Mkutano kati ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jeshi la Polisi na wadau wa siasa nchini waahirishwa

Mkutano kati ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jeshi la Polisi na wadau wa siasa nchini waahirishwa

Hii serikali huwa inafikiri kuwa inaongoza wajinga. Inajulikana hakuna kikao kilichoketi kuamua marufuku ya vyama kufanya siasa, kwanini leo wanaita vyama kujadili marufuku hiyo ambayo ni kinyume na Katiba? Matumizi mabaya ya fedha na muda!
This is very important point to note lakini inashangaza watu kama Babati hawaelewi na hawaoni nia iliyo nyuma ya hawa watu
 
Kuna haja gani ya kushiriki mkutano wa kujadili mambo ambayo yamewekwa wazi na katiba!?
Kimsingi,mkutano huo umelanga kuonesha umma uwepo wa demokrasia katika serikali kitu ambacho si kweli.
Kosa watafanya chadema na nccr ni kushiriki kikao haramu, wao wanafanyakazi kwa mujibu wa katiba na sio kwa huruma za siro na msajili

Wanafanya Hiko kikao ili kuwahadaa donor country
 
Waliosusia ni CHADEMA na nccr tu kwa nini wasiendelee na vyama vingine?
 
Ushauri wangu kwanza kesi ya FAM waifute au kama wanaona aibu basi wamtoroshe aende uhamishoni waseme alitoroka Ukonga kesi iendelee kuwepo ila mwamba mafichoni ughaibuni.

Hili la msajili limefeli kabla halijatekelezwa ukisema SIASA za Nchi hii unazungumzia CCM,CDM wengine wako kwa mbali wanajivuta.
 
Mkutano wa kinafiki kuhalalisha udhalimu wao wa kuwahonga majaji vyeo ili wapindishe sheria makusudi ili kuwaumiza wengine, wakakae wenyewe waongee kwanini wanahairisha?
 
Kuna vyama ambavyo ni mali ya ccm na ndivyo vinaenda ktk huo mkutano.
Chama makini hakiwezi kushiriki mkutano na msajili hata kidogo!
 
Mkuu sijakuelewa vizuri
Ok, nitakuelewesha...

Nimesema maandiko yako mengi kuhusu uamuzi wa CHADEMA, NCCR na ACT Wazalendo kukataa kushiriki mkutano huu wenye ajenda tatatishi ya "kujadili maudhui ya utekelezaji wa sheria inayoviongoza vyama vya siasa kufanya shughuli zao" ukiongozwa na;

1. Msajili wa vyama vya siasa [msimamizi wa sheria inayolea na kuongoza shughuli za vyama siasa na;

2. Polisi [ambao kwa maagizo ya wanasiasa wa upande wa pili walioko madarakani, huivunja sheria hii waziwazi mchana kweupe]

Kwa maoni yako unadhani kuwa, hivi vyama i.e CHADEMA, ACT Wazalendo & NCCR vinafanya makosa kutoshiriki kikao hki kwa sababu umesema "wanakosa fursa ya ku - air out" grievances zao...

Mimi ndo nakuambia sasa, kuwa huoni uovu uliojificha nyuma ya mipango ya CCM kwa kikao hicho...

Na isitoshe mvunja sheria [msajili wa vyama vya siasa na polisi] wanapata wapi morality ya kuitisha kikao cha mapatano na usuluhishi wakati wao wenyewe ndiyo watuhumiwa wa kuvunja sheria...?

Kwa kifupi sana ndg Babati ni kuwa, huwezi kupata matokeo mazuri kwa kutumia njia haramu zisizo sahihi....!

Kama serikali inataka political reconciliation kati ya Makundi mbalinbali vikiwemo vyama vya siasa, basi njia sahihi na nzuri itumike kuleta taifa pamoja ....
 
Mkutano wa kati ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jeshi la Polisi na wadau wa siasa nchini uliopangwa kufanyika Dodoma wiki hii. Sababu za kuahirishwa kwake inaelezwa ni ili kutoa nafasi zaidi kwa wadau wengi zaidi kushiriki kikamilifu.

Mkutano huo uliolenga kujadili maudhui ya utekelezaji wa sheria zinazoratibu shughuli zote za siasa Tanzania' ulikuwa uhudhuriwe pia na waziri mkuu, Kassim Majaliwa.

Msajili msaidizi wa vyama vya siasa nchini Tanzania, Sixty Nyahoza aliiambia BBC kwamba, mbali na waziri mkuu na baadhi ya mawaziri, mkutano huo ulipangwa kuhudhuriwa na pia wadau wote muhimu katika siasa vikiwemo vyama vya siasa, Azaki, waandishi wa habari na viongozi wa dini.

Kama ilivyonukuliwa na mtandao wa gazeti la Mwananchi, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania, Juma Ali Khatib amesema mkutano huo hautakuwepo kama ulivyopangwa awali, lakini maandalizi yanaendelea kwa kuwa utafanyika mwezi Desemba, mwaka huu.

Hata hivyo tarehe ya kufanyika mkutano huo itatangazwa baadaye na utahusisha wadau tofauti wakiwamo wa vyama vya siasa vilivyotangaza kuususia kwa sababu tofauti.

Kabla ya kuahirishwa kwa mkutano huo, vyama vya Chadema na NCCR Mageuzi vilishatangaza kutoshiriki huku vikitoa masharti kwa Ofisi ya Msajili.

Alisema wadau wote wameshajulishwa kuhusu kuahirishwa kwa mkutano huo uliotarajiwa kuleta suluhu ya sintofahamu ya kisiasa nchini, hasa mvutano kati ya vyama vya siasa na Jeshi la Polisi.

Mkutano huo unakuja kufuatia kuwepo kwa mvutano wa muda mrefu kuhusu kuzuiwa kwa shughuli za kisiasa nchini humo, ambapo vyama vya upinzani vimekuwa vikilalamika kunyimwa fursa ya kufanya mikutano ya kisiasa kama sheria zinavyotaka.


BBC
Kwani vyama vya upinzani ni chadema tu?? wafanye na ccm, Chauma, APPT- maendeleo na SAU.
 
Kwani vyama vya upinzani ni chadema tu?? wafanye na ccm, Chauma, APPT- maendeleo na SAU.

Lengo lao ni cdm ili wawape masharti ya kufanya siasa zisizoiumiza ccm. Wanajua Cdm ndio yenye ushawishi kwani hata kwenye chaguzi Cdm wakisusia wapiga kura halali wa ccm huwa wanaonekana maana huwa ni wachache sana. Sasa hivi tumewaachia wenyewe washiriki uchaguzi, chaguzi zimegeuka kuwa kama disco la watu jinsia moja, halinogi kabisa maana hakuna wa kumkumbatia.
 
Ok, nitakuelewesha...

Nimesema maandiko yako mengi kuhusu uamuzi wa CHADEMA, NCCR na ACT Wazalendo kukataa kushiriki mkutano huu wenye ajenda tatatishi ya "kujadili maudhui ya utekelezaji wa sheria inayoviongoza vyama vya siasa kufanya shughuli zao" ukiongozwa na;

1. Msajili wa vyama vya siasa [msimamizi wa sheria inayolea na kuongoza shughuli za vyama siasa na;

2. Polisi [ambao kwa maagizo ya wanasiasa wa upande wa pili walioko madarakani, huivunja sheria hii waziwazi mchana kweupe]

Kwa maoni yako unadhani kuwa, hivi vyama i.e CHADEMA, ACT Wazalendo & NCCR vinafanya makosa kutoshiriki kikao hki kwa sababu umesema "wanakosa fursa ya ku - air out" grievances zao...

Mimi ndo nakuambia sasa, kuwa huoni uovu uliojificha nyuma ya mipango ya CCM kwa kikao hicho...

Na isitoshe mvunja sheria [msajili wa vyama vya siasa na polisi] wanapata wapi morality ya kuitisha kikao cha mapatano na usuluhishi wakati wao wenyewe ndiyo watuhumiwa wa kuvunja sheria...?

Kwa kifupi sana ndg Babati ni kuwa, huwezi kupata matokeo mazuri kwa kutumia njia haramu zisizo sahihi....!

Kama serikali inataka political reconciliation kati ya Makundi mbalinbali vikiwemo vyama vya siasa, basi njia sahihi na nzuri itumike kuleta taifa pamoja ....
Umeeleza vizuri sana Mkuu. Pia ndugu Babati atambue kwamba msajili wa vyama vya siasa na Polisi, wanajua kabisa kwamba KATIBA inaruhusu hicho ambacho kilizuiwa kinyume cha KATIBA, sasa kama hakukuwa na vikao vya kuzuia, kwa nini sasa kuwe na vikao kujadili hii hali ya sintofahamu. Msajili anajua kabisa katika vyama anavyovilea, kuna chama kimoja kinachopewa upendeleo kufanya mikutano bila zuio. Ndugu Babati tafakari hayo aliyoyajadili Mkuu.
 
Umeeleza vizuri sana Mkuu. Pia ndugu Babati atambue kwamba msajili wa vyama vya siasa na Polisi, wanajua kabisa kwamba KATIBA inaruhusu hicho ambacho kilizuiwa kinyume cha KATIBA, sasa kama hakukuwa na vikao vya kuzuia, kwa nini sasa kuwe na vikao kujadili hii hali ya sintofahamu. Msajili anajua kabisa katika vyama anavyovilea, kuna chama kimoja kinachopewa upendeleo kufanya mikutano bila zuio. Ndugu Babati tafakari hayo aliyoyajadili Mkuu.
Mi nakubali lakini ugomvi wowote humalizwa kwa njia ya mazungumzo
 
Back
Top Bottom