Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

Nataka kuona MoU ya Serikali na Jumuia ya Kiislamu (Kama ipo), na kama haipo kwanini? Na kama ipo, ina tofauti gani na hii iliyoanikwa hapa?
 
Nataka kuona MoU ya Serikali na Jumuia ya Kiislamu (Kama ipo), na kama haipo kwanini? Na kama ipo, ina tofauti gani na hii iliyoanikwa hapa?
Unataka serikali na Jumuia za kiislam zitiliane MoU kwa kutuletea Tende, Halua na majambia? Serikali inasaini MoU kwa ishu za Maendelea kama unataka tende subiri mwezi wetu ufike kwanza sio mbali kuanzia leo
 
Inawezekana dini au madhehebu mengine hawana cha kunegotiate sasa walazimishwe tu kunegotiate? Chukulia mfano serikali imeingia mkataba na kampuni fulani kuhusu madini ina maana makampuni yote yaingie mkataba na serikali ili kubalance?
naona unatetea uozo
 
cover.jpg
2-1.jpg
memo3.jpg
4.jpg
tano.jpg
sita.jpg
saba.jpg













sitaki kuamini hili lakini uvumi huu umeeneea sana kiasi cha kwamba umenifanya niwe na shauku kutaka kujua yaliyojiri kwenye kusign hiyo memorandum maana naona kwa taarifa nilizokuwa nazo malalamishi ni kuwa serikali imeipa cct na tec nguvu kubwa ajabu na matokeo yake leo watu watu wanaanza kulalama kwa nini serikali haiipi nguvu hizo ngo zingine kama walivopewa na serikali. Na under this memorandum seriali inatoa nafasi za kazi kwa church candidates kwenye chuo chake cha teachers training college

mfano kuna kipengele kinasema hivi:

Hakuna ubaya hata kidogo kwa serikali kusign hii memorandum lakini nataka kujiuliza je ni sawa serikali kufanya agreements kama hizi na taasisi za kidnini? Na je imefanya gareement kama hii na taasisi za kisslam au wahindu au ni kanisa tu ndio walifanya nao? Je hamuoni hapo mambo ya bilateral negotiations wakaachiwa wataalam wa mambo hayo?
weka vizuri basi documment hizo zisomeke maana tumechoka kugeuza laptop juu chini mikono inaumaa..
 
Nimesoma huo mkataba hapo juu sijaona shida yoyote
.Pia nimesomea sheria ya mikataba wakati nachukua LL.B yangu sijaona shida yoyote KWEYE HUU MKATABA TAJWA HAPO JUU.
Kanisa linabeba mzigo mkubwa sana wa serikali.Kwa mfano nilipokuwa nasomaTumaini Iriga ilikuwa ina miundo mbinu mizuri sana,sema baadae serikali ikailazimisha kuleta wanafunzi wengi kuliko miundo mbinu kwa kutumia chambo ya mikopo.
TUWE WAKWELI,Waslamu mnanini mna mahospitali ya rufaa,vyou vikuu,mashule yenye hadhii,mahoteli makubwa,miradi ya maji,umeme,utalii?LABDA AGHA KHAN,MWISILAMU WA DHEHEBU LA ISMAILIA NDIO KIDUME ANAYO MIRADI YA MAANA.NYIE HAMNA KITU.chuo cha morogoro chenyewe mmepewa!
 
Tatizo siyo mou kati ya serikali na kanisa, tatizo ni nini kilichomo ndani ya hiyo mou!, je kilchomo kinavunja katiba au la?, mimi binafsi naona pamoja na vipengele vingi vizuri katika hiyo mou, lakini kuna kipengele kinavunja katiba ya nchi wazi wazi, kipengele cha serikali kulisaidia kanisa katika kutafuta misaada pindi inapofanya majadiliano na nchi rafiki hususan serikali ya ujerumani.. Serikali haipaswi kujihusisha na shughuli za kidini full stop!!!

Wewe ndo mbwiga kabisa mimi sijaona mhali popote MOU inapotaja shughuli za kidini bali inataja huduma za kijamii hasa elimu na afya. Mwenzetu hizo huduma za kidini umezipata wapi? Kweli walimu wako walikuwa na kazi
 
Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam enzi za ukoloni wa Ujerumani, Askofu Cassian Spiss aliwaambia Wajerumani, msiwape elimu Waislamu. Na ikawa amri. Tazama Tanganyika Notes and Records No. 62/63, 1964. Kwa historia hiyo hiyo kujirudia kuwa kauli ya Kardinali au Askofu kwa serikali ni amri takatifu, hatushangai. Wakati wa utawala wake, Rais, Alhaj Ali Hassan Mwinyi hakupuuza historia hiyo. Aliiendeleza; alimleta Pope, akaamrisha nguvu zote za dola ziwaangukie wale wanaowabughudhi wanaofuga nguruwe na kuweka bucha za nyama hiyo hadi kwenye vibaraza vya Misikiti.
Pia akaleta 'Memorundum of Understanding' ambapo sasa, serikali inawajibu wa kuzipa mabilioni ya fedha hospitali za Kanisa, kuyatafutia makanisa misaada na kuwapa upendeleo katika kusomesha wataalamu wao.
Lakini wakati akifanya yote hayo, kiongozi huyo wa awamu ya pili hakupuuza shinikizo la Maaskofu kwamba hakuna 'rukhsa' Tanzania kujiunga na OIC! Si hivyo tu, viongozi hao pamoja na kuujua ukweli huo wa "kihistoria" unaowanyima Waislamu haki ya kujiunga na OIC, kuvunja jumuiya zao na kufisadi mali zao za Wakfu, baadae hugeuka na kuwalaumu Waislamu eti hawana dira wala mipango ya kuendeleza jamii yao. Wakati mwingine kuwaambia Waislamu kuwa "wenzenu" wanaletewa misaada na "ndugu zao toka nje, nyie mbona hawaji kukujengeeni mahospitali makubwa". Mtadhani hawajui kuwa OIC ndio iliyotaka kuleta mahospitali hayo!

Soma zaidi:
An-nuur Na. 237



Tafadhari.........SOURCE AN-NUUR...??? Hii ina tofauti gani na kuwa FF ndo source...??
 
Nimesoma huo mkataba hapo juu sijaona shida yoyote
.Pia nimesomea sheria ya mikataba wakati nachukua LL.B yangu sijaona shida yoyote KWEYE HUU MKATABA TAJWA HAPO JUU.
Kanisa linabeba mzigo mkubwa sana wa serikali.Kwa mfano nilipokuwa nasomaTumaini Iriga ilikuwa ina miundo mbinu mizuri sana,sema baadae serikali ikailazimisha kuleta wanafunzi wengi kuliko miundo mbinu kwa kutumia chambo ya mikopo.
TUWE WAKWELI,Waslamu mnanini mna mahospitali ya rufaa,vyou vikuu,mashule yenye hadhii,mahoteli makubwa,miradi ya maji,umeme,utalii?LABDA AGHA KHAN,MWISILAMU WA DHEHEBU LA ISMAILIA NDIO KIDUME ANAYO MIRADI YA MAANA.NYIE HAMNA KITU.chuo cha morogoro chenyewe mmepewa!

Huna elimu ya LLB pengine umeforge vyeti au unaumwa ugonjwa wa udini

Soma ibara 19 b ya katiba ya jamhuri inayosema serikali haina dini..

Serikali kusaidia shughuli za kanisa ni kusaidia kueneza ukristo kwa hela umma uwizi sawa tu na epa
 
Serikali kusaidia shughuli za kanisa ni kusaidia kueneza ukristo kwa hela umma uwizi sawa tu na epa


...na kanisa kusaidia serikali?

Ooh! Na serikali kugawa majengo yake kwa dini flani?

Serikali kutumia mali za wakristo kupitia utaifishaji kuwasomesha dini nyingine!? (kuna kiongozi mmoja wa juu zaidi alisema bila kanisa angekuwa anauza karanga chalinze)

Ah! Kumbe ni wivu baada ya kukosa!
 
...na kanisa kusaidia serikali?

Ooh! Na serikali kugawa majengo yake kwa dini flani?

Serikali kutumia mali za wakristo kupitia utaifishaji kuwasomesha dini nyingine!? (kuna kiongozi mmoja wa juu zaidi alisema bila kanisa angekuwa anauza karanga chalinze)

Ah! Kumbe ni wivu baada ya kukosa!

Acha kutetea ufisadi wa kanisa wewe soma ibara 19 b ya katiba ya jamhuri

Kanisa linapewa billions kila mwaka bila kufanyiwa auditing ..kodi za wananchi (waislam na wakristo) zinatumika kulipa priests ..

Kutetea hela za umma kutumika kuendeleza kanisa siyo wivu ni uzalendo
 
Faiza bwana!! Mwalimu alifariki Oktoba 14 1999 hadi Oktoba 13 2000 ni mwaka mmoja kamili. Unadhani msikiti ulianza kujengwa baada ya mwalimu kufa na mwaka mmoja baadaye ukakamilika. Unafikiri leo hii Kikwete akienda marekani akaulizwa apewe zawadi atachagua ya kuwajengea waumini wa Kikiristo kijijini kwao Msoga Kanisa? Pardon Me!!

Msikiti wa Butiama ni kielelezo cha uungwana wa Mwalimu na ukumbuke kwamba Gaddaffi alikuwa ni 'adui" wa Mwalimu lakini mwisho wa siku Mwalimu anawaombea wananchi wake wa Butiama Msikiti. Hivi inaingia akilini kweli mtu aombe msikiti halafu agome kujenga msikiti!!?

Kama ni kweli gaddaf alikuwa ni adui wa mwalimu na bado mwalimu akamwomba gaddaf awajengee waislamu wa butiama msikiti bac hapo picha unayonipa mimi ni kwamba mwalimu alikuwa kubwa la manafiki!!! alikuwa na sababu gani ya kumuomba adui yake wakati alikuwa na uwezo wa kumuomba yeyote akasikilizwa?! mwalimu alitaka kuonesha nini hapo?! usiniambie habari za kwamba mwalimu c mtu wa kinyongo kv uombaji wa mwalimu umeuweka katikati ya uadui wake na gaddaf. Kama hivyo ndivyo; basi one of the two is a perfect answer:
1. wewe ni mzushi wa kutupwa, or
2. mwalimu alikuwa ni mnafiki wa kutupwa.
 
.

WC,
nafikiri sana unaanza kuchanganya mambo. Naomba ujifunze nini wajibu wa Serikali kwa wananchi wake. Jiulize kwanini miaka 50 tokea uhuru wenu mpaka leo baadhi ya sehemu zimeendelea sana kiuchumi na nyingine bado kabisa. Lakini suala la msingi serikali ilikuwa wapi mpaka sehemu moja inandelea sana kuliko nyingine? kwanini isitoe kipaumbele na kuondoa hiyo gap ya maendeleo kwa jamii au wananchi wake?

Jiulize kwanini makanisa yanaanzissha mashule na mahospital? je kwa fedha zao au wanafadhiliwa? Je umepitia bajeti enu (Tanganyika) ya mwaka 2009/2010 na ile ya 2010/2011 kuona misamaha ya kodi hususan kwa hizi taasisi za kidini? vile vile angalia na Mou ya kanisa na serikali ya tanganyika? Je kuna uwiano hapo? Je serikali inalitazamaje suala hilo hicho ndio mjiulize.

Cha msingi ni serikali enu kuwa sikivu kwaa raia wake hususan wale wanaolalama kuonewa na kudhulumiwa haki yao tena wanaweka malalamiko hayo kimaandishi na kuipa serikali. Kumbukeni kuwa hata mbuyu ulianza kama mchicha.

Hakuna amani wala upende penye dhulma na pasipo na haki. Na sasa dalili zote zipo hewani . sasa sijui mnasubiri kifo.
Barubaru,
Wewe mwenzetu una serikali nyingine zaidi ya hii inayoongozwa na Dr JMK? Ufadhili wa makanisa kutoka nje kwa sasa umepungua sana. Unaona wanavyochangishana kwenye miradi hii. Amkeni. Dhuluma kama ilikuwepo, haipo sasa. Mama Salma kajenga shule nzuri sana ya wasichana kule Mkuranga kwa kutumia wafadhili haohao wa nje kupitia WAMA yake. Hayo ya MoU ya Wakristo na serikali yanamshinda Dr JMK na Dr MG Bilal kwa Waislamu kweli? Chagueni vipaumbele vyenu kwa umakini mkubwa. Ninyi mnang'ang'ana na KADHI. Wenzenu wanajenga hospitali kubwa na Vyuo Vikuu! Dawa sio kumchukia aliyenacho au kukitaka hicho alichonacho. Dawa ni kutafuta cha kwako kwa kutumia fursa hizi zilizopo sasa.
 
Barubaru,
Wewe mwenzetu una serikali nyingine zaidi ya hii inayoongozwa na Dr JMK? Ufadhili wa makanisa kutoka nje kwa sasa umepungua sana. Unaona wanavyochangishana kwenye miradi hii. Amkeni. Dhuluma kama ilikuwepo, haipo sasa. Mama Salma kajenga shule nzuri sana ya wasichana kule Mkuranga kwa kutumia wafadhili haohao wa nje kupitia WAMA yake. Hayo ya MoU ya Wakristo na serikali yanamshinda Dr JMK na Dr MG Bilal kwa Waislamu kweli? Chagueni vipaumbele vyenu kwa umakini mkubwa. Ninyi mnang'ang'ana na KADHI. Wenzenu wanajenga hospitali kubwa na Vyuo Vikuu! Dawa sio kumchukia aliyenacho au kukitaka hicho alichonacho. Dawa ni kutafuta cha kwako kwa kutumia fursa hizi zilizopo sasa.

Ukitaka kujua ufadhili umepungua au umezidi ninakupa sehemu ambayo ipo wazi kabisaaaa.

Wewe pitia bajeti za Tz hususan ya 2009/2010 na ile ya 2010/2011 na uangalie misamaha ya kodi hususan kwa taasisi za kidini. Hapo utaona ukweli wa mambo. Jitahidi sana kuwa na sources na takwimu kabla kusema kitu.

Lakini pia kama utajifunza wajibu wa Serikali yoyote ya halali kwa wananchi wake itakuwa na manufaa zaidi. Hiyo MOU ni kielellezo thabiti kwako kwani siku zote kulea mimba si kazi bali kazi na kulea mwana. Kwanini pesa zinazotolewa kutokana na MOU zisielekezwe kwenye shule zenu za kata na zahanati za serikali? Je kunani?

Lakini jiulize kama waliweza kujenga kwnini washindwe kuendeleza na kuchote pesa za Serikali ziendeleze miradi yao?

Lakini mwisho nilikuwa Mtz lakini sasa sipo tena nimerudi kwetu Oman na kuchukua uraia wangu wa asili. Sina uraia pacha.
 
Barubaru,
Wewe mwenzetu una serikali nyingine zaidi ya hii inayoongozwa na Dr JMK? Ufadhili wa makanisa kutoka nje kwa sasa umepungua sana. Unaona wanavyochangishana kwenye miradi hii. Amkeni. Dhuluma kama ilikuwepo, haipo sasa. Mama Salma kajenga shule nzuri sana ya wasichana kule Mkuranga kwa kutumia wafadhili haohao wa nje kupitia WAMA yake. Hayo ya MoU ya Wakristo na serikali yanamshinda Dr JMK na Dr MG Bilal kwa Waislamu kweli? Chagueni vipaumbele vyenu kwa umakini mkubwa. Ninyi mnang'ang'ana na KADHI. Wenzenu wanajenga hospitali kubwa na Vyuo Vikuu! Dawa sio kumchukia aliyenacho au kukitaka hicho alichonacho. Dawa ni kutafuta cha kwako kwa kutumia fursa hizi zilizopo sasa.

Wildcard,

Sidhani kama barubaru na wenzake watakuelwa katika hili. Nilisoma makala ya mwanahalisi inayosema Cheza kama pele, panga mipango kama kaanisa katoliki, kuna mdau aliileta hapa JF pia lakini baadhi ya watu wakaishia kumbeza. Ungeipata hiyo na hawa wenzetu wakiisoma wakiwa open minded watajifunza kitu lakini wasipokubali kwamba wanatakiwa kujitathmini wao wenyewe, watakuwa ni watu wa kulalama siku zote. Wasiwasi wangu mkubwa hali itakuwaje kama tutapata raisi asiye muislamu 2015 na kuendelea, maana sasahivi top cream yote yao lakini wananung'unika!
 
Barubaru,
Nashukuru umeweka wazi URAIA wako. Kumbe unatusaidia tugongane kwa UDINI halafu tusio na pa kwenda kama wewe tufanyeje! Misamaha unayoisema haina tatizo. Hospitali zinajengwa, vyuovikuu vinachipuka kama uyoga, shule zinajengwa sana tu. Tatizo ni mapesa anayokwapua mtu kama Rostam ambaye naye nadhani yuko mbioni kuukana UTANZANIA.

Labda ni suala dogo tu hapa. kama makanisa hayo na wafadhili wao wana uwezo mkubwa sana wa kujenga mashule, vyuo vikuu na hata mahospital je wanashindwaje kuviendesha na kuomba ufadhili tena wa serikali kwa njia ya MOU? Je hawajui kuwa kujenga sio kazi bali kazi ni kuviendesha?
Je waislam wananufaikaje na kodi zao kwa Serikali? Hiyo sio dhulma?
 
Je ni msaada gani au ufadhili gani wakati mnawabainia kwa kila angle. OIC hamtaki na wakipata pesa zozote mnasema za kigaidi au alqaida. sasa mnategemea nini?

Msibeze kitu pasi na kujua ukweli umesimama wapi?

Raisi wenu, makamu wa raisi wenu, IGP wenu, CJ wenu, waziri wa elimu wenu, mkurugenzi TISS wenu. Mnataka mpewe nini tena??

Sasa niambie ni nani anayewabania hiyo OIC. Niliwahi kuisikia siku za mwanzo mwanzo za utawala wa Kikwete lakini baadae ikawa kimyaaaaaaa hadi mlipoibuka na hoja ya mahakama ya kadhi!
 
Labda ni suala dogo tu hapa. kama makanisa hayo na wafadhili wao wana uwezo mkubwa sana wa kujenga mashule, vyuo vikuu na hata mahospital je wanashindwaje kuviendesha na kuomba ufadhili tena wa serikali kwa njia ya MOU? Je hawajui kuwa kujenga sio kazi bali kazi ni kuviendesha?Je waislam wananufaikaje na kodi zao kwa Serikali? Hiyo sio dhulma?

Umesema vizuri,

Je, waislamu wameweza kujenga shule ngapi, hospitali ngapi na vyuo vikuu vingapi?
 
Labda ni suala dogo tu hapa. kama makanisa hayo na wafadhili wao wana uwezo mkubwa sana wa kujenga mashule, vyuo vikuu na hata mahospital je wanashindwaje kuviendesha na kuomba ufadhili tena wa serikali kwa njia ya MOU? Je hawajui kuwa kujenga sio kazi bali kazi ni kuviendesha?
Je waislam wananufaikaje na kodi zao kwa Serikali? Hiyo sio dhulma?
Vyuo Vikuu vyote na Hospitali zote zinahudumia WATANZANIA WOTE bila ubaguzi. Ufadhili ni jambo la kawaida kwa asiye mwizi au fisadi. Hata familia tunaziendesha kwa ufadhili wakati mwingine.
 
Mfumo ukisukwa barabara( sio barubaru!) hao akina JMK, IGP, ....., wangepenyaje wakafika hapo walipo. Kama ambavyo Mkurya hawezi kumlaumu Mchagga kwa kukosa ELIMU, MWISLAMU naye ni makosa kumlaumu MKRISTO kwa kukosa ELIMU. Haya yana historia ya peke yake.

Nimesema mara kadhaa hapo kabla kwamba sisi wakurya tulikuwa nyuma sana kielimu, sababu mojawapo ilikuwa ni mila na tamaduni zetu.

Lakini tulipogundua kwamba kwa mazingira ya sasa, hatuna budi kubadilika na kutilia mkazo elimu, hatukutafuta mchawi.

Tulianza kupambana kwa kujenga mashule na kuhamasisha vijana wetu wasome, na sasahivi kila mzazi anataka mtoto wake asome, tena wengi sasahivi ukiwauliza watakwambia wangependa watoto wao wasome hadi vyuo vikuu. Tembelea vyuo vikuu, shule za sekondari (Kidato cha tano na sita) uone idadi ya watoto wa kikurya wanavyochangamkia shule. Shule za kata tulijenga kabla hata lowasa na JK hawajaanza kuhamasisha.

Bila waislamu wenyewe kuchukua hatua, wataendelea kulalamika hivi hivi miaka nenda rudi.
 
Back
Top Bottom