Mkeo aliwahi kukulaza lock up, baada ya kutoka maisha yalikuwaje?

Mkeo aliwahi kukulaza lock up, baada ya kutoka maisha yalikuwaje?

Hali zenu?

Wakuu, siku ya jumatano majira ya saa 1 jioni nikiwa nimefika nyumbani kutoka mihangaikoni, kulitokea kutokuelewana na wife,nikajikuta napandwa na hasira nikamshika nikachomoa mkanda wangu wa suruali nikamtandika nao hatari alivyopata upenyo akakimbilia nje.

Kumbe mashosti zake wakawa wamemshauri akimbilie kushtaki polisi, akaenda kituo cha police kushtaki,baada kama ya lisaa hivi nikasikia nagongewa na balozi wa nyumba kumi akiwa kaambatana na Askari polisi wawili, wakaniambia nahitajika kituo cha police kwani mke wangu kaenda kushtaki kuwa nimempiga.

Sikuwa mbishi nikawaomba nibadili nguo na niweke mazingira ya nyumba sawa kwani watoto na dada wa kazi hawapo.

Basi bana nikafika kituo cha police pale kaunta nikamkuta wife kakaa yuko na mashosti zake kama wawiili nikachukuliwa maelezo yangu kisha nikafunguliwa kesi ya shambulio la kudhuru mwili, nikaingizwa lock up, kwa sababu ilikua usiku afande mmoja hivi akaniambia kosa linadhaminika kama kuna jamaa zangu wako around niwacheck waje wanidhamini

Lakini pia akanishauri kwa jinsi anavyoona nina hasira bora nilale tu mle lock up kuepusha madhara kwani nikisema nitoke usiku ule ningeweza kumdhuru zaidi wife na pale lock up ni sehemu salama zaidi. Basi nikawa nimemuelewa yule afande nikatulia mpaka asubuhi,kulivyokucha nikaomba simu yangu pale kaunta nikawapigia jamaa zangu wakaja wakaniwekea dhamana.

Hapa nilipo toka nitoke lock up nimeona nikae kwanza kwa jamaa angu kujiepusha na huyo mwanamke,ameisha enda police mwenyewe kuwaambia hana nia ya kuendelea na hiyo kesi hivyo anaomba ifutwe, Askari kama kawaida wamemtoa pesa kidogo.

Sasa toka jana naona ananitumia watu kuja kumuombea msamaha kuwa alikosea kunilaza lock up.

Hapa niko stranded nimsamehe au nimfanyaje na baada ya kumsamehe maisha yetu hapo ndani yatakuwaje?

Kama kuna yeyote amewahi kupitia hii changamoto anisaidie mawazo.
Ningekua Mimi ndo Uyo mkeo ningehakikisha unalala huko siku 3 Na msamaha ungeomba wewe soon Mimi😡😡😡😡😡
 
A
Ilikua leo nipelekwe mahakamani,ila kwa sababu mlalamikaji amesema hana nia ya kuendelea na kesi na ameomba tuyazungumze wenyewe,so tuko hapa polisi kwenye dawati la jinsia sijui wanataka kutuambia nini.
Aisee pole mkuu hyo imeisha mnaenda tu kupewa counseling kwa siku nyingine but tayari wife atakuwa amekupunguzia spidi kwenye kudeal nae next time. Na pia atachukulia hiyo km gia ya kukutishia siku nyingine mtakapogombana so ni lazima tu utapoa kiaina. Maisha kwa sasa lazima yatabadilika mkuu.
 
Wewe ingekuwa mi ndo huyo mkeo, ningempa na buku 10 poti akushughulikie vizuri ili ukirudi uraiani uwe raia mwema. Huna adabu, unapigaje mkeo na mkanda ukimuua??

Mwambie mkeo anitumie namba nimtumie pesa ya soda, kanifurahisha sana’aaa.!! 😹🤣
Alafu wewe ebu njoo huku maana na shida na mtu kama wewe
 
Kuna shemeji yangu hivo hivo alimpiga dada akampeleka polisi alitolewa asubuhi na kesi akaifuta sasahivi wanaishi fresh tu ata ikitokea ugomvi anaondoka uko nje akirudi wanayazungumza yanaisha....nakushauri samehe tu mwanamke apigwi na akipigwa lisiwe pigo la kujeruhi mpige kofi moja tu begani au mgongoni ondoka katafute cha kukufanya hasira zipungue
 
Yaani hapo kosa ishakuwa wewe kulazwa ndani na sio wewe kumpiga yeye!
Wewe uli react ukampiga na yeye ka react akaenda kukushtaki. Nyote mmefanya makosa kama binaadam
Na kwa nini watu wazima mfike kupigana kama wtt. Wewe kwani huyo binti wa watu umekabidhiwa na wazee wake ili umpige au umtunze?
 
Mwanamke wa kukupeleka polisi huyo sio mke ni jangili. Mke yapaswa awe mstahimilivu na mwenye hekima ya kujua akipigwa ni sehemu ya maonyo kuwa anatoka nje ya reli. Sasa mke unampiga kibao tu kashakimbilia polisi kweli?!
Kama nimekuelewa ni kwamba mtu mmoja kumpiga mwingine ni maonyo, ila kupelekwa polisi kwa kosa la kudhuru mwili sio maonyo ni ushetani!!!!! Inafikirisha sana.
 
Hali zenu?

Wakuu, siku ya jumatano majira ya saa 1 jioni nikiwa nimefika nyumbani kutoka mihangaikoni, kulitokea kutokuelewana na wife,nikajikuta napandwa na hasira nikamshika nikachomoa mkanda wangu wa suruali nikamtandika nao hatari alivyopata upenyo akakimbilia nje.

Kumbe mashosti zake wakawa wamemshauri akimbilie kushtaki polisi, akaenda kituo cha police kushtaki,baada kama ya lisaa hivi nikasikia nagongewa na balozi wa nyumba kumi akiwa kaambatana na Askari polisi wawili, wakaniambia nahitajika kituo cha police kwani mke wangu kaenda kushtaki kuwa nimempiga.

Sikuwa mbishi nikawaomba nibadili nguo na niweke mazingira ya nyumba sawa kwani watoto na dada wa kazi hawapo.

Basi bana nikafika kituo cha police pale kaunta nikamkuta wife kakaa yuko na mashosti zake kama wawiili nikachukuliwa maelezo yangu kisha nikafunguliwa kesi ya shambulio la kudhuru mwili, nikaingizwa lock up, kwa sababu ilikua usiku afande mmoja hivi akaniambia kosa linadhaminika kama kuna jamaa zangu wako around niwacheck waje wanidhamini

Lakini pia akanishauri kwa jinsi anavyoona nina hasira bora nilale tu mle lock up kuepusha madhara kwani nikisema nitoke usiku ule ningeweza kumdhuru zaidi wife na pale lock up ni sehemu salama zaidi. Basi nikawa nimemuelewa yule afande nikatulia mpaka asubuhi,kulivyokucha nikaomba simu yangu pale kaunta nikawapigia jamaa zangu wakaja wakaniwekea dhamana.

Hapa nilipo toka nitoke lock up nimeona nikae kwanza kwa jamaa angu kujiepusha na huyo mwanamke,ameisha enda police mwenyewe kuwaambia hana nia ya kuendelea na hiyo kesi hivyo anaomba ifutwe, Askari kama kawaida wamemtoa pesa kidogo.

Sasa toka jana naona ananitumia watu kuja kumuombea msamaha kuwa alikosea kunilaza lock up.

Hapa niko stranded nimsamehe au nimfanyaje na baada ya kumsamehe maisha yetu hapo ndani yatakuwaje?

Kama kuna yeyote amewahi kupitia hii changamoto anisaidie mawazo.
Msamehee mkuu. Ludi nyumbani uishi na mkeo. Uzi ni harakati tu katika kufika inchi ya ahadi. Ludi nyumbani mwamba.
 
Siku wife akifanya hivyo ndio basi tena, we will part ways.
 
Mimi sijawahi

Lakini kichwani mwangu mimi ni kwamba mtu yeyote (siyo mke tu bali hata awe ndugu jirani au rafiki) akishanipeleka polisi, ustawi wa jamii, mahakamani, takukuru au ofisi yoyote ya serikali ya kimamlaka basi tayari huyo namuweka pending katika ubongo wangu. Mara nyingi ikifikia mambo hayo huwa nakaa upande wa kushindwa nauliza tu anavyotaka yeye natimiza kisha navaa tinted mpaka akili imkae sawa. Huyo anaingia kwenye black memory yangu

Labda iwe kwamba njia zingine zote alifanya zikagonga mwamba ikawa hakuna namna yoyote zaidi ya kunipeleka huko lakini siyo kufanya kama fasheni. Mfano jirani mmepishana kidogo kuhusu mpaka hajakuita mzungumze hajawaona hata wazee wanaoweza kukuweka kitako wala hajafanya chochote moja kwa moja kakimbilia ofisi za ardhi kisa anapajua!

Kuhusu ushauri nakushauri chukua uamuzi ambao hauna madhara pande zote (yaani uamuzi unaojenga zaidi kuliko kubomoa)
 
Kila binadamu ana kiwango chake cha uvumilivu

Ikifika hiyo hatua ni rahisi sana ku-react Kwa kufanya jambo ambalo Kwa muda huo anahisi litampa amani

Kitendo cha Mkeo kukupeleka kituo cha Polisi, kinaonesha alivyoshindwa kuzuia hasira zake kwako mara baada ya wewe kumpiga.

Tushukuru Mungu tunaishi Tanzania, Nchi ambayo haijaweka Sheria Kali kuhusu Mume kumpiga Mke/mpenzi

Ingekuwa Nchi zilizoendelea, huwa Wana mashtaka makali sana juu ya hayo

Huku Tanzania Mume anampiga Mke wakati mwingine hadi kumvunja shingo/Mkono ama wakati mwingine hata kumtoa Uhai

Kumbukeni adhabu aliyopewa Mwanamuziki Chris Brown baada ya kumpiga aliyekuwa mpenzi wake Rihanna

Wanaume tujitahidi kuzuia hasira mbele ya hawa wapenzi/wake zetu

Wanawake kiasili ni waongeaji, na kamwe Wanaume hatuwezi kuwafikia Kwa kuongea

Hivyo vyema wakati mwingine kujiepusha hata Kwa kwenda kibanda umiza kuangalia Mpira, hata kama nyumbani umelipia king'amuzi chako

Wanasema kunguru mwoga hukimbiza mbawa zake...

Tukumbuke kuna baadhi ya Wanaume wenzetu walishindwa kuvumilia maneno ya wake zao wakajikuta wanawapiga kawaida, lakini kumbe Mke ndiyo anafariki Dunia hivyo kuishia kufungwa jela maisha
 
Ila wanaume ni viumbe wabinafsi mno, wote hawaongelei kosa la jamaa kumpiga mke wake mnaona la mke kumpeleka polisi. Mijanaume ya Tanzania imeshanomarlize Domestic violence iwe kitu cha kawaida sana.
Kaa chini na mke wako mmalize matatizo yenu sababu hawa wanaokushauri mitandaoni wengi ni mabachelor sugu hata hawajui maana ya familia ndio maana kirahisi anakwambia " piga chini" akili kichwani kwako. Na mwisho acha kumpiga mkeo looh
Hhhhhh turudie wasamehe
 
......Kachuke begi, then potea mwezi mzima,ngoja kwanza mashosti zake waendelee kumpa ushauri.
 
Kuna lugha za maudhi tu alinitamkia, nikajikuta nimemlabua.
Kama ungempiga kimahaba sizani kama angeumia kiasi hicho akatoka nje, kwanza mke na mme inatakiwa ungemalizia chumbani sasa wewe unampiga mtu kwa mkanda? Halafu sasa wewe kwanini umruhusu atoke nje akiwa analia?
 
Back
Top Bottom