Mkuu wa Mkoa, jukumu la kuwaondoa Wamachinga ni lako. Usilikwepe

Mkuu wa Mkoa, jukumu la kuwaondoa Wamachinga ni lako. Usilikwepe

Katika vitu ambavyo ulipaswa uende navyo taratibu tena kwa Umakini mkubwa mno ni hili Suala la Wamachinga ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam nilidhani kuwa Wewe ni Mtoto wa mjini kweli tena wa Kawe na hili ungelishtukia upesi...
Mkuu achana na polojo hizo, sasa hivi hilo linaenda kutendeka na kubakia historia, kwani imekuwa kero kubwa mno!!yaani waenda kwa miguu sasa hivi wanagongwa na magari kisa sehemu zao zimepangwa vitu!!kwa taarifa yako huu ni mkakati wa nchi nzima sasa!

Hatuwezi kukaa na kuwaogopa watu wakijiamulua kufanya wanavyotaka tu eti kisa utachukiwa, nenda mbagala ukaone wachina wanavyopata kazi kwenye ujenzi wa barabara za mwendokasi, hadi wanatishiwa kupigwa, kisa kuwaambia watoe bidhaa zao ili kazi zifanyike!!!, Kwani ccm mnategemea kura zilizopigwa ili kushinda?mmeanza lini?

Wiki iliyopita kule kwenye stendi ya magufuri kwa nje walikuwa wameanza kujenga mabanda, yote yalivunjwa na mgambo!!
 
Jamaa km umemsikiliza msala na mpira amewapa Wakuu wilaya na Wakurugenzi yeye kajitoa kweny hili sakata ili likibuma lisimkute
Kama huelewi utaratibu kaa kimya!!hayo maeneo yote yako chini ya manispaa, na DC, na DED, ndio wahusika , wenye vyombo vya utekelezaji, na wasimamizi wa BY LAWS!!zamu hii lazima wawekewe utaratibu, mtu anafungua grocery juu ya mtalo, wateja wake wanajisaidia barabarani!!
 
SAHAU huyo bwana kutumbuliwa.

Au nikuulize kwa mtego huu ambao wewe kachero "uchwara" unasema amenaswa unategemea mpaka lini atakua ametumbuliwa?

Maana unaweza ukapita mwaka akatumbuliwa ndo useme kisa wamachinga, Hahahahaha..

umebugi, SUPERBUG.
 
Katika vitu ambavyo ulipaswa uende navyo taratibu tena kwa Umakini mkubwa mno ni hili Suala la Wamachinga ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam nilidhani kuwa Wewe ni Mtoto wa mjini kweli tena wa Kawe na hili ungelishtukia upesi.

Kama kuna Kitu ambacho Rais na CCM hawataki Kukisikia ni Wamachinga Kubughudhiwa hapa nchini.

Hakuna asiyejua kuwa Mtaji Mkuu ( Mama ) wa Kiushawishi na Kisiasa wa CCM na ni hawa Wamachinga.

Kwakuwa ulipoteuliwa ghafla ulionekana hufai kuwa RC wa Dar sasa Watu wamekutega nawe umeingi mazima mazima.

Sikushauri tena kuwa uachane na huu Mpango wako, ila ninachojua umeshatoa Sababu ya Wewe Kutumbuliwa rasmi.

Upo uwezekano Mkoa wa Dar es Salaam akapewa Mwanamke au Kijana mwenye Msimamo na Ushawishi ndani ya CCM.

RC Amos Makalla napenda sana ubakie kuwa RC wa Dar ukizingatia ni mwana Simba SC Mwenzangu ila unaondolewa.

Unawaondoa Wamachinga kama ulivyoahidi ila Wamachinga hawa hawa watamfanya akutoe.

Wabaya wako ndani ya Mkoa, System na CCM wamekutafuta na wakakudanganya kuhusu Wamachinga nawe umeuvagaa.

Ni Suala la muda tu, ila Unatumbuliwa!
Acha wanga
 
Labda akaroge na akatambike zaidi pale Kwao Kawe Ukwamani nyuma ya Hotel ya Ghorofa ya Victoria alipozaliwa na Kukulia pia, ili Mizimu imuokoe ila hili la Wamachinga ndilo linaenda Kumuondoa kama RC wa Dar es Salaam muda wowote kutoka sasa.
Acha kuwanga
 
Sijui shule gani mlisoma!?

Yani mawazo yako binafsi unayalazimisha...
 
Nafikiri hivi..kama kuna mtu anajitaftia riziki sehemu na habughuzi riziki zako achana naye!
Hizo ni fikira zako lakini ghasia za wamachinga zimepita kipimo, maeneo mengi watembea kwa miguu inawabidi watumie barabara za magari ambazo nazo zimevamiwa na wamachinga. Janga jingine ni nini kinachoendelea nyuma ya vibanda vyao wakati wa usiku, wizi.
 
Hizo ni fikira zako lakini ghasia za wamachinga zimepita kipimo, maeneo mengi watembea kwa miguu inawabidi watumie barabara za magari ambazo nazo zimevamiwa na wamachinga. Janga jingine ni nini kinachoendelea nyuma ya vibanda vyao wakati wa usiku, wizi.
Chochote kinachofanyika bila utaratibu ni ghasia na fujo
 
Chochote kinachofanyika bila utaratibu ni ghasia na fujo
Utaratibu ni pale unapokuwa haujaruhusiwa, lakini hawa waliruhusiwa na mwendazake kufanya biashara hata kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa na akasema wasibughuziwe.
 
Kilichonisikitisha zaidi ni kwamba RC Amos Makalla ni Mtoto Mjini hasa sasa nimeshangaa ni kwanini ameshindwa Kushtuka mapema kuwa hatakiwi Dar es Salaam na kwamba kuna Watu Maalum wametumwa Kumdanganya Kimaamuzi ili akosee kama watakavyo na Bi. Hangaya amle Kichwa (amtumbue) mazima.
Dar es Salaam inapaswa kuwa safi,sio Kama ilivyo Sasa ipo Kama dampo
 
Labda akaroge na akatambike zaidi pale Kwao Kawe Ukwamani nyuma ya Hotel ya Ghorofa ya Victoria alipozaliwa na Kukulia pia, ili Mizimu imuokoe ila hili la Wamachinga ndilo linaenda Kumuondoa kama RC wa Dar es Salaam muda wowote kutoka sasa.
Lengo la kuwafukuza wamachinga Ni kutengeneza mfumo wa biashara rasmi ili tupate Kodi.Na kwa vile mama Ni muumini wa Tozo,naona Kama Makalla hatafukuzwa
 
Kwa taarifa tu ni kuwa hakuna serikali ya wanyonge Tena

Maazimio ya TISS ni Kila kitu kirudi kama zamani

Hata michango ya shule January inarudi

Mama Samia anajua kila hatua inayofanywa juu ya machinga nyie mtapiga kelele.

Akijitokeza ni kupigilia msumari Kama alivyofanya kwenye tozo.

Huyu Mama ni TV tu walioshikiria remote ni watu wengine.

Huu ni utawala mwingine kabisa mnyonge Hana chake shauri yenu msiseme hatukuwaambia.
Shida machinga wameshindwa kuwa wastaarabu
 
Pedeshee Amos Makalla,baba Gabriel,mzee wa mvomero kwa sauti ya Nyoshi al sadaat au Pablo masai.

Ila jamaa akumbuke alipotoka kutoka kuwa mfyatua matofali na ulinzi wa petrol station.

Machinga pia binadamu na wana watu wanaowategemea nyuma yao.

Naunga mkono.
Kwa hiyo watembea kwa miguu sio binadamu?
 
Back
Top Bottom