Aah kwa hapo lazma mgongano wa maslahi utakuwepo.Hii kampuni nilichoona Kuna magumashi yalifanyika, Ultimate, KK, na kampuni zingine Kwa nje ni kama wameungana kuwa Garda World lakini ndani zimebaki vile vile. Kuna baadhi ya mambo yana misuguano sana kwenye uendeshaji na utawala.
SGA na G4S hawakuingia kwenye hilo shirikisho. Na Kuna baadhi ya maeneo Garda wamepoteza kazi zikachukuliwa na SGA na G4S.
Hahahah kibongo bongo ndo mambo ya kulipana tarehe 34 yanaanzaga.Mkuuu wazungu wengii wakiona wanapoteana au kampuni inapumulia mashine wanasepa wanatafuta mtu mwingine hasa hii rangi nyeusi ili waendeshe kampuni kibongobongo ili iweze kuservival mkuu
Aah kwa hapo lazma mgongano wa maslahi utakuwepo.
Ushauri wa maana kabisa huu.Gardaworld Wana mfumo wanao uogopa... Unaitwa GardaWorld Ethics Hotline kupitia hicho kiunganisha chukua hayo maelezo Yako bila kupunguza ukali wa maneno nenda kayaandike kwenye system yao ya malalamiko ambayo yatafanyiwa kazi makao makuu ya gardaworld Kisha hao unao watuhumu watapokea order ya kurekebisha kero ulizo zifafanua.
System hiyo unaweza kutoa malalamiko Yako kwa kificho bila kutaja utambulisho wako
Ukiona hiyo system inakusumbua unaweza kupiga simu ya malalamiko ambayo itapokelewa moja kwa moja na uongozi wa juu nje ya mipaka ya TanzaniA namba yao ya simu ni 0800780005
Hudumia hiyo ni ya kificho na Siri mno hakuna kiongozi wa garda ane penda wafanyakazi wa chini wafahamu njia hiyo...itumie uje unipe mrejesho
Yap...ngoja tuone kitakacho jiri kama ataitumia hiyo mbinu...!Ushauri wa maana kabisa huu.
Lakini mbona kule Mjengoni tunawekewa Spika na hatulalamiki?Spika imepata hadhi ya kuheshimiwa
Kumbe Garda wababaishaji hivyo!? Ngoja tusubiri utetezi wao tupime maelezo ya pande zote.Salute.
Naomba niende kwenye maada mimi kama askari (mlinzi) wa kampuni binafsi wa Garda world nimeamua kutumia platform hii kuleta kero ya kiongozi wetu mkuu wa kampuni ya ulinzi Garda world.
Kiukweli kiongozi wetu LuQmay tangu umepata kazi kwenye kampuni yetu sisi kama walinzi upande wa ultimate zamani kiukweli umekuwa tatizo kubwa na ni kero katika ufanyaji kazi.
Kwanza tangu umepata nafasi ya kuendesha kampuni ukitokea tigo hujawahi kuitisha kikao ujue wafanyakazi wako wanapitia shida gani na Nini malengo yako katika kampuni badala yake umekuwa (MUNGU MTU).
Naomba nieleze hapa kampuni ya ultimate kabla yakuwa Gardaworld imepitia mikononi mwa wamiliki wengi na Kila walipokuwa wanaamua kuuza kampuni Kwa mmiliki mwingine tulikuwa tuitwa kinafanyika kikao tunaeleweshwa na karibu hao maboss wote watu Ziballa & shivva nk.
Walikuwa wanafanya press tunajulishwa Kila kitu na walitoa pesa ya Asante nakumbuka nilipokea 1.2m maana nilifanya kazi Kwa miaka kumi na kipindi hicho chote tukiwa ultimate Kila baadae ya miezi sita.
Mkurugenzi aliitisha kikao tukasema kero zetu na zikafanyiwa kazi sasa tangu kampuni ya ultimate iuzwe na kuchukuliwa na Garda world.
Kiufupi tunaona tunaendeshwa kihuni hivi inakuwaje tunaenda kumuona mkuu wa mkoa mh chalmila hatupati ugumu wa kumuona iweje kwako Mkurugenzi ndugu luQmay utuwekee uzibe tusikuone kuleta kero zetu.
Pli kampuni imeuzwa mmiliki ambao ni wazungu wamekupa fedha wafanyakazi walipwe kama fidia ya kubadili mikataba Yao kutoka ultimate kwenda Garda world lakini kutokana na roho yako mbaya unataka kutuzima kinguvu Ili fungu uchukue na ni pesa nyingi ukiweza kutuzima tunaamini utatajirika sana tatu week mbili nyuma umenitisha kikao tumekuja kwenye kikao umetuwekea spika ndani ya ukumbi Yani wewe na team yako ya upigaji munaongea bila kuonekana sisi tunasikia tu kwenye spika mtu hatumuoni it's ok hata kama mmeamua kutufanya wajinga lakini sio Kwa level hiyo kikao.
Kilivyoshindikana ukapanga kikao tarehe Saba ulivyosikia na sisi tunakuja na wanasheria wetu mkaahirisha kikao Kwanini kiongozi LuQmay usijifunze
Kwa wenzio akina Eliuta mwanjawike walikuwa wanakula na kipofu alikuwa hakimbiii wafanyakazi mwisho usifikiri utatuendesha kirahisi kama unavyodhani..
Pia sisi tulidhani wewe mtu mweusi uwe mkombozi wetu Kwa hao wazungu lkn wewe ndio umekuwa mwiba kwetu hata kama ukifanikiwa kutudhurumu it's tutakuombea hata Dua mbaya tu maana mahakamini tukipekeleka kesi tukishinda unakuja kuappeal then uinaweka kapuni na kutishia kufukuza kazi wafanyakazi.
Ila Kwa hili la malipo ya mikataba tutaenda hata ubalozi wa Canada kushinikiza waiitwe wamiliki wa kampuni mwisho jifunzeni G4s na SGA uone kampuni zinavyoendeshwa.
Sasa SweetPain kama mpango wake ulikua huo si angesambaza link tu. Kuwjaza chumba kimoja na kuwapigia zoom ilimaanisha nnWapo kwenye majaribio ya online meetings.
Najibu Kwa vile umeninukuu japo ID uliyoiandika sio yangu Mkuu.Sasa SweetPain kama mpango wake ulikua huo si angesambaza link tu. Kuwjaza chumba kimoja na kuwapigia zoom ilimaanisha nn
Inasikitisha sana kwamba ukiwa na swali au maoni unaongea na spika!! PatheticMnafanya kikao na mtu asiyeonekana. Hii kali 😅
Poleni sana wakuuni kweli hapa tunaplan tutume email Canada na tuende ubalozi wa Canada kushinikiza maana Kwa hapa bongo kesi zote tunashinda lkn utekelezaji unaharibiwa Kwa rupia.
Ukiona danadana nyingi ujue mpunga hakunaHata kama kampuni inapitia kipindi kigumu ndio ushindwe kufanya mikutano na wafanyakazi wako zaidi ya miaka 3 na kibaya zaidi hawakujui🤔🤔🤔
Sijambo mkuu. Habari yako.Niachie mm 😅 hujambo?
Njema kabisa. Hili tatizo la walinzi naona tukuachie wewe tuSijambo mkuu. Habari yako.
Mazingira ya walinzi nayaelewa Sana. Garda, G4S, na SGA wanajitahidi Sana. Tatizo ni baadhi ya viongozi wao hasa watanzania, hawajitambui. Haya makampuni mengine ambayo ofisi IPO kwenye fremu, ndio kinyaa kabisa.Njema kabisa. Hili tatizo la walinzi naona tukuachie wewe tu
Ulinzi ni kazi ya Kiphaller sana aisee nilienda kuomba kazi control room pale G4S Nikaambiwa nianze na kulinda kwanza na nikapata training ya ulinzi na ilikuwa ni darasani kama chuo vile kwa miezi miwili. Sasa nikawa nimepangiwa Slip way Hotel yaani ili udumu kwenye kazi ya Ulinzi uwe mnafiki na uwe unajipendekeza sana kwa Ma supervisor, Zone Manager na Viongozi wengine. Aaah kitu hicho kilinishinda nilikuwa naburuzana nao sana kwa mwezi mara mbili napelekwa hearing nikifika hearing nawaburuza tu mpaka nikawa nawaambia tabia ya kunisumbua sumbua sitaki Wanafiki nyinyi nitawashitaki sasa. Duh waliniogopa mpaka wakawa wanajua Mimi ni GetiJeusi. Nikaamua kuachana nao. Yaani Tanzania hii Mlinzi anaonekana kama failure na hana option nyingine ya maisha. Kuna siku nitaanzisha uzi matukio niliyokuwa nakutakana nayo kwenye kazi ya Ulinzi. Tukio kubwa ambalo sitolisahau ni KUWARUHUSU CHURA WA YOMBO KUPIGA PICHA HOTELINI HALAFU WAKAANZA KUMWAGA RADHI MBELE YA WAZUNGU. HILI TUKIO SITOLISAHAU HALAFU WALIKIWA WAMENIPA 30,000. 🤣🤣🤣Nyie wenzenu wanaenda kulala mpo nje mnakesha 😄