Mkuu, huyo mtoto wa mtu unayelala nae kimya kimya siku asipoamka hakuna mtu atakuelewa hapo mtaani

Down To Earth

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
21,940
Reaction score
16,643
Mi nakwambia ukweli kabisa
Haya mapenzi haram unayofanya kila siku kwa kuwaleta watoto wa watu Geto kwako wanalala na wewe kisha alfajiri unawarejesha kwao...

Ipo siku yako nakwambia!

Mtoto wa watu akifia geto kwako, hakuna mtu atakuelewa hapo, we waone tu wanakuchekea na kukupa sifa... eti wewe ni kidume.. acha kabisa ndugu chukua tahadhari!

Sisi binadamu tunapita, hatueleweki tutakatia kamba muda gani, saa gani.. usiku au mchana!

Kama umefikia umefikia uwezo wa kupanga Geto na kuvusha kina dada kila leo, basi unaweza kuoa na kumiliki Mwanamke kihalali kabisa...

NAKUSHAURI OA..
 
Na gharama za kumuweka ndani wa halali ni ndogo tofauti na gharama anazotumia kuwavusha hao wa kimya kimya!
 
Huko huko!
Ajali kazini dume! 💪💪💪
 
Duuuh, utafanya watu waliofungiwa nje wakose msaada wa kulala, unasema unalala na mtu kisiri asipo amka jiulize na wewe vipi kama usipo amka? Kiufupi unawaza sana mkuu acha watu waendelee kuishi kwa upendo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…