Mkataba wa Bandari: Anayekiri makosa na kuomba msamaha asamehewe kisha twende pamoja

Nina wasiwasi sana na elimu yako, hivyo vyeti vyako natakiwa kuvipitia nijiridhishe.
 
MKATABA UNAFAA NA HAUNA SHIDA YOYOTE WALIKUWEPO TICTS WAMESHINDWA WACHA WAJE DP WORLD.
 
Kasheku hata kuongea anaona aibu.
 
Umewataja wakristo hawa vizuri sana ambao wamejibu hoja za kimkataba vizuri kabisa!

Kwa nini hutaki kusikiliza hoja zao unasikiliza hoja za hao wahuni TEC?
Ulivyoandikatu, unaonekana uelewa wako ni duni na hujastaarabika. Aliyestaarabika hawezi kuwaita maaskofu ni wahuni. Labda kama wewe ni wakala wa shetani. Wakala wa shetani humchukia na kumfanya qdui kila anayepunguza wafuasi wa shetani.

Yaani watu waache kuzingarua uchambuzi na maoni ya maaskofu, watu wenye elimu kubwa ya Ulimwengu na theolojia, wamsikilizempiga kelele Mkumbo, mtu ambaye hana uelewa wowote wa masuala ya sheria, uchumi na uwekezaji. Yaani Kitila Mkumbo,profesa wa Saikolojia ndiyo ageuke awe mwalimu wa masuala ya kisheria.

TEC ni taasisi iliyosheheni wataalam wa kila aina, huwezi kuilinganisha na wababaishaji na waimba hadaa, akina Kitila na Chongolo.
 
Ninawaita wahuni kwa sababu wanafanya mambo mengi sana ya hovyo na wakifanya hayo mambo wananchi wanapigaga kelele ila huwezi kuwasikia wakitoa waraka

Mfano sakata la escrow ambapo na baadhi yao walipokea migao ya fedha zetu
 
Umesoma vifungu vya mkataba??? Au unataka uone na risiti kabisa ndo ujue imeuzwa?
Weka iko kifungu kinachosema Bandari imeuzwa? Huko kwenye risiti mbali sana nitakuonea bure
 
Basi itakuwa ni zile degree za pichu au imani ya kidini umeitumia vibaya hadi imekuharibu.
Elewa hata katika makundi ya extremist wanaofanya vitendo vya ajabu visivyo vya kiutu wamo wasomi wakubwa pia.
Ni kweli. Wapo extrimists waliosomasanalakino hawakuelimika, hawakustaarabika wala hawana maarifa.
 
Huo unaouita utafiti wako, hautakiwi kuitwa utafiti. Itakuwa ni takataka fulani iliyomo nafsini mwako uliyoamua kuiita utafiti. Unatakiwa kuiondoa.

TEC ilipinga sera za uwekezaji za Rais Mkapa. Walimpinga kwa sababu ya dini yake?

TEC ilitoa waraka kupinga utawala wa kibabe wa hayati Magufuli, usiozingatia haki za watu. Ilikuwa ni kwa sababu Magufuli alikuwa muislam?

Kwa nini TEC hao hao waliopinga baadhi ya mambo wakati wa utawala wa viongozi wakristo, wakati huo isiwe udini, ila uongozi ukiwa wa muislam, iwe udini?

Yawezekana ukawa umekaa miaka mingi darasani, lakini imeshindwa kukusaidia kuwa na maarifa. Maarifa ni zaidi ya kukaa miaka mingi darasani. Inanikumbusha kuna wakati tulikuwa na mradi wa kati wa hydropower. Tukaomba ushiriki wa serikali uwe katika kutupatia wataalam wa kufanya design na kusimamia. Serikali ikaahidi kutupatia best engineers kwaajili ya hiyo kazi. Wakatupatia engineers wanne, wawili wana masters degree, na wawili wana bachelor. Wakaja na bajeti kubwa ya ajabu. Kwa sababu tumekwishafanya miradi kama hiyo sehemu nyingine pia, hasa South America, tulipatwa na mashaka makubwa. Tukatafuta ushauri kungine. Kila aliyeona andiko lile, alisema ni rubbish. Mradi ule ulikuja kusimamiwa na technician toka Ujerumani, toka hatua ya awali mpaka unakamilika, Gharama ikawa ni kama 35% ya ile bajeti ya wahandisi wa Tanzania. Unaweza kuona dhahiri kuwa huyu mjerumani ana maarifa, hawa wahandisi wa Tanzania walikuwa wamesoma sana lakini hawana maarifa. Na hilo ni tatizo kubwa la Watanzania wengi, wamesoma lakini hawana elimu wala maarifa.
 
Musikitini haiwezekani.
Hilo ni jambo lenu wagalatia
Ninyi kwenu ni sawa, alimradi tu anayepora awe wa imani yenu? Sisi tutaendelea kuzuia uporwaji wa rasilimali za nchi bila ya kuangalia wanaoupigia debe ni wa dini gani. Hatutaangalia ni Mbarawa au Mkumbo, ni Wasira au Johari.

Mporaji ni mporaji, awe mkristo, muislam, hana dini, mwanaume au mwanamke, jina lake linabakia moja tu, kuwa huyo ni adui wa Taifa.letu la leo na la.kesho.
 
Mtu akikosa hoka ya ulinzi wa dhambi alizotenda yeye au mwandani wake kama Kikwete alivyofanya jana, anakimbilia udini ili apate watu wa kumtuliza au sympathy. Mtu anasema udini anaruka hoja kama mkataba wa bandari ni hovyo au siyo hovyo.
 
Usiende kwa hisia bali weka fikra zako huru.

Ni nani anayewachukia waislam? Sisi wengine familia zetu ni za mchanganyiko, waislam na wakristo. Japo kwa kiasi fulani misimamo ya sisi wakristo na waislam, katika imani, ipo tofauti.

Nakumbuka kwnye ukoo wetu, wapo waliobadili dini na kuwa waislam, hasa kutokana na masuala ya kuoana. Waliobadili toka ukristo kwenda uislam, kwa sababu walikuwa ni watu wazima, hawakutengwa na jamaa zao wa karibu. Lakini wao wao, baadhi waliposema wanataka kutoka kwenye uislam na kuwa wakristo, ilikuwa tafrani sana, wengine mpaka kuwatamkia watoto wao kuwa wangeingia kwenye ukristo, wangewaua. Na wakaanza kuwachukia baadhi ya ndugu kuwa wanaamini ndiyo waliowashawishi watoto wao kutofuata dini za wazazi wao, na kuamua kuwa wakristo.

Kwa ujumla, inaonekana waislam ni too sensitive. Kukitokea kitu chochote, fikra za mwanzo kabisa wanalipeleka kwenye fikra za kidini. Hata akafanyiwa jambo fulani, labda siyo la kufurahisha nafsi yake, kama jambo hilo limefanywa na mkristo, cha kwanza anaanza kufikiria jambo hilo limefanywa dhidi yake kwa sababu yeye ni muislam.
 
Umewataja wakristo hawa vizuri sana ambao wamejibu hoja za kimkataba vizuri kabisa!

Kwa nini hutaki kusikiliza hoja zao unasikiliza hoja za hao wahuni TEC?
Kama TEC ni wahuni basi jibuni hoja je mkataba uko na vipengele sawa sawa kwa maslahi ya Taifa au ni mihemuko tu.TEC wahuni sawa,je wewe utakuwa na hali gani?
 
Umenena vyema
 
Ila ujinga umekujaa kichwani pamoja na mlolongo wa elimu uliyonayo unashindwa kufikiri sawasawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…