Mkutano kati ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jeshi la Polisi na wadau wa siasa nchini waahirishwa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mkutano wa kati ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jeshi la Polisi na wadau wa siasa nchini uliopangwa kufanyika Dodoma wiki hii. Sababu za kuahirishwa kwake inaelezwa ni ili kutoa nafasi zaidi kwa wadau wengi zaidi kushiriki kikamilifu.

Mkutano huo uliolenga kujadili maudhui ya utekelezaji wa sheria zinazoratibu shughuli zote za siasa Tanzania' ulikuwa uhudhuriwe pia na waziri mkuu, Kassim Majaliwa.

Msajili msaidizi wa vyama vya siasa nchini Tanzania, Sixty Nyahoza aliiambia BBC kwamba, mbali na waziri mkuu na baadhi ya mawaziri, mkutano huo ulipangwa kuhudhuriwa na pia wadau wote muhimu katika siasa vikiwemo vyama vya siasa, Azaki, waandishi wa habari na viongozi wa dini.

Kama ilivyonukuliwa na mtandao wa gazeti la Mwananchi, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania, Juma Ali Khatib amesema mkutano huo hautakuwepo kama ulivyopangwa awali, lakini maandalizi yanaendelea kwa kuwa utafanyika mwezi Desemba, mwaka huu.

Hata hivyo tarehe ya kufanyika mkutano huo itatangazwa baadaye na utahusisha wadau tofauti wakiwamo wa vyama vya siasa vilivyotangaza kuususia kwa sababu tofauti.

Kabla ya kuahirishwa kwa mkutano huo, vyama vya Chadema na NCCR Mageuzi vilishatangaza kutoshiriki huku vikitoa masharti kwa Ofisi ya Msajili.

Alisema wadau wote wameshajulishwa kuhusu kuahirishwa kwa mkutano huo uliotarajiwa kuleta suluhu ya sintofahamu ya kisiasa nchini, hasa mvutano kati ya vyama vya siasa na Jeshi la Polisi.

Mkutano huo unakuja kufuatia kuwepo kwa mvutano wa muda mrefu kuhusu kuzuiwa kwa shughuli za kisiasa nchini humo, ambapo vyama vya upinzani vimekuwa vikilalamika kunyimwa fursa ya kufanya mikutano ya kisiasa kama sheria zinavyotaka.


BBC
 
Hii ni platform muhimu sana vyama vyote wahudhurie tena mkutano uwe live kwenye tv
 
Mimi Jumamosi jioni nitashiriki naomba posho zije mapema ili nipange bajeti.
 
Huko siyo kuahirishwa bali ni kuufuta! Kuahirishwa isingekuwa zaidi ya mwezi, kwa sasa wafanye mpango wa kuuitisha upya kwa mbinu tofauti!
 
Hii serikali huwa inafikiri kuwa inaongoza wajinga. Inajulikana hakuna kikao kilichoketi kuamua marufuku ya vyama kufanya siasa, kwanini leo wanaita vyama kujadili marufuku hiyo ambayo ni kinyume na Katiba? Matumizi mabaya ya fedha na muda!
 
Kuna haja gani ya kushiriki mkutano wa kujadili mambo ambayo yamewekwa wazi na katiba!?
Kimsingi,mkutano huo umelanga kuonesha umma uwepo wa demokrasia katika serikali kitu ambacho si kweli.
 
Hii serikali huwa inafikiri kuwa inaongoza wajinga. Inajulikana hakuna kikao kilichoketi kuamua marufuku ya vyama kufanya siasa, kwanini leo wanaita vyama kujadili marufuku hiyo ambayo ni kinyume na Katiba? Matumizi mabaya ya fedha na muda!
Wanataka kupiga pesa
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…