Mkopo NMB: Nimekopa 9 mil , nakatwa 250,000 kila mwezi kwa miaka 6 nitarejesha 18 mil !

Mkopo NMB: Nimekopa 9 mil , nakatwa 250,000 kila mwezi kwa miaka 6 nitarejesha 18 mil !

Status
Not open for further replies.
Mikopo ya muda mrefu lazima ile kwa mkopaji... Usidanganywe na makato.
Ni muhimu kukopa kwa muda mfupi mfupi...maumivu hayatakuwa makubwa sana.
 
Mkuu 250 imefikaje??? Mbona wengine ni 196, ambayo inaleta kama 14 hivi!!!!
 
Huu ni uongo eti umekopa mil9 kwamiezi 6x250,000=ni 1,500,000 hio mil 18 kwa hesabu ipi mkuu au umejichanganya
Wewe ndo hujui hesabu mkuu piga hivi
250000×12=3,000,000
3,000,000x6=18,000,000...
Hatari lakini salama
 
Nmb hawana wema hawa
Nilikwenda kuulizia 17 milioni wakaniambia
Makato 378000 kwa mwezi
Muda miaka 6
Bima ya mkopo 1.75%
Process fees1%
Nilichoka,
 
Iko namna hii, Algebra hii na wala sio Albadiri

Kakopa 9m, malipo kila mwezi 250k , muda ni miaka 6 (mwaka 1=miezi 12, zidisha 6mara 12 unapata 72)

Hivyo, fanya namna hii, 250k mara 72=18milioni.

Na hizi bado hajaweka chaji nyingine za kibenki zinazoweza kukaribia mawe kumi

Ila kwa riba ya 100 asilimia naamini hii NMB ya kipekee (wanafanya usury)
Labda huo ni mkopo kwa ajili ya wapita njia! Yenye maximum risk!
 
  • Kicheko
Reactions: Obe
ungechukua kwa muda mfupi may be miaka 4 au 3 kidogo ingepungua
 
Hii nchi kuna mambo mengi ya msingi sana hayapewi kipao mbele mana hayana madili kama ilivyo miradi mikubwa ambayo bila shaka Kuna wachache wananufaika nayo sana kwa niaba ya wengi.
Wenzetu Waarabu wana mfumo wao wa mikopo isiyo na riba wakifuata misingi ya dini ya kiislam.
Waafrika tumefuata mifumo hiyo ya mariba makubwa makubwa lakini yanazidi kutupa umaskini na watu wengi wanashindwa kulipa hasa wafanyabiashara mana riba ni kubwa sana wanaolipa kwa urahisi ni wafanyakazi na wanasiasa ambao Mara nyingine wanaahidiana kusaidiana kulipa alimradi watumikie siasa na kampeni au kuhama vyama.

Sisi tunafuata mifumo yote ya kifedha ya nchi za magaharibi lakini wakitoa ushauri wanaitwa mabeberu.
Sijui Link waafrika tutakua na mifumo wetu wa kifedha.

Waafrika sijui tulilogwa na nani?


...bank na mikopo ipo kwa ajili ya kumsaidia mtu/kampuni, tatizo hapa bado kuna uholela. Mabank ya kibiashara si sehemu nzuri sana kukopa kama unahitaji kujifanyia maendeleo binafsi. Mabenki ya ushirika (credit unions) na vicoba au ndugu, ni sehemu nzuri kukopa kwa ajili ya kujiendeleza (bila kuhusisha biashara)
 
Pigeni hesabu wana jf hapo
2014 nilikopa milioni 8
Wananikata 203000
Miaka5
Namaliza mwezi huu may
Sikopi tena,unataabika kudadadeki ,acha Tu
Kinachoniudhi hawa jamaa ni hizo charge zao
 
Mkopo NMB : Nimekopa 9 mil , nakatwa 250,000 kila mwezi kwa miaka 6 nitarejesha 18 mil !

Umaskini hauishi kamwe.
usijekuta hiyo hela ulihonga kimada na nyingine ukafadhili msiba, pole sana,
 
Labda huo ni mkopo kwa ajili ya wapita njia! Yenye maximum risk!

.....tujipe faida ya dhahania, huyu ni mfanyakazi/mfanyabiashara na ana anuani kamili na dhamana kaweka, hii maximum risk ni sky high.

Kukosa sehemu tu ya mtaji, lakini kama akija mtu na mpango wa kuangalia kukopesheka kwa mtu basi wengi tutapata mikopo rahisi. NMB ni bank ya umma( govt ina hisa nyingi) kwa hiyo masuala ya kumnyonya mtu (ili kutoa gawio) hayana maana.
 
Hivi huwa hamuwaulizi wawape details za kutosha na ufafanuzi on payment terms kabla hamjaingoa mkataba? Majuto baada ya kuingizwa king hayasaidii
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom