Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

Mbona mnashindwa kujibu Pengo ana nafasi gani katika (taifa) la vatican hali ya kuwa yeye si raia wa"nchi" hiyo?
Zinazowagusa mnarukaruka tu! Tuendelee na mada ila najua point ya Mukandara has been driven home and got u thinking!

Hana nafasi katika taifa la Vatican - yeye ni Kardinali wa Kanisa Katoliki lenye makao yake makuu Vatikani.
 
Unataka serikali na Jumuia za kiislam zitiliane MoU kwa kutuletea Tende, Halua na majambia? Serikali inasaini MoU kwa ishu za Maendelea kama unataka tende subiri mwezi wetu ufike kwanza sio mbali kuanzia leo

Una mboyoyo sana kwa ufinyu wa mawazo yako!kwa mtaji huu hamtawahi kujadili mambo kwa ufanisi na kuyapatia ufumbuzi.
Kama huna la kuchangia kuwa msomaji!
 
Kwanini hizo fedha zisijenga na kuendeleza Mahospitali na Mashule ya Serikali? Huko makanisani si ndio mnatuwekea misalaba na masanamu hata kama hatuyaamini? na huko mashule ya kanisani si ndio mnawafundisha watoto zetu kwanya za kanisani?

Wacheni hizo. Hatutaki. Fedha ziende hospitali za Serikali na Mashule ya Serikali. Kanisa lijiendeshe lenyewe, huu ni wizi wa wazi wazi hakuna zaidi.

Yani kama kuna mtu anaona mbali basi wewe unaona mbali hawa jamaa ni waizi ile mbaya hizo hela wakipewa hawakubali kukaguliwa sasa huo si wizi
 
Kwanini hizo fedha zisijenge na kuendeleza Mahospitali na Mashule ya Serikali? Huko makanisani si ndio mnatuwekea misalaba na masanamu hata kama hatuyaamini? na huko mashule ya kanisani si ndio mnawafundisha watoto zetu kwaya za kanisani?

Wacheni hizo. Hatutaki. Fedha ziende hospitali za Serikali na Mashule ya Serikali. Kanisa lijiendeshe lenyewe, huu ni wizi wa wazi wazi hakuna zaidi.

Kama serikali inaweza ikathibitisha, na kujiridhisha kuwa hakuna wananchi wasio wakristo wanaohitaji huduma za afya kutoka katika hivyo vituo, then ita-buy idea yako. Kama serikali ina uhakika kuwa mwananchi ana uhuru wa kuchagua huduma sawa, au bora zaidi kutoka hospitali za serikali kwa sasa, na mahali alipo then ita-buy idea yako.

Ila kama serikali inadhani kuna maelfu ya wasio wakristu, wanaoponywa na kuokolewa maisha ya katika hospitali za kikristu, na kuwa hawana same or better option ya hospitali za serikali kwa sasa na kwa mahali walipo, then itaendelea kusaidiana na kanisa kuokoa maisha ya watu (bila kujali dini zao), na huku ikiendelea na juhudi ya kujenga na kuimarisha vituo vyake vya afya ili viweze kuwafikia wananchi wote kwa wakati na mahali walipo...

FF unaongea kuwa 'hamtaki'... Ni bora ungesema 'hutaki', maana wapo maelfu ya wasio wakristu wenzio kwa dakika hii unaposoma comment hii wapo kwa daktari au muuguzi katika hospitali hizi za 'kikristo' wakiugulia maumivu makali sana, na wengine wakikaribia kukata roho na tumaini lao la pekee kwa sasa na hapo walipo ni hosp au vituo hivyo vya kikristo... Sidhani kama ungewapa nafasi ya kuandika kama ulivyoandika wewe, tungesoma neno 'hatutaki' kutoka kwenye maandiko yao, I swear...
 
Silencer,

Niliiona comment yako asubuhi ila naona umeiondoa. Ulikuwa unauliza kwanini waislamu hawaendi mahakamani. Kama umesoma alichokuwa anaandika Game Theory hii memorandum ingelikuwa illegal kama wasingelibadilisha vipengele vya katiba na baadhi ya vipengele vya sheria ya elimu. Amendements hizo zilifanywa kulegalise MoU (refer to Mohamed Said Books). Kutokana na hilo basi ndugu yangu moderator suala la kwenda mahakamani ni kujisumbua kwasababu kwa mujibu wa kisheria walichokifanya maaskofu ni legal in the eyes of the justice system but illegal in the eyes of the society.

Ukitaka waislamu waende mahakamani kwanza lazima vipengele vile vya katiba vifutwe na sheria zilizobadilishwa kuruhusu biashara hii ya kugaiana hela za walipa kodi ziondolewe zirudishwe either zilikuwapo zamani au zitungwe upya kuondoa masuala haya ya kupeana hela za wavuja jasho nchini.Waislamu watapiga kelele hadi hili suala liondolewe na kufutwa kabisa au kuwepo na uwiano sawa. Binafsi yangu ningelipendelea hili jambo lifutwe hela za walipa kodi ziende kwa shughuli za serikali, shule za serikali na hospitali za serikali. Serikali inatoa Bilioni 91 wakati wagonjwa Muhimbili wanalala chini!!!!! Wagonjwa hospitali ya temeke au magomeni wanalala kitanda watu wanne??? Shule za serikali wanafunzi wanafanya mitihani katika uwanja wa wazi wa mpira.

This morally wrong and socially illegal.
 
Soma UCHAMBUZI wa Saed Kubenea MwanaHALISI Jumatano,Novemba 2-8,2011 Ukurasa wa Tatu(3).Halafu Urudi hapa,Sijui kama umesoma Elimu dunia Lakini Bibie Topical,au Madrasa ilikumaliza kabisa???


Kwanza mimi si bibie niombe radhi

Pili wewe huna hoja..mwanahalisi amechambua vizuri sana kwamba

Kanisa =RA =EL wote ni majasiri wa kufisadi mali ya umma

Kanisa lifanyanya hivyo through MoU fake (e.g. doawans) hela za umma zinaenda kanisani unaudited..huo ni uzuzu

RA anafanya hivyo through Biashara

siajona cha maana zaidi ya kutetea ufisadi period.
 
Kama serikali inaweza ikathibitisha, na kujiridhisha kuwa hakuna wananchi wasio wakristo wanaohitaji huduma za afya kutoka katika hivyo vituo, then ita-buy idea yako. Kama serikali ina uhakika kuwa mwananchi ana uhuru wa kuchagua huduma sawa, au bora zaidi kutoka hospitali za serikali kwa sasa, na mahali alipo then ita-buy idea yako.

Ila kama serikali inadhani kuna maelfu ya wasio wakristu, wanaoponywa na kuokolewa maisha ya katika hospitali za kikristu, na kuwa hawana same or better option ya hospitali za serikali kwa sasa na kwa mahali walipo, then itaendelea kusaidiana na kanisa kuokoa maisha ya watu (bila kujali dini zao), na huku ikiendelea na juhudi ya kujenga na kuimarisha vituo vyake vya afya ili viweze kuwafikia wananchi wote kwa wakati na mahali walipo...

FF unaongea kuwa 'hamtaki'... Ni bora ungesema 'hutaki', maana wapo maelfu ya wasio wakristu wenzio kwa dakika hii unaposoma comment hii wapo kwa daktari au muuguzi katika hospitali hizi za 'kikristo' wakiugulia maumivu makali sana, na wengine wakikaribia kukata roho na tumaini lao la pekee kwa sasa na hapo walipo ni hosp au vituo hivyo vya kikristo... Sidhani kama ungewapa nafasi ya kuandika kama ulivyoandika wewe, tungesoma neno 'hatutaki' kutoka kwenye maandiko yao, I swear...

Swala siyo nani anapata huduma hiyo? kwani hata private schools (ambazo hazipewe ruzuku kila mtu anapata)

Swala ni kwanini kanisa lipendelewe pekee yake na kupewa ruzuku ya umma..

Wakati hata bei zao hospitalini na shuleni ni sawa na private

Mbona waislamu wanaendesha shule na hospitali zao bila ruzuku..
 
Kinachozungumziwa kwenye MOU ni huduma zinazotolewa na CCT na TEC kwenye elimu na afya. TEC ina hospitali nyingi na mashule mengi yanayowahudumia watanzania hali kadhalika CCT. hivi vitu ni msaada mkubwa kwa serikali na vinahitaji kulindwa ili vidumu. Hilo ndilo lililo kwenye MOU. Mou haizungumzii ukristu. Wengine kama wanavyo vya aina hiyo hawajakatazwa kujadiliana na serikali namna ya kuvidumisha. tufikiri kwa kutumia vichwa tuache kuwapotosha wananchi.

Tunajuwa fika mashule hayo na mahospitali hayo wamejenga kwa njia za misaada toka ughaibuni. Kwanini Serikali wasiziachie wenyewe hizo taasisi ya dini kuziendesha iwe bure au hata kwa kutoza pesa hizo facilities zao? na wakti huo huo Serikali hiyo hiyo ikatumia fedha hizo za MOU kujenga hospitali au mashule yake?

Je Serikali inafikiri kweli hapo? Kwanini wategemee cha Kanisa na wasijinasibu kwa kitu chao wenyewe. pasi na shaka kuna namna hapo?
 
Hana nafasi katika taifa la Vatican - yeye ni Kardinali wa Kanisa Katoliki lenye makao yake makuu Vatikani.

Tuwe wa kweli hapa.

Kwanza ana weza kuchaguliwa kuwa Papa yaani kiongozi mkuu wa vatican.
Anaweza kuchaguliwa kuwa balozi wa kuweza kuiwakilisha Vatican kwenye nchi yoyote waliyona mahusiano nayo kama Tanzania.
Ni mmoja kati ya wapiga kura wa kumchagua Papa.
 
Mkandara nimeleta mambo haya kwa ajili ya kuleta mwanga zaidi maana watu wengi wanaangalia kwa mwanga wa 'sisi vs them' hivyo hawataki hata kuangalia ule upande wa pili hoja. Kwa kiasi kikubwa inachangiwa na serikali yenyewe kuficha mambo ya msingi. Fikiria kwa mfano ikija kuwekwa hadharani kuwa hata baadhi ya hospitali za Waislamu zinapokea fedha kutoka serikalini - kwa ajili ya madara, ajira n.k - je watu wanaopinga hospilitali za kanisa kupatiwa watasimama na kusema na misikiti isipewe?

Lakini jambo la pili ambalo nalo ni kubwa ambalo unakutana nalo hata kwenye nchi kama Marekani ambazo zinazo hicho cha "separation of church and state" ni kuwa hata taasisi za makanisa na za kidini zinapata fedha kutoka serikalini (federal au state) kwa masharti kwa mfano haziwezi kuwa na ubaguzi katika huduma au ajira either under civil rights act ya 1964 au Title IX. Hili ndilo ambalo limekuwa likitokea nchini hata kabla ya wakati wa ukoloni na of course hospitali za wamisheni kwenye utawala wa kikoloni ni wazi zilikuwa na advantage zaidi kuliko hospitlai na shule nyingine.

Lakini kubwa ni hili kwa mfano - hospitali za Ndanda, Peramiho na cliniki zao mbalimbali zinaweza vipi kulipa watumishi waende kufanya kazi mazingira ambayo tayari watu wanayakimbia? Lakini kama mtumishi wa Ndanda Hospital au Peramiho Hospital ameajiriwa na serikali kuu na mshahara na posho zake zinatoka serikali kuu - na haijalishi dini yake mtu huyo - je endapo serikali ikijitoa kwenye mishahara yake na kanisa likashindwa kumlipa ni nani anayelipa hilo kama siyo wagonjwa wa maeneo hayo?

Nadhani tatizo ambalo tunalo na ambalo linaweza kuondolewa ni kukaa pamoja na taasisi mbalimbali ili kutengeneza sera ambayo itasimamia mahusiano ya serikali na taasisi za kidni na zile zisizo za kidini. Kuna watu wanafikiria kuwa serikali inaweza kuendesha mashule na hospitali zote ukweli haiwezekani. Kwa kadiri nijuavyo sidhani kama kuna nchi yeyote ambayo serikali inatoa huduma zote mbili bila kusaidiwa au kusaidia taasisi binafsi. Karibu kiila nchi ina mfumo wake wa ushirikiano huu.

Maswali ambayo sisi kama Watanzania jwa pamoja tunahitaji kujiuliza ni:

a. Taasisi za kidini zinaweza vipi kupewa misaada au kuwekewa mazingira ya kufanya kazi zake vizuri katika nchi ambayo bado ina matatizo ya umaskini, maradhi na ujinga? Kwa mfano - tukisema taasisi zote za kidini ziwe kama za kibiashara zilipe kodi katika huduma yake na bei ya vifaa na madawa ni zile zile zinazouzwa madukani je ni taasisi gani zitaweza kusimama?

b. Je sasa hivi mfumo unaotumika una mapungufu gani na ni jinsi gani mapungufu hayo yanaweza kuboreshwa. Kwa sababu kwamba makanisa na taasisi za Kikristu ni nyingi zaidi halina shaka lakini suluhisho ni nini? Wengine wanasema fedha zote ambazo zinatolewa kusaidia taasisi hizi ziondolewe mara moja. Well hiyo ni rahisi lakini matokeo yake ni nini mara moja? Fikiria kwa mfano, serikali inasema kuanzia kesho hakuna hospitali ya kidini ambayo itapewa fedha kutoka serikalini kwa shughuli yoyote na fedha zote zitapelekwa mahospitali ya serikali je hiyo kesho kutakuwa nini kwenye mahospitali ya Bugando, KCMC, Peramiho, Ndanda n.k Nini kitakuwa kwenye zile jamii ambazo hospitali hizo zipo? Nini kitatokea kwa wale wagonjwa Waislamu na Wakristu na Wapagani ambao wanazitegemea hospitali hizo? Wale wanaosema serikali ikatishe ni vizuri watoe pendekezo zuri la jinsi gani serikali iondoe hiyo ruzuku bila kuathiri huduma kwenye mahospitali hayo. Kusema kwamba "makanisa yatatafuta misaada kwingine" is not an option.

c. Upande mwingine ambao watu hawaangalii ni kuwa je hizi hospitali zinahudumia walipa kodi wote kwenye maeneo hayo? Je kuna Waislamu wanaotibiwa Bugando, KCMC, Ndanda au Peramiho? au kwenye kliniki zaidi ya 450 za makanisa? Je hawa Waislamu wanalipa kodi? Kama wanalipa kodi na fedha za kodi zao zikirudishwa kwenye mahospitali ambayo wao wanapata huduma tunaweza kusema kuwa kodi yao imetumika vibaya? Je WAislamu ambao wameshatibiwa huko na watoto wamezaliwa huko kwenye mahospitali ya misheni na Waislamu ambao wameajiriwa katika mahospitali hayo wanaweza kusema kweli kuwa serikali isitoe fedha kwenye taasisi hizo kwa sababu ni taasisi za makanisa? Binafsi ningependa kuona watu wa maeneo ya hospitali hizo waulizwe hata kwa kupiga kura kama wanataka kodi zao ziingizwe kwenye hospitali hizo tuone kama watataka zisitishwe.

MMM
Mkuu wangu nimekuelewa sana na nipo na wewe kabisa...
Tatizo la ruzuku hizi sii swala la Kanisa linahudumia watu gani bali lipo ktk makosa ya kikatiba na morally wrong kiasi kwamba serikali ndio inakuwa ikiendesha Ubaguzi kama ule wa Apartheid. Ebu fikiria tu kwa njia nyingineyo, serikali iwe inawapa wahindi ruzuku ili waendeshe biashara za maduka yao na sii watu weusi. Ukiuliza unaambiwa jiulize wahindi wanatoa huduma kwa wananchi wangapi na wa aina gani? wahindi wanajua sehemu za kufuata mali, wazuri ktk biashara, wanatoa ajira na kadhalika...Yaani sababu ambazo hazihusiani kujibu swali kwa nini weusi HAWAKUPEWA nafasi hiyo kikatiba toka mwanzo...majibu rahisi na ya kihuni hutolewa - Nanyi ombeni mtapewa! wakati ahadi hii haipo kikatiba wala hakuna memorandum.

Hii tayari inawafanya watu weusi second class citizen na hakuna mantiki yoyote kufikiria huduma zinazotolewa na wahindi hata iwe kwa ubora gani... Ndivyo ilivyokuwa South Afrika makaburu wakizungumza kuhusu uwezo wao wa kutoa huduma safi kwa wananchi wote ili hali wazungu ndio waliofanikiwa zaidi ya watu weusi..Na mara zote walijenga hofu ya kwamba wakiondoka wao watu weusi wenye shida nani atawahudumia..

Kwa hiyo hakuna sababu ya kutazama kanisa linawasaidia vipi wananchi wakati kazi hiyo ilitakiwa kuwa ya serikali toka mwanzo na makosa yamefanyika kupendelea upande mmoja na kuweka mkataba. Hii inabadilisha sura nzima ya sera za kitaifa kwa kujumuisha kanisa kuwa sehemu ya serikali na utoaji huduma. Kwa hiyo ugonvi uliopo wa 'US against THEM' umetokana na mkataba huu ambao kwa waislaam wanaona wamebaguliwa kikatiba. Na hakika katiba inapoandikwa huwa ni kwa taasisi zote za aina hiyo zinafungwa na sera kama hii ya MoU na sii kuchagua kundi moja kati ya makundi mengi.. Kwa kutofanya hivyo serikali imefanya ubaguzi na kosa kubwa ambalo Mdondoaji kila siku husema waislaam ni second class citizen..

Mfano wa Marekani hauwezi kujenga hoja Tanzania kwa sababu America was found under Christian values na ndio maana tunasema ukienda Amerika itakubidi uishi kama Waamerika. Hivyo taasisi za dini zilikuwepo toka kujengwa kwa taifa lao, lakini Je, iliwasaidia vipi wenyeji na wakazi wa nchi hiyo Wahindi wekundu ambao kimsingi elimu ilikuwa ikitolewa kwa raia wote! Kwa hiyo tatizo la elimu ya makanisa Marekani ilikuwa kinyume cha wahindi wekundu kwa sababu elimu ilikwenda sambamba na mfumo wa kiutawala...

Sisi Tanzania ambao watu na mazingira yetu ni tofauti kabisa na Marekani hatutakiwi kuiga lolote kutoka ktk mfumo wa Marekani ama nchi yeyote ile isipokuwa tunatazama mfumo bora kwa watu na mazingira yetu kama Azimio la Arusha lilivyoasisiwa na mwalimu Nyerere kwamba shule zote za dini zinazotoa elimu dunia zilichukuliwa na kuwa mikononi mwa serikali isipokuwa zile zinazotoa elimu ya dini..Na Kama kuna taasisi yoyote inafungua shule ya private ifungue lakini hawatapewa ruzuku wala nafuu yoyote ya kodi kwa sababu hiyo ni biashara...Kwa hiyo kunakuwa na ushindani baina ya shule za Private na zile za serikali wakikaa mtihani mmoja darasa la saba kuingia form one, form IV kuingia form V, VI kwenda Chuo kikuu na kadhalika merits zilihitajika kuvuka sehemu moja kwenda nyingine bila kujali uko shule gani..

Kwa hiyo hayo maswala Ndanda, Pehaminho, Bugando, KCMC kote huko kumefanyika makosa na kibaya zaidi ni kwamba vyombo hivi serikali haikushidnwa kuviendesha laa hasha. Ni uhuni umefanyika na toka vyombo hivi viondolewe serikalini elimu nchini imeshuka vibaya sana...Yes, yawezekana elimu bora inapatikana ktk shule za makanisa lakini sii hivi ndivyo ilivyokuwa toka wakakti wa mkoloni? Sii hivi ndivyo ilivyokuwa hata huko South Afrika kwa Makaburu yaani shule za wale Elites ndizo hutoa huduma bora zaidi lakini hakuna haki wala usawa na mwisho wa yote hujenga matabaka baina ya wananchi...

Kwa hiyo mkuu wangu, hali ya Wananchi kielemu ndio inatakiwa ku determine mafanikio ya mfumo huu ulotokana na mkataba wa MoU, na sio kutazama mkataba wenyewe unasaidia watu wangapi...it's morally wrong hakuna sababu ya kutafuta sababu nje ili kupamba makosa yalofanywa na Mwinyi.. Kosa ni kosa, athari za upendeleo wa kutoa ruzuku ndio uloleta mjadala mkubwa na pengine hata kusababisha chuki baina ya waislaam na Wakristu, haijalishi shule hizi zinawafaidisha wangapi.. Ghadaff kaondolewa kwa sababu ya demokrasia tu, watu hawakujali mambo yote alowafanyia isipokuwa ushenzi aloufanya ndio sababu ilomhukumu. Na siku zote mazuri ni sehemu ya wajibu wa binadamu ktk maisha, isipokuwa mabaya ndio mtu huipelekwa mahakamani na akafungwa hata kama ni kosa la kwanza na kafanya mazuri millioni.
 
GT,

..at first nilibabaika na nikaona serikali inajitumbukiza ktk masuala ya kidini.

..lakini baada ya kutulia na kutafakari nadhani hii MOU haina matatizo.

..hata mataifa makubwa kama MAREKANI yana ushirikiano kati ya SERIKALI na FAITH BASED organisations.

..sidhani kama hiyo MOU inaelekeza serikali ktk kusaidia Kanisa ktk shughuli zake za kiroho.

..kwa mazingira yetu Tanzania serikali inapaswa kushirikiana na mashirika ya kidini ktk urahisishaji wa utoaji wa huduma za kijamii kama elimu, afya, maji,mazingira etc.

..kama taasisi ya kidini imejenga hospitali na inatoa madawa na chakula sioni ubaya wa serikali kuwasaidia ktk kutoa waganga na wauguzi na kuwalipa mishahara. ushirikiano wa minajili hiyo nadhani ndiyo unaoelekezwa na MOU hiyo.

..pia tangu kusainiwa kwa MOU hiyo sijaona dalili zozote zile za serikali kuipendelea dini moja dhidi ya nyingine.

..tumeshuhudia serikali ikifadhili mkutano wa Bakwata, ikitoa majengo kwa chuo cha Kiislamu, na kusaidia kutatua ile sakata ya mahujaji kukwama kwenda hijja. pia tumeona serikali ikirudisha shule za kanisa zilizokuwa zimetaifishwa, tumeona viongozi wakuu wakishiriki fundraising za ujenzi wa shule za kanisa etc etc. vilevile kiongozi wa mabohora ametembelea nchini na kupokewa kwa heshima zinazostahili.

..badala ya kukaa pembeni na kulalamika labda madhehebu mengine nayo yachukue initiative na kusaini MOU na serikali kama ambavyo makanisa yamefanya. lakini with or without MOU sidhani kama serikali ina nia ya kubagua madhehebu yoyote ya dini.

Umeongea point mkuu. Me napenda kuwashauri wanajamvi wenzangu kuepuka mijadala ambayo mwisho wake ni ni maudhi na hasira. Sijaelewa vizuri intention ya huyu mtoa mada kama ni kutujuza ama kuchochea uhasama, coz nimefuatilia reply zake, seems ana msimamo wake fulani ambao anataka kuwatwisha wanajamvi. Katika pitapita zangu, nilikutana na kitabu kimoja chenye title ya "MFUMOKRISTU" kitabu hiki kinachochea uhasama na chuki dhidi ya wakristo na moja ya agenda kubwa ya kitabu ni hiyohiyo MoU alokuja nayo huyu jamaa. Am sure huyu jamaa yupo behind that book!
 
Nasikiliza radio maria na tumaini na wanahatarisha amani wanaongelea waislamu vibaya..na wanahatarisha amani

Mkuu Udini ni very subjective term inatagemea wewe unavyoelewa udini

Radio imani wanaongele upendeleo unaofanywa na serikali kwa wakristo hilo ni udini..

Hapana, huo ni kutafuta muafaka na mlango wa majadiliano..

Mkuu ungepunguza udini kidogo alafu utumie busara kuongea!
 
Umeongea point mkuu. Me napenda kuwashauri wanajamvi wenzangu kuepuka mijadala ambayo mwisho wake ni ni maudhi na hasira. Sijaelewa vizuri intention ya huyu mtoa mada kama ni kutujuza ama kuchochea uhasama, coz nimefuatilia reply zake, seems ana msimamo wake fulani ambao anataka kuwatwisha wanajamvi. Katika pitapita zangu, nilikutana na kitabu kimoja chenye title ya "MFUMOKRISTU" kitabu hiki kinachochea uhasama na chuki dhidi ya wakristo na moja ya agenda kubwa ya kitabu ni hiyohiyo MoU alokuja nayo huyu jamaa. Am sure huyu jamaa yupo behind that book!

Kitabu cha mfumo kristo kinasemaje unaweza kutuwekea jamvini utatusaidia sana...

Acha uoga na udini wako..sasa tunyamaze wakati hela za umma zinaenda kuendesha shughuli za kanisa

Mbona waislam wanaendesha shule zao bila ruzuku ya serikali..
 
Mkandara,

..lakini hakuna mahali katiba imeelekeza kwamba Waislamu hawawezi kuandikishana mou kama walivyofanya Wakristo.

..infact unachoweza kusema ni kwamba hii mou inaweza kuleta vurugu ambapo kila dhehebu la dini nchini linaweza kudai nalo liandikishwe mou ili kutoa huduma kwa jamii.

..swali ambalo wengi wanalikwepa ni kwanini Waislamu wameishia kulalamika tu toka 1992 bila na wao kuandaa mou na kusaini na serikali? Kuna wanaotoa kisingizio cha mou ya Sheikh Ponda, bila kubainisha kwamba Sheikh huyo amekuwa na mikwaruzano ya muda mrefu na serikali.

..vilevile kuna Waislamu wamepewa majengo na serikali kuanzisha Chuo Kikuu in Morogoro. Je hao wamepewa bila maandishi au "mou"? Vilevile kwanini kumuenzishwa chuo kikuu cha Waislamu, na si hospitali ya wilaya/mkoa/rufaa ya Waislamu? Je, ni suala la kukosa uwezo au utaalamu, au both?

..binafsi nadhani mjadala na malalamiko kuhusu "mou" na the so called "mfumo Kristo" unawanyima nafasi Waislamu kuji-saili wenyewe na kuona ni wapi wanakosea ktk kuyashughulikia matatizo yanayowakabili.

..Lets say leo hii serikali inatoa tamko kusitisha mou yake na taasisi za Kiislamu, je hiyo ndiyo suluhu ya matatizo yanayowakabili Waislamu nchi hii? Mind u, kuna kipindi shule zilikuwa zimetaifishwa, pass mark imeteremshwa[which is affirmative action of some sort] kwa ajili ya jamii za pembezoni, Waislamu included, but look at what we ended up with.

NB:

..halafu hili suala la "WE" vs "THEM" naona hata limehamia miongoni mwa Waislamu wenyewe. kwa mfano Muislamu mwenye elimu nzuri na madaraka serikalini naye anatumbukizwa ktk kundi la "THEM" kana kwamba anakwenda kinyume dhidi ya Waislamu wenzake.
 
Halafu ikisemwa hapa kuwa Tanzania kuna udini (hivyo watu watibu ugonjwa huu badala ya kujaribu kuuficha) mimacho na mipovu inawatokaaaa..... Phewwwww

Miafrika bana ndivyo tulivyo

Unamaanisha serikali isiyo na udini haitakiwa kusaini MoU na mashirika yoyote ya kidini??? Au unamaanisha contents za hiyo MoU ni za kidini na haziko kwa maslahi ya taifa??
 
Unamaanisha serikali isiyo na udini haitakiwa kusaini MoU na mashirika yoyote ya kidini??? Au unamaanisha contents za hiyo MoU ni za kidini na haziko kwa maslahi ya taifa??

Iko kwa maslahi ya kanisa na miradi zake

Na si taifa na wananchi wake..
 
kama serikali inaweza ikathibitisha, na kujiridhisha kuwa hakuna wananchi wasio wakristo wanaohitaji huduma za afya kutoka katika hivyo vituo, then ita-buy idea yako. Kama serikali ina uhakika kuwa mwananchi ana uhuru wa kuchagua huduma sawa, au bora zaidi kutoka hospitali za serikali kwa sasa, na mahali alipo then ita-buy idea yako.

Ila kama serikali inadhani kuna maelfu ya wasio wakristu, wanaoponywa na kuokolewa maisha ya katika hospitali za kikristu, na kuwa hawana same or better option ya hospitali za serikali kwa sasa na kwa mahali walipo, then itaendelea kusaidiana na kanisa kuokoa maisha ya watu (bila kujali dini zao), na huku ikiendelea na juhudi ya kujenga na kuimarisha vituo vyake vya afya ili viweze kuwafikia wananchi wote kwa wakati na mahali walipo...

Ff unaongea kuwa 'hamtaki'... Ni bora ungesema 'hutaki', maana wapo maelfu ya wasio wakristu wenzio kwa dakika hii unaposoma comment hii wapo kwa daktari au muuguzi katika hospitali hizi za 'kikristo' wakiugulia maumivu makali sana, na wengine wakikaribia kukata roho na tumaini lao la pekee kwa sasa na hapo walipo ni hosp au vituo hivyo vya kikristo... Sidhani kama ungewapa nafasi ya kuandika kama ulivyoandika wewe, tungesoma neno 'hatutaki' kutoka kwenye maandiko yao, i swear...

point!
 
Tuwe wa kweli hapa.

Kwanza ana weza kuchaguliwa kuwa Papa yaani kiongozi mkuu wa vatican.
Anaweza kuchaguliwa kuwa balozi wa kuweza kuiwakilisha Vatican kwenye nchi yoyote waliyona mahusiano nayo kama Tanzania.
Ni mmoja kati ya wapiga kura wa kumchagua Papa.

Nadhani mwalimu hujalisoma swali na unachanganya - kama wengi wafanyavyo - Kanisa Katoliki na Vaticani nchi. Na kosa la pili "kuweza" siyo sawa na "kuwa"...
 
Silencer,

Hii memorandum ingelikuwa illegal kama wasingelibadilisha vipengele vya katiba na baadhi ya vipengele vya sheria ya elimu.
Ebu taja kipengele cha Katiba lkilichabailishwa kilikuwaje kabla ya mabadiliko na baada ya mabadiliko kikawaje? MEmorundum hii ilivyo kinachoweza kuifanya iwe tatizo ni kama kuna pesa zinatumika nivyo sivyo. ni kama ikionekana labda Hopitali zinpkena blioni 22 kumbe inawezekana zinapoke bilioni 3 au 40.

nakuomb tena QUOTE kipngele cha katiba kilichobadilishwa just kukidhi na kulegalise Mou Ya serikali na kanisa

Amendements hizo zilifanywa kulegalise MoU (refer to Mohamed Said Books). Kutokana na hilo basi ndugu yangu moderator suala la kwenda mahakamani ni kujisumbua kwasababu kwa mujibu wa kisheria walichokifanya maaskofu ni legal in the eyes of the justice system but illegal in the eyes of the society.

Mohamed Said haja quote hicho kifungu na kilichobadilishwa just kukidhi mahitaji ya Mou ya kanisa . What wengine wakisema kipengele kilipiitishwa kukidhi mahitaji ya huduma bora kwa wananchi . Sio ndio maana kuna sifa mwinyi anapata dhidi ya nyerere wakati wa winyi hatawatotot tulianza kukamata noti za elfu.

Mimi naomba kiwekeni hadharani hicho kipengele kilichobailishwa tupime kabla kilikuwaje na baadae kikawaje.


Na walioandaa ,walioshauri Mou wala sio Maasofu na wala sio entity moja ya Kanisa. Ni watu proffesional walijairwa kushghulikia mambo ya nje ya dini . ni watu walipewa kuangalia mahitaji ya kimwili ( elimu na afya) . Ndio Maana nimekuuliza katik waislam Ni mtu gani anahusika na ambo ya Elimu. Ni nani anahusika na ambo afya. nahitaji kuwa na coridanted structure lakini yenye mipaka kuwa Sheikh atfany haya na atapokea ushauri wa abo ya Elimu kutoka kwa irector wa elimu wa taaisisi fulani.

Na sio kweli kwamba Mou ni illegal kwenye society. Serikali inayowabagua wananchi wa vijijini ndio inaweza kuonekan iko defunct na illegal kwenye society. Ndio maana walikuwa wepesi hata Kusign Mou.
Hayo mafanikio ya afya ya serikli ambayo tunayasikia kama ya huduma za wamama na watoto bila hizo fund zingekuwaje.

Ukitaka waislamu waende mahakamani kwanza lazima vipengele vile vya katiba vifutwe na sheria zilizobadilishwa kuruhusu biashara hii ya kugaiana hela za walipa kodi ziondolewe zirudishwe either zilikuwapo zamani au zitungwe upya kuondoa masuala haya ya kupeana hela za wavuja jasho nchini.

Mdondoaji Hilo la Mou Sio katiba na Mou haina Nguvu kama mkataba. Hili jambo Serikali ya Kiwete au CCM wakiamua wanaweza kusema Kuanzia mwaka ujao wa fedha Hakuna fund kwenye Hospitali zozote za mashirika ya Dini. Lakini itakapofika hapo serikali itkuwa haina share kwenye maamuzi kama tunavyoona zilivyo hopistali za aghakhan. The loosing team itakuwa ni afya, serikali na wananchi wakiweo baadhi ya waislam na the winning team itakuwa baadhi ya waislam.

Kwa sababu hili jambo limeongelewa sana na linaonekana tunaliongelea kiisiasa napenda nione japo Hii Mou inafutwa. Faida na hasara zake my be ndiyo zitatupa majibu. Lakini to me ni wazi. Que ya wagonjwa wa KCMC, bugando, Ndanda, itahamia Muhimbili. Que ya wagonjwa wa vijijini wilayani itahamia Hopitali za Mikoa. Kwa watu wa Dar mwanza mjini, Arusha Tanga Atasema Sawa lakini.............

I wish JK afanye pata potea za kufuta hiyo Mou.
Je
  • atakuwa ni hero kwa waislam
  • takuwa ni Hero kwa sera ya afya. na huduma bora ya afya Tanzania.

@Mdondoaji
JK anakuuliza umpe ushauri . Anakumbia baada ya miezi sita serikli yake itaacha kutoa pesa kwenye hopitali za kanisa. Sasa wewe kama Muislam unayeumizwa na kodi yako kutmiwa na hopitali ya Kanisa na kama mtanzania unayetaka wananchi wapate huduma Bora unatakiwa kuwamabia nini kifanyike ili baada ya hiyo miezi sita huduma ziwsiwe from bad( Assuming hosptli za kansa zinatoa huduma mbaya na gharama juu ) to worse

Nini serikai inatakiwa kufanya ili Offloading ya wagonjwa wataolazimika kukimbia Ndanda kwenda mbeya isisababishe matatizo. na kero

Waislamu watapiga kelele hadi hili suala liondolewe na kufutwa kabisa au kuwepo na uwiano sawa. Binafsi yangu ningelipendelea hili jambo lifutwe hela za walipa kodi ziende kwa shughuli za serikali, shule za serikali na hospitali za serikali.


Mdondoaji wewe mara nyingi unaongea kama mtoto wa mjini. Huna sense na touch wa watu wa culture, mila maeneo na sehemu mbali mbali ya Tanzania . Huna sense of touch ya life ya country side.of Tanzania . Hata unapooogelea waislam elewa wametapakaa na kuna wengine wengi wanahudumiwa na hopitali kama za Ndanda . Na bila hizo mhhhhh.......

Serikali inaweza kujenga hospitali nzuri kibondo kigoma. Lakni hiyo hiyo serikali imeshindwa kuwavutia madakatari na wataalam kwenda ufanya kazi sehemu za reomote. Hizi hela manzooonglea inawezekana mnaaona nyingi sababu mnafikiria dar,mwanza rusha na tanga mjini. Jamani Tanzania ni kubwa.


Na hili sula kuodolewa litaonolewa labda sabbau ya Kisiasa au sabbau za kidini( Kuwafurahisha baadhi ya waislam) lakini kiutendaji sio maamuzi sahihi. Sio katika hali hii ambayo iliyopo.

Serikali inatoa Bilioni 91 wakati wagonjwa Muhimbili wanalala chini!!!!! Wagonjwa hospitali ya temeke au magomeni wanalala kitanda watu wanne??? Shule za serikali wanafunzi wanafanya mitihani katika uwanja wa wazi wa mpira.
Bilioni 91
  • zinafanya nini?
  • Ni kwa hospitali ngapi ziko wapi
Kama kuna hospitali ya kanisa iko karibu na muhimbili nitaunga mkono hata kesho kuandamnaa ifutiwe ruzuku lakini kama wewe unona kwa ku serikali haina hospitali ya hadhi Kigoma basi mgonjwa wa Kigoma afe just because hospitali nzuri iliyopo kigoma ni ya kanisa hapo nitakataa.

kam wewe unaona kwa kuwa Serikali haina hospitali ya hadhii turiani Morogoro basi Wananchi wa turiani na maeeno jirani hawatawiki kuwa na "muhimbili" yao just because ni mali ya Kanisa uko corurptlly wrong.


This morally wrong and socially illegal.
Mdondoaji wewe unaweza kuwa sio tu uko morally wrong but hata ethically. Yes something might not be not right but sio katika hali unayotaka kuonyesha.
Ukichukua tawimu za fedha tu hupati picha kamili. tutafute traffic pia za wagonjwa. tutafute pia unafuu au ughali wa huduma. Tafuta idadi ya hizo hospitali. tafuta takwimu za wapi zilipo na jiulize haya makanisa yaewezaje kuwaweka watalam maporini wakati serikali inashindwa.
 
Ebu taja kipengele cha Katiba lkilichabailishwa kilikuwaje kabla ya mabadiliko na baada ya mabadiliko kikawaje? MEmorundum hii ilivyo kinachoweza kuifanya iwe tatizo ni kama kuna pesa zinatumika nivyo sivyo. ni kama ikionekana labda Hopitali zinpkena blioni 22 kumbe inawezekana zinapoke bilioni 3 au 40.

nakuomb tena QUOTE kipngele cha katiba kilichobadilishwa just kukidhi na kulegalise Mou Ya serikali na kanisa



Mohamed Said haja quote hicho kifungu na kilichobadilishwa just kukidhi mahitaji ya Mou ya kanisa . What wengine wakisema kipengele kilipiitishwa kukidhi mahitaji ya huduma bora kwa wananchi . Sio ndio maana kuna sifa mwinyi anapata dhidi ya nyerere wakati wa winyi hatawatotot tulianza kukamata noti za elfu.

Mimi naomba kiwekeni hadharani hicho kipengele kilichobailishwa tupime kabla kilikuwaje na baadae kikawaje.


Na walioandaa ,walioshauri Mou wala sio Maasofu na wala sio entity moja ya Kanisa. Ni watu proffesional walijairwa kushghulikia mambo ya nje ya dini . ni watu walipewa kuangalia mahitaji ya kimwili ( elimu na afya) . Ndio Maana nimekuuliza katik waislam Ni mtu gani anahusika na ambo ya Elimu. Ni nani anahusika na ambo afya. nahitaji kuwa na coridanted structure lakini yenye mipaka kuwa Sheikh atfany haya na atapokea ushauri wa abo ya Elimu kutoka kwa irector wa elimu wa taaisisi fulani.

Na sio kweli kwamba Mou ni illegal kwenye society. Serikali inayowabagua wananchi wa vijijini ndio inaweza kuonekan iko defunct na illegal kwenye society. Ndio maana walikuwa wepesi hata Kusign Mou.
Hayo mafanikio ya afya ya serikli ambayo tunayasikia kama ya huduma za wamama na watoto bila hizo fund zingekuwaje.



Mdondoaji Hilo la Mou Sio katiba na Mou haina Nguvu kama mkataba. Hili jambo Serikali ya Kiwete au CCM wakiamua wanaweza kusema Kuanzia mwaka ujao wa fedha Hakuna fund kwenye Hospitali zozote za mashirika ya Dini. Lakini itakapofika hapo serikali itkuwa haina share kwenye maamuzi kama tunavyoona zilivyo hopistali za aghakhan. The loosing team itakuwa ni afya, serikali na wananchi wakiweo baadhi ya waislam na the winning team itakuwa baadhi ya waislam.

Kwa sababu hili jambo limeongelewa sana na linaonekana tunaliongelea kiisiasa napenda nione japo Hii Mou inafutwa. Faida na hasara zake my be ndiyo zitatupa majibu. Lakini to me ni wazi. Que ya wagonjwa wa KCMC, bugando, Ndanda, itahamia Muhimbili. Que ya wagonjwa wa vijijini wilayani itahamia Hopitali za Mikoa. Kwa watu wa Dar mwanza mjini, Arusha Tanga Atasema Sawa lakini.............

I wish JK afanye pata potea za kufuta hiyo Mou.
Je
  • atakuwa ni hero kwa waislam
  • takuwa ni Hero kwa sera ya afya. na huduma bora ya afya Tanzania.

@Mdondoaji
JK anakuuliza umpe ushauri . Anakumbia baada ya miezi sita serikli yake itaacha kutoa pesa kwenye hopitali za kanisa. Sasa wewe kama Muislam unayeumizwa na kodi yako kutmiwa na hopitali ya Kanisa na kama mtanzania unayetaka wananchi wapate huduma Bora unatakiwa kuwamabia nini kifanyike ili baada ya hiyo miezi sita huduma ziwsiwe from bad( Assuming hosptli za kansa zinatoa huduma mbaya na gharama juu ) to worse

Nini serikai inatakiwa kufanya ili Offloading ya wagonjwa wataolazimika kukimbia Ndanda kwenda mbeya isisababishe matatizo. na kero



Mdondoaji wewe mara nyingi unaongea kama mtoto wa mjini. Huna sense na touch wa watu wa culture, mila maeneo na sehemu mbali mbali ya Tanzania . Huna sense of touch ya life ya country side.of Tanzania . Hata unapooogelea waislam elewa wametapakaa na kuna wengine wengi wanahudumiwa na hopitali kama za Ndanda . Na bila hizo mhhhhh.......

Serikali inaweza kujenga hospitali nzuri kibondo kigoma. Lakni hiyo hiyo serikali imeshindwa kuwavutia madakatari na wataalam kwenda ufanya kazi sehemu za reomote. Hizi hela manzooonglea inawezekana mnaaona nyingi sababu mnafikiria dar,mwanza rusha na tanga mjini. Jamani Tanzania ni kubwa.


Na hili sula kuodolewa litaonolewa labda sabbau ya Kisiasa au sabbau za kidini( Kuwafurahisha baadhi ya waislam) lakini kiutendaji sio maamuzi sahihi. Sio katika hali hii ambayo iliyopo.


Bilioni 91
  • zinafanya nini?
  • Ni kwa hospitali ngapi ziko wapi
Kama kuna hospitali ya kanisa iko karibu na muhimbili nitaunga mkono hata kesho kuandamnaa ifutiwe ruzuku lakini kama wewe unona kwa ku serikali haina hospitali ya hadhi Kigoma basi mgonjwa wa Kigoma afe just because hospitali nzuri iliyopo kigoma ni ya kanisa hapo nitakataa.

kam wewe unaona kwa kuwa Serikali haina hospitali ya hadhii turiani Morogoro basi Wananchi wa turiani na maeeno jirani hawatawiki kuwa na "muhimbili" yao just because ni mali ya Kanisa uko corurptlly wrong.



Mdondoaji wewe unaweza kuwa sio tu uko morally wrong but hata ethically. Yes something might not be not right but sio katika hali unayotaka kuonyesha.
Ukichukua tawimu za fedha tu hupati picha kamili. tutafute traffic pia za wagonjwa. tutafute pia unafuu au ughali wa huduma. Tafuta idadi ya hizo hospitali. tafuta takwimu za wapi zilipo na jiulize haya makanisa yaewezaje kuwaweka watalam maporini wakati serikali inashindwa.

Zing,

Angalia usije kuadhirika tu maana unazungumza na mtu makini na najua nini nazungumza ulitaka kujua kifungu gani kimebadilishwa? Soma hapa namnukuu Sheikh Mohamed Said katika paper yake Christian Hegemony and Rise of Muslim militancy. anasema hivi;
"
This agreement was prepared by Dr. Costa Mahalu , Dar Es Salaam University Faculty of Law and was signed by Minister of State in Prime Minister’s Office and First Vice-President, Edward Lowassa. The main purpose of the agreement was to turn over education, health and social services to Christian Council of Tanzania (CCT) and Tanzania Episcopal Conference(TEC). These social services were to be run jointly between the government and the Church. This agreement, that is, the Memorandum of Understanding was prepared and signed without even consulting or informing Muslims. In order for the memorandum to take effect the government had to ammend article 30 of the Education Act No. 25 of 1978."


Katafute hiyo Act uisome na ujiulize maswali. Narudia tena this MoU is morally wrong and socially illegal period.
 
Back
Top Bottom