The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,541
This is very important point to note lakini inashangaza watu kama Babati hawaelewi na hawaoni nia iliyo nyuma ya hawa watuHii serikali huwa inafikiri kuwa inaongoza wajinga. Inajulikana hakuna kikao kilichoketi kuamua marufuku ya vyama kufanya siasa, kwanini leo wanaita vyama kujadili marufuku hiyo ambayo ni kinyume na Katiba? Matumizi mabaya ya fedha na muda!
Mkuu sijakuelewa vizuriThis is very important point to note lakini inashangaza watu kama Babati hawaelewi na hawaoni nia iliyo nyuma ya hawa watu
Kosa watafanya chadema na nccr ni kushiriki kikao haramu, wao wanafanyakazi kwa mujibu wa katiba na sio kwa huruma za siro na msajiliKuna haja gani ya kushiriki mkutano wa kujadili mambo ambayo yamewekwa wazi na katiba!?
Kimsingi,mkutano huo umelanga kuonesha umma uwepo wa demokrasia katika serikali kitu ambacho si kweli.
Wawepo kufanya nini?Muhimu wawepo viongozi wa dini wa kweli kama Shoo, Bagonza, Mwamakula na Sheih Ponda
Kuhakikisha amani inatawalaWawepo kufanya nini?
Washiriki upuuzi? Upuuzi mwingine...Kuhakikisha amani inatawala
Hatuhudhurii kwenye maigizo. Aende Shibuda,CCM na TLPHii ni platform muhimu sana vyama vyote wahudhurie tena mkutano uwe live kwenye tv
Mbona kwenye kampeni huwa wanaalikwa viongozi wa kisiasa! Huwa wanafanya Nini?Viongozi wa dini wa nini kwenye vikao vya kisiasa
Ok, nitakuelewesha...Mkuu sijakuelewa vizuri
Viongozi wa dini wa nini kwenye vikao vya kisiasa
Kwani vyama vya upinzani ni chadema tu?? wafanye na ccm, Chauma, APPT- maendeleo na SAU.Mkutano wa kati ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jeshi la Polisi na wadau wa siasa nchini uliopangwa kufanyika Dodoma wiki hii. Sababu za kuahirishwa kwake inaelezwa ni ili kutoa nafasi zaidi kwa wadau wengi zaidi kushiriki kikamilifu.
Mkutano huo uliolenga kujadili maudhui ya utekelezaji wa sheria zinazoratibu shughuli zote za siasa Tanzania' ulikuwa uhudhuriwe pia na waziri mkuu, Kassim Majaliwa.
Msajili msaidizi wa vyama vya siasa nchini Tanzania, Sixty Nyahoza aliiambia BBC kwamba, mbali na waziri mkuu na baadhi ya mawaziri, mkutano huo ulipangwa kuhudhuriwa na pia wadau wote muhimu katika siasa vikiwemo vyama vya siasa, Azaki, waandishi wa habari na viongozi wa dini.
Kama ilivyonukuliwa na mtandao wa gazeti la Mwananchi, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania, Juma Ali Khatib amesema mkutano huo hautakuwepo kama ulivyopangwa awali, lakini maandalizi yanaendelea kwa kuwa utafanyika mwezi Desemba, mwaka huu.
Hata hivyo tarehe ya kufanyika mkutano huo itatangazwa baadaye na utahusisha wadau tofauti wakiwamo wa vyama vya siasa vilivyotangaza kuususia kwa sababu tofauti.
Kabla ya kuahirishwa kwa mkutano huo, vyama vya Chadema na NCCR Mageuzi vilishatangaza kutoshiriki huku vikitoa masharti kwa Ofisi ya Msajili.
Alisema wadau wote wameshajulishwa kuhusu kuahirishwa kwa mkutano huo uliotarajiwa kuleta suluhu ya sintofahamu ya kisiasa nchini, hasa mvutano kati ya vyama vya siasa na Jeshi la Polisi.
Mkutano huo unakuja kufuatia kuwepo kwa mvutano wa muda mrefu kuhusu kuzuiwa kwa shughuli za kisiasa nchini humo, ambapo vyama vya upinzani vimekuwa vikilalamika kunyimwa fursa ya kufanya mikutano ya kisiasa kama sheria zinavyotaka.
BBC
Kwani vyama vya upinzani ni chadema tu?? wafanye na ccm, Chauma, APPT- maendeleo na SAU.
Umeeleza vizuri sana Mkuu. Pia ndugu Babati atambue kwamba msajili wa vyama vya siasa na Polisi, wanajua kabisa kwamba KATIBA inaruhusu hicho ambacho kilizuiwa kinyume cha KATIBA, sasa kama hakukuwa na vikao vya kuzuia, kwa nini sasa kuwe na vikao kujadili hii hali ya sintofahamu. Msajili anajua kabisa katika vyama anavyovilea, kuna chama kimoja kinachopewa upendeleo kufanya mikutano bila zuio. Ndugu Babati tafakari hayo aliyoyajadili Mkuu.Ok, nitakuelewesha...
Nimesema maandiko yako mengi kuhusu uamuzi wa CHADEMA, NCCR na ACT Wazalendo kukataa kushiriki mkutano huu wenye ajenda tatatishi ya "kujadili maudhui ya utekelezaji wa sheria inayoviongoza vyama vya siasa kufanya shughuli zao" ukiongozwa na;
1. Msajili wa vyama vya siasa [msimamizi wa sheria inayolea na kuongoza shughuli za vyama siasa na;
2. Polisi [ambao kwa maagizo ya wanasiasa wa upande wa pili walioko madarakani, huivunja sheria hii waziwazi mchana kweupe]
Kwa maoni yako unadhani kuwa, hivi vyama i.e CHADEMA, ACT Wazalendo & NCCR vinafanya makosa kutoshiriki kikao hki kwa sababu umesema "wanakosa fursa ya ku - air out" grievances zao...
Mimi ndo nakuambia sasa, kuwa huoni uovu uliojificha nyuma ya mipango ya CCM kwa kikao hicho...
Na isitoshe mvunja sheria [msajili wa vyama vya siasa na polisi] wanapata wapi morality ya kuitisha kikao cha mapatano na usuluhishi wakati wao wenyewe ndiyo watuhumiwa wa kuvunja sheria...?
Kwa kifupi sana ndg Babati ni kuwa, huwezi kupata matokeo mazuri kwa kutumia njia haramu zisizo sahihi....!
Kama serikali inataka political reconciliation kati ya Makundi mbalinbali vikiwemo vyama vya siasa, basi njia sahihi na nzuri itumike kuleta taifa pamoja ....
Mi nakubali lakini ugomvi wowote humalizwa kwa njia ya mazungumzoUmeeleza vizuri sana Mkuu. Pia ndugu Babati atambue kwamba msajili wa vyama vya siasa na Polisi, wanajua kabisa kwamba KATIBA inaruhusu hicho ambacho kilizuiwa kinyume cha KATIBA, sasa kama hakukuwa na vikao vya kuzuia, kwa nini sasa kuwe na vikao kujadili hii hali ya sintofahamu. Msajili anajua kabisa katika vyama anavyovilea, kuna chama kimoja kinachopewa upendeleo kufanya mikutano bila zuio. Ndugu Babati tafakari hayo aliyoyajadili Mkuu.