyingi ni kodi zetu toka kwa wapigaji aliodili nao Magu akiwemo Dalali wa meno ya tembo kada muenezi.
 
Hawa ndio watu tunao wahitaji,masikini wanaharibu miji yetu,dsm ilitakiwa ijengwe majengo mazuri ya kisasa apartments za magorofa kisha watu waje wapange,sio kuruhusu ujenzi holela.
Vijumba vingi dar vinatia huruma sijuwi waliachiwa na babu zao bati zimeoza hovyo yani hata huko mnakoita mkoani ukiwa na nyumba kama mazosemea hapa unachekwa.
 
Unazo namba zake?
 
Watu waongo Sana, unafikiria angeweza kumlipa bakhresa kwenye uwekezaji wake na wengineo watoke?
Yeye alitaka kuanzia ukivuka reli kama unatokea Nyerere road hadi barabara ya kutoka shell kuelekea Vingunguti na upande ule hakuna kiwanda chochote zaidi ya makazi ya watu na biashara za chini na za kati yakiwemo mabaa na magesti house.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…