Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

Kweli Dr.W.Slaa wewe ni mtu makini sana. Ahsante kwa darsa japokuwa kuna watu kazi yao ni kujaribu kukupiga propaganda za kila aina lakin mpaka leo wanahaha kwani m naona siku hadi siku unazidi kushine na kuwa tishio kwa maCCM na washirika wao masalia.

"Mungu akisema ndiyo hakuna mwanadamu yeyote mwenye pumzi na nyama wa kusema hapana"
 
Last edited by a moderator:
Dr. Slaa kaelezea kwa kirefu tu mantiki nyuma ya MoU. Nimeelewa.

Je, wafahamu na dhehebu za Kiislamu nazo zimenufaika sana?

Je niwangapi wanafahamu Aga Khan ni equivalent ya Papa wa Ismailia kama ilivyo Papa Benedict kwa wakatoliki?

Hizi hapa mali za dhehebu la Ismailia:

1. Aga Khan University
2. Aga Khan Hospitals
3. Diamond Trust Bank
4. Dar Es Salaam Serena Hotel

Mzizima au Shaaban Robert ilikuwa ya Ismailia pia. Baada ya kutaifishwa ndio watoto wa kimatumbi nao wakaanza kuhudhuria.

Shyrose Banji ni muismailia. Ndio maana mpambanaji.
 

Nyie endeleeni kulumbana, mimi naomba kuuliza kama huko kwenu kuna shule nzuri za kiislamu zinayopokea watoto wa kikristo nimlete mwanangu aanze chekechea. naogopa nikizubaa wanangu watakuwa walalamikaji siku zijazo, na lengo la mafisadi litakuwa limetimia. Maana hizi st. kayumba zinaandaa watu wa dizaini hii, mafundi wa kulalamika tu.
Cha Muhimu: Shule hiyo isimlazimishe mwanangu kujifunza dini, mimi nataka ajifunze elimu ya kidunia tu na maadili ya mtanzania, ajuwe haki za binadamu na kuziheshimu.
 
Unauhakika kuwa mashek wengi hawana uwezo wa kufanya resarch?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

kwani ili uwe sheikh ni elimu gani unapaswa kuwa nayo, kwanini watanzania hatutaki kuambiwa ukweli..
 
Labda kabla hamjamsifu Dr Slaa mie nianze kwa kumuulize haya yafuatayo:

Mosi ni shule ngapi zilitaifishwa za seminary (mission schools). Na shule ngapi za Islamic seminary zilitaifishwa ? Tukijua hayo then tuweze kukuelewa hoja yako ya kwanza ati Serikali ilikuwa ikitaifisha mashule ya dini.

Pili nakuuliza dr Slaa ni sahihi kudai eti Serikali ilishindwa kutoa huduma na taasisi za kidini zilikuwa na uwezo wa kusaidia. To me huo ndio ufisadi wenyewe kwasababu mie nalipa kodi ili Serikali itoe huduma na sie ikahudumie mtu mwengine halafu mie ndio nihudumiwe. Huo unaitwa white collar theft. Kwasababu kama serikali imeshindwa kuhudumia basi wameshindwa nini kuruhusu sekta binafsi ziwasaidie ????

Na mwisho kabisa ni kwanini hii MOU isiwe short term plan halafu long term plan iwe serikali ijenge hospitali zake na shule zake yenyewe?? Tunaibiana tu kwa kutengeneza mazingira ati kuna shida fulani basi ndio maana tunachota hizo kodi. Mwisho wa siku kanisa ndio linakinga ndoo yake.

Sasa hivi naona ati kanisa linaanza kuzalisha umeme ati mahitaji ya kusaidia wananchi wapate umeme. Swali nauliza hivi kanisa linafanya biashara? Kwani wanadai wanatengeneZa umeme halafu wawauzie wananchi halafu huo unaitwa msaada . Msaada unauzwa ?? Mwishoe tutasikia Serikali imeingia makubaliano na kanisa kupeleka umeme. In short hii nchi inapoelekea sio kuzuri tutagawana mbao maana haingilii mie kodi yangu kama muislamu iibwe huku tunaona huo ni wizi wa mchana . Serikali ijitenge na mambo haya yatapelekea kwenye machafuko nchini.
 
Mimi nilichogundua ni kuwa CDM na CCT/TEC ni faces of the same coin! Hushangai wapambanaji wa CHADEMA ndio hawa wanaopigania MOU!

kwanza umeielewa MOU inafanyaje kazi au umekurupuka tu kama umebanwa na mavi?
kwahiyo tuseme BAKWATA na CCM ni face of the same coin?
Asante kwa kutambua kwamba chadema ni chama kinachotetea haki na usawa wa watu, kwakuwa umekiri mwenyewe kuwa kila anayetetea haki. na usawa humu ni mpambanaji wa chadema!
 

Humjui Shyrose Bhanji...mama yake Mjita wa Musoma, baba ni Muhindi wa Mwanza. Ismailia ukishachanganya na mweusi una tena hadhi ya kuwa Ismailia labda uchanganye na mzungu.
 

Hivi Muslim University of Morogoro si mlipewa Bure au
 

... 'umesikia' .... Mbona nyie ni watu wa kuambiwa tu, weka hapa huo ushahidi wa hiyo MoU yenu iliyokua too late..... Waislam wa kawaida wametulia na wanaendelea na maisha yao vizuri, nuie wachache wa elimu ndogo ni wasumbufu kwa sababu ya kupotoshwa kwa manufaa ya wengine
 
Slaa kasema vizuri tu,msingi wa mou ndio huo waislam wenzangu,masheikh waache sasa hii habari jambo la msingi walilopaswa kulivalia njuga ni urejeshwaji wa mahakama ya kadhi ambayo mkapa aliwaahidi waislam akiwa mwenyekiti wa ccm na kuonyesha msisitizo kwamba jemedari mkapa alipania kutupatia waislam kadhi kama alivyopigana kiume licha ya upinzani mkali wa kanisa kuhakikisha chuo kikuu cha kiislam kinaanzishwa ndani ya utawala wake,tatizo la utekelezaji wa uanzishwaji wa mahakama ya kadhi lilianza kulegalega walipoingia madarakani kikwete na lowassa angekuwepo mkapa muda huu mahakama ingekua ilishaanza muda mrefu,masheikh muulizeni kikwete kwanini aliiondoa kabisa kwenye ilani issue ya mahakama ya kadhi?????????pengine tuanzie hapo,mjadala wa mou umefungwa rasmi sababu ni wa kitoto
 
Hata bugando kumbe ilikuwa hosptali ya kanisa! Hapa nimepata kitu.

siyo ilikuwa ya kanisani ni kanisa pamoja na ya kcmc iliyoko kilimanjaro..ukitaka kuona kazi ya kanisa tembelea vijiji vya mikoa ya kanda ya ziwa utaona madaraja, dispensary na shule kuna barabara zina hudumiwa na makanisa lakini ndugu zetu wamebaki kulalamika tu..
 
Hivi Muslim University of Morogoro si mlipewa Bure au

... Hujamalizia mkuu, wamepewa bure halafu wamebadilisha kuwa chuo sawa na madrasaaa ....sio kwa manufaa ya wananchi wote! ..... hapo hawatasema
 

... Kila kitu mnataka mfanyiwe, si mmeambiwa ruksa kuianzisha, muiendeshe wenyewe na muigaramie wenyewe ...... Mnataka nini cha ziada...... Mi nasubiri kucheka tu mtakapoianzisha halafu waislam wenzenu wagome kuitumia watake kutumia mahakama ya kawaida ya jamhuri ya muungano wa tanzania
 
Ufisadi wa MoU uko hapa ambapo DR Slaa nasikitika hakuweza kutuelezea kwa undani:

‘The government shall provide vacancies in its Teachers training colleges for training qualified persons as teachers earmarked for church owned schools'. Article xi


‘The government shall endeavour to include financial assistance for church run social services in its bilateral negotiations particularly with the Federal Government of Germany. Consideration shall be made during its bilateral negotiations with other donors'. Article xiii.


Sasa wakristo tujadiliane kwa hoja:


1)
Hivi ni haki kwa serikali isiyokuwa na dini kutowa nafasi za upendeleo kwenye elimu kama artcle xi inavyosema, tena isitoshe kw manufaa ya kanisa?

2)
Ni haki kwa serikali isiyokuwa na dini kuombea kanisa misaada katika Nyanja za kimataifa.

Sasa hapa ni kipi mnahitaji kuoneshwa ili muamini kwamba serikali inawazunguka waislam?
 
My take: "Tukumbuke kubomoa ni kazi nyepesi sana, sekunde lakini kujenga tena inachukua muda mrefu na ni kazi ngumu, na wakati mwingine hata ukifanikiwa huwezi kujenga kama ilivyokuwa."
 

ccm na kanisa havijawahi kutengana/kutenganishwa msichanganye mambo,mmesahau kanisa ndio lilitamka kwamba kikwete huyu ni chaguo la mungu na waislam tukasema astaghafirullah,wakristo wakakenua sana leo mnajidai kujitenganisha nae??!!kikwete ni chaguo la kanisa na kawekwa pale na kanisa,mkapa hakua chaguo la mungu wa wakatoliki aliwekwa pale na nyerere ndio mana alikua halisikilizi kanisa na ndio mana hata siku anamnadi kikwete uchaguzi wa 2010 siku ile kikwete alipoanguka kabla mkapa aliwasemea ovyo kina pengo kwamba kama wanatamani siasa wavue majoho waje kwenye siasa tupambanie huku,tuongee tu mambo mengine haya mambo achaneni nayo
 

Hivi kwa nini Serikali isiyokuwa ns Dini igawe Majengo kwa taasisi moja iyafanyw chuo kikuu cha Kiislam cha Morogoro
 
mkuu KIM KARDASH umesema vema sana na kuhusu mahakama ya kadhi nalo liliwekwa wazi tu kuwa lisiwa husu wakristo kwa vyovyote vile na siyo serikali ianze kutumia kodi za watanzania kwa kitu ambacho ni cha dini fulani na kama serikali itafanya makosa hayo mjue waislmu iko siku tutadai mahakama zenu ni za watanzania na siyo za waislam hivyo tunaweza kubadilisha matumizi yake mfano kubadilisha kuwa machinjio ya nguruwe..
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…