Mkuu wa Mkoa Songwe ni Mtanzania? Jina kama Mkongo au Mrundi?

Mkuu wa Mkoa Songwe ni Mtanzania? Jina kama Mkongo au Mrundi?

Umetoa mfano mzuri wa huyo muisrael ambaye alijipachika jina linalofanana na jamii ya Syria na alifanya hivyo ili asitambulike kwahiyo hata hapa kwetu nina imani adui yeyote hawezi kujiweka katika hali ya kutiliwa shaka ndio maana watu wanambeza mleta uzi kwa sababu huyo angekuwa jasusi hawezi tena kutumia jina la kwao kiasi cha kumtilia shaka.
Usikaze kichwa. Point sio jina, alikozaliwa, alikosomea, alikofanya kazi au nini. Point ni kuwa na taarifa za mtumishi nyeti wa serikali na ikiulizwa kama hivi usibeze.

Mfano Marekani wana 5 levels of security clearance. Level ya chini anaweza kuwa fundi kurekebisha bomba la ofisini ameitwa, level ya staff kama mpishi ni nyingine, level ya mfanyakazi mwenye access ya taarifa za kuagizwa ni nyingine, level ya juu kabisa ya mwenye maamuzi ni Confidential clearance. Hata kama mtu kazaliwa nje anapitia security clearance kufanya kazi fulani akifaulu ndio anapata hata baba yake awe nje kama Obama.

Albert Einstein usalama walimkataa hawakumpa security clearance kwa kuwa ni Mjerumani na katoka uko ukubwani, hawakutaka ahusike na Manhattan project kutengeneza nuclear weapons wakati at the time alikuwa top scientist.
Ukienda nchi nyingine kama UK ukauliza historia ya wazazi au uraia wa viongozi utaambiwa Rish Sunak Waziri Mkuu ambavyo mama yake alizaliwa Tanzania na baba akazaliwa Kenya. Taarifa unapewa kwa uwazi kabisa, bongo ukiuliza background ya kiongozi unafichwafichwa as if haikuhusu. Kama mnataka private life si mfanye biashara au kilimo, huwezi taka kuongoza watu kisha maisha yako wasiyajue
 
Sitaki tujadili sana huko maana ni mjadala mpana sana, ila kwa hili ni heshima ya ID yake tu ndo inafanya tumshangae sikutegemea km ni mtu anaeendeshwa na mihemko ya kidini tena katika kila jambo na bora hapa walau waweza sema anatetea utz, kuna mada inamzungumzia mtoto wa madam prezidaa kukwepa kodi,,kasome boko alilitoa humo😂
Nilianza naye kule...aibu tupu
 
Usikaze kichwa. Point sio jina, alikozaliwa, alikosomea, alikofanya kazi au nini. Point ni kuwa na taarifa za mtumishi nyeti wa serikali na ikiulizwa kama hivi usibeze.

Mfano Marekani wana 5 levels of security clearance. Level ya chini anaweza kuwa fundi kurekebisha bomba la ofisini ameitwa, level ya staff kama mpishi ni nyingine, level ya mfanyakazi mwenye access ya taarifa za kuagizwa ni nyingine, level ya juu kabisa ya mwenye maamuzi ni Confidential clearance. Hata kama mtu kazaliwa nje anapitia security clearance kufanya kazi fulani akifaulu ndio anapata hata baba yake awe nje kama Obama.

Albert Einstein usalama walimkataa hawakumpa security clearance kwa kuwa ni Mjerumani na katoka uko ukubwani, hawakutaka ahusike na Manhattan project kutengeneza nuclear weapons wakati at the time alikuwa top scientist.
Ukienda nchi nyingine kama UK ukauliza historia ya wazazi au uraia wa viongozi utaambiwa Rish Sunak Waziri Mkuu ambavyo mama yake alizaliwa Tanzania na baba akazaliwa Kenya. Taarifa unapewa kwa uwazi kabisa, bongo ukiuliza background ya kiongozi unafichwafichwa as if haikuhusu. Kama mnataka private life si mfanye biashara au kilimo, huwezi taka kuongoza watu kisha maisha yako wasiyajue
Mleta uzi ameuliza jina na ndicho kinachompa shaka hadi kuuliza asili ya huyo mtu na ndicho watu wanamjibu,acha kujitia ujuwaji kwa kutoa maelezo marefu ambayo mleta uzi sio hitaji lake.
 
Mleta uzi ameuliza jina na ndicho kinachompa shaka hadi kuuliza asili ya huyo mtu na ndicho watu wanamjibu,acha kujitia ujuwaji kwa kutoa maelezo marefu ambayo mleta uzi sio hitaji lake.
Jamaa kajibu mantiki ya kuulizwa kwa asili ya jina lake. Ujuaji ndio nini sasa!?
 
Eti outsiders. Hawa huwa hawasahau asili zao.

Kwa mfano akitoka Rwanda akaja Tz ni full chinja chinja
Hatukua makini 2015 na mayokeo yake tuliyaona, hivi mleta mada kakosea wapi kuuliza?
Nani hajui madhara ya 2015 kuchomeka Mrundi madarakani na tuliyokutana nayo hadi Mungu akagundua kuwa sisi ni taifa la hovyo akatupigania?
Tuache maamuzi ya kichovu, hawa outsider tujichunge nao sana
 
Mkuu wa mkoa mpya wa Songwe
Francis Kasavubu Michael...ni Mtanzania??niliposikia jina hili wakati yupo katibu wizara ya sayansi. Nilijiuliza hili swali..ni Mtanzania? Mbona jina kama Mcongo au mrundi?...

Kuna anaemjua vizuri hapa JF?

Mtu hadi anateuliwa bado unakuwa na shaka ya uraia wake??
 
Kwa kidogo ninachokifahamu...huyu Jamaa ni Mtanzania...origin yake kama sikosei ni Kigoma(nt sure)...ila huko nyuma aliwahi kuwa pale UDSM kama Lecturer...,Magu ndie aliemuintroduce Serikalini...alianzia kuwa mjumbe wa Bodi TPA .. akaja Naibu Katibu Mkuu..kipindi hicho hicho cha Magu...ndio mpaka leo hapa...
Navyofahamu Dr.Francis ni mzima sana kichwani na ni Mtendaji mzuri sana...yaani ni wale watu ambao wana uwezo wa kuanzisha jambo..na kulisimamia mpaka mwisho...hata kitaalum alianzia kuwa Mwalimu huko akajiendeleza mpaka kuwa na PHD..(unaweza kuona alivyo na juhudi)

Kilichonishangaza sijui kafanya kosa gani hapo...manaake nilisikia kuwa alipewa hiyo nafasi ya KM-ELIMU kwa sababu ya Restructuring inayoendelea kwenye mfumo wa Elimu kutokana na Uwezo alio nao..
Nadhani unafahamu hata Waziri wake nae anasemekana ni kichwa fulani hv...kwa wanaomfahamu...kwa hiyo nadhani combination yao ilidhaniwa ingefanya kitu kizuri...(Wasalam...nilipokosea si kwa makusudi kwani baadhi hasa sifa za academic ni za kuhadithiwa na watu waliosoma nae)

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
Mkuu mpaka hapo basi, huyu ni fwasi ya bukavu au kwa Slimboy, Tanzania hatuna akina Kasavubu piga ua huyu atakuwa mkimbizi kama akina Shusho.
 
Huwa nawashangaa sana watanzania kwa kuwa na vitabia vya kibaguzi, hasa wakiwa na wadhifa fulani Serikalini...
Hawataki kabisa kusikia majina asilia ya Kigoma, Rukwa, na Kagera hasa pale yanapofanana na majina ya nchi jirani za DRC, Rwanda na Burundi.
Kuna wapemba, waarabu, Wahindi, waoman wacomoro na wahindi kibao wamejazana nchi hii na baadhi wako kwenye nyadhifa Serikalini kwa majina ya kiarabu, kihindi na kiajemi ....
huwezi kusikia ngozi nyeusi akihoji!... Sana sana atasilimu na kujiita Abdallah na maisha yataendelea akijisikia kuwa mtanzania halisi,tena mwenye uhalali tosha wa kuhoji watu wa makabila mengine halali ya JMT......Kasumba mbaya sana hii. 😳
 
Surnames za mipakani hasa Kigoma na hata Kagera zinaingiliana na nchi jirani.

Akina Bizimungu,Kwizera,Havyarimana utawakuta Manyovu wakiwa na ID za NIDA.
 
Mleta uzi ameuliza jina na ndicho kinachompa shaka hadi kuuliza asili ya huyo mtu na ndicho watu wanamjibu,acha kujitia ujuwaji kwa kutoa maelezo marefu ambayo mleta uzi sio hitaji lake.
Nimechagua kuwa mjuaji na wewe umechagua kuwa kilaza, hapo hakuna tatizo baki na ukilaza wako kama unakufaa.
Turudi kwenye mada, kuna tatizo gani Mtanzania akiuliza taarifa za wazi za kiongozi wa serikali?
Kuna maficho gani yanafanyika kutaja jina la kiongozi na asili yake. Mwaka 1961 tulimpata Kambarage na jina lake tunajua linatoka wapi likimaanisha nini, mwaka 2023 inakuwa ugomvi kuulizwa kwa jina la kiongozi.
 
Tatizo swali limekuja baada badala lingekuwa limekuja kabla, sasa kama kweli mrundi au mkongo itabadili nini hapa? Ndio maana kuna watu wanasema huu ni unoko kama unoko mwingine
 
Ni Mtanzania by Birth Mha wa Kigoma. Kwa wale tuliopitia UDSm tunamfahamu alikuwa Lecturer akifundisha HRM na Mengineyo Kwa muda mrefu. Ameandika Machapisho Mengi tuu juu Management Principles.
Francis Michael was the UDASA Chairman from 2012 to 2014. He is currently the Deputy Permanent Secretary (DPS) in the President’s Office Public Service Management and Good Governance (PO- PSM&GG).

Before his appointment as a DPS in 2019, he was a Lecturer at the University of Dar es Salaam Business School in the Department of General Management. He holds a PhD in Human Resource Management (HRM), a Master of Business Administration, and a Bachelor of Arts in Public Administration, all from the University of Dar es Salaam. Also, he has a Licentiate degree (MPhil) in HRM from Umea Sweden and a Postgraduate Diploma in Law from the University of Dar es Salaam (UDSM), which is an important qualification for an HRM career practice.

Prior to joining the UDSM for undergraduate studies, he obtained a Diploma in Education from Marangu Teachers College. His research and areas of expertise include HRM, Industrial Relations, Corporate Governance and all other Behavioural Sciences related fields of study.

Dr Michael has held positions in various public organisation’s boards of directors, including The University of Dar es Salaam Council, the Board of Tanzania Ports Authority (TPA) for two different terms, and the Board of Tanzania Workers Compensation Fund (WCF). He held the chairperson position of the Researchers’ Academicians and Allied Workers Union (RAAWU) at the UDSM branch for several terms and was a member of the national executive committee of the Trade Unions Confederation of Tanzania (TUCTA). As a DPS, he sits on the country’s high-level decision-making platforms like the Inter-Ministerial Technical Committee (IMTC).

Dr Michael and his HRM expert counterpart, the late Dr Cleo Ngirwa, constituted for the first time the HRM program at the UDSM and a number of other higher learning institutions in the country.

In his private time, Dr Michael likes to play basketball and read books.
Haya maelezo umeandika yanapatikana kwa urahisi tu,swali limeuliza unajua kuwa anaitwa Kasavubu? Na mtoa mada anaulizia asili ya hili jina Kasavubu.
 
Majina ya koo mtu hajipi au kupewa na mzazi, huyakuta tu. Hata kama utaitwa George Washington Mwainyekule, hiyo Mwainyekule bado itatambulisha asili yenu.

Kwani Kasabubu ni la Ukoo? Ni AKA kama za unavyoona Dr Joseph Kasheku Msukuma au Livingstone Lusinde Kibajaji au Kama Said Sued Scud.

Hao watu wana majina ya official na la kitaa ndiyo maana unaweza ukakuta huko kwao wanamuita "Franswa" au "Misheli".
 
Kwani Kasabubu ni la Ukoo? Ni AKA kama za unavyoona Dr Joseph Kasheku Msukuma au Livingstone Lusinde Kibajaji au Kama Said Sued Scud.

Hao watu wana majina ya official na la kitaa ndiyo maana unaweza ukakuta huko kwao wanamuita "Franswa" au "Misheli".
Ni aka i ayotumika kwenye official documents!? Aisee! Hii ni kali!
 
Mkuu wa mkoa mpya wa Songwe
Francis Kasavubu Michael...ni Mtanzania??niliposikia jina hili wakati yupo katibu wizara ya sayansi. Nilijiuliza hili swali..ni Mtanzania? Mbona jina kama Mcongo au mrundi?...

Kuna anaemjua vizuri hapa JF?
Record yake ya kuzaliwa, shule, vyuo nk inasemaje
 
Mkuu wa mkoa mpya wa Songwe
Francis Kasavubu Michael...ni Mtanzania??niliposikia jina hili wakati yupo katibu wizara ya sayansi. Nilijiuliza hili swali..ni Mtanzania? Mbona jina kama Mcongo au mrundi?...

Kuna anaemjua vizuri hapa JF?
Anaweza kuwa mkongo au mrundi au UK ila kama alizaliwa Tz ni Mtanzania hivyo huna haja yakuwa na shaka naye.
 
Back
Top Bottom